Na wewe uko kwenye mradi wa kumsafisha nani? Isije ikawa kuna habari ikiandikwa tofauti na mtizamo wa kambi yako halafu unasema yamenunuliwa? Je kama yangekuwa yanaandika unavyotaka wewe na kambi yako ungetaka sisi watanzania tuaminije?
Ushauri kwako: Siyo wote wenye mtizamo hasi ktk hayo magazeti kama unavyotaka wewe na hao waliokutuma. Na kwa taarifa yako; hayo ndiyo magazeti yanayonunuliwa na watanzania kuliko hayo mengine unayofikiri yanaandika tofauti na unavyotaka wewe.
Halafu lazima ujue kwamba hatuwezi kufikiria sawa unavyotaka wewe!
Magazeti kipenzi ya wana Chadema, Mwanahalisi, na Tanzania Daima, yote kwisha habari yake!
Ifuatayo ni orodha ya magazeti ya Tanzania ambayo wamiliki wake au wahariri wake au wote wamiliki na wahariri wamekuwa wakitumika kumsafisha Edward Lowassa katika mradi wake wa kutaka kwenda Ikulu 2015 kwa gharama yoyote ile. Magazeti haya yalitumiwa sana kupotosha umma kuhusu matokeo ya vikao vya NEC na Kamati Kuu ya CCM Dodoma juzi na kutoa habari na picha za kumpamba Lowassa kila mara akitumia viongozi wa dini njaa kujisafisha:
1. Mtanzania na RAI
Ingawaje hayasomwi tena na Watanzania makini, magazeti haya yanamilikiwa na Rostam Aziz, kingmaker wa viongozi mafisadi Tanzania na chief financier wa Lowassa.
2. MwanaHalisi
Gazeti linalomilikiwa na Saeed Kubenea ambaye sasa amefika bei kwa mafisadi na anawatumikia kama kibarua wao kuwasafisha na kuwatukana maadui wao, hususan Waziri Samuel Sitta.
4. Tanzania Daima
Gazeti linalomilikiwa na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe ambalo mhariri wake mkuu, Absalam Kibanda, yuko kwenye payroll ya Lowassa na Rostam kwa miaka mingi sana
5. Jamhuri (soon-to-be launched)
Gazeti la Lowassa ambalo litazinduka hivi karibuni, wahariri wake wakiwa ni vijana wa Lowassa wa siku nyingi -- Deodatus Balile na Manyerere Jackton -- ambao amewaazima kutoka kwenye magazeti ya rafiki yake Rostam. Hii ni baada ya jarida la Lowassa la Umoja linaloendeshwa na Absalom Kibanda wa Tanzania Daima kufeli na mpaka kufikia hatua ya kushindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi wake.
6. Mwananchi
Kuna "mdudu" ameingia hivi karibuni kwenye gazeti pendwa la kila siku la Tanzania ambalo na gazeti hili nalo sasa linatumiwa kwenye mradi wa kumsafisha Lowassa. Hii ilijidhihirisha kwenye mkutanon wa juzi wa NEC ambapo habari kuu iliyotoka kwenye kikao cha NEC iliandikwa na mtu mmoja na kuchapishwa kwenye magazeti matatu -- Mwananchi, Tanzania Daima na Mtanzania -- neno kwa neno.
7. Daily News
Kaimu Mhariri Mkuu wa Daily News, Mkumbwa Ally, amejisalimisha kambi ya Lowassa ili athibitishwe na kupewa cheo kama Mhariri Mkuu wa magazeti ya serikali, TSN. Wakati huo huo, gazeti la Habari Leo lililo chini ya TSN limekuwa likipambana kuleta habari za ukweli kuhusu mafisadi. Hii imesababisha habari za Daily News na Habari Leo kuhusu kujivua gamba kutofautiana kabisa wakati yote ni magazeti ya serikali chini ya kampuni moja.
- Mpaka hivi sasa, genge la kina Lowassa limejaribu na kushindwa kufanikiwa kwenye kila jitihada za kuyaingia au kuyamaliza kabisa magazeti mawili pekee yaliyosimama kidete kuueleza umma wa Tanzania ukweli. Nayo ni RAIA MWEMA na DIRA.
Kuna habari nyingi za aibu katika magazeti yote lakini hizo zisiyaponze magazeti kama taasisi. Magazeti yte yaliyotajwa tutakua hatuyatendei haki kwa kusema yamenunuliwa maana haiwezekani. Pengine mtoa mada angejadili habari husika kwa kila gazeti. Nakubaliana na hoja kwamba kwa sasa mafisadi wana nguvu kubwa sana, si ktk media tu, utakuta hata katika dola na ktk asasi nyingine hata za kidini. Inatisha sana, lakini ndio ukweli hata mahakama wamezishika na hii ni kwamba wameibaka serikali yote na mihimili mingine.. Mahakama na Bunge na mhimili wa nne nao kwishnehi... Tusilaumu magazeti, maana hata mtoa mada kesho anaweza kwenda kuendesha moja ya magazeti husika. Kuhusu MwanaHalisi, mafisadi hawaliamini maana huwa halitabiriki. Lolote linaweza kutokea... Japo hiyo dhana lazima iwepo, hasa baada ya hoja ya kuvua gamba ianze!!!
