Mada maalum: Tuijadili Tanganyika

Mada maalum: Tuijadili Tanganyika

Kwa mapana yake
Tulipotoka
Tulipo na tuendako
Tupopatia tulipokosea na tulipoumizwa
Tulipopotea, tulipokengeuka, tuliporubuniwa na tulipojisahau
Tuwajadili pia wazalendo waliojaribu kuipigiania Tanganyika. Timu ile ya G55 original, Rev. Mtikila na Akina Mwabukusi kwa sasa

Tuyajadili kwa undani yale yanayosemwa kwa sasa.. Utawala wa mamluki .. Watu wasio na huruma na Tanganyika yetu.. Na tuhuma zisizosemwa kwa sauti
Tujadili kwa mapana namna wachache kati yetu walivyokubali kuiua Tanganyika kwa kukosa uzalendo na kupokea mafungu ya shekeli za laana
Hii ni mada ya Tanganyika kwa watanganyika.. Kama wewe ni mamluki kaa pembeni tafadhali

Una lolote la kuiambia Tanganyika? Karibu

Ref: Plato: Myth of the caveView attachment 3366497
Ni kupoteza muda wako tu, Tanganyika mumeizika wenyewe mumebaki kuwapa lawama wasiohusika.. hapa ni sawa na kupaka rangi upepo kijana, vunja muungano brick back your ghost country acha ulalamishi.
 
CCM wameiuza Tanganyika kwa Wazanzibari. Naipenda nchi yangu Jamhuri ya Tanganyika
 

Attachments

  • TANGANYIKA.jpg
    TANGANYIKA.jpg
    1.6 KB · Views: 10
  • MTANGANYIKA (2).jpg
    MTANGANYIKA (2).jpg
    53.6 KB · Views: 9
Si busara wala si uadilifu mnapozungumzia changamoto za Taifa lenu Tanganyika kisha mkawapa lawama wazanzibar

Si busara wala hekima kuwaona wanzibar wote ni wenye makosa kwa makosa ya mzanzibar mmoja

Huu ujinga pia niliuona X, watu mnaweka chuki kwa watu ambao nao kama watanganyika tu wanaathirika kama sisi tunavyoathirika

Lakini tuwe wakweli tu,je matatizo ya wananchi wa Tanzania yameanza hii awamu ya sita tu?

Unapojadili mambo jitahidi sana kuwa objective,kwakuwa objective utayaona mambo katika uhalisia wake lkn ukiwa tayar na Tanganyika yako mkononi lazima uteleta ujinga wa kuwalaumu wazanzibar wote
 
Mpaka sasa kusema ukweli hamna ambae anaweza kutupa faida tatu za muungano kwetu Tanganyika dhidi ya wenzetu wazanzibar

Tunatamani kumlaumu nyerere lakini hatujui kitu gani kilimsukuma kuiunganisha nchi na hao wenzetu.
 
NAOGOPA SANA
Tuna
Taifa la Tanzania halafu tuna Taifa la Zanzibar
Tuna nchi ya Tanzania halafu tuna nchi ya Zanzibar

Kwahiyo tunapata
Mipaka ya Tanzania na mipaka ya Zanzibar
Bunge la Tanzania na  baraza la wawakilishi Zanzibar
Serikali ya Tanzania na serikali ya mapinduzi Zanzibar
Jeshi la wananchi Tanzania na jeshi la kujenga uchumi Zanzibar
Bendera ya Tanzania na Bendera ya Zanzibar
Wimbo wa taifa wa Tanzania na wimbo wa taifa wa Zanzibar
nknk

Tanganyika iko wapi?
Tumebakiwa na vichache visivyo na sauti
Tanganyika law society
Tanganyika arms
Tanganyika library


Naogopa sana...‼❗❕
 
wengi labda hawaelewi jambo moja muhimu khs historia, zanzibar ni mali ya english monarchy na tanzagiza ipo kwa ajili ya kumlindia english monarchy zanzibar isichukuliwe na arabs kama oman, hivyo muungano hauwezi kufa kwa maana umesimikwa huko juu na wakubwa kwa maslahi yao, inaitwa indirect rule, someni historia ili muweze kuelewa mlipo na kwa nini mambo yapo jinsi yalivyo …
 
Ni kupoteza muda wako tu, Tanganyika mumeizika wenyewe mumebaki kuwapa lawama wasiohusika.. hapa ni sawa na kupaka rangi upepo kijana, vunja muungano brick back your ghost country acha ulalamishi.
Tofautisha mjadala na malalamiko..
 
