Daimler
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 556
- 973
Katibu Mkuu wa CUF -Lipumba, Magdalena Sakaya, akiongea na Mwananchi amemshauri Maalim Seif kuachana na mpango wake wa kuhamia CHADEMA na badala yake atulie kulinda heshima yake. Alisema ingawa ni hiari ya mtu, itakuwa jambo la ajabu kama Maalim atahamia CHADEMA kisha kugombea Urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020. "Akienda CHADEMA hawezi kushinda nafasi hiyo .... kwa sababu Chama hiki hakina nguvu Zanzibar."
Sakaya aliongezea kuwa, "Mimi kama mwanaye na yeye ni baba, ninamshauri atulie tu ili ajenge heshima yake kwa sababu alishawahi kuwa kiongozi mkubwa katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar."