Mafisadi + CCM ngao imara ya Freeman Mbowe

Status
Not open for further replies.
Mwafrika,

Mwafrika jaribu kusoma vizuri maandishi ya JokaKuu na utaona jinsi ambavyo amemhusisha Zitto kuhusika na hiko kikundi kilichoandika waraka huu. Hapo chini ni quote yake.



Ina maana ndani ya Chadema mtu yeyote atakayetoa tuhuma za ukabila ndani ya Chama basi anamuwakilisha Zitto au wanatoa hizo tuhuma kwa niaba yake?

Ni kweli GQ,

Lakini pia, alichoandika huyo siku ikifika hapa JF kwa muda sasa (Soma post zake), kina uhusiano na yaliyotokea kwenye kampeni ya Zitto ya kutaka uenyekiti wa CHADEMA.

Labda Jokakuu anampa Zitto nafasi ya kumkana sikuikifika hapa JF.
 
Asante sana Phillemon Mikael.

Umenena mambo ya maana.

Hata mke na mume wanakwaruzana ndani ila wakitoka nje wanacheka.
 
Sasa nimeamini kuwa wananchi tuna safari ndefu ya kufika kanani...

Juzi CCM walikuwa na mtafaruku mkubwa kuliko huu wa CHADEMA ....wakapigana kwenye kamati kuu wametoka ..angalau hawakuja hapa kuanikana...

Wapinzani sasa mmejeuza jamboforums kuwa kamati kuu ya CHADEMA????....KWANINI mambo yenu ya ndani yasiishie ndani....hamuoni kuwa kwa mara nyingine mnawakatisha tamaa wananchi!!????

Tangu mwaka 1992 tunapambana tumeona wapinzani wakiendelea kuumizwa kwa mambo kama haya ...NCCR ya mwaka 1989 ilikuwa moto na wasomi wote ....lakini kumbe lilikuwa gari la UT la kusanya wapinzani waliokuwa wakichomoza....walishindwa kuifanya NCCR KUWA CHAMA PEKEE...

KAMAHURU na baadaye CUF ...baada ya kuungana na JAMES MAPALALA....yuko wapi mapalala?????

MREMA ..aliyevuma kama tsunami ...yupo wapi????

CHADEMA ambacho mwanzo kilikuwa chama wachache makini kisicho kuwa na watu....wengi ,miaka yote nyuma kilikuwa hakioneshi cheche..tunashukuru vijana mliochukua madaraka baada ya wazee...MTEI NA BOB MAKANI....miaka hii mitano tumeona mnapanuka na kuwapa matumaini wananchi kwa kasi ya ajabu .....sasa kwanini mnafikia kuja kuvuana nguo hapa....mmekosa vikao...

kwanini CHADEMA mnataka kuwasaliti watanzania??/

ni CHAMA gani hakina siri za ndani??? haata ndoa ina siri....na siri ni siri..???...miliosoma vitabu vya siasa mnajuwa ...wanachowashinda CCM ndio hicho...?? watu wao wameapa kutunza siri...hata waulizeni waliokuwa humo..watawambia...

chukulia mfano wa mtu kama MREMA ..Pamoja na uropokaji wake ...mambo aliyoyajuwa kwa kiapo ambayo anajuwa akiongea itakuwa kinyume hajapata kuyasema..nasema hivyo kwa sababu kuna mengi tumepata kumuuliza..anazungusha...!..anajuwa maana ya siri na adhabu ya kutowa siri anaijuwa!

Tena wapinzani mjuwe ikiwa umeenda ccm unaweza kuongea porojo zote lakini ukisema siri ambayo imekuwa rated secret...simply they kill you!!! mifano mnayo...!!!...sitaki wapinzani mfikie huuko lakini lazima mjuwe hamtakiwi kukwaruzana na kuwayumbisha wananchi namna hii......

CCM waanajuwa kuwagombanisha .....na wanaofanikiwa huzawadiwa vyeo lakini tayari wanakuwa wameshajiaharibia historia na kubeba usaliti...

watu kama ....lamwai,hizza,akwilombe.,kaborou[aliyekuwa kipenzi cha wananchi]....leo hii wakitokea mbele ya wananchi hata wanaona haya ...ukiachilia mtu kama hizza ambaye anajulikana ni mpiga domo...hawa wasomi wengine...dhamira zinawasuta....na tayari wamekosa uhalali mbele ya macho ya watu!!

