Madaktari waanza kuikimbia nchi..

Madaktari waanza kuikimbia nchi..

Yaonyesha wewe ni mbumbumbu kwelikweli katika yanayoendelea, au umechagua umeamua kutumika;
Si mara ya kwanza kwa madaktari kuondoka nchini, tena wale ambao tu ndio wamemaliza shule hata internship hawajafanya, nafahamu fika kwa kuwa nina jamaa zangu tuliosoma nao sekondari walitimkia kusini

  • Kamwe ubalozi wetu huko hauhusiki kuwachunguza
  • wanachohitaji ni vyeti vyao vya shule na ubongo wao kufanya mitihani ya usajili (katika baadhi ya nchi kama Botswana, Afrika Kusini, USA). Kama hajafanya internship anafanya huko na anasajiliwa, kama alishafanya, anafanya mtihani na kusajiliwa
  • Ni kweli kuna kazi nyingi huko sio zile za kutibu moja kwa moja, kama tu ilivyo hapa. We jiulize kuna chuo kama Muhimbili kila mwaka kinatema si chini ya 80 plus vyuo vingine wote hao wanakwenda wapi mbona mahospitalini mikoani hatuwaoni? Wapo kwenye taasisi na miradi mingine inayohusiana na afya ambayo wala hawahitaji kuwa na usajili (kufanya Internship) ili kufanya kazi hizo! Hata wizarani wapo (Mwinyi akiwa kinara wao hakumaliza internship yake muhi2)
  • Daktari anaweza kuwa mbunge lakini kamwe mbunge yeyote tu hawezi kuwa daktari, injini etc, kokote duniani kazi za kitaaluma kama madaktari wanalipwa zaidi kuliko wanasiasa kama wabunge na beurocrats (refer UK, Germany etc). Ndio maana wameweza ku-retain skilled labour force yao, nyinyi maskini halafu mnaipoteza na kuona sawa.... Kwa upumbavu wenu wa siasa za maji machafu
  • Kwa yeyote kuendelea kufikiri kuwa eti madai ya madaktari ni kwamba wametumwa na watu fulani, either mwenye kufikiri hivyo ni punguani asiyeweza kufikiri (na hivyo kufikiri wote wako kama yeye) au umetumwa kulamba uozo wa uchemfu wa mabwana zako wa serikali!

Mkuu mweleze huyo gamba, asiyejua hata utaratibu wa kusafiri nje ya nchi, ati lazima ubalozi wetu uwachuje! Mwisho wake atasema ubalozi wetu hautawapa viza!
 
Umesema ukweli mtupu lakini sasa hawa wanaondoka sii nao watakutana na matatizo hayo hayo huko wanakokwenda kama ya Wairan kuja hapa?. Kwa nini tumwapongeze hawa wanaoondoka kwa kufuata malipo bora zaidi lakini tunawakashifu wale wanaokuja kwa Uzalendo wao kuponya watu ktk mazingira magumu zaidi!..

Jamani serikali yetu imeshindwa kutuletea maisha bora na hali hii ipo kwa kila mfanyakazi nchini toka huyo Karani unayemsema hakufanya kiapo lakini ana umuhimu wake sana tu kwa sababu huwezi kumwona Daktari utibiwe bila kupitia kwa karani, akiondoka huyu Karani sidhani kama daktari ataweza kazi zote..Tunahitajiana sote hakuna mbora zaidi, na swala la mishahara bora nchini ni janga la watumishi wote wa serikali...

nchi hizi ambazo hawa madaktari wengi wanaenda angalau wananchi wao wengi wanaongea kiingereza sasa hawa wairan wakija hapa bongo watakuwa wanatibia wanaojua kizungu au kiarabu tu au?fikiria hapa!

Huko wanakoenda mazingira ya kazi yameboreka kulinganisha na Bongo ndugu! hata hapo rwanda tu maisha ya binadamu na afya yake inathaminiwa sana yaani wametuacha mbali sisi nchi tajiri duniani

Sasa swali lingine hili, yaani wewe kulipwa kamshahara kaduchu wakati wengine wanakula mkate wa taifa na huku wengine wakila makombo that is majority of tanzanians kwako ni poa tu au?

