MADAM SPEAKER: Rai...

Eng. Y. Bihagaze

JF-Expert Member
Sep 8, 2011
1,488
908
Spika.jpg

karibu sana nimefuatilia shughuli zako za bunge hili la saba ambalo limetwikika mabegani mwako sawasawa. Ni kazi nzito, Ngumu yenye changamoto nyingi..

Kumbuka kwamba Bunge Hili la Tanzania kwa miaka mingi sana liliongozwa kiimla chini ya Mzee wetu Adam Sapi Mkwawa, Imagine Tokea 1962 hadi 1994 alikikalia kiti cha Bunge, tulishajua ndiye Speaker wa Milele wa Bunge,hatukuwa tunaelewa na Chochote maskini ya mungu toka kwenye kajengo ka pale Karimjee.. Mie sijui walikuwa wanafanyiana nini humo ndani, ingawa pale katikati yaani 1973-1975 Chief Erasto Mangenya alikikalia kiti cha ubunge kwa-tumiaka tuwili kabla ya Mzee Mkwawa kuendelea tena.

Ingawa kwa heshima Bunge lako lililovumbuliwa mnamo 1953 na spika wa kwanza Mzee Karimjee alikalia uspika kwenye vuguvugu la vyama vingi TANU, UTP na ANC akatuvusha kwenye Uhuru Tukajipatia Mwalimu Nyerere Julius ambaye alisaini sheria zetu badala ya kuzivusha baharini hadi kwa malkia.

Madam Speaker, Ukumbuke pia kwamba Vuguvugu la vyama vya kisiasa vilifufuka tena 1992, na kufuatiwa na uhuru mkubwa wa vyombo vya habari ambapo ndipo kwa mara ya kwanza matongotongo yanatutoka kwa kuona ITV ilipoanza 1994 baada ya kukaa kwenye kiza cha kupata habari-picha makumi ya miaka, ingawa Kenya "redio hii ya sinema" wenzetu tokea 1960 wanaangalia TV. Hali hii ikafuatiwa na uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995 ambapo Mhe Pius Msekwa aliendelea kuutwaa uspika alioupokea kwa Mkwawa tokea 28,April 1994. Yeye alidumu nao kwa miaka Kumi na moja hadi 2005, ambapo alitamani nae kuendeleanao tuu ila mzee Sita akamwekea Kigingi. Yeye Sita akakishika kijiti cha uspika kwa miaka mitano tu hadi 2010. Alitamani sana kuendelea na uspika ila mama wewe Ukasema No.. na wanawake embu Tujaribu .. wakatiule kamsemon""wanawake wanaweza wakiwezeshwa" kakitawala, ingawa sasa kameshachakachuka sana "wanaweza hata wasipowezeshwa".

Sasa kwanini nakutupia hoja hii,Kumbuka wakina baba hawa wamefanya kazi nzuri ya uspika, hasa mzee sita na bunge la kasi na viwango na Msekwa. Sasa niko makini nakufuatilia kila bunge ila nina mashaka na mwenzetuwewe.. unaturudisha kwa bunge la Mzee Sapi Mkwawa ..

Kwanza Ulipoingia kwenye kiti hicho ulianza na mbwembwe kwa ile kaulimbiu yako kwamba, "Bunge linaongozwa na kanuni, na Ni kanuni hizo za bunge ndizo utakazo zitumia kwa kwenda mbele hatuangalii sura ya mtu " tutukasema mwanamke hapa kaamua, tukatarajia sheria kweli zitachukua mkondo wake,baadae ukajaziliza mavitabu mengi ya sheria na kanuni zake. mara katiba, mara kanuni za Bunge..mezani kwako, ukayasoma mpaka ukawa unayachanganya changanya, ukawakuta mjengoni vijana ambao wanazijua kanuni za bunge as if wao ndio waliozitunga. Ukataka ushauri kwa wazoefu wakakwambia usiwe serious sana bungeni, do it as a kitchen job, akalegeza msimamo hadi ukawa unapwaya, wewe kwa asili hujui matani sasa ukimtania mtu atadhani unamtukana, huna kipaji hicho..

