Madiwani wa CHADEMA Arusha wagawanyika

Mkuu labda ungepitia tena kamusi ya kiswahili neno "mpuuzi' lina maana gani halafu ujitazame kati yako wewe na aliyetoa hoja nani mpuuzi.

PUUZI=SILLY=showing a lack of common sense or judgment;

Na hii aina TOFAUTI na wewe, naamini ni MMOJA wao amabye unaamini kuwa Barabara anajenga Diwani au Mbunge kwa kuhudhuria VIKAO.
Na mbaya zaidi utakuwa unaamini kuwa CCM wanaleta maendeleo ya nchi hii kwa kutumia hela zao kutoka CCM kwa hiyo bila muafaka na CCM au kuwapigia magoti CCM maendeleo HAKUNA .

Pole sana ila unajulikana jinsi ulivyo na chuki na ulivyokuwa tayari kUTETEA UPUUZI kwa kuwa tu unashabihiana na wewe .
 
Hapa ishu ya muhimu ni kuomba msamaha,unapokuwa mtoto ukakosewa na mkubwa na ukalazimisha akupigie magoti na kukuomba msamaha hata kama kakukosea wewe mtoto utakuwa na shari,madiwani kushindana na uongozi wa juu wa chama ni kwa faida ya nani?je hii si ndo kama mfano wa mtoto nilioutoa hapo juu?

Kwa faida ya chama unatakiwa kuomba msamaha,hata kama utakuwa umekosewa hii baadae inaweza kuonyesha busara zako kwamba mbele ya chama masrahi ya chama yanatangulia kwanza siyo misimamo yako,ili mwishowe iweje?ili uonekane super dhidi ya chama?na hivi wakati hiki chama kimeanza huyu diwani alitegemewa ili awe nabii kwenye chama?wewe wa chini kushindana na juu kimaamuzi ni nini?

Hapo juu 'Ngonini' umenene vyema,hatuhitaji vilaza wa hivi chadema...ktk somo la Organization Management kuna 14 scientific management principles,m1wapo inasema hivi ,subordination of Individual interests over organization interests,nadhani hawa madiwani waelewe ya kuwa chama kiko juu yao na kama wanataka kuwa juu ya CDM basi hawatufai kukaa CDM,waondoke waende kwingine
 
ben
Kwanza nikupongeze kwa uwazi lakini nitofautiane na wewe kujaribu kuonyesha kuunga mkono utovu wa kimaadili unaofanywa na madiwani .
Hata kama wanahoja ya kupinga hawakupaswa kupinga hadharani maamuzi ya kamati kuu ya chama huku wakitishia kumshtaki katibu mkuu tena walimpa muda kabla ya jana awe ameitisha mkutano na kuwaomba radhi mbele ya wananchi lasivyo wanamuongezea kesi kwani kwa sasa anayo ya kuandamana jan .

Huu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu nakushangaa ww mwanacdm ambaye unajua maamuzi yale hayakuwa ya mtu mmoja kufurahia taasisi yenu kupuuzwa na kudhalilishwa ili mradi kundi lenu la zitto lipate kunyooshea kidole la mbowe its crazy
Mala sasa anajaribu kujificha nyuma ya bifu lao na lema kutaka kuhalalisha utovu wake wa nidhamu haiwezekani agome kwenda kujieleza kamati kuu halafu arudi kuhoji kwa nini kamati kuu iwahukumu na si wilaya huyu ameshaharibiwa akili kama si pombe basi fedha
Mala amelipa waandishi fedha nyingi kutoa tamko na wameandika wakati tamko linatolewa nje alikuwepo kada wa ccm gambo akiwasubiri madiwani wa cdm swala la kujiuliza gambo lini kawa swahiba wao wkt ni kijana na chatanda ukiunganisha dots u'l get something
Nina mengi ila kwa sasa naachia hapa
 