Labda kama na wewe ni among the ccm mafisadi i will understand ila kama ur a common citizen then ur brain is rotten
 
Ushabiki wetu utaponza wengi na tutegemee mengi madhara mengi zaidi
Muda utaongea yupi aliyesahihi
Hata siku moja Ukweli na Uongo haukai pamoja
Ujuzi/ Utalaam na Ubabaishaji haukai pamoja
Kama hospitali zetu zina mahitaji yote au hazina patajionesha tu
Kama hospitali zetu zina madawa ya kutosha au hayana pataonekana tu
Kama hospitali zetu zina vitanda au hazina patajulikana tu
Kama madaktari walihitaji maslahi yao au la patajulikana tu
Kama mama zetu,dada zetu na nk wanapata huduma za uzazi bure au patajulikana tu
Wanaoshabikia madaktari kuondoka wakisema wauaji kama kweli walikuwa wauaji au la patajulikana tu
Kama madaktari wa kukodisha wanatufaa au hawatufai patajulikana tu
Kama madaktari walikuwa ni waongo au wa wakweli patajulikana tu
Kama kweli walikuwa na dai moja la posho/mishahara au la patajulikana tu
Kama kweli wanakimbia nchi au la patajulikana tu
Kama kweli vyombo vya habari vilisema ya kweli au la patajulikana tu.
"THE TIME WILL TELL US THE TRUETH" MUDA UTASEMA UKWELI JUU YA YOTE YANAONGELEWA HAPO JUU
Kama kweli au si kweli. Kwasasa tusilaumiane kwani hakuna asiyehitaji maisha bora na akiamua ameamua kwa faida yake na familia yake ndo maana alisoma kama wewe unaona wanafanya vibaya peleka mwanao,ndugu,nk akasomee na afanye yale unayoona kwako yanafaa kwani muda ni mfupi tu (miaka ya msingi 7+ sekondari 4+ sekondari ya juu 2+ udaktari 5+ Intership 1) na atakukuta bado uko hai na kama unaumwa atakukuta bado unaumwa kidigokidogo ili awahi kukuktibu kwa muda huo mdogo. Au una anaweza kuanzia sekondari ndo pafupi zaidi
Lakini kama ni miaka na si dakika basi tutegemee madhara zaidi na si faida na kwa wanyonge tusiokuwa na uwezo hata wa milo miwili kwa siku tutakufa wengi ili kulipia ushabiki wa wachache wenye uwezo wa kwenda India na kwingineko.
 
Kufuatia mgomo wa madaktari wa hivi majuzi pamoja na uamuzi wa kuwafutia leseni baadhi ya madaktari waliogoma, wimbi la madaktari wameamua kukimbia nchi na kwenda kufanya kazi nje ya nchi...Habari zenye uhakika kutoka katika baadhi ya balozi za nchi wanachama wa SADC hapa mjini dar es salaam zinasema kumekua na wimbi la madaktari kukimbilia nchi za Namibia, Zimbabwe, South Africa, Botswana, Lesotho na Swaziland. ambako maslahi ni mazuri tofauti na huku kwetu bongo..

Mpaka sasa idadi rasmi ya madaktari waliokimbia ni 50 lakini inavyoelekea idadi ni kubwa zaidi ya hii kwani wapo wengi mno wanaoondoka kimya kimya bila taarifa.

"exodus of medical specialists has peaked over the past week in response to what the professionals see as the arrogance and vindictiveness of senior state officials." says The Tanzania Medical Association

" we pleaded with the doctors not to leave due to the invaluable services they offered. But the doctors said it was the only alternative given the government was in no hurry to resolve the situation" said Namala Mkopi, president of the Medical Association of Tanzania

Katika hatua nyingine serikali imeamua kutenga sh billion 200 kama gharama ya kuleta madaktari wa dharura huku gharama ya kumsomesha daktari mmoja kwa miaka mitano inakadiriwa kufikia millioni 100

SOURCE: gazeti la The EastAfrican

MY TAKE:
kuingiza siasa kwenye mambo ya taaluma na kutunishiana misuli kunakofanywa na WAKUBWA kutaiathiri sana hii nchi
serikali imemwaga mboga wao wamemwaga ugali...


Siyo makosa yao mkulu wa kaya alwaambia wasepe
 
Ondoa habari za mafumbo na za kusadikika, kama una jambo lete hoja watu wajadili na si kuficha ficha, hii siyo facebook!

I hope jana umesikia issue ya Gwajima Mchungaji wa kule Kawe. I hope ushapata jibu.
 