Magazeti kipenzi ya wana Chadema, Mwanahalisi, na Tanzania Daima, yote kwisha habari yake!
Hiyo mizungu yake labda akaichezee tlp,wenzake wanataka kumvua gamba kwa sababu za "kiintelijensia"EL kwa sasa ana 'mizungu' yote,'dume','jike',na 'ng'anda' sita!!! Wengi waliobaki huko CCM wana 'magalasha'!
Ifuatayo ni orodha ya magazeti ya Tanzania ambayo wamiliki wake au wahariri wake au wote wamiliki na wahariri wamekuwa wakitumika kumsafisha Edward Lowassa katika mradi wake wa kutaka kwenda Ikulu 2015 kwa gharama yoyote ile. Magazeti haya yalitumiwa sana kupotosha umma kuhusu matokeo ya vikao vya NEC na Kamati Kuu ya CCM Dodoma juzi na kutoa habari na picha za kumpamba Lowassa kila mara akitumia viongozi wa dini njaa kujisafisha
Uko sahihi, anacheza kamari kama ulivyosema ana mizungu yote, lakini karata zao na CCM yao ni mauti yetu!!EL kwa sasa ana 'mizungu' yote,'dume','jike',na 'ng'anda' sita!!! Wengi waliobaki huko CCM wana 'magalasha'!
Naungana mkono na unayempinga. Pamoja na kuwapo uchafu katika media, bado magazeti tajwa kama taasisi ni safi (kisera) maana tatizo la rushwa ni janga la kitaifa ambalo hakuna sekta iliyo salama, na sasa hata asasi nyeti kama vyombo vya dola zimeingiliwa na mdudu rushwa. Magazeti tajwa yana mchango mkubwa katika vita ya ufisadi, tusiyahukumu Kiujumla, tuhukumu habari husika, tuhukumu waandishi binafsi (kwa hoja) tusiwakatishe tamaa waandishi wasafi wanaofanya kazi katika vyombo husika maana wapo na wana mchango mkubwa. Tuendelee kujadili ufisadi wa Lowassa na wengine, tujadili walipoishia mitume 12 wa vita ya ufisadi, kimewapata nini? Mjadala uwe mpana zaidi!!Jaribu vyovyote upendavyo ku-justify uovu huu, lakini ukweli unabaki kwamba magazeti haya yamekuwa ni disgrace kwa umma sasa hivi. Hatua hii inayatafuna magazeti yenyewe na wamiliki wao ambao wanachekelea hali hii na huku mauzo mtaani yakiwa yanapungua na kuyageuza magazeti haya kuwa vijarida vya udaku. The good news ni kwamba bado yako magazeti ambayo yamesimama imara na kusimamia maadili ya uandishi na kupambana na maovu, katikati ya temptations za vipande thelathini vya fedha.
sio jamii forum kuna watu wametumwa humu nadhani ahata hele ya internet cafe wanalipiwa,hao kazi yao ni moja tu kuanzisha thread za kumfagilia lowassa na kuchangia wenyewe kwa majina tofautiti lakini watu ni walewale,lowassa anaigopa sana jamii forum kwa sababu hajui amuone nani ili aishike masikio jamii forum sasa ndio akaja na sttrategy hiyo ya kutafuta wasio na kazi mjini na kuwatuma kuja kushinda humu siku nzima kuanzisha thread zao na kudandia kwa fujo positively thread yeyote inayomuhusu lowassa ili kuuonyesha ummma kwamba lowassa anakubalika kila sehemu mpaka jf,sisi kwishagundua siku nyingi hiyo kitu,haitamsaidia!'gazeti' jingine linalomsafisha lowasa ni "jamiiforums" - the home of ....
Lowasa agundua chanzo kingine cha umeme
http://majira.co.tz/kurasa.php?soma=...bariNamba=1307. Abaini maporomoko yenye uwezo wa kuzalisha megawati 222
. Ashangaa TANESCO kukalia taarifa za utafiti uliofanyika
. Aahidi kumwagiza Waziri, Wataalamu wa Wizara kufuatilia
Na Magnus Mahenge, Makete
WAZIRI Mkuu, Bw. Edward Lowassa ameshangazwa na kile kilichoelezwa kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO ) kukalia taarifa za utafiti za utafiti wa maporomoko ya mto Luvanyina, ulioko Makete, mkoani Iringa ambayo yanaweza kuzalisha megawati 222 na kusaidia tatizo la mgowo wa umeme unaoendelea nchini
Taarifa iliyosomwa juzi kwenye maporomoko hayo yaliyopo
Madihani na Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Lepy Gembe ilieleza kuwa kama TANESCO ingetumia utafiti huo na kujenga mtambo wa kuzalisha umeme kwenye maporomoko hayo Taifa lingeondokana na tatizo sugu la mgawo wa umeme ambao umekuwa kero kubwa kwa wananchi.
