Madiwani wengine wawili wa CHADEMA jiji la Arusha watimkia CCM

Madiwani wengine wawili wa CHADEMA jiji la Arusha watimkia CCM

Taratibu mpaka chaduma atafutika katika historia ya chama kikuu cha upinzani
 
Na si ajabu hujui kuwa hao viongozi ni sehemu ya hao wananchi. Hujui pia kuwa mwananchi wa kawaida anakuwa hajui mengi ya Chadema. Anapokuwa kiongozi ndio anaujua ukweli na uzandiki wa Chadema. Hapo ndio anabwaga manyanga. Hata wewe Tindo ukiwa kiongozi wa Chadema utakimbia tu, labda kama wewe ni MBOWE in pseudo name!!!

Wananchi wa Arusha sio viazi wana uelewa wa kutosha. Ni kweli cdm wanaweza kuwa na matatizo, lakini wananchi wa Arusha walio wengi hawaikubali ccm. Kwani sio automatically kuwa cdm ikiwa na matatizo basi ccm ikawa nzuri. Hao viongozi wameenda kuwinda mlo baada ya kugundua chaguzi ni za kishenzi na ccm ndio wanajitangaza washindi.
 
Mimi kila nikisikia kiongozi yoyote wa upinzani amehamia CCM, nasisitiza wasibezwe, wameona mbali.
P
Pascal si kweli kuwa wanaohamia CCM hivi sasa wanaona mbali, la hasha. Hawa Ni wabinafsi, wapenda vyeo na walio tayari kuisaidia CCM katika azma yake ya uroho wa madaraka. Kumbuka katika suala la madaraka ya dola CCM iko tayari si tu kuvunja Katiba ya nchi bali pia kuua wapinzani wake na Watanzania kwa ujumla!!!
 
Nashangaa sana CCM isivyo tumia hata chembe ya akili!
Unashangilia kumrubuni mbunge mmoja akiache chama chake ajiunge na chako kwa mbwembwe, lakini wakati huo huo unapoteza imani ya wanachama 1000 wapigakura na wanakuacha kimya kimya!
Sasa Polepole furaha yake in kuona vichwa vya magazeti vya kumfurahisha kumbe chama kwa ndani kinaoza.
Chadema ni imara sana kwa sasa, hata Waziri mkuu mstaafu wanaweza kumnyima kura tena na ndio/hapana?
Leteni ushahidi wa wanachama wa CCM wanaohama kimya kimya kwenda vyama vingine.

Viongozi ni vielelezo vya watu. Kila mwanasiasa ana watu wake wanaomuunga mkono, msidhani wanaohama wanaondoka wenyewe wana wafuasi wao wanaondoka nao.

Huyo Sumaye mnaojitapa mmemsulubu kwa kura za hapana, kila mtu anajua ni kwa maelekezo ya uongozi wa juu wa chama siyo kwa utashi wa wanachama.

Ukweli ni kwamba, mambo yanayoendelea ndani ya CDM hali siyo shwari. Watu wamechoka na viongozi wamechoka wameamua kuwaachia wenye chama chao. Huyu Sumaye nae alikua anatafuta EXIT door siku nyingi tu. Sasa kaipata.

Halikadhalika, Sumaye alishapoteza mvuto wa kisiasa tangu akiwa CCM ndo maana alikimbia. Huwezi kutoka nafasi ya uwaziri Mkuu halfu ukagombanie uenyekiti wa kanda hii ni ushahidi tosha kwamba alishakufa kisiasa.

Prof. Safari nae kaamua kubwaga manyanga, Tundu Lissu kagoma kurudi Tz kuja kuongeza nguvu kwenye chama chenu, mnadanganywa eti anaogopa wasiojulikana. Kumbe ameshawajua, wasiojulikana wamejulikana, ameamua kuangalia maisha yake. Wabunge, Madiwani, Mameya n.k wote wanakimbia bado hamshtuki tu kwamba kuna tatizo.

Jiulizeni pia kwanini siku hizi hatuoni viongozi wa vyama vingine wakihamia CDM kama ilivyokua zamani? Kila siku viongozi wa CDM ndiyo wanaohamia vyama vingine au kuamua kuachana kabisa na siasa. Hili nalo mnalizungumziaje?

Sasa nyinyi endeleeni kujifariji na kujidanganya kwamba chama chenu kipo imara wakati kila siku jahazi linazidi kuzama. kila siku mnakimbiwa na viongozi.Mwanzo mlisingizia wananunuliwa, sasa hivi mnawaita wanaondooka ni mamluki na wasaliti.

