Mabomu ya machozi yarindima tena Zanzibar leo

Mabomu ya machozi yarindima tena Zanzibar leo

Mkuu kama ukiwasikiliza vizuri wanataka na maili kumi za ukanda wa pwani ya Tanganyika uko tayari? Wapigwe tu kama noma iwe noma.

...Hivi unadhani hakukuwa na mpaka kati ya Zanzibar na Tanganyika kabla ya Muungano wa 1964?...
 
Hiyo sio dawa. Wanasema unaweza kumuua mjumbe lakini huwezi kuua ujumbe, au fikra ya mjumbe, you can never kill an idea.

Leo ni UAMSHO. Kesho ataibuka mwingine kubeba ujumbe, kubeba ile idea iliyoko vichwani mwa baadhi ya Watanzania, kwamba hawataki Muungano. Kwa hiyo, hata ungefuta usajili wao na kuwafunga, hata ungewapiga risasi UAMSHO wote, kesho hiyo idea itachipuka tena. Huo ndio ukweli. Martin Luther King, wa Marekani, alisema, "a truth buried to the ground will rise again"! Huwezi kuangamiza ukweli. Hata ungewapoteza, nini kufuta usajili, hata ungeficha milele viongozi wa UAMSHO wote, hiyo si dawa.

Dawa ni nini?

Nimesema "baadhi" ya Wananchi hawataki Muungano. Baadhi. Kinachotusumbua mpaka sasa ni, "baadhi" hao ni wangapi wetu? Jibu la hilo swali, ukipata jibu la hilo swali ndio umeanza kutafuta dawa!

Taso, suppose serikali ikiruhusu kura ya maoni juu ya Muungano na hao ambao hawataki Muungano wakawa ni minority Je kitafanyika nn ili hao wasiopenda Muungano waridhike.Mimi na amini serikali imeshanzisha mchakato wa katiba mpya kwa hiyo ni bora kila mtanzania akashiriki katika kutoa maoni juu ya muundo wa Muungano.

Tatizo la watu wengi ni kutokutambua matatizo tuliyonayo na hali ya umaskini wetu umesababishwa nanini, na nini tufanye kujikwamua mahali tulipo.

Muungano kuuvuja haiwezi kusaidia watu wa zanzibar kuridhika na wanachokitafuta maana wapo watakaoibua kutaka utawala washeria za Kiislamu zitumike wakati kuna wazanzibar wasio waislam, pia wataibuka wengine zanzibar ni yakina yahe wanyamwezi na wapemba watoke zenj.

So Muungano siyo tatizo na tunatakiwa kuujadili namna ya kuuboresha namna yakuwa sulubu mafisadi wanaorudisha nyuma maendeleo ya taifa letu.

UAMSHO ni vizuri wangefanya kazi ya kuamsha Roho za watu ambazo bado zinateseka na yadunia na kuwahimiza waislam kushika mafundisho juu ya neno upendo kwa watu wote.
 
Last edited by a moderator:
Kwa vile Tanzania tuna mchakato unaoendelea wa Katiba Mpya, Tume ya Warioba ipendekeze kura ya maoni, yaani referandum, ili Wazanzibari na Watanganyika waamue kama muungano uwepo au la.

Endapo ama Zanzibar au Tanganyika zaidi ya asilimia 50 hawataki muungano, basi hiyo Tume itoe ripoti moja juu ya Katiba ta Zanzibar na ripoti nyingine ihusu Katiba Mpya ya Tanganyika. Hakuna haja ya kulazimisha muungano.
 
Muungano ufe. Zenj ibaki kivyake!!!!!! Waislam watatuangamiza, imani zao zinawajengea chuki kwa makafiri na kuwa utapata thawabu kwa kuharibu mali za khafiri au kuwamaliza kuutetea uislam!!! Vunja hii kitu Muungano!!

Hata ukivunja Muungano magaidi yapo kila sehemu hata Tanzania bara waislamu wapo wengi tena kuzidi visiwani.So cha kufanya ni kuuboresha Muungano na serikali kusimamia utawala wa sheria.Dini iliyosafi ..................... nikujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.
 