6
kumbe elimu kwako ni kigezo cha utawala?sasa mbona ccm wasomi ni wengi ila hamna wanacho fanya pia ulishajiuliza hao madiwani na cdm nani kamkuta mwinzie(madiwani wamekikuta chama?ama chama kimewakuta wao)mpangaji amtishi mwenye nyumba hata iweje ndugu
 
ben
Kwanza nikupongeze kwa uwazi lakini nitofautiane na wewe kujaribu kuonyesha kuunga mkono utovu wa kimaadili unaofanywa na madiwani .
Hata kama wanahoja ya kupinga hawakupaswa kupinga hadharani maamuzi ya kamati kuu ya chama huku wakitishia kumshtaki katibu mkuu tena walimpa muda kabla ya jana awe ameitisha mkutano na kuwaomba radhi mbele ya wananchi lasivyo wanamuongezea kesi kwani kwa sasa anayo ya kuandamana jan .

Huu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu nakushangaa ww mwanacdm ambaye unajua maamuzi yale hayakuwa ya mtu mmoja kufurahia taasisi yenu kupuuzwa na kudhalilishwa ili mradi kundi lenu la zitto lipate kunyooshea kidole la mbowe its crazy
Mala sasa anajaribu kujificha nyuma ya bifu lao na lema kutaka kuhalalisha utovu wake wa nidhamu haiwezekani agome kwenda kujieleza kamati kuu halafu arudi kuhoji kwa nini kamati kuu iwahukumu na si wilaya huyu ameshaharibiwa akili kama si pombe basi fedha
Mala amelipa waandishi fedha nyingi kutoa tamko na wameandika wakati tamko linatolewa nje alikuwepo kada wa ccm gambo akiwasubiri madiwani wa cdm swala la kujiuliza gambo lini kawa swahiba wao wkt ni kijana na chatanda ukiunganisha dots u'l get something
Nina mengi ila kwa sasa naachia hapa

Carefree,

Mimi nilisizitiza juu ya umuhimu wa kujenga hoja na kumjibu ngongo kwa hoja kama kuna umuhimu huo badala ya Matusi,tujitofautishe na vijana wa CCM huku kwenye mtandao.Heshima ya u-Chadema ni hoja,haiba ya U-CCM ni ukada,ushabiki,matusi,zomezomea ghiliba na mtaji wao mkubwa wa Ufisadi na ujanja ujanja tu.Chadema hakuna shortcut,lazima kila kitu kiwe wazi na haiba yetu ni ujasiri.Kombati siyo vazi tu,hilo vazi linafalsafa yake...hata unapojibu hoja ni lazima hoja zako zivae combat! ! ! hapa nadhani nimeleweka.....................................! ! !

Kwa kweli hakuna mahali popote nimeunga mkono madiwani wa arusha,na hakuna mahali popote nimewapinga.Pia kuna thread nyingine tangu mwanzo nilitoa msimamo wangu juu ya swala la Arusha.Ndiyo maana sasa nikasema tuvute subira,maamuzi ya busara yachukuliwe....Ilimradi haki itendeke kwa pande Zote kwa kuzingatia pillars nilizozitaja hapo mwanzo
 
Madiwani wasaliti wa CDM mjini Arusha:Malla,Charles na Bayo wameshiriki kikao cha Madiwani wakiwa wameshikilia nyadhifa zao za Kamati muhimu na Unaibu Meya wakati tokea juzi Alhamisi walitakiwa kujivua nyadhifa hizo amri iliyotolewa na Makao Makuu na Kamati Kuu ya Chama.Huku madiwani hao baada ya Kikao hicho walipata chakula na pia wakapark vyakula kwenye bahasha za khaki A4 jambo lililofanya mvutano na walinzi wa eneo hilo na pia maneno tokea kwa madiwani wa Ccm wakitaka kuonyesha umasikini na njaa waliyo nayo madiwani hao wa CDM na pia wengine wakisikika wakisema "Ndio maana tumewahonga mmekubali kamati na unaibu meya Mmmh lakini pesa tamu bwana Malla kala zake M 70 maisha poa"mwisho wa kunukuu.Jamani wana CDM Arusha tutafika wapi na hawa viongozi Mamluki?
 
