Sibonike
JF-Expert Member
- Dec 23, 2010
- 17,277
- 17,983
Naogopa wasije wakamdedisha
Short chasis Chiluba alimdedisha Levy Mwanawasa kule Zambia baada ya kuchenjia.
Naogopa wasije wakamdedisha
Tuko naye rais wetu make hii ni kwa faida yetu na vizazi vyetu
tutampima kwa matokeo kama vifaa vya kutosha mahospitalini, madawa ya kutosha, wafanyakazi wa kutosha hasa elimu na afya, vitendea kazi vya kutosha mashuleni, wanafunzi wenye sifa elimu ya juu wote wanapata mikopo, barabara nzuri, maji salama, umeme wa uhakika, uchumi wa mtu mmoja mmoja umekua n.k hatutampima kwa ziara maofisini
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Tovuti Rasmi ya Rais
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT?S OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli , leo mchana amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kukutana na hali ya kumsikitisha.
? Rais amesikitishwa na kuhuzunishwa na hali ya huduma kwa wagonjwa hususan wanaolala chini. Pia amekasirishwa na hali ya kutokujali wala kushughulikia vifaa vya kufanyia kazi ambapo amekuta mashine muhimu za uchunguzi wa magonjwa kama vile MRI na CT-SCAN zikiwa hazifanyi kazi kwa muda wa miezi miwili sasa, ilihali mashine kama hizo katika Hospitali za binafsi zinafanya kazi na wagonjwa wanaelekezwa kwenda kutafuta huduma huko?. Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema na kutoa maelekezo yafuatayo :
​Rais amevunja Bodi ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambayo ilishamaliza muda wake na amemteua Prof. Lawrence Mseru , kukaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Muhimbili kuanzia kesho tarehe 10 Novemba, 2015.
Dkt. Hussein L. Kidanto ambaye ndiye anayekaimu hivi sasa, amehamishiwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambako atapangiwa kazi nyingine.
Balozi Sefue pia amesema, Rais ametoa wiki moja na kwa vyovyote si zaidi ya wiki mbili kwa uongozi mpya wa Muhimbili kuhakikisha kuwa mashine zote za uchunguzi wa magonjwa ambazo hazifanyi kazi zinafanya kazi na kuhudumia wananchi kama ipasavyo.
Tayari Wizara ya Fedha imetoa shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kazi hiyo na kulipa madeni ya ukarabati wa mashine za uchunguzi wa magonjwa nchini.
Hata hivyo Katibu Mkuu Kiongozi amesema kuanzia sasa hospitali zote nchini zinatakiwa kutenga fedha kutoka kwenye mapato yao wenyewe na kuhakikisha mashine na vifaa vyote vya kazi vinafanya kazi wakati wote (Regular Maintenance).
Balozi Sefue pia metumia nafasi hii kuwaagiza watendaji na viongozi wote katika sehemu za kazi kuhakikisha wananchi wanahudumiwa ipasavyo na kazi za umma zinatekelezwa ipasavyo.
?Hakutakuwa na huruma kwa watumishi wa Umma wasiojali wananchi na mahitaji yao? Amesisitiza Balozi Sefue.
???Mwisho???
Imetolewa na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu ? Dar es Salaam.
9 Novemba, 2015
Kifuu cha uchawi Wa bibi yako!
Tatizo watu wanashabikia siasa kama wanvyoshabikia mpira. Mtu akishakua yanga basi ni yangu tu milele ndiowanavyofanya siasa, hawaangalii kazi na sera za wanasiasa.Jibu hili limekaa vizuri sana. Tatizo la hawa wanaojiita "wapinzani" wanafikiri maana ya upinzani ni kujitoa ufahamu.
Wewe mwenye dharau tuambie maendeleo yako binafsi na mkeo uliyoyafanya kwa wiki moja baada ya ndoa yako. Usiwe mjeuri bila ya sababu.
Usemacho ni kweli kabisa.Tatizo watu wanashabikia siasa kama wanvyoshabikia mpira. Mtu akishakua yanga basi ni yangu tu milele ndiowanavyofanya siasa, hawaangalii kazi na sera za wanasiasa.
Binafsi nilikua nimeichoka CCM lakini kwa kasi hii ya Mheshimiwa raisi inanipa matumaini. Tunamuomba mungu aje apate wasaidi na mawaziri wema wenye niya nzuri na nchi yetu.
Kikwete alianza kama JP.
Tusubiri matokeo tu.
Magufuli rais wetu inabidi awekewe ulinzi mkubwa na mkali. wako watu wamekaa mkao wa kutaka kuhujumu kila kitu..