Tumeruhusu viongozi wa ccm wajinga wachezee akili za watu wanaoaminika kuwa wanaakili kuliko wanasiasa, Maisha ni popote nao ni Binadamu wanahitaji thamani kama ilivo kwa watu wengine wenye thamani, Ujinga wetu ndo mauti yetu, tunayataka haya kwa kujiangamiza wenyewe. ukicheka na Ngedele utavuna mabua
 
Bilioni 200 kuleta madaktari wa dharura. Bilioni 200 kuboresha sekta ya afya nchini... Upande upi mzito?
 
Nani ni mzalendo? viongozi wezi wanapora mchana kweupe, wabunge na Mipasho posho nene na wengine ni kulala 2, kama wasira, majaji rushwa, polisi rushwa na kusindikiza mali za wizi, wananchi wako kimya watu wanapora mali za umma, Ninani Nimzalendo? nchi ipoipo kama haina mwenyewe unatafuta mzalendo? Ni wendawazimu kuwataka maDoctor wawe wazalendo ktk nchi inayoongozwa na watu wanaojaza matumbo yao 2
Kwahiyo usipopewa haya au yasipofanyika dawa yake ni kugoma? shida yenu hamna uzalendo na watanzania wenzenu
 
Nani ni mzalendo? viongozi wezi wanapora mchana kweupe, wabunge na Mipasho posho nene na wengine ni kulala 2, kama wasira, majaji rushwa, polisi rushwa na kusindikiza mali za wizi, wananchi wako kimya watu wanapora mali za umma, Ninani Nimzalendo? nchi ipoipo kama haina mwenyewe unatafuta mzalendo? Ni wendawazimu kuwataka maDoctor wawe wazalendo ktk nchi inayoongozwa na watu wanaojaza matumbo yao 2

Mkuu kumbe tunaongea lugha moja sasa kwani wengi wetu tunalalamikia mambo kama haya uliyotaja, usifikiri tunaridhishwa na utendaji wa serikali yetu isiyo makini. Ila hujajibu swali langu la pili kwamba dawa yake ni kugoma?
 
JAMANI WAAACHENI WAENDEEEE, HUENDA HII DHAHAMA YA KUTISHANA YA KITOTO KABISA ITAISHA
Mimi nakubali kabisa hawa madaktari walikuwa hawanisaidii ntabaki natibiwa hata na Manesi au MaMedical ambao walipita huko JKT wanaujua Uzalendo, hao wanaojidanganya eti ataenda Botswana wakati Leseni yake imefutwa ni uongo Mtupu hawatapokelewa,

  • Kwanza ni lazima Ubalozi wetu uwachuje,
  • Pili Nchi za wenzetu huwezi kumgusa Raia wao na kumuandikia sindano wakati huna Leseni toka nchi uliosomea au cheti cha Chuo husika
  • Hao Madaktari tuwaombee safari njema kuna kazi nyingi tu huko hata km si za Udaktari wakafanye
  • Ni kweli walikuwa sio wazalendo maana walitaka kujipima na wabunge, hivi na Wahasibu Mainjinia wanajeshi, Polisi wanasheria nao wafanye hivyo?
  • Acheni waende wametumwa hao tutawasiliana nao humuhumu JF wakitutukana lakini msg send na picha imefika THE END tusubiri mgomo wa wengine, Wakulima


  • MBUMBUMBU=kwenye red. anatumia masaburi kufikiri. waulize wenye profession yao wakupe facts. najua huna ubongo wa kufikiri, tumbo linakusumbuA!
 
KUna wakati family doctor wangu huku ughaibuni alikuwa mtanzania aliyesomea Muhimbili, ila sijui njia aliyopitia baada ya kumaliza Muhimbili hadia akafikia kufanya kazi huku ughaibuni. Tulikuwa tunakutana na kuchoma mishikaki nyumbani kwangu karibu kila week-end. Baadaye akahamia hospitali nyingine nje ya state ambako alipata maslahi mazuri zaidi kwenye eneo la infectious diseases.

Nina uhakika kuwa madakatari wote ambo serikali yetu imewakomoa watapokelewa sehemu nyingine za dunia na watatulia na kutumia taaluma zao vizuri tena kwa amani sana.

Man unapiga exam inaitwa USMLE "united states medical licence exam " step 1 to 3 kwa africa huko kuna kituo nairobi ...ukipass step one and two inatosha kufanya residency step three unafanya any time ukiwa kazini ...

Sikweli kwamba unahitaji kibali cha nchi au ruhusa toka serikalini. Ni wewe na ubongo wako na cheti kutoka chuoni
 
Back
Top Bottom