Maazimio ya Wanakagera(KYL) kuelekea Kagera mpya

Maazimio ya Wanakagera(KYL) kuelekea Kagera mpya

Mkuu hata mie binafsi sielewi ndugu zetu wa hapo mjini mpaka sasa kusema kweli ndo wanatukwamisha make tayari tumejitoa kuwaghalamia gharama za vikao lakini haonekani hata mmoja hapa tena
Juzi M.Byabato kaja hapa akasema kusaidia na yeye yuko hapo mjini lakini simuoni tena naye ...lakini subiri kwanza ikishindikana kabisa tuna plan B ya hili jambo.

Hapa kuna tatizo na sijui ni nini! kama hapo mjini watu wakujitolea wamekosa labda tujaribu wilayani!
 
Hapa kuna tatizo na sijui ni nini! kama hapo mjini watu wakujitolea wamekosa labda tujaribu wilayani!
Nimesoma thread ya kurudishiwa uanachama wa madiwani wanane wa manispaa ya Bkb,naona wana Kagera tumekua baridi. Natumaini wengi walitamani watimuliwe ili wachaguliwe madiwani wanao weza sukuma mbele maendeleo.

Mkuu Rweye na wakuu wengine,mimi nimekaa nimetafakari sana,napendekeza kwenu wana Kagera tumuombe mama Anna Tibaijuka agombee ubunge wa Bkb mjini ktk uchaguzi ujao. Na kwa kuwa wagombea binafsi wataruhusiwa,tuanze kuwatafuta watu wanaofaa kuwa madiwani! Sina imani na wagombea toka vyama vya siasa!
 
Haya tuje hapa tutoe maoni/maazimio yetu juu ya nini tunafanya,tufanyeje,tuanzie wapi n.k ili baada ya hili zoezi kaka yetu Omutwale atuongoze kuelekea kwenye majukumu na utekelezaji

Tunaomba tutumie siku 3 kwanzia leo hadi J2 ili hatua inayofuata ianze,njooni nyote hapa mwambie na yule jirani ilimradi awe mwanakagera na aliye tayari kwa shughuri hii

Kwa mara nyingine tena karibuni sana ..Mnyegere ba tata na ba mawe!!!!

Wazo ni zuri sana.
Ila ningeshauri jukwaa hili lingekuwa kwenye Bukobawadau.com ingekuwa vizuri zaidi.
 
.....pia
1. Tuunde kamati ya kuhamasisha na kuhimiza wana-Kagera waishio nje ya Mkoa wa Kagera ili walau mara mbili kwa mwaka tuwe tunakutana katika Wilaya mojawapo ndani ya Mkoa wa Kagera kujadili na kuhamasisha maendeleo ya Mkoa.

2. Tutengeneze KATIBA maalumu kwa wana-Kagera ambayo itaweka misingi ya kumbana kila mmoja aishie ndani ya mkoa atakama si mzaliwa na yule ishio nje ya mkoa ambaye ni mzawa, kutambua umuhimu wa kuchangia maendeleo ya Kagera.
Hili lilikuwa ni wazo zuri sana kwa malengo yetu na tukumbuke maendeleo hayana likizo. Tuendelee kuyatafakari haya na kuyatafutia ufumbuzi, yatakuja na yatapita mengi lakini ni lazima Kagera isimame tena. Tunafanya na tunalazimika kufanya haya ili kuenzi historia ya mkoa wetu, historia haifi, historia hujirudia.

Karibuni tuendeleze mapambano. Buhaya root, Bukoba mpya n.k lengo letu ni moja tushikamane, tusaidiane. Na kama mwitikio ulivyo mzuri kwa miradi inayotengenezwa na Buhaya root, yeyote anayeweza kubuni vitu vya namna hii tumpongeze na tumsapoti lakini tumkumbushe na kumsaidia, hii miradi kama iko nje basi hima tusaidie iwe na tawi pale Bkb mjini ambayo ndo makao makuu yetu.
Karibuni kwa mara nyingine tena wanakagera, uwe mzaliwa, uwe mkaazi, uwe na ubini, uwe na kazi huko n.k ilimradi una connections na mkoa wa Kagera tunawakaribisha na tutawakaribisha nyote kwa pamoja.

Kagera mpya ni wajibu wetu, mimi wewe na jirani yangu/ yako.
 
Nimesoma thread ya kurudishiwa uanachama wa madiwani wanane wa manispaa ya Bkb,naona wana Kagera tumekua baridi. Natumaini wengi walitamani watimuliwe ili wachaguliwe madiwani wanao weza sukuma mbele maendeleo.

Mkuu Rweye na wakuu wengine,mimi nimekaa nimetafakari sana,napendekeza kwenu wana Kagera tumuombe mama Anna Tibaijuka agombee ubunge wa Bkb mjini ktk uchaguzi ujao. Na kwa kuwa wagombea binafsi wataruhusiwa,tuanze kuwatafuta watu wanaofaa kuwa madiwani! Sina imani na wagombea toka vyama vya siasa!


Mkuu kuna jambo uliligusia na linabaki kama changamoto kweli. Juzi ndugu yangu kanambia alishangaa kuona kwenye kikao cha BMC chini ya mbunge walikuwepo watu wachache sana na hata hao wachache michango yao ni ya wa lakini. Hawachangii kwa kumaanisha, wanaogopana na kuoneana aibu. Facts na aggression vinakosa katika masuala hayo ndo maana utakuta wengi hawaoni umuhimu wa vitu vya namna hii, wa kumbana mbunge hayupo, wa kuibana halmashauri hayupo. Kuna haja ya wananchi kuambiwa umuhimu wao katika taratibu za kimaamuzi na maendeleo, mkisusa mnajisusa wwnyewe na hakuna atakayekuja kuwafanyia zaidi ya kuendelea kulalama na kupoteza fursa.
 
Wazo ni zuri sana.
Ila ningeshauri jukwaa hili lingekuwa kwenye Bukobawadau.com ingekuwa vizuri zaidi.
Ndugu yangu ni kweli, utafikiria lipitie kule kama walau uliwahi kuona hiyo blog ikiwa mstari wa mbele kuliendeleza hili. Ukiingalia hata blog yenyewe kwa umakini mkubwa utagundua wala ajenda ya hivi haijawahi kufanywa wala kuonekana ni moja ya objective yao. Hata kama ipo basi itakuwa kwenye maandishi tu, matendo hayaonekani kokote pale
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom