Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Ishu ni kwamba

(1)Zitto Kabwe alisema, JM ni raisi wa barabara, maji na umeme lakini kwa Mwanadamu mahitaji ni zaidi ya vitu hivyo, Mwanadamu anahitaji UHURU, JM Anaondoa UHURU wa habari kwa kasi ya kutisha, mfano ni hilo la Bunge Live!, kiufupi anaturidsha enzi za Zidumu fikra za Mwenyekiti.

(2) Pili, anasema anapenda haki na anasema umuombee, lakini Kuna Mioyo iliyoumizwa ya Wazanzibari, Sijui Wale kama wanamuombea kwa Wema

(3) Tatu, ana nia njema sana na Taifa hili, hilo wala halina mjadala, ila Baba wa Taifa mwalimu JKN alisema " Nia njema yaweza kuwa na maangamizi tele" akimaanisha waweza kufanya jambo jema sana lakini kwa approach isiyo sahihi, Consequences zake huwezi kuleta excuse ya kwamba ulitenda kwa nia njema!

(4) Nne anatumbua hapa na pale, hatumbui pote na mahali zote, na matokeo yake anadeal na mafisadi (watu) lakini Hajadeal na UFISADI (Mfumo). Inabidi katika hatua zitakazofuata anajenga taasisi, anaimarisha taasisi, na Anacomputerize mifumo
 
Tanzania zaidi ya unavyoijua.
Niliandika mapema sana hapa wakati serikali hii ikiwa na miezi miwili tu kuwa utawala wa nchi za kiafrika umejengwa katika kumuangalia Rais anataka nini?
Hilo ni kosa namba moja, mawaziri wakaanza kufanya kazi kwa namna ambavyo rais anataka.
Hivi uzembe umeisha kwenye taasisi na idara za umma?
Kilichotokea uwanja wa ndege ni ushahidi/ishara tosha kuwa serikali haiwezi kututoa hapa tulipo kwa ziara za kushutukiza.
Kuna shida gani tukiwa na aina ya serikali na utawala ambao kila kiongozi anakuwa na majukumu ambayo yapo wazi?
Unaweza kuona issue ya machinjio tu pale Vingunguti wanakwenda mawaziri watatu.
Narudia kusema Mheshimiwa Rais Kama Ana nia ya dhati ya kuboresha hali ya maisha ya mtanzania lazima awe na serikali ambayo kila kiongozi/cheo linakuwa "defined" kwa majukumu yake.

Utashangaa mkanganyiko uliopo,
1. Mkuu wa mkoa anakuwa na kazi ya kukagua shule, afisa elimu anafanya nini?
2. Mkuu wa mkoa anajivika jukumu la kutafuta wafanyakazi hewa? Wakurugenzi na maafisa rasilimali watu, maafisa tawala wanafanya nini?

Ikifika siku tukawa na serikali ambayo kila mtu ana majukumu yake yanayoeleweka na akayatekeleza ipasavyo basi tutafika mbali.

Tusimwachie mzigo huu Rais peke yake hawezi kufanya ziara za kushtukiza kila mahali hata kama atatawala miaka 100.
Tuwajibike.
 
Huwezi kuendesha nchi kwa ufanisi ukitengeneza sifa binafsi. Tatizo la kupenda sifa sana ndilo linaiangusha serikali hii, kukosolewa ndio nafasi nzuri ya kuendesha mambo smoothly. Awamu ya nne pamoja na ubovu wake wote lakini ile hali ya kukubali kusemwa hadharani ilikuwa inawapa watu nafasi ya upunguza machungu yao.
Magu kaona Nape anafunga magazeti, anazuia matangazo ya Bunge na anakataa kusemwa akadhani itamsaidia lakini inammaliza kabisa, miezi sita hali iko hivi jee miaka miwili?
Kwa kweli hali ni mbaya sana kwa wananchi wa kawaida.....BAHATI mbaya bajeti asilimia 46 yote anaenda kuwalipa wachina ambao ni wakandarasi....wachina nao watazichukua na kupeleka kwao ukiacha vimanunuzi vidogo vidogo,mtaani pesa itaendela kuadimika
 
M mwanzon nliamin kua amejitoa mhanga na kuamua kuweka Chama pemben IL kuwakomboa wananchi ila mhhh naanza kupata mashaka ni kma vile Chama kimeanza kumbinya hiv hata waziri mkuu na vice n kama vile wamerud nyuma katika mapambano na kubaki neutral.
 
