Madereva kutumia mwanga mkali (Full Beam) katika mazingira yasiyo sahihi barabarani ni hatari kwa wengine

JF Toons

Digital Art by JF
Feb 19, 2024
32
66
IMG_1652.PNG

Kweli, matumizi ya taa za gari ni muhimu sana kwa usalama barabarani. Kutumia mwanga mkali (full light) katika mazingira ya foleni au msongamano wa magari kunaweza kuwa hatari kwa sababu ya athari ya kumulika moja kwa moja kwa madereva wengine.

Hii inaweza kusababisha kutopata mwelekeo mzuri wa kina, kuchanganyikiwa, au hata kusababisha usumbufu au ajali.

Kwa bahati mbaya, baadhi ya madereva hutumia taa za gari kwa njia isiyo sahihi au bila kuzingatia mazingira yanayowazunguka.

Elimu juu ya matumizi sahihi ya taa za gari na uelewa wa jinsi mwanga unavyoathiri madereva wengine ni muhimu kuboresha usalama barabarani.
---
Matumizi ya taa barabarani yanaongozwa na kifungu cha 39C cha sheria ya Usalama Barabarani, yaani The Road Traffic Act, Cap.168
Nini Maana ya Neno Usiku?
Kwa mujibu wa kifungu cha 39C (1), neno “Usiku” linamaanisha kipindi kati ya jua kuzama na jua kuchomoza, na pia inahusisha wakati wote ambapo kunakuwa na uoni hafifu kwa sababu ukungu, mvua, kupita kwenye handaki au kwa sababu nyingine yoyote ile.

Wakati wa Kutumia taa na aina ya taa zinazoruhusiwa
Sheria hii inalazimisha kila dereva anayeendesha gari barabarani usiku kuwasha taa na atatumia taa zilizotengenezwa maalumu kwaajili ya gari hilo.

Na wakati wowote dereva atatumia taa kubwa mbili zenye kutoa mwanga mweupe zilizopo upande wa mbele wa gari lake na taa nyekundu mbili zilizopo nyuma ya gari lake. [Kif.39C (2)]

Pikipiki au chombo kingine chenye magurudumu mawili kitatuma angalau taa moja nyeupe mbele na taa moja nyekundu nyuma. [Kif.39C(3)]

Matumizi Sahihi ya Taa
Gari linapoendshwa barabarani, dereva wa gari hilo atatumia taa za mwanga mkali (full beam) au taa za mwanga wa kawaida (dipped headlights) kulingana na mazingira ya uoni ya wakati huo. [Kif.39C(4)]

Matumizi ya taa zenye Mwanga kidogo [Dippled headlights]
Taa zenye mwanga kidogo zitatumika
(a) Maeneo yote ya makazi yenye taa za kuangaza barabarani(street lights);
(b) Dereva anapopishana na gari jingine
(c) Dereva anapotaka kuovateki na kulipita gari jingine ili kumfanya dereva mwenzie aendelee kuona vizuri.

Je, ushawahi kushuhudia madereva huadhibiwa kwa matumizi mabaya ya taa?
 
Mwongozo upo;
1. Tumia taa hafifu unapokuwa unaendesha mjini au unapoendesha maeneo yoyote unayoyafaham vizuri/salama. Ukiwa unaendesha mjini kama kuna kitu unakiona kwa mbali ila hukielewi (yaweza kuwa Guta, trekta, mlevi nk), unawasha high kwa muda mfupi ili tu kuweza kufanya utambuzi na kurudi low (hafifu).

2. Tumia taa kali (high) unapoendesha mahala nje ya mji hasa ambapo hapana magari mengi au ambapo huna uhakika na usalama ili uweze kuona mbali na kufanya maamuzi sahihi.

Angalizo: ukiwa unaendesha kwa taa kali (high) ukiona chombo kingine cha moto kina kuja upande wako, unashauriwa uweke mwanga hafifu ili muweze kupishana kwa usalama

Huo ndio muongozo na adhabu zipo za kutokufuata huo utaratibu
 
Kamara ITs drivers wote na peleka pale veta wakajifunze matumizi ya hizi taa, yaani ni craze mkuu usiku, wao ni vitu viwili tu,speed na full lights, ila Nkanini ni wa push back ,sasa nipo sambamba nao, warning ⚠️ moja asipo dim ,kinachofuata yeye mwenyewe anakwenda pembeni
 
pombe + bangi.

hawa watu ni wendawazimu kama wale wanaoliza piki piki na alteza kwa mlio mkubwa sana kwamba wanasikia raha,majinga kabisa.
 
Hii nchi ya kujiamulia tu mwenyewe ukae road kwa mtindo gani hasa usiku maana sheria ukizingatia utaishia kuumia na kupata hasara ya kwenda service kila siku madereva wengi tomato sana.
 
Back
Top Bottom