Ilielezwa kwamba umeme huo ungezidi kiwango cha ule unaozalishwa Mtera ambao katika hali ya kawaida ni megawati 80 na sasa zimefikia megawati 30 tu .
Akiwahutubia wananchi wa Bulongwa, Bw. Lowassa alisema atamwagiza Waziri wa Nishati na Madini na watalaamu wake kwenda kwenye mto Luvanyina kuhakiki uwezo wa maporomoko hayo haraka, yaliyo kwenye mwinuko wa mita 3,000 kutoka usawa wa bahari.
Bw. Lowassa alitoa kauli hiyo baada ya wananchi wa Makete
kuiomba Serikali itupie macho maporomoko hayo, kwa lengo la kupata chanzo kingine kitakachosaidia kuapatikana ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la umeme.
Waziri Mkuu, alishangaa kusikia kwamba pamoja na TANESCO kufanya utafiti miaka mingi iliyopita na kuthibitisha uwezo wa maporomoko hayo kuzalisha umeme , hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kuandaa miundo mbinu ya upatikanaji wa nishati hiyo.
Mbali na utatifiti huo, Bw. Lowassa alishangaa kusikia kuwa miaka miwili iliyopita, Kampuni iitwayo Sudpower kutoka Swedeni kwa kushirikiana na nyingine kutoka Afrika Kusini, zilifanya utafiti mwingine na kubaini uwezo wa mto huo kuzalisha umeme lakini hakuna kilichofanyika.
Ilielezwa kuwa kutokana na sababu ambazo hazieleweki hadi sasa , iliamuliwa mtambo huo ujengwe bwawa la Kihansi lenye uwezo wa kuzalisha megawati kati ya 80 na 100, badala mto Luvanyina wenye uwezo wa kuzalisha mara mbili zaidi yake.
Utafiti mwingine kwenye maporomoko hayo ulifanywa mwaka 1992 na Idara ya Maji kwa lengo la kujua uwezo wa mto huo kuongezeka na kupungua wakati wa kiangazi na ikabaini kuwa una nguvu za kutosha kusukuma maji hayo misimu yote.
"Maji yanayotoka wilayani Makete asilimia 90 yanaingia katika Ziwa Nyasa, na mito mingi ukiwemo Luvanyina, haikauki, imejaa wakati wote na inafaa kwa kuzalisha umeme lakini hadi sasa haitumiki.." alisema Bw. Gembe.
Alieleza kuwa mwaka huo Kanisa na Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) , Dayosisi ya Kusini Kati, Bulongwa Makete, baada ya kupata wafadhili kutoka Swideni, lilijenga mashine ya umeme na miaka miwili baadaye, umeme ulianza kutumika.
Umeme unaozalishwa na kanisa hilo, unatumika katika hospitali ya Bulongwa na Shule ya sekondari ya Bulongwa zinazomilikiwa na kanisa hilo na maeneo ya vijiji jirani kwenye mashine za kusaga ,ambazo zinatumia asilimia tano tu ya umeme huo.
Ilielezwa kuwa kama umeme wa maporomoko hayo ungetumika, ungeongeza kiwango cha mahitaji ya taifa ya megawati 500, ambapo kwa sasa megawati 200 zinazalishwa na Songas, 100 na IPTL .
Bw. Lowassa amekuwa akifanya juhudi kubwa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la umeme hapa nchi. Hivi karibuni alipokuwa ziarani Asia, aliwasilisha ombi lake kwa Taasisi ya Kifalme ya Thailand, kuangalia uwezekano wa kupatiwa teknolojia ya kutengeneza mvua , kwa lengo la kujaza kina cha bwawa la Mtera ambalo ni chanzo kikuu cha kuzalisha umeme.
Mengi ya magazeti uliyoyataja ni magazeti makini na ambayo habari zake zote zinashirikisha pande zote zinazohusika ukiondoa Habarileo na Daily News ambayo kama sio ruzuku ya kodi zetu yangelikua yameisha kufa zamani.
Unapashwa kuelewa kuwa habari hazizuki kama unavyofikiri. Habari ni reflection ya nayotokea katika jamii ikiwemo chama tawala CCM. Nani asie fahamu ya kua CCM kunamakundi, nani asie fahamu ya kua CCM mambo ovyo ovyo, nani asiefahamu ya kua ndani ya CCM vurugu tupu nani asiefahamu ya kua kama mafisadi ndani ya CCM na serikali ni karibu ya asilimia 99 akiwemo rais mwenyewe?.
Magazeti yaliyo makini yanaandika haya na kufuatilia nani asiefahamu ya kua siasa na sera ya CCM ni kusafishana. Kama kweli zoezi la kujivua gamba lingetekelezwa kama kweli walikua na nia thabiti kwa kuwachukulia hatua wahusika wote mara moja bila kujali nafasi zao serikali na CCM tusingekua na ngojera zinazoendelea, siku tisini, wajipime wenyewe, mkutano mkuu, NEC,CC n.k. CCM msitafute Mchawi tatizo na chimbuko la matatizo liko ndani ya CCM KUCHAFUANA NA KUSAFISHANA NI SERA YA CCM.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.