Ukabadili stail ukaona uliongoze Bunge Kibabe kwa kamsemo "hivi hawa wananiona mie mwanamke ndio wanichezee sio, ngoja niwaonyeshee", ukaingia kibabe lakini ukagonga ukuta wa vikanuni .. mpaka wabunge wanakutaka ujitolee mwongozo, ukatorokea nyumbani, wiki kadhaa unaliangalia bunge ukiwa hom..

Tabia ya Kumwachia Ndugai Bunge, imekuwa haiwafurahishi "mabosi"ambao wanasema wewe spika ndiye uliyemezeshwa siri za serikali sasa kwanini muda mwingi gari liendeshwe na dereva asiyejua siri za safari. Sasa maneno hayo yamekufanya ukikalie kiti upende usipende , na sasa huna msimamo kamili, kadiri siku zinavyoendelea bungeni changamoto kali zinaibuka zenye vuguvugu kali za kisiasa. Na kadiri unavyolihandle Vuguvugu hilo hali inazidi kuwa dhoofu sana kiutendaji na kwa kasi unapoteza mvuto kwa jamii..

Inshu sio CHADEMA kama unavyolalamika all ways. Mbona Mhe Sita, Mhe Msekwa waliongoza Bunge kama hilihili.. Inshu ni wewe..

Labda Nikushauri yafuatayo

1. Bunge sio Yote katika maisha yako, Kukubali kushindwa ni Ushindi. Achia Uongozi wa spika, atauchukua mwingine tena tujitahidi awe mwanamke na ataendelea tu. Kubali kwamba Huwezi kuwa kiongozi wa kila kitu. Uongozi ni kipaji, kama huna huna tu.

2. Au Achana na sura za watu Bungeni, Chapa kazi yako, Tenda haki, Fuata kanuni na taratibu za bunge, Usipendelee Upande wa wabunge wala usipendelee upande wa serikali. Mwenye haki mpe haki.. Usiogope kwamba baadhi ya maamuzi ya Bunge yataathiri Chama Chako, achana na mambo ya chama, weka wananchi mbele kwanza, kazi mbele , chama baadae. Chama kikibeba wajibu wake hakitakufa, kikikaidi kufa kitakufa tu.

3. Wanawake wengi wanakuangalia kama ishara ya uadilifu na uthabiti wa uongozi. Utavyotenda Bungeni sasa utahamasisha bunge la 2015 kujaa au kupungua kwa idadi ya wanawake. ukiendelea kuongoza Bunge kwa staili hizi za Kimanati utaua Sifa ya mwanamke kwenye Uongozi huku ukiwasaliti, kuwatosa na kuwaabisha wanawake. mvuto wa uongozi kutoka kwa wanawake Tanzania utauangamiza mbele ya jamii, hata wanawake kujihisi si kitukukamata nafasi kubwa za uongozi. itachukua miongo mingi baadae ili jamii iweze kubariki tena dhima ya kuongozwa na Mwanamke kwenye sekta nyeti na kubwa. Nina imani bado una Muda mzuri wa kusahihisha makosa, Tunakutaka uwe jasiri, shupavu na usiyeyumbishwa.

4. Uwe unakunywa maji mengi pamoja na cocacola,..

Asante Madam Speaker.

...
YA LEO

wabunge wote wa upinzani yaani wa CUF, CDM, TLP ,NCCR wametoka bungeni kupinga kitendo cha spika kukataa kuahirisha bunge kwa dharura ili kuweza kutoa nafasi kwa serikali kuchukua hatua dhidi ya meli inayozama Znz.

Alitoa hoja Hamad Rashid kuwa Bunge lipitishe bajeti kabla ya mawaziri kuhitimisha ili kutoa nafasi kwa wabunge kufuatilia na kuweza kusafiri. Spika akamjibu kuwa hoja hiyo ingefaa kama maafa yametokea karibu na Bunge kama Chamwino etc ili wabunge waende wakatoe damu .

Hali ni mbaya , Bunge linapitisha bajeti kwa suala gani?

update nyingine 2013
  • Kama kila linalosemwa na Wabunge wa CCM ni jema na linapita wakati linalosemwa na Wabunge wa vyama vya upinzani linapingwa na kutupiliwa mbali,Bunge halina maana.


