Mabomu ya machozi yarindima tena Zanzibar leo

hivi wewe ni polisi mzuri sana ??? Wale watu 30 waliokamatwa na polisi wakafikishwa mahakamani wameonewa ?? Wewe kumbe unawajua waliochoma kumbe ni uamsho ??? Tafadhali fanya haraka ufike mahakamani uwaokowe hawa watu 30 na badala yake uiambie polisi iwakamate uwamsho
hawaitaji kuambiwa wanawajua na hao waliokamatwa pia ni uamsho,kwani unajua uamsho ina watu wangapi?hicho kikundi kinafanya mikutano msikitini kina watu wengi kuliko kawaida
 
wewe ndio muhuni mkubwa pumbavu sana
Hahahahah! Sasa hasira za nini? Unatetea maandamano ambayo hayana mpango? Mbona mmechoma makanisa watu hawakuandamana!!! Au mnadhani haki inapatikana kwa style hiyo, haya basi andamana! @$mbafu sana!
 
Polisi wanaendelea kutumia nguvu nyingi kutuliza watu hivi mpaka lini? Leo boko haramu wamechoma makanisa matatu nigeria, kwa nini serikali isiwasikilize hawa watu jamani?

Au kama inajua haitawasikiliza kwa nini isikivunje hiki mkikunde? Tutaendelea kuishi hivi mpaka lini?


Mkuu kichwa cha habari na hapo nilipokandamiza haviendani sasa sijui ulikuwa unatupa habari za Zanzibar ama Nigeria!
 
Kuwaruhusu Wazanzibari kujiita Nchi na pia kukaa kimya walipobadili katiba mwaka 2004 na kuifuta jina la Tanzania katika katiba yao ndio kosa letu kubwa. Wamejidanganya lakini na viongozi wa nchi kwa nini wamewaruhusu?
 
Viongozi wa uamsho wa ajenda pamoja na vigogo fulani wa chama na serikali. Hivo basi vijana wa zenji msikubali kutumika kutimia malengo msoyajua.
 
Ningelipenda kunukuu baadhi ya maoni lakini kwa kuwa ni mengi ingekuwa kuchuka nafasi kubwa, lakini baadhi ya niliyoyaona ni haya:
1 - Picha za "UAMSHO" wa leo ni tafauti na zile za nyuma za wafuga ndevu na vikanzu vifupi kama alama ya UAMSHO kwa hivyo nina wasiwasi na kile kinachozungumzwa.

2 - Inasemekana mabomu yalitokea Donge kwa Wadonge kupinga UAMSHO huko. Sishangai kwani kwani hata katika kampeni za chaguzi zilizopita Wadonge walikuwa wanawazuwia CUF kwenda Donge. UAMSHO=CUF? Inasemekana kuwa lao moja.
3 - Wengine mnadai wasikilizwe, sio vibaya lakini uhuni huu wa kuchoma makanisa moto na kuwatishia na kuwanyanyasa Wabara walioko Zanzibar, dawa yake ni mkong'oto tu tena wa nguvu.

4 - Wengine mnadai kuwa UAMSHO wanapaswa kutoa maoni yao kwa njia halali kupitia mchakato wa Katiba Mpya; msishau kuwa katika mchakato huo imeshaelezwa kuwa suala la Muunano lisiguswe, kwa hivyo kuwaambia hivyo ni sawa na danganya toto.

5 - Ninakubaliana na Mzee Mtei kuwa suluhisho ni kuitisha kura ya maoni, lakini hata kukiwa na kura hiyo ya maoni na matokeo yakawa NDIYO kwa kuvunja Muungano kwa asilimia kubwa, (tukitilia maanani kuwa asilimia kubwa ya Watanganyika nao pia hawautaki) bado UAMSHO wataendelea na madai mengine. Nina wasiwasi kuwa dhamira ya UAMSHO ni zaidi ya Muungano, na kama niko sahihi, iko haja ya kuwashughulikia ipasavyo. (Rejea Nam. 3 juu).

6. Suluhisho ni serikali kuwa na dhamira ya kweli ya KUTATUA KERO ZOTE ZA MUUNGANO, zilizopo na zinazoweza kutokea mbele, vyenginevyo kuzipuuza ni kuendelea kulea donda ndugu. Siku sio nyingi na Watanganyika nao watasema INATOSHA na HAPATAKALIKA.
 
Jamani hao watu wapewe nchi yao kama wanaitaka maana tusilazimishe vitu kijinga alafu madhara yakaja yakawa makubwa, hebu wawachie nchi yao zanzibar na sisi tubakie na tanganyika yetu ambayo CDM tutashinda kwa kishindo.
Mkuu hata tanganyika kuna vi-nchi vidogo vidogo vingi tuu....uchaga, usukuma, unyiramba, uislam, upagani, ukristo......sasa sijui cdm itashinda nchi ipi kwa kushindo???
 
hivi wewe ni polisi mzuri sana ??? Wale watu 30 waliokamatwa na polisi wakafikishwa mahakamani wameonewa ?? Wewe kumbe unawajua waliochoma kumbe ni uamsho ??? Tafadhali fanya haraka ufike mahakamani uwaokowe hawa watu 30 na badala yake uiambie polisi iwakamate uwamsho

Upeo wako wa kuelewa ni mdogo, subject hapa ni kwanini wachome makanisa ambayo hayahusiki kwa namna yoyote na muungano? si suala la kukamatwa watuhumiwa, je uamsho madhumuni yao ni nini? ni ugaidi? au kuvunja muungano? kama ni udini basi umekithiri kuwa ugaidi, bado wanastahili kuwaosama.
 
Mkuu Mvumbuzi,

Ni kweli Zanzibar hana mchango wowote katika pato la taifa badala yake Tanzania bara inatumia rasilimali zake kugharamia masuala ya ulinzi na usalama.Posho na marupurupu mengi ya viongozi wa wa Zanzibar yanalipwa na hazina ya Dar es Salaam.Usisahau hata deni la TANESCO wameshindwa kulipa hadi likafutwa kisiasa na waziri wetu wa Megawat Bwana Ngeleja.

Hakuna faida ya huu muungano sana sana Tanzania bara itaingia hasara nyingine ya kupokea ya wakimbizi muda mfupi baada ya kuwaachia visiwa vyao wajitawale wenyewe.Watachinjana kuliko wanyarwanda sasa hivi ni wamoja lakini nje ya muungano umoja wao utaparaganyika.



Uamsho wasikilizwe tunaogopa nini kuiacha Zanzibar ijitawale jamani. Contribution ya rasilimali za ZANZIBAR kwenye pato la taifa ni asilimia ngapi kiasi cha Tanganyika kupata uchungu wa kuiachia iende zake?
 
Naunga mkono kuvunjwa muungano na tuone haki hiyo waitakayo itapatikana? maisha ya hofu na mashaka ni sumu ya maendeleo. sioni fursa ya maendeleo kwa wanaofikiri kuwekeza Unguja, mara mia ukawekeza Pemba kuliko Unguja. Chondechonde JK waachie nchi yao, SMZ inaunga mkono kundi hili kama hujui basi tambua hilo.
 
KWA KWELI SASA TANZANIA INAKUWA KAMA SOMALIA AU AFGHANISTANI KWA HALI HII,HUKO ZNZ NIMEONGEA WABARA KAMA WANNE WANASEMA MAISHA NI YA HOFU KAMA VILE LABDA WAO NI WAUAJI WANATAFUTWA.kuna jamaa mmoja wa hapa ni msambaa kajenga huko znz in anasema hao hao uamsho mameamua kukata kabisa fensi yake makusudi kisa ni ili tu aondoke arudi kwao tanga,sasa maisha ya hivi kweli tutafika
Kwa nini na sisi wabara tusiwatimue wa pemba waliojazana kwenye taasisi zilizoko tanganyika? Wao wanashabikia wabara wauawe ama kuvujiwa nyumba zao huko visiwani wakati wanafanya kazi bara, hivi tunangoja nini kuwaomba warudi kwao hadi hapo suala la muungano litakapoamriwa na katiba mpya?
 
