Madereva wa mikoani wasitisha mgomo wao!

Mkaa Mweupe

JF-Expert Member
Jun 29, 2007
654
183
Leo hii madereva wa mabasi ya kwenda mikoani wamegoma, mpaka sasa hivi hamna basi lolote lililoondoka katika stendi kuu ya Ubungo. Hii ni kutokana na adhabu iliyotolewa kwa dereva aliyekuwa akiendesha basi la Mohamed Trans lililopata ajali baada ya kupasuka gurudumu la mbele. Dereva huyo alihukumiwa kifungo cha miaka thelathini jela.

Jamani Tanzania tunaelekea wapi. Dereva miaka 30, mafisadi wanapeta...
Kulikoni?...
 
Last edited by a moderator:
Nadhani madereva wamekosea kidogo, naona bora wangekata rufaa kuliko kuwapa usumbufu abiria wasio na hatia!
 
Nadhani madereva wamekosea kidogo, naona bora wangekata rufaa kuliko kuwapa usumbufu abiria wasio na hatia!

Nafikiri ni dalili ya kuwa hawana imani na mfumo wa sheria. Hivi ile kesi ya Chenge naye si aliua, nasikia kesi yake itaanza kusikilizwa Sept 18. Ajali ilitokea March 27!
 
Nadhani madereva wamekosea kidogo, naona bora wangekata rufaa kuliko kuwapa usumbufu abiria wasio na hatia!

Ajali haikuwa driver's faulty. Nadhani mambo mengine yanafanyika kisiasa zaidi. Hukumu nyingine zinatolewa kwa shinikizo. Mgomo wa madereva utalfanya haki itendeke haraka.
 
Yeah nimepita asubuhi saizi Ubungo pale sijaona bus. Nimeona Coaster za Moro ndo zinakula vichwa kweli kweli kufa kufaana.
 
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana. Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?

Madereva wanagoma kwani wengi wanatabia ya kuendesha kwa kasi na kutozingatia sheria za barabarani, wanaogopa wasikumbwe na mkasa wa mvua ya miaka. Mini naendeshaga mwenyewe kutoka Dar hadi Moshi. Lakini huko njiani kuna ukiukwaji sana wa sheria za barabarani. Utakuta mtu ana overtake kwenye kona, pasiporuhusiwa, wanapaki ovyo hasa malori, speed kali sana, penye speed 50km/h anaendesha mia

Mimi nadhani adhabu hii itakua fundisho kwa madereva wazembe na ninaiomba mahakama zetu hapa nchini zisicheleweshe kesi za namna hii. Mtu akiua halaiki ya watu namna hii haina tofauti sana na wanaojitolea mhana uko mashariki ya kati au mauajia ya jimbari, Darful n.k

Ungekua wewe ni mfiwa mmojawapo usingemtetea dereva hata kidogo. Umesababisha ajali kwa speed kali na kutofuata sheria za usalama barabarani then sheria ichukue mkondo wake.

Ila mimi nashangaa kwa nini mmiliki wa basi lile hajatiwa hatiani kwa makosa ya watendaji wake. Kifungu ni Skendo la Richmond amabapo Luwasa aliwajibishwa kutokana na Utendaji mbovu wa watendaji wake. Pia Mwinyi alijiuzuli akiwa waziri wa mambo ya ndani kutokana na utendaji wa askari wake.

Nawasilisha hoja
 
Wakuu huyo dereva ni wa basi la Mhd trans wa hii ajali ya juzi juzi au ? kama ndivyo hukumu ina matatizo yahitaji uchunguzi huru wa mwenendo wa hiyo kesi,nijuavyo mimi kesi hizo upelelezi wake huchukua muda si chini ya miezi sita,iweje kwa muda mfupi hivi upelelezi umekamilika na dereva kahukumiwa.Ni kweli ajali zimezidi na kwa kiwango kikubwa kunakuwa na uzembe iwe ni kwa dereva au mmiliki. Kwa basi kupasuka tyre inaniwia vigumu kumhusisha derva na uzembe,labda uchunguzi wa kina ungefanyika kujua nani hasa mhusika wa uzembe huo,yaweza kuwa ni uzembe wa mamlaka zinazodhibiti uingizaji wa matairi ya magari nchini kuruhusu tairi za kiwango cha chini kuingizwa na kutumiwa kwenye mabasi ya abiria, lakini pia mmiliki wa gari anaweza kuwa ni mzembe kama ameacha tairi iendelee kutumika wakati muda wake au kilomita za matumizi yake zimekwisha (Matairi mengi ya sikuhizi yana kiwango cha kilomita ambacho kikitimia yabidi libadirishwe hata kama laonekana bado zima)
 
Leo hii madereva wa mabasi ya kwenda mikoani wamegoma, mpaka sasa hivi hamna basi lolote lililoondoka katika stendi kuu ya Ubungo. Hii ni kutokana na adhabu iliyotolewa kwa dereva aliyekuwa akiendesha basi la Mohamed Trans lililopata ajali baada ya kupasuka gurudumu la mbele. Dereva huyo alihukumiwa kifungo cha miaka thelathini jela.