Madiwani wasaliti wa CDM mjini Arusha:Malla,Charles na Bayo wameshiriki kikao cha Madiwani wakiwa wameshikilia nyadhifa zao za Kamati muhimu na Unaibu Meya wakati tokea juzi Alhamisi walitakiwa kujivua nyadhifa hizo amri iliyotolewa na Makao Makuu na Kamati Kuu ya Chama.Huku madiwani hao baada ya Kikao hicho walipata chakula na pia wakapark vyakula kwenye bahasha za khaki A4 jambo lililofanya mvutano na walinzi wa eneo hilo na pia maneno tokea kwa madiwani wa Ccm wakitaka kuonyesha umasikini na njaa waliyo nayo madiwani hao wa CDM na pia wengine wakisikika wakisema "Ndio maana tumewahonga mmekubali kamati na unaibu meya Mmmh lakini pesa tamu bwana Malla kala zake M 70 maisha poa"mwisho wa kunukuu.Jamani wana CDM Arusha tutafika wapi na hawa viongozi Mamluki?

Duu mkuu hebu tupe source ya hii kitu inaonekana tamu sana halafu ongezea mahabari mengine hapa...
 
Vijina nawaone huruma, wamelewa madaraka, hao ccm wala hawata wachukua wakitolewa chamani
 
Siyo suala la Mbowe au Pinda kukanusha kwa sababu hakuna muafaka wewe unasema mlisikia sisi wengine hatujasikia



Umekuwa mkweli hapa kuwa madiwani wamekula rushwa "kutokana na usemi wa Mala kupitia TV"




Matokeo ya uchunguzi yako Lumumba na amekabidhiwa Mallah ili aendelee kukaidi chama.



Slaa alitaja list of shame akiwemo JK hata gamba hajivui. Sasa subiri wafukuzwe warudi CCM waliko na thamani.




Asafishwe kwa kujinyea mwenyewe halafu source yako ni TV na siajabu TBC. Ni CCM pekee yenye uwezo wa kusafisha wanachama wake.



Katiba itafuatwa na ilifuatwa hadi hapa, sasa washauri kina Mallah kuwa katiba itafuatwa.



Saa imefika lakini sikio la kufa halisikii dawa, yaani ni lazima life.



Mallah ni sawa sawa na wewe FF; INZI KUFIKIA KWENYE KIDONDA SI HASARA



Wewe si ndiye bosi wa Slaa mfukuze kazi. Aliyeutoa huu mfupa ndiye anajua ugumu wake si Dr. Slaa.



Anastahili kupewa Heko na wapuuzi wenziwe, ILA MAJUTO NI MJUKUU



Anza kujiuzuru wewe najua ungependa Dr. Slaa siyo ajiuzuru bali asiwepo kwenye uso wa dunia. LAKINI KUMBUKA MNALO MPAKA KIELEWEKE


1) "Taarifa hizo zilieleza kuwa Mwenyekiti Mbowe alikuwa ameshakutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuhusu jinsi ya kutafuta muafaka wa kudumu kuhusu mgogoro huo na walikubaliana kumaliza suala hilo kabla ya Julai mosi mwaka huu."

Source: Raia Mwema

2) Usini quote out of context, hayo ni maneno ya Malla akimnukuu Slaa na akaendelea kusema Slaa "alete ushahidi" na Marando kaja kuchunguza na kasema hakuna dalili za rushwa. Hayo ni maneno ya Malla. Jee, mnakubaliana nae au mnakataa? kama mnakataa leteni ushahidi.

3) Limekushinda kujibu?

4) Limekushinda kujibu, umerukia kwingine. Aibu!

5) Huna jibu.

6) Saa 7:20 naona bado haijafika?

7) Saa 7:20 naona bado haijafika?

8) Huna jibu!

9) Huna jibu!

10) Huna jibu!