  • Kama Wabunge wa chama tawala wanaachwa kutumia lugha za kuudhi na wale wa upinzani wakitolewa nje ya Bunge na kutakiwa kuwasilisha maelezo,basi Bunge letu linakosa maana.


  • Kama ushahidi unaoletwa mbele ya Spika na Wabunge wanaotakiwa kuuwasilisha unafichwa na kunyamaziwa,Bunge letu linakosa mshiko.


  • Kama maazimio mbalimbali ya Bunge hayatekelezwi na yanapuuzwa,kuna maana gani ya kuwa na Bunge lenye nguvu ya kikatiba kuisimamia Serikali?


  • Ikiwa Wabunge wanakuwa mstari wa mbele kuongoza watu kupiga wenzao na kufanya vurugu(tukio la jana Dodoma),i wapi heshima ya Bunge?

Tujadili...
 
Kuanzia sasa natangaza rasmi kuna baadhi ya watu nitakuwa nasoma thread zao mojawapo ni wewe Salma25. Unanibariki sana. Mfano nakumbuka rai yako wakati wa uchaguzi wa Igunga, Arumeru na leo hii. Big up mdada.
 
Mama kigeugeu sn,anahitaji maombezi huenda anapepo wa kuchukia taifa,chama siyo kitu tena mama anatakiwa awe mtu wa taifa na si wa sisiem kwa nafasi aliyonayo.
 
Salma25 umeandika vizuri. Nakupa big up! Lakini binafsi nina shaka moja, je mbuzi atacheza chuni ya nyizi za gitaa lako? Kuna uchawi ambao ukiisha logwa hakuna tena dawa wala mganga wa kukutibu. Ukinywa maji ya bendera ya sisiem kamwe hutakaa uweze kutofautisha kati ya haki na dhulma na kwa kuwa kuna watu wasioweza kuhitimisha jambo kwa kumpaka mnafiki mafuta kwa mgongo wa chupa, mnahitimisha kwa kusema dawa ya mnafiki na msaliti ni kuvunjika shingo.
.
 
Yani anachonikera zaid ni pale mbunge anapomaliza kuongea na yeye anadakia na vijimaneno vya kebehi, natamani siku moja akiropoka ashtukie katandikwa ngumi ya taya kihere+here kitaisha
 
It is a wonderful piece.... Salute to you Madam!

Madame Speaker is a "Disgrace" to CCM, to herself, to Women na wananchi in Particular.... Toka mwanzo alitaka afanye ile kazi kwa kuonesha/kujionesha kua anaweza na NOTHING can go wrong. Akasahau na hakutambua kua haya mambo as much as yategemea ushauri katika jopo lake la pembeni la washauri Muhimu zaidi ni relying on one's Intelligence, Insticts and honor. Angetenda haki kwa kufuata what is right and what na what is wrong.... badala yake matendo yake ni kua she always wants to prove kua anaweza/yeye ndie yeye/yupo strong (ambayo haelewi maana yake for Ubabe sio kua strong).

Kwa upande mwingine naona tusimlaumu saana.... Ukweli ni kwamba HAWEZI, HAFAI, wala hana the intelligence required for the job. Huwezi kukimbiza upepo... kama HUWEZI - HUWEZI tu! Na kwa kweli as sad as it is to say... katika wanawake ambao wanawakilisha mahala mbali mbali katika nafasi nyeti hapa nchini... Katuangusha na katutia aibu. Sio kwa wanawake tu bali na Wananchi kwa Ujumla... she is useless kwa kweli.... Sad.
 
It is a wonderful piece.... Salute to you Madam!

Madame Speaker is a "Disgrace" to CCM, to herself, to Women na wananchi in Particular.... Toka mwanzo alitaka afanye ile kazi kwa kuonesha/kujionesha kua anaweza na NOTHING can go wrong. Akasahau na hakutambua kua haya mambo as much as yategemea ushauri katika jopo lake la pembeni la washauri Muhimu zaidi ni relying on one's Intelligence, Insticts and honor. Angetenda haki kwa kufuata what is right and what na what is wrong.... badala yake matendo yake ni kua she always wants to prove kua anaweza/yeye ndie yeye/yupo strong (ambayo haelewi maana yake for Ubabe sio kua strong).

