Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Pia ameagiza kuwasilishwa kwa mkakati wa kudumu wa kudhibiti eneo hilo na maeneo yote korofi nchini ambayo hupata changamoto pindi mvua zinaponyesha.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa
Aidha, Bashungwa amewaelekeza Mameneja wa TANROADS mikoa yote nchini kuhakikisha wanaendelea kukagua maeneo yote ya barabara na madaraja na kuchukua hatua za haraka kutokana na hitilafu zozote zinazoweza kusababisha kufunga kwa mawasiliano ya barabara.
Hata Hivyo, Bashungwa amewapongeza Mameneja hao kwa kazi nzuri wanazoendelea kufanya na kuchukua hatua za haraka pindi changamoto inapotokea.