Mwanzoni mwa utawala wake ilikuwa kila gazeti linamwandika yeye tena vizuri. Vijiwe vyote kuanzia vya kahawa, daladala, bar na maofisini story alikuwa ni yeye tena watu wakimsema kama malaika mkombozi.

Ghafla upepo ukabadilika, watumishi wakaanza kukosoa utumbuaji majipu, wafanyabiashara wakakosoa mbinyo wake kwenye kodi, wanasiasa wakahoji style yake ya uongozi. Wananchi wa kawaida wakanigwa na maisha magumu (ingawa hawa bado wamebakiza kaimani fulani). Vyombo vya habari wanalalamikia kuminywa uhuru wao.

Kiujumla upepo unavuma vibaya kwa JPM naye ameshakiri ugumu wa kiti chake mpaka akasema angejua asingegombea urais. Je, rais wetu amekosea wapi mpaka hali imegeuka mapema hivyo?

Kwasababu hajui Free Market Economics, anachojua ni ubabe wa kiafrika ambao maraisi wengi wakiafrika wanao ambao unaharibu nchi
 
Kuna sababu kama 4 hivi naziona ndizo zinazomfanya achuje haraka hivi:

1. Kushindwa kwake kudili na majipu (wala rushwa wakubwa) na kubaki kuangaika na kesi za kuku. Hii imejionyesha kwa yeye kunywea kwenye swala la Lugumi, Wezi wa Escrow (kutekeleza maamuzi ya Bunge), kuendelea kukumbatia viongozi majizi, HSC na mambo kama hayo.

2. Kuendesha nchi pasipo kufuata utawala wa sheria. Anajiona yeye ndio ultimate decision maker wa kila kitu na hakuna anayejua zaidi yake. Sasa watu wameamua kumuacha afanye kazi zoootee peke yake.



3. Nchi kukosa muelekeo wa kiuchumi. Hii inapelekea kuwa na hali ngumu pasipo sababu. Bado anaangaika na kodi za machinga na mama Ntilie, wakati kule kwenye madini wanawaanchia wazungu wanachukua madhahabu na Almasi bureee kabisa. Hana vyanzo vipya vya kodi zaidi ya kumbana mwananchi wa kawaidi.

4. Kunyima Uhuru wa habari. Hii imejionyeshwa kupitia kukataa kuonyesha Bunge Live kwa sababu ya kuogopa wananchi kuona serikali yake ikikosolewa. Yeye anataka kusifiwa tu, ukimkosoa ni shida.
hivi ndivyo majibu ya wanajaami forum wote wanaopaswa kuchangia uzi huu,,,ile unapinga au kusapoti,,,toa hojaa,,,,asante mkuu na wengine,,matusi peleka tandaale na uvinza mkachezeshane chura
 
M mwanzon nliamin kua amejitoa mhanga na kuamua kuweka Chama pemben IL kuwakomboa wananchi ila mhhh naanza kupata mashaka ni kma vile Chama kimeanza kumbinya hiv hata waziri mkuu na vice n kama vile wamerud nyuma katika mapambano na kubaki neutral.

Akiwa Singida kwenye miaka 34 ya CCM alisema chama kwanza mengine baadaye.Tafakari.Hapo ndipo nilipomalizia yale niliyokuwa nayafikiria.............
 