....tunaomba vita dhidi ya ufisadi isitumike vibaya kuyumbisha wananchi...narejea maneno ya POLYCAP CARDINAL PENGO.."wanaopingana na ufisadi lazima wajiulize wanapigana toka moyoni au wanapigana kwa kuwa tu na wao wamekosa fursa ya kuwa mafisadi....""

CHADEMA MSIKUBALI KUTUMIWA NA MAFISADI AU HATA HAO MAKAMANDA WA MAFISADI...KWANI WANANCHI WOTE WANAJUWA NYIE NDIO WAAZILISHI WA HII VITA....MBOWE .,SLAA,...ZITTO NA WABUNGE WOTE WA CHADEMA ....SASA IWEJE LEO MNAKUBALI KUWA UNDERDOGS......ITAKUWA NI FURAHA SANA KWA MKIFARAKANA KAMA HIZI...NAPATA PICHA WANAKUNYWA MVINYO SASA.......

MSITUPELEKE HUKO!!!
PM amini usiamini makada wa chama cha kijani wako hapa kazini kama kawaida yao na mimi ni mmoja wa wale wanaopuuzia ujinga wao.
Wajinga ndio watanaswa na mtego wao!
Hapa ni akili mkichwa. Kaa mbali na kanda mbili na kundi lake!
 
Alipopindisha na kutoa majina yaliyokuwa yameteuliwa ya Wabunge wa viti Maalum na kupeleka Wachaga watano kati ya nafasi sita na moja akampa demu wake toka Kigoma alikuwa ametumwa na nani?

alipochukua kurugenzi zote nyeti akawapa wachaga: Kurugenzi za fedha, utawala, Rasilimali, bunge na halmashauri alikuwa katumwa na nani?

alipolazimisha yeye na kujiweka signatory wa akaunti ya chama, na Ndugu yake Komu, John Mrema na Mweka Hazina Mchaga alikuwa katumwa na nani?

alipopeleka tenda za kutengeneza bendera china na kumpa mchaga zabuni, na hata pikipiki za chama zikaenda nunuliwa Kilimanjaro badala ya Dar alikuwa katumwa na nani?
Naomba kumuuliza huyu mjinga aliyeandika pumba hizi hivi hawa wachaga waliojaa kila idara za serikali, mashirika ya umma na hata TRA je wamewekwa na Mbowe pia?
Wacha nchi tuwape wachaga kuliko wakwere wezi!
 
PM amini usiamini makada wa chama cha kijani wako hapa kazini kama kawaida yao na mimi ni mmoja wa wale wanaopuuzia ujinga wao.
Wajinga ndio watanaswa na mtego wao!
Hapa ni akili mkichwa. Kaa mbali na kanda mbili na kundi lake!

MF,

Ni ukweli usiopingika kwamba watanzania wengi wanaopenda kuona ustawi wa demokrasia ya kweli nchini walitegemea sana chama kama CHADEMA kuwa mfano wa kuijenga demokrasia ya kweli.
Lakini tulichoshuhudia katika kipindi hiki cha vuguvugu la uchaguzi ndani ya chadema ni vituko juu ya vituko.
kwahiyo kuna watu wamesikitishwa kwa namna wazee wa chadema walivyotumia busara zao kumshinikiza Zitto ajitoe kugombea uenyekiti wa chama chake, ingawa pia kuna wale ambao wamefurahia uamuzi huo.

Kwahiyo sidhani kama wote wasiokubaliana na uamuzi wa wazee wa chadema watakuwa ni ccm, au wanatumiwa na mafisadi. Kuna wanachadema wazalendo tena kwa nia safi kabisa wamepingana na busara za wazee wa chadema na ambao walikuwa wanamuunga mkono zitto na bado wataendelea kumuunga mkono.

kwahiyo sio kila anyeonekana kuwa against na mbowe mnamshambulia kuwa ccm, fisadi na mambo mengine kama hayo ingawa pia ccm wanachekelea kuona chadema mnavyokorogana.

CCM kwa upande wao wanaendesha mchakato wa kura za maoni kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa, na wamechapana makonde sana huko lakini watu hawawafuatilii kama wanavyowafuatilia chadema, kuna sababu ya msingi watu kufuatilia uchaguzi wa chadema na si kufuatilia mambo ya nambari wani.

watu wangetegemea kuona demokrasia inashamiri ndani ya chadema na zaidi sana watu wanataka wajivunie kuwa na chama mbadala wa ccm na chadema kilionekana kuwa mbadala, sasa huu mtafaruku wa uchaguzi usiwafanye mkaanza kuvuana nguo, safari bado ni ndefu na ndio kwanza mnaanza kupiga hatua.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom