Maandamano makubwa Songea!

Maandamano makubwa Songea!

Poleni sana wafiwa, ila tuokote silaha zao za ujasiri, mapambano yaendelee. Mpaka kieleweke.
 
Kweli kabisa watu 56 ndio wameshindwa kudhibitiwa na polisi bila kuwafyatulia risasi? kweli wengine tumesema hili jeshi linahitaji kuvunjwa na kuundwa upya bado lina mawazo ya kikoloni sana!
Mkuu taratibu zetu au tuseme katiba yetu ni mbovu, inatakiwa kueleweka wazi ni hatua gani zichukuliwe kunapotokea maandamano, makusanyiko, shughuliyoyote yenye watu wengi kama sherehe!!!!! Sio jeshi eti la polisi linatawanya maandamano tena ya amani bila vurugu zozote kwa risasi, serikali na katiba haithamini wananchi, inatakiwa polisi aliye toa amri watu wapigwe risasi apelekwe mahakamani kujibu mashitaka ya kuua!!!! Mbona wanaua na ni kimya, kifo chetu ni katiba mbovu isiyo na uzito namsisitizo wa kulinda raia na mali zao!!!! Mwananchi anatakiwa kuheshimiwa sio kuuwawa kama kuku, kiongozi mkuu wa nchi anatakiwa awajibike pindi polisi wanapo wauwa raia bila hatia!!!! KATIBA MPYA YENYE MAMLAKA ITAKUWA MKOMBOZI WA WATANZANIA!!!!!!!

 
Ndugu zangu, kutokana na jeshi la polisi jana kuua kwa "makusudi" wananchi waliokuwa wanaandamana kupinga mauaji ya wananchi yanayoendelea pasipo jeshi la polisi kuchukua hatua yoyote, huu ndio ukweli na sio maelezo ya RPC-Ruvuma MICHAEL KAMUHANDA alivyodanganya Taifa.

Mosi, RPC anasema kuwa maandamano yale yalichochewa na ushabiki wa kisiasa huku akidai waandamanaji walipiga mawe ofisi ya CCM. Ndugu zangu hapa RPC kadanganya, waandamaji wengi walikuwa madereva wa pikipiki (boda boda) ambao ndio waathirika wakubwa wa mauaji yale na sio CHADEMA, pili, kamanda anadai walifanya maandamano bila kuomba kibali, uzuzu mwingine wa RPC ni huu, hivi polisi ndo wanaolalamikiwa then utoke ukaombe kibali kwao(polisi) ili uende kwa RC kuwalalamikia polisi.

Kituko eee! Halafu RPC asiwe mbumbumbu wa sheria. Polisi hawaombwi kibali cha maandamano bali wanapewa taarifa ya muda, madhumuni na kutakiwa watoe ulinzi kwa waandamanaji. Mwisho RPC anataka ajifiche ili aonekane ameua ili kulinda CCM (watawala) dhidi ya CHADEMA ili asihojiwe na watawala kwa mauaji aliyofanya.

Mbunge wa songea mjini Dr.Emanuel Nchimbi (0754 033388) RPC-Ruvuma (0754 252415) . Said mwema(0754 705557). Je hawa ni watu au miungu wenye haki ya kuua?
 
RPC amejisahau sana huyu hapo ndio utajua vilaza waliomo jeshi letu la mtu mmoja mzee wa intelijensia kazi ipo jeshi halina control tena
 
Kiukweli tanzania ni nci yangu kweli lkn nikikumbuka mambo yake naichukia
 
Ukweli ni kwamba Tanzania yetu itaanza kuombewa amani muda si mrefu!serikali ina dharau sana watu wake tangu wawapake mafuta kwa mgongo wa chupa ati wana 'amani'..ujinga mtupu!!!imeanza songea,ningekuwepo huko nami ningeua askari hata kwa kumvizia tu japo ni makosa na dhambi pia!
 
Mimi Nimejiuliza Hadi Machozi kwa sasa Yananitoka!! Mauwaji Yamekithiri!! Jeshi la polisi ni walinanda amani, Watu wanaandamana kuomba walinda amani wawaongezee Ulinzi!! Walinda Amani wanawaua!! Jamani Tanzania Tumefikia Hapa!! Mtu akiandamana Kwenda kwa Mtawala wa Eneo, Si unamruhusu ila unahakikisha Hasabishi Madhara?
Ok sasa hawa Vijana Wanatuhumiwa Kupiga mawe Jengo la Chama Fulani!! Je adhabu yake ni kifo!! Je Tanzania Tumefikia Hapa!!

