Eng. Y. Bihagaze
JF-Expert Member
- Sep 8, 2011
- 1,488
- 908
karibu sana nimefuatilia shughuli zako za bunge hili la saba ambalo limetwikika mabegani mwako sawasawa. Ni kazi nzito, Ngumu yenye changamoto nyingi..
Kumbuka kwamba Bunge Hili la Tanzania kwa miaka mingi sana liliongozwa kiimla chini ya Mzee wetu Adam Sapi Mkwawa, Imagine Tokea 1962 hadi 1994 alikikalia kiti cha Bunge, tulishajua ndiye Speaker wa Milele wa Bunge,hatukuwa tunaelewa na Chochote maskini ya mungu toka kwenye kajengo ka pale Karimjee.. Mie sijui walikuwa wanafanyiana nini humo ndani, ingawa pale katikati yaani 1973-1975 Chief Erasto Mangenya alikikalia kiti cha ubunge kwa-tumiaka tuwili kabla ya Mzee Mkwawa kuendelea tena.
Ingawa kwa heshima Bunge lako lililovumbuliwa mnamo 1953 na spika wa kwanza Mzee Karimjee alikalia uspika kwenye vuguvugu la vyama vingi TANU, UTP na ANC akatuvusha kwenye Uhuru Tukajipatia Mwalimu Nyerere Julius ambaye alisaini sheria zetu badala ya kuzivusha baharini hadi kwa malkia.
Madam Speaker, Ukumbuke pia kwamba Vuguvugu la vyama vya kisiasa vilifufuka tena 1992, na kufuatiwa na uhuru mkubwa wa vyombo vya habari ambapo ndipo kwa mara ya kwanza matongotongo yanatutoka kwa kuona ITV ilipoanza 1994 baada ya kukaa kwenye kiza cha kupata habari-picha makumi ya miaka, ingawa Kenya "redio hii ya sinema" wenzetu tokea 1960 wanaangalia TV. Hali hii ikafuatiwa na uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995 ambapo Mhe Pius Msekwa aliendelea kuutwaa uspika alioupokea kwa Mkwawa tokea 28,April 1994. Yeye alidumu nao kwa miaka Kumi na moja hadi 2005, ambapo alitamani nae kuendeleanao tuu ila mzee Sita akamwekea Kigingi. Yeye Sita akakishika kijiti cha uspika kwa miaka mitano tu hadi 2010. Alitamani sana kuendelea na uspika ila mama wewe Ukasema No.. na wanawake embu Tujaribu .. wakatiule kamsemon""wanawake wanaweza wakiwezeshwa" kakitawala, ingawa sasa kameshachakachuka sana "wanaweza hata wasipowezeshwa".
Sasa kwanini nakutupia hoja hii,Kumbuka wakina baba hawa wamefanya kazi nzuri ya uspika, hasa mzee sita na bunge la kasi na viwango na Msekwa. Sasa niko makini nakufuatilia kila bunge ila nina mashaka na mwenzetuwewe.. unaturudisha kwa bunge la Mzee Sapi Mkwawa ..
Kwanza Ulipoingia kwenye kiti hicho ulianza na mbwembwe kwa ile kaulimbiu yako kwamba, "Bunge linaongozwa na kanuni, na Ni kanuni hizo za bunge ndizo utakazo zitumia kwa kwenda mbele hatuangalii sura ya mtu " tutukasema mwanamke hapa kaamua, tukatarajia sheria kweli zitachukua mkondo wake,baadae ukajaziliza mavitabu mengi ya sheria na kanuni zake. mara katiba, mara kanuni za Bunge..mezani kwako, ukayasoma mpaka ukawa unayachanganya changanya, ukawakuta mjengoni vijana ambao wanazijua kanuni za bunge as if wao ndio waliozitunga. Ukataka ushauri kwa wazoefu wakakwambia usiwe serious sana bungeni, do it as a kitchen job, akalegeza msimamo hadi ukawa unapwaya, wewe kwa asili hujui matani sasa ukimtania mtu atadhani unamtukana, huna kipaji hicho..
Ukabadili stail ukaona uliongoze Bunge Kibabe kwa kamsemo "hivi hawa wananiona mie mwanamke ndio wanichezee sio, ngoja niwaonyeshee", ukaingia kibabe lakini ukagonga ukuta wa vikanuni .. mpaka wabunge wanakutaka ujitolee mwongozo, ukatorokea nyumbani, wiki kadhaa unaliangalia bunge ukiwa hom..
