Na ukisikia wamepata kazi utajinyonga?????dua la kuku halimpati mwewe, wao acha wabaki na hizo leseni unafikiri wewe ndio unajua kuliko wao????kalaga baho.JAMANI WAAACHENI WAENDEEEE, HUENDA HII DHAHAMA YA KUTISHANA YA KITOTO KABISA ITAISHA
Mimi nakubali kabisa hawa madaktari walikuwa hawanisaidii ntabaki natibiwa hata na Manesi au MaMedical ambao walipita huko JKT wanaujua Uzalendo, hao wanaojidanganya eti ataenda Botswana wakati Leseni yake imefutwa ni uongo Mtupu hawatapokelewa,
- Kwanza ni lazima Ubalozi wetu uwachuje,
- Pili Nchi za wenzetu huwezi kumgusa Raia wao na kumuandikia sindano wakati huna Leseni toka nchi uliosomea au cheti cha Chuo husika
- Hao Madaktari tuwaombee safari njema kuna kazi nyingi tu huko hata km si za Udaktari wakafanye
- Ni kweli walikuwa sio wazalendo maana walitaka kujipima na wabunge, hivi na Wahasibu Mainjinia wanajeshi, Polisi wanasheria nao wafanye hivyo?
- Acheni waende wametumwa hao tutawasiliana nao humuhumu JF wakitutukana lakini msg send na picha imefika THE END tusubiri mgomo wa wengine, Wakulima
Kufuatia mgomo wa madaktari wa hivi majuzi pamoja na uamuzi wa kuwafutia leseni baadhi ya madaktari waliogoma, wimbi la madaktari wameamua kukimbia nchi na kwenda kufanya kazi nje ya nchi...Habari zenye uhakika kutoka katika baadhi ya balozi za nchi wanachama wa SADC hapa mjini dar es salaam zinasema kumekua na wimbi la madaktari kukimbilia nchi za Namibia, Zimbabwe, South Africa, Botswana, Lesotho na Swaziland. ambako maslahi ni mazuri tofauti na huku kwetu bongo..
Mpaka sasa idadi rasmi ya madaktari waliokimbia ni 50 lakini inavyoelekea idadi ni kubwa zaidi ya hii kwani wapo wengi mno wanaoondoka kimya kimya bila taarifa.
"exodus of medical specialists has peaked over the past week in response to what the professionals see as the arrogance and vindictiveness of senior state officials." says The Tanzania Medical Association
" we pleaded with the doctors not to leave due to the invaluable services they offered. But the doctors said it was the only alternative given the government was in no hurry to resolve the situation" said Namala Mkopi, president of the Medical Association of Tanzania
Katika hatua nyingine serikali imeamua kutenga sh billion 200 kama gharama ya kuleta madaktari wa dharura huku gharama ya kumsomesha daktari mmoja kwa miaka mitano inakadiriwa kufikia millioni 100
SOURCE: gazeti la The EastAfrican
MY TAKE:
kuingiza siasa kwenye mambo ya taaluma na kutunishiana misuli kunakofanywa na WAKUBWA kutaiathiri sana hii nchi
serikali imemwaga mboga wao wamemwaga ugali...
Muhimbili Ina daktari wa upasuaji wa watoto mmoja tu.
Kutokana na manyanyaso ya SERIKALI kwenye mgomo huu wiki iliyopita katangaza kuacha kazi Muhimbili.
Inachukua si chini ya miaka 12 kama utabahatika kusoma moja Kwa moja bila kusimama baada ya kumaliza form six kuwa paediatric surgeon.
Watoto wenye matatizo mbalimbali waliokuwa kwenye list ya kufanyiwa upasuaji hawatapata hiyo huduma labda hao wanasiasa waje wawafanyie hao wagonjwa operesheni. Bahati mbaya hata wakienda kutafuta nje paediatric surgeon ni wachache sana.
madai yalikuwa 8,hayo mengine wameongeza kina mwinyi na wenzao. Hivi wewe, kupunguza viongozi kwenda nje ilid fedha ziboreshwe haikusaidii? Nyumba ya daktari ikiwa karibu na hosp ili asichelewe haikusaidii? Daktari akiwezeshwa vizuri ili akuhudumie with full conc haikusaidii? After all kila mtu atapigania haki yake.
Umenena vema sana,ni kwa vile wale wasioelewa hili,naamini wana nta masikioni.Mkuu, hivi unadhani tuna watu wenye akili humo serikalini??
tiba si sawa na ufundi mwingine wowote.... daktari hawezi kutibu bila kuwasiliana directly na mgojwa na ndio maana kila nchi inalinda madaktari wake, na kama inapokea wageni basi lzima wasome, wafanye mitihani na wafaulu. In the US alone dr anaweza kufaulu clinicals na akafeli TOEFL hata kwa miaka mitatu na kuendelea... Lengo ni kuweza kuwasiliana vyema na wateja/wagonjwa
hata wanaotibu wanyama, huwasiliana na wanyama hao kabla ya kutibu vizuri, ni utaalam maalum
Leo ukileta Dr. toka iran utawasiliana vipi?? ukiweka mkalimani, ile privacy ya mgonjwa inakua wapi??? what about "lost in translation"?
OUR GOVERNMENT IS FAILING HERSELF, HAKUNA VIAPO MTU KUWA KARANI, LAKINI KUNA VIAPO MTU KUWA DAKTARI!!! SASA UNAPOWACHUKULIA WALIOAPA POA, BASI NA WANAKUONA DADA POA TU, AND THAT IS WHERE OUR GOVERNMENT IS RIGHT NOW
THE WRITINGS ARE ON THE WALL.... AND GUESS WHAT, IT ISNT PRETTY
sion kama kuna ubaya kama madai ya vifaa yamejitokeza mara moja,,,,,,,hakuna asotaka maisha mazuri bhana,,,,waache wapigane nao waishi kama wanavoishi wezi halali(wanasiasa)
Mkuu unalo jibu sema maana nimesoma hoja ya mtoa mada ili nipate kuelewa tunazungumzia watu gani.unahitaji kutafuta maana ya daktari kwanza.
Katika hatua nyingine serikali imeamua kutenga sh billion 200 kama gharama ya kuleta madaktari wa dharura huku gharama ya kumsomesha daktari mmoja kwa miaka mitano inakadiriwa kufikia millioni 100
Umesema ukweli mtupu lakini sasa hawa wanaondoka sii nao watakutana na matatizo hayo hayo huko wanakokwenda kama ya Wairan kuja hapa?. Kwa nini tumwapongeze hawa wanaoondoka kwa kufuata malipo bora zaidi lakini tunawakashifu wale wanaokuja kwa Uzalendo wao kuponya watu ktk mazingira magumu zaidi!..Mkuu, hivi unadhani tuna watu wenye akili humo serikalini??
tiba si sawa na ufundi mwingine wowote.... daktari hawezi kutibu bila kuwasiliana directly na mgojwa na ndio maana kila nchi inalinda madaktari wake, na kama inapokea wageni basi lzima wasome, wafanye mitihani na wafaulu. In the US alone dr anaweza kufaulu clinicals na akafeli TOEFL hata kwa miaka mitatu na kuendelea... Lengo ni kuweza kuwasiliana vyema na wateja/wagonjwa
hata wanaotibu wanyama, huwasiliana na wanyama hao kabla ya kutibu vizuri, ni utaalam maalum
Leo ukileta Dr. toka iran utawasiliana vipi?? ukiweka mkalimani, ile privacy ya mgonjwa inakua wapi??? what about "lost in translation"?
OUR GOVERNMENT IS FAILING HERSELF, HAKUNA VIAPO MTU KUWA KARANI, LAKINI KUNA VIAPO MTU KUWA DAKTARI!!! SASA UNAPOWACHUKULIA WALIOAPA POA, BASI NA WANAKUONA DADA POA TU, AND THAT IS WHERE OUR GOVERNMENT IS RIGHT NOW
THE WRITINGS ARE ON THE WALL.... AND GUESS WHAT, IT ISNT PRETTY
Mkuu FJM nchi nyingine duniani zinawathamini watalaamu mbali mbali toka Tanzania wakiwemo madaktari. Waache waende kule wanakothaminiwa watalipwa vizuri na kupewa vitendea kazi vya kileo na hivyo kuwawezesha kufanya kazi zao katika mazingira bora zaidi.
Mwenyezi mungu amesikia kilio cha wanyonge, madaktari wakatili hao ametuepushia. Waende huko wakajiuze.