Kwa vile Tanzania tuna mchakato unaoendelea wa Katiba Mpya, Tume ya Warioba ipendekeze kura ya maoni, yaani referandum, ili Wazanzibari na Watanganyika waamue kama muungano uwepo au la.

Endapo ama Zanzibar au Tanganyika zaidi ya asilimia 50 hawataki muungano, basi hiyo Tume itoe ripoti moja juu ya Katiba ta Zanzibar na ripoti nyingine ihusu Katiba Mpya ya Tanganyika. Hakuna haja ya kulazimisha muungano.

Mzee wangu ,Muungano ni lulu natunapaswa kuulinda kwa kila hali kinachotakiwa ni kutoa maoni juu ya kuboresha Muungano wetu uwe wa serikali moja na utawala wa majimbo , tuzike kuwa na SMZ na Zanzibar iwe ni jimbo,pemba jiomb,na bara tuwe na majimbo instead of mikoa Au tuwe na serikali 3, Zanzibar, Tanganyika na Tanzania
 
Hata ukivunja Muungano magaidi yapo kila sehemu hata Tanzania bara waislamu wapo wengi tena kuzidi visiwani.So cha kufanya ni kuuboresha Muungano na serikali kusimamia utawala wa sheria.Dini iliyosafi ..................... nikujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.

Ni kweli mkuu bemg, ila mimi naona waislam wa Zenj wameuweka sana uislam mbele, Waislam wa bara kidogo wako neutralized na wakristu, to some extent, kiasi kwamba hata kule zenj hawapendi waislam wa bara wanasema si washika dini. Kuna kisa cha binti zenj alipata mchumba wa kiislam bara na alikataliwa kuolewa kisa eti waislam bara si washika dini. Na waislam wa bara sina tabu nao sana, tumeishi kwa amani tu na wala hatuchomeani makanisa na majumba.

Lakini kule Zenji makanisa, mabaa, nk. Bara baa ziko kila kona hadi vibarazani na waislam wanachukua time zao wala hisikii wakiingilia mambo. Ninachorudia kusema zenj asili yao ni ya ugomvi. Kwani tukiachana kuna shida gani!! Wagawane mali kila mtu achukue ustaarabu wake. Kila siku Zenj wanaishi kwa tensio, why?
 
Wewe ulitegemea nini pale mkuu wa nchi alivyo mteua Mh. Dr wa kufoji ( Nchimbe) kuwa waziri wa mambo ya kunyumba? Haya ndi matokeo ya kuchukua nafasi muhimu na kuwapa wauza sura!!!! In short hatuna serikari!
 
Kwa vile Tanzania tuna mchakato unaoendelea wa Katiba Mpya, Tume ya Warioba ipendekeze kura ya maoni, yaani referandum, ili Wazanzibari na Watanganyika waamue kama muungano uwepo au la.

Endapo ama Zanzibar au Tanganyika zaidi ya asilimia 50 hawataki muungano, basi hiyo Tume itoe ripoti moja juu ya Katiba ta Zanzibar na ripoti nyingine ihusu Katiba Mpya ya Tanganyika. Hakuna haja ya kulazimisha muungano.

Well said mzee wetu. Kwa historia huu mungano ni taabu kubwa na wazanzibari hawautaki na hali ilianzia pale kwa mzee wetu Jumbe. Kwa kuwa historia inaonyesha hivyo, ni vema tusikilize maoni kwa pande zote mbili, bara na visiwani ili taarifa ya kina itoe uamuzi sahihi. Mpaka leo serikali tatu ndiyo muafaka tu, Tanganyika, Zanzibar na ya Muungano, tena masuala ya muungano yaangaliwe kwa kina na marekebisho yafanyike. Pia masuala ya muungano yawe machache zaidi ili kila nchi iweze kushughulika na masuala yake muhimu. Nchi hii iwe na demokrasia ya kweli, si mabavu na kulazimisha visivyowezekana!
 
Wakuu naomba kuuliza huyu Edwin Mtei ninaye muona humu jamvin ni Yule mwasisi wa CDM? Kama ni yeye nampa big up sikutegemea Mzee wa makamo haya awepo humu ndani?
 
