Maandamano ya kumlaani Spika Makinda

Maandamano ya kumlaani Spika Makinda

kile ambacho CCM haihafanya for 50 years ni pamoja na kuzuia sauti za wananchi kutetea nchi yao kupitia bunge. CDM kuandamana kumpinga spika ina maana kuwa wanawasaidia watanzania wafaidi thamani ya mabilioni ya kodi zao zinazotumika kuendesha mhimili huu wa nchi.
Pili, CDM kuandamana kumpinga spika ni juhusi za kurescue fursa yao ya kutumia jukwaa la bunge kuwaeleza wananchi itafanya nini beyond 2015 ambacho CCM haijafanya kwa miaka 50. Kwa namna bunge linavyoendeshwa sasa CDM imepokonywa fursa ya kutumia jukwaa la bunge kujitangza.
Bw Pasco utakubaliana nami kuwa mic za bungeni zilisaidia sana kupaaza sauti kuhusu EPA, Richmond, BOT twin towers, Mramba+Yona+mgonja, mabilioni ya uswis, ngeleja+mhando+tanesco, twiga wa kia, mgao wa umeme na madudu mengi mengine.
Serikali ya CCM kupitia kwa Makinda na Ndugai wamezima mic za bunge kwa hiyo wananchi hatutapata tena nafasi ya kutetea nchi yetu kupitia bunge.
Je, Mr Pasco, tukae kimya?
Mkuu Tuko, nimekupata na nimekuelewa!.
P.
 
Kweli ila sheria ifuatwe katika kupata vibali vya maandamano la sivyo tusije poteza watu
 
Mkuu Mwita Maranya, asante nimekupata, nimeguswa, na sasa ninajitafakari, nikikata shauri, utajua tuu!.
Pasco.

Mkuu Pasco nashukuru kwa kunielewa. Natamani ukate shauri leo hii saa hii lakini bado najipa muda nikiamini kwamba tafakari yako itakupelekea kwenye kufanya uamuzi wa haki na busara kwa ajili ya kupigania mustakabali mwema wa nchi hii.

Nchi hii ni yetu sote sasa kama kuna mtu/watu tumempa/tumewapa dhamana ya kutuongoza lakini yeye/wao anaamua/wanaamua kutumia fursa hiyo kutupotosha ni lazima tumkatae/tuwakatae kwa nguvu zote kwakuwa tunaoathirika na udhaifu wa serikali ya ccm na sera zake ni sisi sote huku baadhi ya watu wachache sana wakiogelea katika neema inayotokana na rasilimali za nchi hii ambazo kimsingi zilipaswa kutunufaisha wote.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Arushaone huyu Pasco wakati mwingine anapenda tu kuanzisha ligi bila sababu ya maana. Mubarak alikuwa na jeshi lenye nguvu kuliko yote katika Afrika lakini kupitia maandamano nguvu ya umma ikampiga chini. Na hili la maandamano kuangusha madikteta na mafisadi limetokea nchi nyingi tu duniani. Imagine ile hali iliyotokea Mtwara hivi karibuni na kuitikisa Serikali iwe nchi nzima. Msanii na mafisadi wenzie lazima waikimbie nchi.

Pasco. Kama hujawahi kuona nguvu ya maandamano huishi dunia hii. I swear it won't be the same again!
 
Last edited by a moderator:
Mwanamke mpumbavu huivunja nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe mwache BINTI KINDA aivunje CCM kwa mikono yake mwenyewe
Ila kumbuka ndoa ikivunjika watoto ndio wanaopata taabu wanakuwa wahanga wa kwanza.Huyu bi Kiroboto kasahau majukumu yake kabisa.
 
Hakuna haja yakuandamana,tuwafunze watu juu ya ukatili huu wa wazi ili waje kuamua miaka miwili ijayo
 
Najua yapo mambo mengi ya kuandamana kwa sasa. Hata hivyo mi nadhani hili la bunge kuendeshwa ki-hovyo hovyo na Spika Makinda ni kubwa na jambo la hatari sana kwa maendeleo ya taifa letu. Nawashauri CHADEMA, na wote wanaokerwa na mama huyu, wafanye maandamano nchi nzima au sehemu kadhaa za nchi, kulaani uendeshaji mbovu wa bunge unaofanywa na spika. Ingawa najua haitafanya aondolewe madrakani, naamini itamoa msg, na itamfanya ajue kuwa anachokifanya bungeni kinawaudhi wengi. Mi nadhani kwa sasa anadhani kuwa hajashtukiwa kuwa anaendesha bunge visivyo, so akiona maelfu wameandamana kumlaani, atapata funzo fulani/

------------------------------------------------------------------------------------
------------------------------------------------------------------------------------

UPDATE

Nimefuatilia kwa karibu jinsi mama huyu anavyoendesha kikao cha bajeti, na ukisoma taarifa ya jinsi anavyomkingia kifua Pinda, naona bado haya maandamano hayaepukiki.

mwaka huu mpaka ajikojolee
 
Back
Top Bottom