Kuna sababu kama 4 hivi naziona ndizo zinazomfanya achuje haraka hivi:

1. Kushindwa kwake kudili na majipu (wala rushwa wakubwa) na kubaki kuangaika na kesi za kuku. Hii imejionyesha kwa yeye kunywea kwenye swala la Lugumi, Wezi wa Escrow (kutekeleza maamuzi ya Bunge), kuendelea kukumbatia viongozi majizi, HSC na mambo kama hayo.

2. Kuendesha nchi pasipo kufuata utawala wa sheria. Anajiona yeye ndio ultimate decision maker wa kila kitu na hakuna anayejua zaidi yake. Sasa watu wameamua kumuacha afanye kazi zoootee peke yake.



3. Nchi kukosa muelekeo wa kiuchumi. Hii inapelekea kuwa na hali ngumu pasipo sababu. Bado anaangaika na kodi za machinga na mama Ntilie, wakati kule kwenye madini wanawaanchia wazungu wanachukua madhahabu na Almasi bureee kabisa. Hana vyanzo vipya vya kodi zaidi ya kumbana mwananchi wa kawaidi.

4. Kunyima Uhuru wa habari. Hii imejionyeshwa kupitia kukataa kuonyesha Bunge Live kwa sababu ya kuogopa wananchi kuona serikali yake ikikosolewa. Yeye anataka kusifiwa tu, ukimkosoa ni shida.

Na kulifanya Bunge kama Department ndani ya ofisi yake kwa kuteua mpaka waziri wa Bunge aka NS
 
Utaratibu wa kumhukumu au kumpa mtu adhabu aliyekosea aliuanzisha mungu mwenyewe pale alipowahoji Adam na Hawa ktk bustani. Soma kitabu cha Mwanzo sura ya 3 mstari wa 1 hadi 19.
 
TB Joshua alikuja Tanzania akatembea peku....kibiblia hii ni mbaya sana.....ni sawa na wale manabii waliovaa magunia kulaani wafalme ambao baadae falme zao zilipigwa mapigo makali



Ktk Biblia hyo unayozungumzia ktendo cha MTU kutoa viatu na kukanyaga peku c ktendo kbaya wakati wote, Bali ni kuonesha mahali hapo ni patakatifu. Anza na Musa, uje Joshua njoo had agano jipya.

Exodus 3:5
Then He said, "Do not come near here;
remove your sandals from your feet, for
the place on which you are standing is
holy ground."


Joshua 5:15
The captain of the LORD'S host said to
Joshua, "Remove your sandals from your
feet, for the place where you are
standing is holy." And Joshua did so.

Acts 7:33
"BUT THE LORD SAID TO HIM, 'TAKE
OFF THE SANDALS FROM YOUR FEET,
FOR THE PLACE ON WHICH YOU ARE
STANDING IS HOLY GROUND.

Pia ktk manabii kama Isaya, Ezekiel nk rudi usome uone ni wapi ilikua laana. Afu utupe legitimacy ya T.B Joshua aliyesema Mugabe na mutharika watafark b4 1 April 2016 na leo ni may 19 hata homa hawana.
 
Mlilipwa kumshambulia JPM kipindi cha kampeni mkashindwa,mlivyo na akili fupi mnadhani mtafanikiwa na mtu ameshakuwa Raisi??,kweli akili zenu fupi sana,ndo maana Mzee Mkapa aliwaita WAPUMBAVU NA MALOFA.,ndo maana Mlikuwa mkizungusha mikono kama wendawazimu,nimeanza kuelewa.
 
Tanzania zaidi ya unavyoijua.
Niliandika mapema sana hapa wakati serikali hii ikiwa na miezi miwili tu kuwa utawala wa nchi za kiafrika umejengwa katika kumuangalia Rais anataka nini?
Hilo ni kosa namba moja, mawaziri wakaanza kufanya kazi kwa namna ambavyo rais anataka.
Hivi uzembe umeisha kwenye taasisi na idara za umma?
Kilichotokea uwanja wa ndege ni ushahidi/ishara tosha kuwa serikali haiwezi kututoa hapa tulipo kwa ziara za kushutukiza.
Kuna shida gani tukiwa na aina ya serikali na utawala ambao kila kiongozi anakuwa na majukumu ambayo yapo wazi?
Unaweza kuona issue ya machinjio tu pale Vingunguti wanakwenda mawaziri watatu.
Narudia kusema Mheshimiwa Rais Kama Ana nia ya dhati ya kuboresha hali ya maisha ya mtanzania lazima awe na serikali ambayo kila kiongozi/cheo linakuwa "defined" kwa majukumu yake.

