Mafuriko yakatisha mawasiliano Barabara ya Morogoro – Dodoma, Waziri Bashungwa atoa maelekezo kwa TANROADS

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991

014981c2-15f7-40a8-a4c9-52729c28cff8.jpeg
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Eng. Mohamed Besta kufanya tathmini ya eneo la Mtanana katika barabara kuu ya Morogoro – Dodoma ambalo leo Januari 9, 2024 lilijaa maji na kusababisha barabara hiyo kufungwa majira ya asubuhi.

Pia ameagiza kuwasilishwa kwa mkakati wa kudumu wa kudhibiti eneo hilo na maeneo yote korofi nchini ambayo hupata changamoto pindi mvua zinaponyesha.
ed5a6514-e0d0-43da-a3f3-8c874f0149f7.jpeg

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa
“Mawasiliano ya barabara yamekuwa yakifungwa kutokana na maji kuvuka eneo la Mtanana, hivyo lazima tutafute suluhu ya kudumu ili barabara ipitike vipindi vyote vya mwaka,” amesisitiza Bashungwa.

Aidha, Bashungwa amewaelekeza Mameneja wa TANROADS mikoa yote nchini kuhakikisha wanaendelea kukagua maeneo yote ya barabara na madaraja na kuchukua hatua za haraka kutokana na hitilafu zozote zinazoweza kusababisha kufunga kwa mawasiliano ya barabara.

Hata Hivyo, Bashungwa amewapongeza Mameneja hao kwa kazi nzuri wanazoendelea kufanya na kuchukua hatua za haraka pindi changamoto inapotokea.
c90ecaad-cb27-4693-a47f-0cc3ecc14b8c.jpeg

0332124a-71ab-44c4-bf9b-e1ec03ef591d.jpeg

e2a3abe8-667e-4eb7-83ba-9b82ce44f63d.jpeg
 
Anatoa pongezi kwa mameneja kuchukua changamoto tatizo linapotokea..kwahyo hilo tatizo halitatuliki ni endelevu??it means ni kawaida yao kuchukua hatua tuu wkt wakati wa tatizo na sio kutatua tatizo kabisa..mhhh hii nchi siasa itatuua...
 
bado wanazima umeme wakisema ni ukame, evil exists and its real …
 
Hilo eneo la mtanana-kibaigwa ni hatari mno hususani kipindi cha mvua nyingi kama za mwaka huu... Mwaka juzi almanusura tufie hapo,changamoto kubwa ya hapo maji husambaa eneo kubwa na hutiririka kwa kasi kwenda upande wa pili wa barabara.

Mbaya zaidi barabara inakaribia level moja na mashamba yanayopakana na barabara hivyo kuleta ugumu wa kujenga madaraja makubwa yatakayopitisha maji mengi kwa haraka.

Tukumbuke njia hii ni muhimu sana katika sector ya usafirishaji mikwamo ya aina hii inaleta usumbufu mwingi kwa wadau wa usafilishaji na wasafiri, natumai serikali itafumbua fumbo hili... Mara Zote serikali imekua sikivu kwa Wananchi wake.
 
bado wanazima umeme wakisema ni ukame, evil exists and its real …
Usiilaumu sirikali.

Juzi si wametoa taarifa kuna samaki amagata kwenye gati, anazuia maji kuingia.. sasa wafanyaje mtu a dive mpka huko chini?

Wanasubiri aoze, mambo mengine kwa uwezo wa binadamu hayawezekani.
 
Kama vipi wachimbe bwawa kubwa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji kama lile bwawa la Mindu, jirani na hilo eneo ili maji yaende huko.

Au waweke basi madaraja mengi ya kuruhusu maji kupita upande wa pili wa barabara kwa urahisi zaidi.
 
Hilo eneo la mtanana-kibaigwa ni hatari mno hususani kipindi cha mvua nyingi kama za mwaka huu... Mwaka juzi almanusura tufie hapo,changamoto kubwa ya hapo maji husambaa eneo kubwa na hutiririka kwa kasi kwenda upande wa pili wa barabara.

Mbaya zaidi barabara inakaribia level moja na mashamba yanayopakana na barabara hivyo kuleta ugumu wa kujenga madaraja makubwa yatakayopitisha maji mengi kwa haraka.

Tukumbuke njia hii ni muhimu sana katika sector ya usafirishaji mikwamo ya aina hii inaleta usumbufu mwingi kwa wadau wa usafilishaji na wasafiri, natumai serikali itafumbua fumbo hili... Mara Zote serikali imekua sikivu kwa Wananchi wake.
Serikali sikivu
 
Hilo eneo la mtanana-kibaigwa ni hatari mno hususani kipindi cha mvua nyingi kama za mwaka huu... Mwaka juzi almanusura tufie hapo,changamoto kubwa ya hapo maji husambaa eneo kubwa na hutiririka kwa kasi kwenda upande wa pili wa barabara.

Mbaya zaidi barabara inakaribia level moja na mashamba yanayopakana na barabara hivyo kuleta ugumu wa kujenga madaraja makubwa yatakayopitisha maji mengi kwa haraka.

Tukumbuke njia hii ni muhimu sana katika sector ya usafirishaji mikwamo ya aina hii inaleta usumbufu mwingi kwa wadau wa usafilishaji na wasafiri, natumai serikali itafumbua fumbo hili... Mara Zote serikali imekua sikivu kwa Wananchi wake.
Inatakiwa iwe sikivu kwa mvua pia, ijue mvua inataka nini.
 
Ukiacha tatizo namba 1 la uwezo mdogo wa usimamizi ambalo mamlaka za Tanzania linalo, tatizo namba 2 ambalo Watanzania na wenye mamlaka wanalo pia ni uwezo mdogo wa usanifu kwa kisingizio cha kupunguza gharama za matumizi...

Maeneo ya uwanda wa chini yaliyo katika njia au mikondo ya maji, usanifu wa barabara hizo ulikuwa ni kujenga barabara juu ya nguzo mithili ya daraja...

Kinachoisumbua Jangwani ya Dar es Salaam ni uwezo mdogo kwenye usanifu, hilo eneo tajwa ni hivyo hivyo pia, maeneo fulani ya Same hapo, na maeneo mengine...

Bahati mbaya sana huwa pia hatujifunzi kwa sababu mtu mwenye uwezo mdogo hana muda wala sababu za kujifunza, maeneo ya Bahi, Kilosa reli zoshawahi kusombwa na maji lakini hakuna mafunzo tuliyopata...
 
Bara bara ipo mtoni hiyo kila mwaka mtatoa tamko...wekeni daraja hapo tuache matamko kila kukicha kwa vitu vinavyowezekana...
 
Kama vipi wachimbe bwawa kubwa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji kama lile bwawa la Mindu, jirani na hilo eneo ili maji yaende huko.

Au waweke basi madaraja mengi ya kuruhusu maji kupita upande wa pili wa barabara kwa urahisi zaidi.
Ni kweli mkuu lakini hakuna anaefikiri vema kuhusu wazo lako jema. NI KAMA HATUNA WATAALAMU WA MABWAWA VILE
 
Back
Top Bottom