Magdalena Sakaya, Prof. Lipumba atakupoteza

Magdalena Sakaya, Prof. Lipumba atakupoteza

mwembemdogo

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2016
Posts
2,282
Reaction score
1,253
Namshauri dada yangu Magdalena Sakaya akae mbali na Prof. Lipumba kwani yatakayomkuta atayajutia.

Nimemshangaa Magdalena Sakaya anadiriki kusema eti leo ndio wanataka watafakari uchaguzi mkuu ulivyokuwa.

Muda wote walikuwa wapi? Kwanza Prof. Lipumba alitangaza eti kamfukuza kazi Maalim Seif sasa iweje leo anadai wanamsubiri Maalim Seif?
 
Mgogoro wa CUF unazidi kutanuka, busara itumike kwa pande zote kwa maslahi ya Chama ili dhoruba mbaya ipite.
 
Sakaya ni mwanamke mwenye msimamo na anasimamia kile anachokiamini kuwa ni sahihi
 
Cuf watakubakiana tu, gharama ya kugombana na lipumba ni kubwa sana, kuna watu wanaweza kupoteza kazi
 
Lipumba kashapoteza credibility zote za uongozi. Hana future tena CUF, atajitutumua sasahiv ila maji yatapoa tu na atakubali yaishe
 
Yule mmama nilimhurumia kabisa. Muongo mwangalie atoavyo mimacho, utadhani katafuna kamongo mkavu. Dah! Sijui, siku ya siku Lipumba akimwaga vumbi Magdalena utakwenda wapi??
Lipumba ana ofisi Kigali, weye mama, utaenda wapi??
 
Sakaya ni mwanamke mwenye msimamo na anasimamia kile anachokiamini kuwa ni sahihi
safi sana mkuu,ni kweli,Magdalena anajua anachokifanya.

Tatizo mleta uzi na colabo lake hawajamuelewa Magdalena wala Lipumba.
Hayo ni maamuzi Binafsi,kwani EDO alipohama nani alimpoteza,si aliondoka na watu wake?wakapotea wote
 
CUF walipotea zamani sana,na waliingia mtego wa choo sicho
Kutoka ni issue.
Sasa wanamtafuta mchawi ni nani,yaani wamekuwa kama watoto vile
Sasa anaemuona mwenzie ana makosa aende mahakamani,hahaha
Kila mtu anaogopa kwenda,maana kila mmoja amechemka kwa upande wake.
 
Watu wamepiga mpunga,tehetehetehe
Chezea Siasa weweeeeeeee
Magdalena kastukia mchezo,walimziba mdomo kaona atibue sasa
Na alisema bado hajapewa barua mpaka,leo na wakimpa anatibu,jamaa wakaona wausweke
 
Sakaya ni mtu mzima anaweza kujiamulia, anazijua sheria na anajua anacho kifanya kita mkost vipi, huwezo sema kirahisi anapotea tuu.
sasa sie tukae tujionee movie hii inaishia wapi
 
Yamkute yepi tena na keshafukuzwa cuf jengo wamesharudisha washapata jengine wao wache wabakie humo
 
Kuna mtoa mada huu nadhani no wale buku 7 wa Lumumba eti anauliza lini Maalim Seif na kina Ntatiro watahamia CHADEMA.

Nimeona nimjibu ili atuambie kwanza ni lini Process wao Lipumba na mbunge Sakaya watajiunga na CCM chama wanachokifanyia kazi?
 
Huyu mwanamama mwanasiasa machachari sikutegemea kama angepumbazwa na Lipumba. Najiuliza kampa nini? Ni miongoni mwa viongozi na wabunge wa CUF niliokuwa nawaamini sana. Baada ya Lipumba kujiuzulu kashikamana na chama na hatimaye kuukwaa ubunge kwa tiketi ya CUF na backup kubwa ya UKAWA.

Ni miongoni mwa akina mama niliowaona shupavu na wenye kutetea hoja.
Sasa simuelewi, mbona hakumuunga mkono wakati anajiuzuru tukamuelewa?

Sakaya mama sikuelewi hata kidogo.
 
bilisi alimuingia lakin nina uhakika huyu mama hatakuwa sambamba tena la Lipumba naamini kimya chake huwenda watu wa jimboni kwake na familia yake watampa msimamo mzuri zaidi ili kulinda heshima yake ya upinzani bungeni.
 
Back
Top Bottom