Jamani Tanzania tunaelekea wapi. Dereva miaka 30, mafisadi wanapeta...
Kulikoni?...

Mafisadi wanaua wengi kwa mwendo wa taratibu, Madereva wanaua na kujeruhi wengi kwa mwendo wa spidi kali....

Kutetea maderava wahuni na wauaji waliojaa katika barabara zetu ni sawa tu na kuwatetea mafisadi wahuni na hatari waliojaa miongoni mwetu ambao wengine tunakunywa, kucheza, kusali, kuomboleza na hata kulala nao....

omarilyas
 
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana. Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?

Madereva wanagoma kwani wengi wanatabia ya kuendesha kwa kasi na kutozingatia sheria za barabarani, wanaogopa wasikumbwe na mkasa wa mvua ya miaka. Mini naendeshaga mwenyewe kutoka Dar hadi Moshi. Lakini huko njiani kuna ukiukwaji sana wa sheria za barabarani. Utakuta mtu ana overtake kwenye kona, pasiporuhusiwa, wanapaki ovyo hasa malori, speed kali sana, penye speed 50km/h anaendesha mia

Mimi nadhani adhabu hii itakua fundisho kwa madereva wazembe na ninaiomba mahakama zetu hapa nchini zisicheleweshe kesi za namna hii. Mtu akiua halaiki ya watu namna hii haina tofauti sana na wanaojitolea mhana uko mashariki ya kati au mauajia ya jimbari, Darful n.k

Ungekua wewe ni mfiwa mmojawapo usingemtetea dereva hata kidogo. Umesababisha ajali kwa speed kali na kutofuata sheria za usalama barabarani then sheria ichukue mkondo wake.

Ila mimi nashangaa kwa nini mmiliki wa basi lile hajatiwa hatiani kwa makosa ya watendaji wake. Kifungu ni Skendo la Richmond amabapo Luwasa aliwajibishwa kutokana na Utendaji mbovu wa watendaji wake. Pia Mwinyi alijiuzuli akiwa waziri wa mambo ya ndani kutokana na utendaji wa askari wake.

Nawasilisha hoja

Naamini yote uliyoyasema yangeweza kuhalarisha hukumu kama yangetokana na uchunguzi na si swala la kusikia tu,mazingira ya tyre kupasuka ni muhimu yaangaliwe,kumbuka gari haikupinduka bali iligongana na gari nyingine,kama ww ni dereva lazima utakuwa unajua kuwa kupasuka kwa tyre kunasababisha gari iwe inakuvuta dereva upande ule ambao tyre limepasuka na ikitokea bahati mbaya kama ilivyokuwa kukawa na gari nyingine inakuja mbele yako ni hatari kwa sababu uwezekano wa kugongana unaongezeka, Na spidi ya 80km/hr unayoisema inategemea sana sehemu ya barabara unapopata tatizo la tyre kupasuka,kama ni kwenye kona 80km/hr bado ni spidi inyoweza kuleta madhara.
 
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana. Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?
Nani kakwambia mafisadi hawatoi roho za watu? Hizo hela wanazoiba na kukimbizia nchi za nje unategemea nini? Huduma za hospitalini mbovu watu hawana madawa, barabara na miundo mbinu mingi mibovu. Then hata hiyo ajali ya Tabora iliyopelekea Kifungo cha Dereva huyu inawezekana kabisa ni matokeo ya ufisadi kwani barabara hiyo si barabara bali ni mahandaki.
 
Ajali haikuwa driver's faulty. Nadhani mambo mengine yanafanyika kisiasa zaidi. Hukumu nyingine zinatolewa kwa shinikizo. Mgomo wa madereva utalfanya haki itendeke haraka.

Haki itakayopatikana kwa shinikizo hili la mgomo wa madereva bado tutaiita haki?

omarilyas
 
you guys are funny bana!HAWAJAGOMA HATA KIDOGO.wanafanya mkutano kujadili ajali nyingi za mfululizo za barabarani!

-chanzo
-namna ya kudhibiti

Watu bana!mnatoa wapi uzushi ninyi?
DAMN IT!
 
JUZI RAIS AKIWA SINGIDA ANARIPOTIWA KUTOA AMRI KWAMBA MADEREVA WANAO SABABISHA AJALI NA KUUA ABIRIA WAFUNGWE MAISHA. HII ILITOKEA BAADA YA AJALI YA MKOANI SINGIDA/MANYARA ILIYO UA WATU WENGI KIDOGO.