Mpaka sasa kusema ukweli hamna ambae anaweza kutupa faida tatu za muungano kwetu Tanganyika dhidi ya wenzetu wazanzibar

Tunatamani kumlaumu nyerere lakini hatujui kitu gani kilimsukuma kuiunganisha nchi na hao wenzetu.
Chako chetu lakini changu changu
 
Mpaka sasa kusema ukweli hamna ambae anaweza kutupa faida tatu za muungano kwetu Tanganyika dhidi ya wenzetu wazanzibar

Tunatamani kumlaumu nyerere lakini hatujui kitu gani kilimsukuma kuiunganisha nchi na hao wenzetu.
Kuna kitu kimoja ambacho nakifahamu siku zote maamuzi ambayo umeyafanya nyuma ukija kuyatathimini utaona kuna kitu hakikuenda sawa au ulifanya makosa kwa maamuzi hayo

Ila kwa wakati ule maamuzi hayo yalikuwa ni sahihi,haya yapo hata katika maisha yetu ya kawaida,mfano ulipata shida ambayo ilikulazimu kukopa mkopo wa kausha damu,lkn ukija kujitathimini baadae utaona ulifanya ujinga

Kwahiyo naamini kwa wakati ule,maamuzi waliyofanya akina comrade Nyerere na comrade Karume yalikuwa maamuzi sahihi kutokana na mahitaji ya wakati ule

Sasa kizazi baada ya uhuru tunaona hawa wazee walifanya makosa,lakini hatupaswi kuwalaumu bali tunapaswa kutafuta njia ya kutatua mapungufu ambayo yamejitokeza
 
Tulipotoka tunapajua, tulipokuwa tunataka kwenda tunajua, ila hapa tulipo kuna WAHUNI wametufikisha makusudi ili watupoteze tusifike kule tunapotaka kwenda ili yao yawaendee, wanufaike zaidi.
 
NAOGOPA SANA
Tuna
Taifa la Tanzania halafu tuna Taifa la Zanzibar
Tuna nchi ya Tanzania halafu tuna nchi ya Zanzibar

Kwahiyo tunapata
Mipaka ya Tanzania na mipaka ya Zanzibar
Bunge la Tanzania na  baraza la wawakilishi Zanzibar
Serikali ya Tanzania na serikali ya mapinduzi Zanzibar
Jeshi la wananchi Tanzania na jeshi la kujenga uchumi Zanzibar
Bendera ya Tanzania na Bendera ya Zanzibar
Wimbo wa taifa wa Tanzania na wimbo wa taifa wa Zanzibar
nknk

Tanganyika iko wapi?
Tumebakiwa na vichache visivyo na sauti
Tanganyika law society
Tanganyika arms
Tanganyika library


Naogopa sana...‼❗❕
Unaogopa nini?

Kuna aina mbali mbali za muungano

Moja wapo ni huu wa kwetu,waazilishi waliamua kuwa na aina hiyo ya Muungano,kwamba kila upande utakuwa na Raisi wake na bendera yake

Kwahiyo mimi na wewe tumeyakuta hayo,kama haturidhiki basi tutafute namna ya kupaza sauti na kurudisha Tanganyika yenu

Kama wakubwa hawaoni haja ya kufanya hivyo na waona la kheri ni kuendelea kutatua changamoto kama wanavyofanya siku zote,basi tukae kwa kutulia
 
Tulipotoka tunapajua, tulipokuwa tunataka kwenda tunajua, ila hapa tulipo kuna WAHUNI wametufikisha makusudi ili watupoteze tusifike kule tunapotaka kwenda ili yao yawaendee, wanufaike zaidi.
Muliyatimba kuungana na wanzanzibar ambao hamkuwa ata na unasaba nao sijui kitu gani kilipelekea maamuzi ya ujimaa kama yale now you pay the price ..Nyerere hakuwaza kuna siku rais atakufa madarakani , angekuwa ana elimu ya ghaib angekipeperusha icho kisiwa .
 
Back
Top Bottom