Kuchomwa moto Saibaba ni matokeo ya polisi wa barabarani kutowachukulia hatua bodaboda wanapovunja sheria barabarani

maiyanga1

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
1,317
1,790
Jana tumesikia bodaboda wa Korogwe walivyojichukulia sheria mkononi na kulichoma moto bas la Saibaba, baada ya mwenzao kugongwa na kufariki. Mashuhuda wanasema bodaboda aliingia barabarani bila tahadhari.
Maeneo kadhaa nchini bodaboda hawazingatii sheria, chakushangaza zaidi wanaweza kufanya hivyo mbele ya askari wa usalama barabarani. Lakini inapotokea ajali hata kama imesababishwa na bodaboda bado dereva atashambuliwa na gari itaharibiwa.

Mara kadhaa tunashuhudia wanavyo pitia kushoto wakati wa kulipita gari lililoko mbele, wanavyopita bila kusimama kwenye vivuko vya wenda kwa miguu, wasivyotii taa za kuongozea magari, achilia mbali pikipiki kubeba abiria zaidi ya mmoja na kutokuvaa helmet.

Kwanini bodaboda huwa hawachukuliwi hatua wanapovunja sheria za barabarani?
 
Hao bodaboda washadakwa

Hivi wanawajuwa vizuri matajiri wa

Mabasi...na walivyokuwa mafia

Ova
 
Kwa uzoefu wangu hapa dar

Ugomvi wa boda na waendesha magari

Ni Kama ugomvi wa palestina vs Israel

Upo upo sana na hauishi leo Wala kesho

Chanzo cha ugomvi huu,
Ni KILA mmoja anamwonea wivu mwenzie wote wawapo kwenye foleni barabarani
 
bodaboda wameshindikana hata ile faini yao ya 30,000 kwa kosa moja ikirudishwa bado haitasaidia, pia ikichangiwa na rushwa kwa askari wetu wa usalama barabarani
 
Waliochoma wafilisiwe mali zao pamoja na mali za wazazi wao.
Wazazi wanaingiaje bwege, Kwa hiyo na tajiri wa saibaba aunganishwe kwenye kesi ya kugonga na kuua kama dereva wake alivyofanya? Usifikiri Kwa kutumia makamasi tumia ubongo wewe
 
Jana tumesikia bodaboda wa Korogwe walivyojichukulia sheria mkononi na kulichoma moto bas la Saibaba, baada ya mwenzao kugongwa na kufariki. Mashuhuda wanasema bodaboda aliingia barabarani bila tahadhari.
Maeneo kadhaa nchini bodaboda hawazingatii sheria, chakushangaza zaidi wanaweza kufanya hivyo mbele ya askari wa usalama barabarani. Lakini inapotokea ajali hata kama imesababishwa na bodaboda bado dereva atashambuliwa na gari itaharibiwa.

Mara kadhaa tunashuhudia wanavyo pitia kushoto wakati wa kulipita gari lililoko mbele, wanavyopita bila kusimama kwenye vivuko vya wenda kwa miguu, wasivyotii taa za kuongozea magari, achilia mbali pikipiki kubeba abiria zaidi ya mmoja na kutokuvaa helmet.

Kwanini bodaboda huwa hawachukuliwi hatua wanapovunja sheria za barabarani?
Inawezekana kinyume chake kwamba bodaboda wakigongwa na magari ni kama mbwa kagongwa na boda boda hawaoni wahusika kuchukuliwa hatua hivyo wameamua kujichukulia sheria mkononi. Na hii ndiyo ukweli licha ya ukweli kwamba bodaboda aligongwa na kufa lakini mjadala ni kuchomwa basi. Basi litanunuliwa lingine, bima inaweza kulipa lakini bodaboda aliyekufa hawezi kurudishwa.
Tujifunze kutii sheria za Barabarani sote bila kujali wewe nani.
 
Back
Top Bottom