Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
akili ya kuambiwa changanya na yako,fanya maamuzi.....
Akisafishwa utakufa? Unafaidi nini akiwa mchafu?
Duh, mbona hasira hivyo kaka? Ni dalili ya kupakatwa na mafisadi hayo, sasa ukiona mtu anampiga vita anayekupakata lazima uwe mbogo. Natamani Mwalimu Nyerere angekuwa hai na kuona jinsi mafisadi walivyoshika hatamu.. Tanzania ni nchi yangu, naipenda Tanzania!
Sasa kama anasafishwa na wewe hutaki asafishwe si mchafue. Sasa unataka nani amchafue.
Waulize Barare Limited ni ya nani? Ni ya Lowassa na Regina Mumba Lowassa kama ilivyo ANBEM... More to come
wanajf mwenye ushaidi kuwa lowasa ni fisadi atujuze,kwani tnaweza hukumiwa bila sababu,tmechoka na tetesi jaman u thinkers,juzi nec ddma kaeleza wazi khsu richmond,ni upi ufisadi wake mwingine????
wanajf mwenye ushaidi kuwa lowasa ni fisadi atujuze,kwani tnaweza hukumiwa bila sababu,tmechoka na tetesi jaman u thinkers,juzi nec ddma kaeleza wazi khsu richmond,ni upi ufisadi wake mwingine????
Jamhuri halijaanza kutoka unathibitishaje? Kama unahiyo Pay roll ya wanaolipwa na Lowassa scan weka wazi kama huwezi kaa kimya.
Mchafu ni mchafu tu na atabaki mchafu. Lowassa ni mchafu wa maadili, hata Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alijua hilo na alituonya tuepukane na huyu mtu. Ni kama nguruwe amezoea kuchea kwenye matope, hata umuogeshe vipi halisi yake ni kuchafuka tu na ataendelea kuwa mchafu tu come what may.
Unatushauri tusome uhuru sio!
na wewe unamsafisha nani? wewe kwa nafasi yako na uelewa wangu kamwe HUWEZI kuniambia nini cha kufanya hata kama nitakuwa mbali na kambi yako. Na kwa taarifa yako sina kambi isipokuwa ninachokataa ni kutaka kutuaminisha jinsi wewe na kambi yako, hasa wanaokutuma kutaka kutufanya tuamini ktk mawazo yenu yenye chuki kwenye biashara zenu.
Unapoongelea kikao cha NEC kwenye Mtanzania, kwani Viongozi wa CCM wamesemaje? -"SIRI ZA VIKAO VYA NEC ZIMEVUJA", sasa nini kosa la magazeti hayo? tuache ushabiki usiokuwa na mwelekeo chanya kwa nchi yetu na badala yake tuelekeze nguvu zetu ktk kukemea maovu ambayo kwa mwelekeo wako, katu huwezi kuyakemea.
Ufisadi wa Lowassa huu hapa:
1. Kununua jumba la kifahari London, Uingereza, lenye thamani ya zaidi shilingi bilioni 1 za Tanzania.
Metropolitan police wa Uingereza wanachunguza suala hili. Wamewasiliana na anti-money laundering unit ya Tanzania kuchunguza suala hili.
2. Ufisadi wa Nyumba ya Sanaa
Lowassa amehisika kufanya uporaji wa ardhi ya Nyumba ya Sanaa iliyopo karibu na Movenpik Hotel (zamani Serena Hotel). Nyaraka zinaonesha yeye ni mmiliki wa kampuni inayojenga gorofa kubwa kwenye eneo hilo la Nyumba ya Sanaa.
3. Utajiri usioelezeka (unexplained wealth)
Akiwa kama kiongozi wa umma, Lowassa amejilimbikizia mali nyingi sana za thamani ya mabilioni ya shilingi. Mali alizo nazo haziendani na kipato chake kama kiongozi wa umma. Sheria ya kupambana na rushwa Tanzania iko wazi kuwa kiongozi wowote wa umma mwenye utajiri usioendana na mapato yake halali anastahili kufikishwa mahakamani. Kutokana na sera za kulindana na kuogopana, Lowassa, Andrew Chenge, na viongozi wengine wa umma hawajafikishwa mahakamani kwa kosa hili na PCCB. Pia kwenye fomu za kila mwaka za kutaja mali, Lowassa haja declare assets zake zote. Ana miliki Alphatel, Alpha Schools, Alpha House, apartment blocks Dar es Salaam, Arusha na nje ya nchi.
4. Land grabbing
Alipokuwa Waziri wa Ardhi enzi za utawala wa Mwinyi alihusika na uporaji mkubwa wa ardhi sehemu mbali mbali nchini.
5. Richmond
Lowassa ndiye aliyeagiza TANESCO waporwe madaraka ya kusimamia tenda ya umeme kinyume na sheria ya manunuzi, PPRA. Aliunda kamati ya makatibu wakuu na kusimamia kwa karibu majadiliano ya kamati hii na nRichmond na kuagiza wapewe tenda wakati Tanesco waliikataa Richmond kuwa haifai. Lowassa ndiye mhusika mkuu wa kashfa ya ufisadi ya Richmond ndio maana alilazimika kujiuzulu.
6. Need I say more?
Lowassa ni mchafu wa maadili. Anapenda sana mali, amejilimbikizia utajiri kuliko kipato chake halisi. Wafuasi wake wanamfanananisha na Jacob Zuma wa Afrika Kusini. Tofauti ya Zuma na Lowassa ni kuwa Zuma alifikishwa mahakamani na kusafishwa na mahakama. Lowassa apelekwe kortini kujibu shutuma za ufisadi, akishinda kesi ndio atakuwa amesafishwa kweli. Si kwa kutumia vyombo vya habari na waandishi wa habari wenye njaa.
tengeneza thread humu jf na andika kichwa cha habari MBALI NA RICHMOND HUU HAPA UFISADI WA LOWASA,ili umma ujue