baada ya kaz kubwa ya kusoma comments zote humu nilichokingudua ni kwamba ndungu zetu WATANGANYIKA hamujui tuna dai nini
jawabu
mwaka 1964 rais wa tanganyika huru nyerere alimtaka rais wa jamuhuri ya watu wa zanzibar karume waunganishe nchi mbili huru .zikaunganishwa kufanya TanZania mwaka huo.
nyerere alinukuliwa akisema ikiwa wazanzibar kwa maslahi yao wataona muungano hauna faida katika maisha yao wakaamua kujitoa sitawapiga mabomu.
karume alisema muungano kama koti likikubana unalivua.
sasa wazanzibar tunaona muungano hauna faida tena na sisi tumeamua kujitoa TUNAITAKA SEREKALI ITISHE KURA YA MAONI KUHUSU MUUNGANO UWEPO AU USIWEPO ili ukweli ujulikane kama wengi wanautaka au la, kabla ya mabilioni kuteketea kwa katiba ya muungano ambao hautakiwi znz!(kikwete na serekali yake wanatupiga mabomu na kututisha WATAWAJIBIKA KWA WANACHOKIFANYA KWA WAZANZIBAR KAMA MUBARAK WA MISRI wakati ukifika)
jamani wazanzibar tuliukataa ukiristo kabla haujaingia bara wamishonari wakaomba kujenga kanisa tukawapa viwanja bure tukawasaidia kujenga kisha sisi tukenda kusali msikitini wazungu wakatushanga, wakaomba wapewe ruhusa ya kutangaza ukiristo bara wakaruhusiwa nendeni mkawabatize kwa hiyari yao msiwalazimishe wakasema sawa....leo wazanzibar tuyachome makanisa yaliyojengwa na ndugu zetu wa bara tulioungana nao tena na udugu wa damu...''ama kweli mbwa ukitaka kumuuwa mpe jina baya'' lakini mungu atawahukumu hawa wachoma makanisa na ukweli ataubainisha ujulikane hadharani ''kwani mwisho wa ubaya aibu''.......wanatuchimbia kisima wazanzibar ili wapate uhalali wa kutukandamiza na kutudhulumu DUNIA ikichekelea kama ingekuwa si mapenzi yangu kwa watanganyika wa kawaida ningeomba hilo wanalotuletea viongizi wenu mungu aligeuzie tanganyika mpambane wenye kwa wenye ili ile shari waiyonje vingozi mafisadi wafitinishaji ,wazushi hawa, lakini hapana lisitokee hilo bara wala visiwani.

tunaipenda zanzibar kuliko roho zetu
tutaipigania zanzibar tutamuangamiza adui yetu
kila alie mwezetu aungane nasi tuilinde nchi yetu
zanzibar daima ndio fahari yetu
karibuni ndugu zetu
''JAMUHURI YA WATU WA ZANZIBAR KWANZA''
 
baada ya kaz kubwa ya kusoma comments zote humu nilichokingudua ni kwamba ndungu zetu WATANGANYIKA hamujui tuna dai nini
jawabu
mwaka 1964 rais wa tanganyika huru nyerere alimtaka rais wa jamuhuri ya watu wa zanzibar karume waunganishe nchi mbili huru .zikaunganishwa kufanya TanZania mwaka huo.
nyerere alinukuliwa akisema ikiwa wazanzibar kwa maslahi yao wataona muungano hauna faida katika maisha yao wakaamua kujitoa sitawapiga mabomu.
karume alisema muungano kama koti likikubana unalivua.
sasa wazanzibar tunaona muungano hauna faida tena na sisi tumeamua kujitoa TUNAITAKA SEREKALI ITISHE KURA YA MAONI KUHUSU MUUNGANO UWEPO AU USIWEPO ili ukweli ujulikane kama wengi wanautaka au la, kabla ya mabilioni kuteketea kwa katiba ya muungano ambao hautakiwi znz!(kikwete na serekali yake wanatupiga mabomu na kututisha WATAWAJIBIKA KWA WANACHOKIFANYA KWA WAZANZIBAR KAMA MUBARAK WA MISRI wakati ukifika)
jamani wazanzibar tuliukataa ukiristo kabla haujaingia bara wamishonari wakaomba kujenga kanisa tukawapa viwanja bure tukawasaidia kujenga kisha sisi tukenda kusali msikitini wazungu wakatushanga, wakaomba wapewe ruhusa ya kutangaza ukiristo bara wakaruhusiwa nendeni mkawabatize kwa hiyari yao msiwalazimishe wakasema sawa....leo wazanzibar tuyachome makanisa yaliyojengwa na ndugu zetu wa bara tulioungana nao tena na udugu wa damu...''ama kweli mbwa ukitaka kumuuwa mpe jina baya'' lakini mungu atawahukumu hawa wachoma makanisa na ukweli ataubainisha ujulikane hadharani ''kwani mwisho wa ubaya aibu''.......wanatuchimbia kisima wazanzibar ili wapate uhalali wa kutukandamiza na kutudhulumu DUNIA ikichekelea kama ingekuwa si mapenzi yangu kwa watanganyika wa kawaida ningeomba hilo wanalotuletea viongizi wenu mungu aligeuzie tanganyika mpambane wenye kwa wenye ili ile shari waiyonje vingozi mafisadi wafitinishaji ,wazushi hawa, lakini hapana lisitokee hilo bara wala visiwani.