11) Kama ameshindwa madiwani watatu ataweza Watanzania zaidi ya million 40? Jiulize, tafakari, chukua hatua!
 
Mbunge hawezi kufanya kazi yake ipasavyo bila kupata sapoti ya madiwani.Na wenzetu CCM wanatumia huo Mwanya kuhakisha shughuli za Arusha zina-paralyse ili ikifika 2015 ionekane Chadema wameshindwa kazi Arusha.Kwa kiasi kikubwa madiwani ndiyo bridge kati ya wananchi na mbunge ambaye naye huwakilisha Interest za wananchi kwa mapana na katika level ya juu.Kwa kweli kipimo cha kiongozi ni kutafuta Diplomatic approach katika ku-solve conflict or crisis.Hili suala kwa kuwa limefikia hatua nzuri ya decision sasa,nadhani maamuzi ya busara kabisa ambayo ni diplomatic and more democratic orientedHuwa nafika mahala nafikiria pengine uchanga wa siasa na ulimbukeni ndiyo unatufikisha hapa tulipo.
we jamaa kigeugeu mnafiki sana, leo unamtazamo huu kesho ule,tunafurai twazidi kukufahamu
 
Kama ni kweli hawatakiwi kusogelea hata bendera ya CDM,hatutaki u cuf hapa si wameolewa watupieni na vilago vyao wahamie rasmi,CDM hawatakiwi watu vinyonga kama hao SHAME ON THEM *@#-+?%@/= DAMN.
 
I will be the last person kukubali kuwa hawa madiwani watatu wa CHADEMA wamekwa vyeo kwa kile walichokiita 'kuleta maendeleo'.
CHADEMA wakichunguza hii issue kwa umakini mkubwa wanaweza kugundua u-jairo wa hali ya juu.
 
Chama lazima kionyeshe kina miongozo isiyoyumbishwa. Kinaendeshwa kwa katiba mathubuti. Kina viongozi wenye kufuata maadili. Ukomavu na utawala wa sheria, haki na usawa unaanzia nyumbani. Madiwani wa Arusha wameonyesha ukaidi, dharau, utovu wa nidhami, shiriki na mbwa mwitu. Hawawezi kuaminiwa wala kuthaminiwa tena ndani ya chama. Vyovyote vile haingii akilini kufikia muafuka wa kufanya kazi na CCM chama tunachoamini ni cha kifisadi bila kuhakikiwa na vikao halali vya chama.

Pili siamini kwamba Dr Slaa alikaa chumbani mwenyewe na kufikia maamuzi ya kuwawajibisha wale madiwani. Dr ni katibu Mkuu, baada ya vikao halali vya chama wameona Madiwani walikengehuka, tamko limetolewa waachie pipi waliyopewa na CCM. Madiwani wamegoma na kuanza kutoa lugha za maudhi, dhalilishi, vitisho nk, jeuri hii wanaitoa wapi???????????????????

Siasa za makundi zinadhoofisha sana vyama vya siasa. Nakumbuka Joe liberman wa Democrati part nchini USA alipoamua kuungana kihoja na GOP alitemwa na Chama chake bila kujali kwamba wangepoteza jimbo. Ile ilionyesha sera na falsafa za chama ndizo nguzo imara za chama. Spika wa bunge la USA Boehner alisema tofauti zake na Obama ni pamoja na wao kila mmoja kuchagua chama cha siasa tofauti kwani vina mitazamo tofauti.

Madiwani wa Arusha kama wamekataa maelekezo ya viongozi, na vikao vya juu vya chama wanatakiwa kuwajibishwa. CDM lazima ijue kuwa haipambani na Madiwani wa Arusha tu ila inapamabana na mbinu chafu za CCM kujaribu kusambaratisha chama. Ni wakati wa kutuma ujumbe mahususi si kwa madiwani tu ila na kwa mawakala wao wanaoona kuleta migogoro ndani ya chama kunawasaidia wao.

