Naomba hapa JF kuwe na mjadala huru ili tujue nini maana ya over speeding,naamini gari imeundwa kwa kuzingatia tafiti mabalimbali muhimu ili kuhakikisha zinaundwa na kuwekewa kiwango cha mwendo kasi ambacho hakitakiwi kusababisha ajari kama mazingira tarajiwa ya gari yatakuwepo,si kweli kwamba basi likiendeshwa kwa speed ya 120km/hr litapata ajali,ajali yaweza kutokea hata kama unaendesha kwa speed 60kms/hrs,lilio la muhimu inabidi tuangalie mazingira ya ajari kwa ukumla wake tukianzia na barabara na alama husika,ubora wa magari yenyewe na uwezo wa madereva.
Uzembe ni chanzo kikubwa cha ajali,wala kuendesha kwa speed kubwa hakuna uhusiano na uzembe,ni muhimu basi ajali inapotokea tuchunguze ni aina gani ya uzembe uliosabaisha ajali badala ya kukimbilia kuhukumu speed ya dereva. Huwezi ukaendesha gari Dar-Songea kwa 80kms/hr.labda kama abiria watakuwa na mkataba wa kudumu nawe,safari ni ndefu sana inafupishwa na speed inayotumiwa na madereva ambayo ndcho kivutio kwa abiria walio wengi.
Umakini wa madereva,wamiliki na mamlaka zinazohusika na miundo mbinu utaopunguza au kuoandoa ajali na si speed ya magari,speed itapunguza maafa lakini si kuondoa ajali