Kwa upande mwingine naona tusimlaumu saana.... Ukweli ni kwamba HAWEZI, HAFAI, wala hana the intelligence required for the job. Huwezi kukimbiza upepo... kama HUWEZI - HUWEZI tu! Na kwa kweli as sad as it is to say... katika wanawake ambao wanawakilisha mahala mbali mbali katika nafasi nyeti hapa nchini... Katuangusha na katutia aibu. Sio kwa wanawake tu bali na Wananchi kwa Ujumla... she is useless kwa kweli.... Sad.

Is this Speaker having proper job description and smart objectives? are these objectives SMART [specific, Measurable, Achievable, Relevant and Time bound] enough? Where is she answerable to?
 
Hivi Hugh mama ana mime na watoto kweli? Mwanaume kutokuwa na uchunngu na nchi si ajabu sana, kwani hatafamilia huwa wanatelemeza na kwenda kufight! But sijaona mwanamke Mwenge watoto akawakana watoto wake kwani anakumbuka uchungu alioupata, sa nikimwangalia makinda Mapatano wasiwasi!
 
Tusimlaumu sana, hiyo post aliipata kwa njia ya "Viti Maalum", viti maalum vingi havipatikani kwa merit bali kwa upendeleo. CC ya CCM walisema this time wanataka Spika Mwanamke, maana wanawake wakiwezeshwa ... wanaweza!

Sikumbuki kwenye hiyo post alipambanishwa na nani, wakati mwingine huwa naona hata yule Mwalimu wa Shule ya Msingi Jenister Mhagama ana uwezo mkubwa kuliko hata Mama Makinda pamoja na usomi wake na kuwa kwenye politics kwa zaidi ya miaka 35 sasa.

Haya ndio madhala ya "Viti Maalum", huyu Mama atakuwa loyal kwa CCM kuliko hata kwa Wabunge waliompa kura, maana CC ndio iliamua kuwakata wanaume competent ili wampe mwanamke hiyo nafasi. Kwa hiyo bila msaada wa CC leo hii huyu Mama asingekuwa Spika. Kwa sasa analipa fadhila kwa waliomuweka hapo ambao ni CC kwa kushirikiana na mafisadi waliom-tip tangu mapema kwamba gombea then tutajua namna ya ku-fix mambo kwenye vikao vya uteuzi. Ogopa politics za CCM, na ndio maana tunaishia kupata magarasa kila kona!
 
Mkuu, I secind you,
Jenister ni mashine nyingine kabisa.
Ni mfano halisi wa walimu - sio hawa wa siku hizi lakini!!!:rolleyez:
Tusimlaumu sana, hiyo post aliipata kwa njia ya "Viti Maalum", viti maalum vingi havipatikani kwa merit bali kwa upendeleo. CC ya CCM walisema this time wanataka Spika Mwanamke, maana wanawake wakiwezeshwa ... wanaweza!

Sikumbuki kwenye hiyo post alipambanishwa na nani, wakati mwingine huwa naona hata yule Mwalimu wa Shule ya Msingi Jenister Mhagama ana uwezo mkubwa kuliko hata Mama Makinda pamoja na usomi wake na kuwa kwenye politics kwa zaidi ya miaka 35 sasa.

Haya ndio madhala ya "Viti Maalum", huyu Mama atakuwa loyal kwa CCM kuliko hata kwa Wabunge waliompa kura, maana CC ndio iliamua kuwakata wanaume competent ili wampe mwanamke hiyo nafasi. Kwa hiyo bila msaada wa CC leo hii huyu Mama asingekuwa Spika. Kwa sasa analipa fadhila kwa waliomuweka hapo ambao ni CC kwa kushirikiana na mafisadi waliom-tip tangu mapema kwamba gombea then tutajua namna ya ku-fix mambo kwenye vikao vya uteuzi. Ogopa politics za CCM, na ndio maana tunaishia kupata magarasa kila kona!
 