tunaipenda zanzibar kuliko roho zetu
tutaipigania zanzibar tutamuangamiza adui yetu
kila alie mwezetu aungane nasi tuilinde nchi yetu
zanzibar daima ndio fahari yetu
karibuni ndugu zetu
''JAMUHURI YA WATU WA ZANZIBAR KWANZA''

Poleni sana ndugu zetu kwa dhulma inayofanywa na viongozi wenye uchu kwa maslahi yao! nilishangazwa sana na Rais mstaafu Al-Hajj Ali Hassan MWinyi alipokuwa akibwatuka kumbe anakhofia kwamba muungano ukivunjika ataosa ulaji na watoto wake ambao wapo katika system, ama kweli unaweza kumuuza nduguyo kwa uchu tu ! nampa pole mzee mwinyi ambae namuona anaharibikia ukubwani amekuwa mung'unye anaharibikia ukubwani?

NAshangaa kwa nini serikali haitaki muungano ujadiliwe, HAPA NDIO PANAPOANZA MACHAFUKO! waruhusu ujadiliwe na kama watu hawautaki na uvunjwe na kama kuna kasro zirekebishwa, kauli ya kikwete kutaka muungano usijadiliwe ndio umezua balaa lote hili , hebu na kaa chini utafakari na uone umuhimu wa jambo hili kujadiliwa,

Ninshawishika kuamini kuwa kuna mkono wa watu wa magharibi katika hili, hapa kuna shinikizo lazima lakini mwisho wake lazima serikali ijue kuwa inasababisha MAAFA MAKUBWA HUKO MBELE!

Mwenye ez Mungu atakuwa nanyi na tupo nyuma yenu sisi ndugu zenu wa bara tukiwaombea mjiokoe!
 
Upeo wako wa kuelewa ni mdogo, subject hapa ni kwanini wachome makanisa ambayo hayahusiki kwa namna yoyote na muungano? si suala la kukamatwa watuhumiwa, je uamsho madhumuni yao ni nini? ni ugaidi? au kuvunja muungano? kama ni udini basi umekithiri kuwa ugaidi, bado wanastahili kuwaosama.

wewe mwenye upeo mkubwa wa kuona si umeona uamsho ndio walichoma makanisa ??? Ni kitu gani kinachokuzuia kwenda mahakamani na ukawaomba mahakama iwaachie wale watu 30 waliokamatwa na Polisi kwa kuchoma makanisa na badala yake waende wakawakamate uamsho????

munayaingiza kanisa kwenye biashara ya ndere munapokamatwa munayatia moto kuomba pesa ya sadaka kwa waumini https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/230825-askofu-mwingine-adakwa-na-unga.html
 
Mwalimu Julius Kambarage aliwahi kusema"UBUBISUBISU OBUWERE EKIRO KIRIMBURA" maana yake "Mfichaficha maradhi kilio kitamfichua".
 
Back
Top Bottom