SASA KOSa la hakimu liko wapi kuhukumu miaka 30 wakati mkuu wa nchi amekwisha toa agizo. sio lazima kubadilisha sheria za traffic kwanza!!!

macinkus
 
Naomba hapa JF kuwe na mjadala huru ili tujue nini maana ya over speeding,naamini gari imeundwa kwa kuzingatia tafiti mabalimbali muhimu ili kuhakikisha zinaundwa na kuwekewa kiwango cha mwendo kasi ambacho hakitakiwi kusababisha ajari kama mazingira tarajiwa ya gari yatakuwepo,si kweli kwamba basi likiendeshwa kwa speed ya 120km/hr litapata ajali,ajali yaweza kutokea hata kama unaendesha kwa speed 60kms/hrs,lilio la muhimu inabidi tuangalie mazingira ya ajari kwa ukumla wake tukianzia na barabara na alama husika,ubora wa magari yenyewe na uwezo wa madereva.
Uzembe ni chanzo kikubwa cha ajali,wala kuendesha kwa speed kubwa hakuna uhusiano na uzembe,ni muhimu basi ajali inapotokea tuchunguze ni aina gani ya uzembe uliosabaisha ajali badala ya kukimbilia kuhukumu speed ya dereva. Huwezi ukaendesha gari Dar-Songea kwa 80kms/hr.labda kama abiria watakuwa na mkataba wa kudumu nawe,safari ni ndefu sana inafupishwa na speed inayotumiwa na madereva ambayo ndcho kivutio kwa abiria walio wengi.
Umakini wa madereva,wamiliki na mamlaka zinazohusika na miundo mbinu utaopunguza au kuoandoa ajali na si speed ya magari,speed itapunguza maafa lakini si kuondoa ajali
 
Dereva wa mohamed trans alihukumiwa juzi baada ya kuua mtu 1 na kujeruhi 9
mnamo sept. 12 mwaka jana sasa mshaija nauliza dereva wa mohamed trans
iliyoua lundo la abiria likitokea mwanza kupitia nairobee judy cross
multiplication hapo na sheria zetu za ramli.
Dereva aliyehukumiwa ni basi lilikua linatoka tbr to muanza oooops mwanza
kahukmiwa tabora. Wadau mlio na wasafiri leo ni hayo waandishi wanazidi
miminika ubungo terminal.
 
Naamini yote uliyoyasema yangeweza kuhalarisha hukumu kama yangetokana na uchunguzi na si swala la kusikia tu,mazingira ya tyre kupasuka ni muhimu yaangaliwe,kumbuka gari haikupinduka bali iligongana na gari nyingine,kama ww ni dereva lazima utakuwa unajua kuwa kupasuka kwa tyre kunasababisha gari iwe inakuvuta dereva upande ule ambao tyre limepasuka na ikitokea bahati mbaya kama ilivyokuwa kukawa na gari nyingine inakuja mbele yako ni hatari kwa sababu uwezekano wa kugongana unaongezeka, Na spidi ya 80km/hr unayoisema inategemea sana sehemu ya barabara unapopata tatizo la tyre kupasuka,kama ni kwenye kona 80km/hr bado ni spidi inyoweza kuleta madhara.
Of course watu wengi hapa wanajadili kwa kusikia tu, naamini kuwa kati ya sisi tunaojadili, hakuna aliyekuwa ndani ya basi hilo wakati linapata ajali. Kwa maana hiyo, kwa kutegemea simulizi za waliokuwepo kwenye basi tulizozisikia, wala hakukuwa na kupasuka kwa tairi. Nimesoma hiyo kwenye gazeti moja lililoknukuu abiria aliyenusurika. Huyo abiria alisema basi lilikuwa bovu tangu walipoanza safari na kuna wakati dereva aligoma kuendelea na safari, wakafanya matengenezo (ya uowongo na kweli) na safari kuendelea. Abiria anasema basi lilikuwa linayumba barabarani na dereva alikuwa anakwenda kasi.
Kwa hiyo, kama maenelezo haya ni sahihi, kuna aina fulani ya uzembe wa dereva hapa
 
Kuna jambo la msingi hapa la kutazamishwa.Ubovu wa usimamizi wa sheria za barabarani na utendaji mzima wa kazi wa jeshi la Polisi kuna mafungufu ya kina.Hata twende ahera wote kama kazi ya udereva haikuendewa shule za kina za kuwafunza sheria na uendeshaji haitatokea hata siku moja kusiwe na ajali katika nchi hii.Mfumo duni wa utoajia mafunzo ya udereva,sheria finyu zisizokuwa shirikishi,na miundo mbinu mibovu.Hayo sawa twaweza kusalimisha roho zetu na watu wetu pia.Ajali nyingi nchi hii ni kwa ajili ya uzembe wa watumiaji wa barabara na vyomborushwa vya usalama barabarani.
 
Back
Top Bottom