Dada yangu
AshaDii
Tatizo la CCM ni kwamba huwa wanatafuta majibu mepesi kwa maswali magumu. Kuhusu hiyo nafasi ya Spika, CCM was supposed kuteua mtu makini, mwenye uelewa wa kutosha na anayeweza ku-counter hoja za wapinzani kwa namna ambayo haiwezi kukiweka Chama au serikali au Spika mwenyewe kwenye matatizo. Ukiangalia jinsi Madam Speaker anavyoendesha Bunge, tayari watu washaanza kusema heri ya Job Ndugui. Sasa kama Spika anaweza kufunikwa na Job Ndugai, basi hilo ni boya kabisa.
Shida ninayoiona kwa watu wa CCM ni kwamba huwa hawapendi kuweka mtu ambaye anaweza kuwaambia ukweli, na once ukianza kwenda kinyume nao watakuchukia na kukusukia zengwe ili uondoke. Mawakili wanaoshinda kesi, sio kwamba mtuhumiwa anakuwa hana kosa, bali ni namna ambavyo wanaweza kujenga hoja ya kumtetea mteja mpaka akaonekana hajatenda kosa. Sasa ukiweka Wakili Boya huwezi kushinda kesi, maana badala ya kukutea anaweza kuishia kukuangamiza. Hicho ndicho kinachotokea Bungeni chini ya uongozi wa Makinda na sasa hata Boyo jingine (Job Ndugai) anaonekana ana afadhali zaidi.
Anyway, kama anafanya damage kwa CCM nadhani CC watakuwa wamejifunza, next time hawatakuja kurudia kuweka boya kwa visingizio ambavyo havina kichwa wala miguu, may be watakuwa makini.
Kwa kifupi Strategists wa CCM wameishiwa, kila move wanayofanya ina backfire.
Ila hapo mwishoni uliposema, "hana hata chembe ya busara" imebidi nicheke tu ....