Yupo tayari kutolewa govi.
Ingekuwa ni Mimi ningempeleka jando la kienyeji kama nilivyofanyiwa Mimi.
Sipendi mb** iwe imezungushiwa nyuzi za hospital zinaleta manundu kwenye Njia- anakuwa siyo smooth.
Enzi zetu tulitahiriwa na viwembe,wakati wa kubadilisha na kuisha bidonda tulikuwa tunat*mb* vifuu vyenye maji kutoa plaster kisha inawekwa dawa. Full kienyeji.
Mkuu umenikumbusha mbali sana!
Kuna wale wazee wa kusimamia watoto polini—asee, ni wakuda kinoma. Picha linaanza unakatwa bila ganzi kudadadekiii! 🤣🤣
Ukilia wakati wa kukatwa, unachekwa na kuchezewa mbata za mgongo huku unasindikizwa na maneno:
"Kazaaaa mwanaume! Qhuma tamu kuliko soda. Usipotolewa hilo dude huwezi kula tunda."
Babu yako anakupakata anakupa maneno ya kishujaa. Basi, kiume tu, chozi linakatika, unakaza!
Sasa, kimbembe kinakuja siku ya kuondoa bandage ya zamani uweke mpya pamoja na dawa. 🤣🤣🤣
Aseeh, ukitaka amani jitatue mwenyewe baba. Watakupa maji ya moto uloweshe dushe, alafu ujitatue taratibu mwenyewe. Oyaaaa yale maumivu sio kweli daaaah!!!
Unajitatua, af kuna sehemu lazima inakuwa na usumbufu fulani ilimradi tu ukwame, aje mrombo wa jando akutatue. Aaaah watu hawana huruma hao!
Pilika za jando aseeeh, zimetufanya tuwe wanaume haswaa!
Zamani hadi unakaa msituni mwezi na nusu—humuoni mama wala bibi, kifupi huoni mwanamke yeyote hadi siku ya kurudi home.
Na ile siku mnaambiwa
"Sasa leo ni siku ya kurudi nyumbani."
Lile boma (jengo la miti) la msituni linatakiwa lichomwe moto wakati mpo ndani. Likishawashwa tu, mnatakiwa mu-escape huo moto kwa namna yoyote (hii ishu mnakuw trained wiki mbili, so haiwi risk at all). Ni ishara ya ukomavu kwa watoto waliokaa msituni mwezi mmoja na wiki mbili.
Hii ishu ndo inafanya kwetu kusiwe na tabia ya kutahiri watoto wakiwa wadogo lazima apitie hizi ishu. Imagine unampeleka mtoto wa miaka 4, atatoboa hapo? Ngumu sana!
Tohara kwetu sio kuondoa govi tu; ni mafunzo ya kuandaa mtoto kuwa mwanaume jasiri.
Mtoto akirudi home, hatakiwi kuogeshwa na mama wala dada—ni kaka au baba tu. Ndololo haitakiwi ionekane na dada tena.
Oyaaa, kwetu kuna zile kamba wanafungaga ndololo ikiwa imepona, ili ipate kukua na kweli inakua kudadekiii!
Midume mnashindana kuonesha dushe tuuuu. Sio poa aseeh.
Hii mitoto ya sasa hivi inatahiriwa na kuogeshwa na bimkubwa—ovyo kabisa! Hahahahaha
Mtoto analilia soda! Hatari sana.
Zamani ukililia soda unasimamishwa juu bila nguo, unakunja mguu mmoja mtindo wa 4, halafu chini wanaweka makaa ya moto. Sasa shusha mguu uungueee! Hakuna huruma kwenye kuandaa mtoto wa kiume!
Sasa hivi? Looool!
Watoto hawa acha tu!