Ni kweli mkuu bemg, ila mimi naona waislam wa Zenj wameuweka sana uislam mbele, Waislam wa bara kidogo wako neutralized na wakristu, to some extent, kiasi kwamba hata kule zenj hawapendi waislam wa bara wanasema si washika dini. Kuna kisa cha binti zenj alipata mchumba wa kiislam bara na alikataliwa kuolewa kisa eti waislam bara si washika dini. Na waislam wa bara sina tabu nao sana, tumeishi kwa amani tu na wala hatuchomeani makanisa na majumba.

Lakini kule Zenji makanisa, mabaa, nk. Bara baa ziko kila kona hadi vibarazani na waislam wanachukua time zao wala hisikii wakiingilia mambo. Ninachorudia kusema zenj asili yao ni ya ugomvi. Kwani tukiachana kuna shida gani!! Wagawane mali kila mtu achukue ustaarabu wake. Kila siku Zenj wanaishi kwa tensio, why?

Ni kweli waislam wa bara wanashika mafundisho ya dini yao na siyo waislamu wa zenji uswahili ni mwingi na wanashika mafundisho yasiyo sahihi kwa mfano aya moja kwenye Qur'an (Al -Qiyamah).

Lakini mtu anataka kufanya makosa (hata) katika wakati wa mbele yake kwa kiingereza wametafasiri hvi But man wishes to do wrong (even) in the time in front of him). kwahiyo hawa waislam kila wakati wanawaza kufanya makosa kwa kufikiri kwamba wanaonewa, wanachoma bar, kanisa kwa kufikiri kwamba bar, makanisa yameushikiria uislamu wao na Muungano.
 
Jamani serikali iwasikilize iwape hiyo nchi yaoooooo let them go jamani hawa watu ni hatari sana maana hawamumunyi maneno hata kidogo kwenye page yao wanasema moja ya kigezo cha kushindwa kujiunga na EAC eti wanawakilishwa na Tanganyika duh hawa jamaa wameona mbali hakika nilifikiri wapemba watarudi kwao kumbe wataendelea kuwepo maana wakijiunga na EAC kila kitu kinakuwa sawa mbona kasheshe hapo.
 
Wakuu naomba kuuliza huyu Edwin Mtei ninaye muona humu jamvin ni Yule mwasisi wa CDM? Kama ni yeye nampa big up sikutegemea Mzee wa makamo haya awepo humu ndani?

Mkuu ni vema umaliona angalizo hilo maana si sahihi kabisa kuchukua ID ya mtu maarufu kama yule halafu umsemee, haitakiwi na mods wanatakiwa wawe makini kwa hili. Ngona niwashtue mods.
 
Taarifa kutoka Zanzibar zinaeleza kwamba Polisi wamezima mkutano wa Jumuiya ya Uamsho kwa kuwapiga mabomu wafuasi wa jumuiya hiyo eneo la Mahonda visiwani Zanzibar waliokuwa wakielekea Dole kwenye mihadhara ya mikutano ya uamsho iliyokuwa ifanyike kwenye msikiti mmoja huko Dole.

Taarifa zinaeleza kwamba mabomu ya machozi yamerindima na kuipa polisi ushindi baada ya wafuasi wa uamsho kurejea mjini.

Uamsho umeendelea kuamka kupinga muungano.
 
Taarifa kutoka Zanzibar zinaeleza kwamba Polisi wamezima mkutano wa Jumuiya ya Uamsho kwa kuwapiga mabomu wafuasi wa jumuiya hiyo eneo la Mahonda visiwani Zanzibar waliokuwa wakielekea Dole kwenye mihadhara ya mikutano ya uamsho iliyokuwa ifanyike kwenye msikiti mmoja huko Dole.

Taarifa zinaeleza kwamba mabomu ya machozi yamerindima na kuipa polisi ushindi baada ya wafuasi wa uamsho kurejea mjini.

Uamsho umeendelea kuamka kupinga muungano.

Hivi hao polisi hawawezi kuwalaza kimoja!! Sorry!! Mwishowe watahamia bara, kwenye amani, hatutaki ugomvi. Waislam wetu wa bara tunapendana.
 
Lisemwalo lipo na kama halipo hakika laja!


Hv lakini hawa UAMSHO ni nini wanataka haswa?
 
Back
Top Bottom