Utashangaa mkanganyiko uliopo,
1. Mkuu wa mkoa anakuwa na kazi ya kukagua shule, afisa elimu anafanya nini?
2. Mkuu wa mkoa anajivika jukumu la kutafuta wafanyakazi hewa? Wakurugenzi na maafisa rasilimali watu, maafisa tawala wanafanya nini?

Ikifika siku tukawa na serikali ambayo kila mtu ana majukumu yake yanayoeleweka na akayatekeleza ipasavyo basi tutafika mbali.

Tusimwachie mzigo huu Rais peke yake hawezi kufanya ziara za kushtukiza kila mahali hata kama atatawala miaka 100.
Tuwajibike.

Heshima kwako mkuu. Hii ndiyo hoja yenyewe; hakuna cha kuongeza. Wanaosherehekea Magufuli kutengenezewa "personality cult" wajiandae kuhuzunika muda si mrefu. Kwa kifupi, hao ndio maadui zake wakuu wanaomharakisha kujiunga na safu za marais wengi hapa Afrika na dunia ya tatu wanaoaminishwa kuwa wao pekee ndiyo dola "L'etat? C'est moi!".

Hata Marekani walijaribu kumkuza George W. Bush kihivyo (asiyekuwa nasi yuko dhidi yetu). Hadi leo wanajutia kwa sauti na kimyakimya adha alizowaletea kwa kadhia zisizo na mantiki alizoasisi huko Iraq, Libya, n.k. Wakati ule ukikosoa maamuzi yake (na ya gwiji Dick Cheney) ulikuwa ukibandikwa nembo ya adui wa taifa la Marekani.
 
Mlilipwa kumshambulia JPM kipindi cha kampeni mkashindwa,mlivyo na akili fupi mnadhani mtafanikiwa na mtu ameshakuwa Raisi??,kweli akili zenu fupi sana,ndo maana Mzee Mkapa aliwaita WAPUMBAVU NA MALOFA.,ndo maana Mlikuwa mkizungusha mikono kama wendawazimu,nimeanza kuelewa.
Duh! Kweli wewe ni Great Thinker!
 
wengi wanaokosoa wameguswa kimaslahi, Imagine wafanyakaz wengi walioharibiwa dili zao za kupiga hela, wengi ni wasomi haswaaa, wanajua kucheza na kalamu na wanajua kuongea haswa, wana wafuasi waliokula nao bata, zaidi ya yote wanasikilizwa balaa.
Uje wafanyabiashara nap wameguswa haswaa, biashara yao imeyumba sababu walizoea mkato, hawajazoea kufuata taratibu, wamejaribu mbinu nyingi lakini mkono wa serikali umeonekaumeonekana kuwafikia.
Tunalalamika Mizigo imeshuka bandalini but nani amefuatilia jinsi mizigo ilivyoshuka Kenya Mombasa? Na hali itakuwa mbaya coz juzi waziri wa biashara Rwanda kafunga mjadala na kuwa mizigo yao itapita zaid Far ports
wananchi wengi tulikuwa tunalia lia Matajir wakikwepa kodi, sisi wenyewe hatujazoeshwa lipa kodi, hatutaki kulipa kodi sababu hatuoni hela zetu zinavyoenda tumika kutusaidia.
Tutajifunza na kuelewa halitakuwa tatizo tena na wale wenzetu watakao pita njia za mkato tutawaona ni wabaya na wahujumu uchumi.
ni swala la muda tu kila kitu kitarudi kwenye mstali, Trust Magufuli
 
Back
Top Bottom