Sasa hivi Chadema haina msingi tena. Kuanzia Ngazi ya shina mpaka tawi. Viongozi wa mtaa hakuna tena. Sasa sijui watatumia miujiza gani kupata hata wabunge watano tu kwenye uchaguzi ujao.

Lowassa ameondoka na kura zake milioni sita. Nani mwingine atakaeweza kuzileta kura hizo ili chama kipate ruzuku ya kujiendesha. Au ndo tunawavizia kina membe na kuendelea kumbembeleza Tundu Lissu arejee nchini.

Tuwe na akiba ya maneno, tuweke ushabiki pembeni. Baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2020 ndo tutajua kama kweli Chadema ipo imara.
 
Huko cdm wanahama viongozi tu, wananchi wala hawako nao, ndio maana idadi ya kujiandikisha kupiga kura ilikuwa ndogo ajabu.
Kuna sababu lukuki za kutojiandikisha kubwa ikiwa mgombea hana mpinzani, ya nini kupoteza muda wako maana atashinda tu. Tunajiandikisha iwapo kuna ushindani
 
Kuna sababu lukuki za kutojiandikisha kubwa ikiwa mgombea hana mpinzani, ya nini kupoteza muda wako maana atashinda tu. Tunajiandikisha iwapo kuna ushindani

Sio kwa Arusha. Siasa za kishenzi za jiwe ndio sababu fullstop.
 
Ndio hao nimeona mdude chadem a akilalamikia huko twiter kuwa kaona sumae akiwa nao kwenye kikao cha siri ndio anawashawishi wahame ili waonekane eti walikuwa timu sumae?
Hii imetokea Leo tarehe 6/12/2019 hii ni Taa nyekundu kwa CHADEMA
 
Sio kwa Arusha. Siasa za kishenzi za jiwe ndio sababu fullstop.
Ni kosa kuwasemea watu, mawazo yako hayawezi kuwa ndiyo mawazo kwa jamii nzima. Achana na fikra potofu
 
Nashangaa sana CCM isivyo tumia hata chembe ya akili!
Unashangilia kumrubuni mbunge mmoja akiache chama chake ajiunge na chako kwa mbwembwe, lakini wakati huo huo unapoteza imani ya wanachama 1000 wapigakura na wanakuacha kimya kimya!
Sasa Polepole furaha yake in kuona vichwa vya magazeti vya kumfurahisha kumbe chama kwa ndani kinaoza.
Chadema ni imara sana kwa sasa, hata Waziri mkuu mstaafu wanaweza kumnyima kura tena na ndio/hapana?
😂😂😂😂😂 Sijaona watu wenye mioyo migumu Kama wewe...kwa spidi ya kuhama unaweza stukia hata Mbowe akahamia ccm ukabaki pekeyako. Viongozi wooote waandamizi wenu wanaondoka wanaenda kumuunga mkono Magufuli. Juzi tuu Prof Safari kawatoka..angalia usije Baki mwemyewe
 
Mimi kila nikisikia kiongozi yoyote wa upinzani amehamia CCM, nasisitiza wasibezwe, wameona mbali.
P
nampataje mzee Slow slow nataka kuchukua changu mapema
nisaidie
 
Co kuona mbal n kuangalia matumbo yao
Mimi kila nikisikia kiongozi yoyote wa upinzani amehamia CCM, nasisitiza wasibezwe, wameona mbali.
P
 
Wameshindwa ushawishi wa sera znatumika njia haramu
Mngekuwa mnawanunua na waliowapigia kura ningewaona mna akili sana, lakini mnanunua waliopigiwa kura wakati mnajua wenye maamuzi ya mwisho ni wananchi!, na huko Arusha nyie nunueni tu, si hamna kumbukukumbu kilichowapata mwaka ule mlionunua halafu kwenye uchaguzi mdogo hamkuamini kilichowapata, na safari hii hamtaamini tena.

Chama kinachojiita kikongwe barani Afrika kutwa kununua wapinzani wao, ajabu sana!, na msijitetee hamuwanunui, kwanini muwarudishe kugombea nafasi zao kwani ccm hamna watu wakugombea hizo nafasi?!
 
Huko cdm wanahama viongozi tu, wananchi wala hawako nao, ndio maana idadi ya kujiandikisha kupiga kura ilikuwa ndogo ajabu.
Nani kakwambia wananchi hawako nao, ndivyo mnavyojipooza eh. Subirini 2020, mje na kisingizio chenu cha kuibiwa kura.
 
Back
Top Bottom