Madiwani wachukuliwe hatua dhabiti za kinadhamu. Ikibidi wafukuzwe hata chama. Leo CDM wakilegalega kuchukua hatua kali watakuwa wanatoa tafsiri nyingi sana. Nataka kuona chama cha siasa kisichoogopa kuwajibisha watu kwa haki. Kesho kikiwa ikulu kitakuwa na wengi wa kuwaenzi na kuwawajibisha. Haki itendeke, madiwani waamue kuitumikia CDM au kutumikia CCM.

CDM waonyeshe uimara wao kuilinda katiba, na maamuzi ya vikao halali vya chama. Hili litakuwa fundisho kwa miaka mingi ijayo dhidi ya walowezi.

Ni mimi
Chief Mkwawa wa Kalenga
 
Mimi sitakuwa na mengi ya kusema kuhusiana na hawa Madiwani ambao kwa kiburi chao ama kutofahamu wameamua kuchukua hatua za kihuni. Ila labda niwakumbushe tu kwamba pengine CDM ndio wenye makosa kwa kutowapa somo MADIWANI kuhusu majukumu wanyochukua na pengine kutokuwa na mwongozo (katiba) unaohusiana na nafasi hii ila nitawaomba sana hawa madiwani wapitie tu link hii ya CCM wapate kuona jinsi gani chama kinahusika na kila walifanyalo. Bofya
Kama mlivyoona katika kanuni za chama CCM wameanza na mashrti kama ifuatavyo:-

MASHARTI YA UONGOZI KATIKA SERIKALI
1. Kila Kada wa CCM anayegombea na hatimaye kuchaguliwa kushika nafasi yoyote ya uongozi katika Serikali anapaswa kukiri kwa dhati kwamba maendeleo halisi ya wananchi yanayosimamiwa na Serikali ya CCM katika kipindi kinachohusika, yanapatikana kwa njia ya utekelezaji uliokamilika wa ILANI za CCM za uchaguzi. Kwa hiyo wajibu wake wa kwanza ni kusimamia utekelezaji wa ILANI zetu katika eneo lake la uongozi kwa uwezo wake wote.
Sasa sielewi kama hawa madiwani wanaelewa uzito wa maneno haya. CCM kwa ujumla wamekuwa na vision yao ambayo ndio wanataka kuijenga na ndio sababu ya msisitizo wa kanuni hizi. Wanahitaji sana nguvu ya pamoja kuwezesha kutimiza ahadi na sera zao na diwani ni mjumbe anayewakilisha . chama kuwafikia wananchi ngazi ya wilaya..

Vile vile CDM kama chama wana malengo (vision) yao ambayo ndiyo yamewapa ushindi wa majimbo ya Arusha. Na ili chama kiweze kuetelekeza ahadi hizi, kinachohitajika ni uwezo wa viongozi wake ngazi za wilaya kuwa na msimamo wa chama na sio mawazo yao binafsi kama vile wao ni wagombea binafsi.. Inatakiwa kufikiria sawa kwa namna inayojulikana kama kuona mbele kwa pamoja. Ndio maana CCM hawawezi kumchagua Spika wa Bunge wa CDM hata kama swala zima la kuwepo bunge ni kuwatumikia wananchi wote.. na ndivyo inatakiwa ktk ngazi za chini mshindi kulinda nafasi alopewa na wananchi ili apate kutekeleza wajibu alokabidhiwa.