Is this Speaker having proper job description and smart objectives? are these objectives SMART [specific, Measurable, Achievable, Relevant and Time bound] enough? Where is she answerable to?

sanjo CV ya madame Speaker is Impressive on paper..... However that alone is not enough, for any Leader to be Great at what they do they also have to have inborn natural insticts and Intelligence to be able to Lubrically run the area they are committed and those within reach. She was Sitta's right hand for God sake! That alone ilikua tosha for her to perfom better... She has no excuse whatsoever of being such a blunder.
 
Tusimlaumu sana, hiyo post aliipata kwa njia ya "Viti Maalum", viti maalum vingi havipatikani kwa merit bali kwa upendeleo. CC ya CCM walisema this time wanataka Spika Mwanamke, maana wanawake wakiwezeshwa ... wanaweza!

Sikumbuki kwenye hiyo post alipambanishwa na nani, wakati mwingine huwa naona hata yule Mwalimu wa Shule ya Msingi Jenister Mhagama ana uwezo mkubwa kuliko hata Mama Makinda pamoja na usomi wake na kuwa kwenye politics kwa zaidi ya miaka 35 sasa.

Haya ndio madhala ya "Viti Maalum", huyu Mama atakuwa loyal kwa CCM kuliko hata kwa Wabunge waliompa kura, maana CC ndio iliamua kuwakata wanaume competent ili wampe mwanamke hiyo nafasi. Kwa hiyo bila msaada wa CC leo hii huyu Mama asingekuwa Spika. Kwa sasa analipa fadhila kwa waliomuweka hapo ambao ni CC kwa kushirikiana na mafisadi waliom-tip tangu mapema kwamba gombea then tutajua namna ya ku-fix mambo kwenye vikao vya uteuzi. Ogopa politics za CCM, na ndio maana tunaishia kupata magarasa kila kona!


Haya mambo ya kuwezesha wanawake yana Mipaka yake.... Hio ni wazi na hata JK, Viongozi et al wanaelewa hilo. Basi tu sababu tu wameshazoea "power abuse". Huwezi mpa mwanadamu yeyote nafasi kama "Speaker wa Bunge" kwa vigezo vya upendeleo na Kuwezeshwa... It is Crazy.

One thing I can vouch ni kua hata wao CCM wameona kua ni Mistake kubwa walifanya kumuweka Madame Makinda katika hio nafasi. Ukikumbuka wakati wa mchakato wa U-speaker, ilikua ni wazi kabisa kua Makinda alichaguliwa sio sababu ya kuwezeshwa bali kwa sababu tu ya Kuepusha Sitta kupata hio nafasi tena (just because the guy alikua haangalii Chama ama sura ya mtu when it came to matters of the Parliament, among other reasons/propagandaz).

Wakawa wameangalia tu hilo suala on the surface wakisahau kabisa kufanya utafakari wa timing (kua saizi Siasa zilikua zinawiva kwa kasi ya juu na Upinzani una nguvu kubwa hivo ilitakiwa a Strong reliable Parliament Speaker); wakisahau kabisa kuangalia Circumstances (ni wazi kabisa hio ni nafasi ambayo ni lazima madame awe challenged for kwanza ni CCM, wazi kapendelewa na tupo katika jamii ambayo a Woman has to work twice as hard to be appreciated). Kitendo ambacho hakija cost wananchii tu... Bali hata wao wenyewe CCM (Mfano halisi ni her remarks on JK na mambo ya posho wakati wa migomo wa madaktari dhidi ya Serkali iliyo kua contrary na tamko la JK that morning.... hana hata chembe ya busara - a catasrophy kwa nafasi aliyopo).
 
Hivi Hugh mama ana mime na watoto kweli? But sijaona mwanamke Mwenge watoto akawakana watoto wake kwani anakumbuka uchungu alioupata,
Binadamu tupo wa aina nyingi. Hujaona mwanamke analea mimba miezi 9 halafu anatupa mtoto chooni, kwenye mfuko wa rambo; anazaa, analea, ikifika wiki, miezi, miaka anatupa mtoto?

Huyu Mama anaweza kuwa wa aina hiyo au kubwa zaidi, anaweza hata kuwa mchawi. Mchawi hutoa kikoa (mtu) wake kwanza. Huyu Mama amewatoa kikoa wanawake wenzake na Watanzania kwa jumla.
 
Back
Top Bottom