Tabia ya Kumwachia Ndugai Bunge, imekuwa haiwafurahishi "mabosi"ambao wanasema wewe spika ndiye uliyemezeshwa siri za serikali sasa kwanini muda mwingi gari liendeshwe na dereva asiyejua siri za safari. Sasa maneno hayo yamekufanya ukikalie kiti upende usipende , na sasa huna msimamo kamili, kadiri siku zinavyoendelea bungeni changamoto kali zinaibuka zenye vuguvugu kali za kisiasa. Na kadiri unavyolihandle Vuguvugu hilo hali inazidi kuwa dhoofu sana kiutendaji na kwa kasi unapoteza mvuto kwa jamii..
Inshu sio CHADEMA kama unavyolalamika all ways. Mbona Mhe Sita, Mhe Msekwa waliongoza Bunge kama hilihili.. Inshu ni wewe..
Labda Nikushauri yafuatayo
1. Bunge sio Yote katika maisha yako, Kukubali kushindwa ni Ushindi. Achia Uongozi wa spika, atauchukua mwingine tena tujitahidi awe mwanamke na ataendelea tu. Kubali kwamba Huwezi kuwa kiongozi wa kila kitu. Uongozi ni kipaji, kama huna huna tu.
2. Au Achana na sura za watu Bungeni, Chapa kazi yako, Tenda haki, Fuata kanuni na taratibu za bunge, Usipendelee Upande wa wabunge wala usipendelee upande wa serikali. Mwenye haki mpe haki.. Usiogope kwamba baadhi ya maamuzi ya Bunge yataathiri Chama Chako, achana na mambo ya chama, weka wananchi mbele kwanza, kazi mbele , chama baadae. Chama kikibeba wajibu wake hakitakufa, kikikaidi kufa kitakufa tu.
3. Wanawake wengi wanakuangalia kama ishara ya uadilifu na uthabiti wa uongozi. Utavyotenda Bungeni sasa utahamasisha bunge la 2015 kujaa au kupungua kwa idadi ya wanawake. ukiendelea kuongoza Bunge kwa staili hizi za Kimanati utaua Sifa ya mwanamke kwenye Uongozi huku ukiwasaliti, kuwatosa na kuwaabisha wanawake. mvuto wa uongozi kutoka kwa wanawake Tanzania utauangamiza mbele ya jamii, hata wanawake kujihisi si kitukukamata nafasi kubwa za uongozi. itachukua miongo mingi baadae ili jamii iweze kubariki tena dhima ya kuongozwa na Mwanamke kwenye sekta nyeti na kubwa. Nina imani bado una Muda mzuri wa kusahihisha makosa, Tunakutaka uwe jasiri, shupavu na usiyeyumbishwa.
4. Uwe unakunywa maji mengi pamoja na cocacola,..
Asante Madam Speaker.
...
YA LEO
wabunge wote wa upinzani yaani wa CUF, CDM, TLP ,NCCR wametoka bungeni kupinga kitendo cha spika kukataa kuahirisha bunge kwa dharura ili kuweza kutoa nafasi kwa serikali kuchukua hatua dhidi ya meli inayozama Znz.
Alitoa hoja Hamad Rashid kuwa Bunge lipitishe bajeti kabla ya mawaziri kuhitimisha ili kutoa nafasi kwa wabunge kufuatilia na kuweza kusafiri. Spika akamjibu kuwa hoja hiyo ingefaa kama maafa yametokea karibu na Bunge kama Chamwino etc ili wabunge waende wakatoe damu .
Hali ni mbaya , Bunge linapitisha bajeti kwa suala gani?
update nyingine 2013
- Kama kila linalosemwa na Wabunge wa CCM ni jema na linapita wakati linalosemwa na Wabunge wa vyama vya upinzani linapingwa na kutupiliwa mbali,Bunge halina maana.
- Kama Wabunge wa chama tawala wanaachwa kutumia lugha za kuudhi na wale wa upinzani wakitolewa nje ya Bunge na kutakiwa kuwasilisha maelezo,basi Bunge letu linakosa maana.
- Kama ushahidi unaoletwa mbele ya Spika na Wabunge wanaotakiwa kuuwasilisha unafichwa na kunyamaziwa,Bunge letu linakosa mshiko.
- Kama maazimio mbalimbali ya Bunge hayatekelezwi na yanapuuzwa,kuna maana gani ya kuwa na Bunge lenye nguvu ya kikatiba kuisimamia Serikali?
- Ikiwa Wabunge wanakuwa mstari wa mbele kuongoza watu kupiga wenzao na kufanya vurugu(tukio la jana Dodoma),i wapi heshima ya Bunge?
Tujadili...