Kibwagizo:-
Hekima ya uongozi iko kwenye namna viongozi wanavyoona na kutenda kuhusiana na maadili na motisha za wafuasi wao. Katika demokrasia msisimko hutokana na kuona maadili na motisha zako sambamba na zile chama na wafuasi wake ambao hupelekea kuchaguliwa kwako kwa kura nyingi, hivyo Uongozi wenye msisimko ni ule uwezo wa kutenda kuhusiana na hayo maadili na motisha kwa ujasiri na dhati...Wachina wana msemo usemao kwamba Ili kuongoza watu, tembea nyuma yao..
Visionary:-
Kwa namna moja naweza kusema ni dhana ya kuona mbele, uwezo wa kuwaza juu ya siku zijazo kwa namna ya kujiuliza ni nini kinachohitajika kufanywa kulingana na rasilimali watu na mazingira yake ili kukabiliana kwa namna ya kufaulu na yale tunayofikiria yatakuja siku zijazo. Kwa hiyo viongozi wote ktk ngazi zote ni lazima wafuate msimamo unaolenga kutekelezeka katika muktadha wa uhalisia huo. lakini muktadha ambao kiongozi wa jamii anafanya maamuzi yake kwa kubalidilika haraka na kirahisi sana kufuata mambo ya mpito ni jambo ambalo litamfanya kiongozi huyo kuachwa nyuma..

Hivyo basi, toka kiongozi wa chama makao makuu hadi kiongozi wa mji ktk eneo alochaguliwa hutumia sera na ilani za chama kuwahamasisha wananchi wategemee yapi na katika ujenzi upi..Na jambo hili linahusu uwezo wa kufanya matayarisho imara yakukabiliana na siku zijazo, kufanya maamuzi yanayoweka msingi ili jamii isuluhishe matatizo kwa namna ambayo wanaweza kubadilisha, au kuondolea mbali ikihitajika, ili kukabiliana na mahitaji na changamoto za uhalisi unaojitokeza.

K
wa ujmla wa yote haya ndio tunapata chama yaani nguvu ya harambee ktk kuwezesha dhana tangulizi ufanikiwe..Na ili kuwe na msisimko, kuona mbele kunapaswa kuchochea mawazo ya ufanisi wa hali ya juu katika jamii ili kuweka viwango vya juu zaidi vya kiufanisi. Kuona mbele kunatoa mwongozo na mwelekeo wa siku za usoni ambazo hazina uhakika ijapokuwa zina matumaini kwa sababu ya msingi uliokwisha tayarishwa kukabiliana ipasavyo na siku zijazo. Na chama ni nguvu ya pamoja kukabiliana na changamoto hizo.

Kuona mbele huku kunaleta umuhimu na nguvu kutokana na kushiriki katika mtazamo huu wa mbele. Kuna msemo kwamba kiongozi hufaulu kwa kadri wafuasi wake wanavyofaulu. Uongozi unahitaji wafuasi na jambo muhimu zaidi katika kuona mbele ni kuwa na shabaha. Sasa hawa wafuasi wa CDM ambao ndio chanya ya malengo ya chama wanapoanza kwenda hovyo, hawaoni kama wapoteza vision ya chama badala yake wanatekeleza ile wananchi waloipinga..
 
Wanajamvi hali ni ngumu kwa upande wa CDM NA Lema Arusha bila kuchukua hatua thabiti mapema hali itakuwa Tete na tutapoteza Jimbo.
 
Mbunge hawezi kufanya kazi yake ipasavyo bila kupata sapoti ya madiwani.Na wenzetu CCM wanatumia huo Mwanya kuhakisha shughuli za Arusha zina-paralyse ili ikifika 2015 ionekane Chadema wameshindwa kazi Arusha.Kwa kiasi kikubwa madiwani ndiyo bridge kati ya wananchi na mbunge ambaye naye huwakilisha Interest za wananchi kwa mapana na katika level ya juu.

Kwa kweli kipimo cha kiongozi ni kutafuta Diplomatic approach katika ku-solve conflict or crisis.Hili suala kwa kuwa limefikia hatua nzuri ya decision sasa,nadhani maamuzi ya busara kabisa ambayo ni diplomatic and more democratic oriented

Huwa nafika mahala nafikiria pengine uchanga wa siasa na ulimbukeni ndiyo unatufikisha hapa tulipo.

Sijakuelwa Comrade! ila nitachambua

Negotiation yeyote lazima iwe na pande mbili ambapo kila pande ina kitu inahitaji. Huwezi tu kukubali muafaka kama kasuku. Diplomatic solutions huwa zinashindikana kwani upande mmoja ukiona hakuna faida ya solution inakataa maafikiano. Ni ukweli Mbunge anahitaji sana Madiwani ili kufanya kazi zake vizuri na kuharakisha Maendeleo.

Kwa miaka zaidi ya 18 sasa Tanzania tunalilia demokrasia ya uchaguzi, haki na kufuatwa sheria. Vyama vikongwe kwenye nchi Masikini dunia hutumia hila na ghiliba kushinda chaguzi. Utakuwa ni uhayawani kusahau nini wananchi wanapigania. Wananchi wanaililia Demokrasia ya kweli, haki kwenye sanduku la kura na usawa kwenye sheria. Uchumi imara na uongozi unaotoka kwa wananchi. Kama swala ni kukubaliana kwa nini tusikubaliane wote tuwe CCM???? Wengi tumeona CCM ni kichaka cha wezi, mafisadi, wabakaji wa demokrasia ndio maana tunaukataa huu muafaka mfu.

Mandela alipopewa uhuru bandia akiwa jela alitoa masharti atoke yeye na wapigania uhuru wote waliofungwa, na asipewe sharti lolote akiwa nje. CDM iliingia kwenye majadiliano na kauli mbiu uchaguzi wa Meya urudiwe apatikane mshindi kwa misingi ya haki, sheria, taratibu sheria za uchaguzi ule. Hii ina maana kubwa sana, kukomesha kabisa ghiliba za CCM. Kuonyesha sheria ni msumeno. Kaka Ben nachelea kusema siasa rahisi, muafaka rahisi, makubaliano ilimradi unapata paycheki hatuyataki. Sisi tupo kwenye mapambano ya kubadili mfumo wa utawala, mapambano ya kudai haki na usawa mbele ya sheria sio kujaza tu nafasi za uongozi. Yeyote anayetaka njia ya mkato aende CCM. Sisi tuliokuwepo CDM tangia kukiwa na wanachama wachache tuliamini tatizo kubwa la Maendeleo yetu ni utwala mbovu, na ubovu unaanzia kwenye kununua au kuhonga viongozi kwa njia ya vyeo, fedha nk na kupata watu wanaotumikia viongozi wachache. Tunahitaji viongozi wa watu kutoka kwa watu watakowajibika kwa watu.
 
Madiwani wasaliti wa CDM mjini Arusha:Malla,Charles na Bayo wameshiriki kikao cha Madiwani wakiwa wameshikilia nyadhifa zao za Kamati muhimu na Unaibu Meya wakati tokea juzi Alhamisi walitakiwa kujivua nyadhifa hizo amri iliyotolewa na Makao Makuu na Kamati Kuu ya Chama.Huku madiwani hao baada ya Kikao hicho walipata chakula na pia wakapark vyakula kwenye bahasha za khaki A4 jambo lililofanya mvutano na walinzi wa eneo hilo na pia maneno tokea kwa madiwani wa Ccm wakitaka kuonyesha umasikini na njaa waliyo nayo madiwani hao wa CDM na pia wengine wakisikika wakisema "Ndio maana tumewahonga mmekubali kamati na unaibu meya Mmmh lakini pesa tamu bwana Malla kala zake M 70 maisha poa"mwisho wa kunukuu.Jamani wana CDM Arusha tutafika wapi na hawa viongozi Mamluki?
Mangi,Usilete mipasho ya kwenye Kitchen Party, weka ushahidi hapa kama Madiwani wamechukuwa Rushwa kutoka Magamba JF, sio sehemu ya porojo!Naibu Meya wa CDM Mpambanaji Mallah, ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa kifedha anamiliki makampuni, yake binafsi tumeona wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu katumia pesa za pamoja na magari yake kuitangaza CDM, sasa leo unasema kapewa milioni 7, halafu kagombania chakula, Mallah usikubali kuwa mateka wa mbowe na A loser Dr Slaa,Bora kufa umesimama kuliko kuhishi umepiga magoti
 
Back
Top Bottom