MACHOZI YANANITOKA NAOMBA NIISHIE HAPA
 
Hayo ndo mafunzo ya polisi wale wasiokua na kazi (FFU)waliyopata pale ccp moshi tuwalaumu wale waliowapa mafunzo huenda ndo waliwaelekeza njia ya kuzima maandamo ya raia wasiokua na silaha ni kutumia silaha za moto tu
Mi napendekeza hawa askari wasiokua na kazi (FFU) wawawepeleke somalia wakambanane na Al shabab maana hapa bongo hakuna kazi ya kuwapa
 
Kinachonisikitisha ni kitendo cha polisi kuamua kuzuia watu wanaoandamana kwa wamani na kuwazuia kwa kutumia risasi za moto isitoshe wanaopambana nao silaha yao ni mikono yao, kwa kweli jeshi la polis linazidi kuna wasiwasi juu ya uwepo wao ni kwaajili ya kuwalinda wananchi au kuwatetea viongozi waliopo madarakani
 
Mimi Nimejiuliza Hadi Machozi kwa sasa Yananitoka!! Mauwaji Yamekithiri!! Jeshi la polisi ni walinanda amani, Watu wanaandamana kuomba walinda amani wawaongezee Ulinzi!! Walinda Amani wanawaua!! Jamani Tanzania Tumefikia Hapa!! Mtu akiandamana Kwenda kwa Mtawala wa Eneo, Si unamruhusu ila unahakikisha Hasabishi Madhara?
Ok sasa hawa Vijana Wanatuhumiwa Kupiga mawe Jengo la Chama Fulani!! Je adhabu yake ni kifo!! Je Tanzania Tumefikia Hapa!!

MACHOZI YANANITOKA NAOMBA NIISHIE HAPA
vipi mkuu, uko sawa!?

Hivi unaongelea lile Jeshi la Polisi ambalo mkuu wake mmoja alikuwa akilaumiwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Mh. Mwakyembe!? ...si ndilo hilo hilo alilolilaumu Dr. W. Slaa!? ...wele walioua wananchi pale Arusha, ....wale ambao leo Mh. Tindu Lissu amesikika akilalamika kuwa wamehamisha wachimbaji wadogo huko Singida Mashariki ili wapishe kampuni nyingine ichimbe hiyo dhahabu!?

Ina maana mpaka sasa hujawaza kuwa na alternative idea (Plan B) juu ya hii TAASISI!?

 
Wakuu nimepigiwa simu na rafiki'angu toka Songea anasema kumekuwa na mauwaji ya kutisha kwa mda wa wiki sasa na inasemekana watu zaidi ya kumi wamesha uwawa ingawa RPC amedai wananchi wasihofu.

Pia nasikia wananchi waliandamana mpaka kwa mkuu wa Wilaya ila bado uvumbuzi haujapatikana na inasemekana wananchi waliwachoma moto watu wawili kutokana na tuhuma za kuhusika na mauwaji hayo na ndipo wauwaji wakasema sasa wataendeleza mashamulizi.

Mwenye ndugu pande hizo anaweza mpigia simu ili tuweze pata taarifa zaidi ila kuna jamaa yangu mwingine ni polisi nae ameniakikishia kuwa hali si nzuri kwa sasa.



PICT0021-1.jpg
PICT0024-2.jpg
PICT0020.jpg
PICT0024-1.jpg

Mauaji yamehamia Songea baada ya Arusha,then who is next?
 
Tuwe wakweli pale inapobidi,polisi sio miungu wa kuota na kuzuia uhalifu ,kazi yao inategemea ushirikiano wa raia,mauaji ya waendesha pikipiki yalikuwa mengi sana kanda ya ziwa miaka btn 2008-2011 na yalimalizwa na waendesha pikipiki wenyewe.Wao ndio wanaokaa mitaani,wanawafahamu vibaka wote na wanawafahamu dealers wa used spare parts za pikipiki etc kitu walichofanya waendesha pikipiki wa kanda ya ziwa ilikuwa ni kuunda umoja wao against wezi wa pikipiki,walikuwa wanapeana taarifa wanapoona sura inayotia mashaka,wanasaidiana kufuatilia nyendo za watu mbalimbali,wanafuatilia pale mwenzao anapokodishwa na mtu asiye eleweka vizuri na pale mwenzao anapochelewa kurudi etc pia wame track na kukamata wezi mbali mbali na kuwakabidhi polisi,sasa kuandamana wakati wao wenyewe hawafanyi ulinzi shirikishi na baadhi yao ndio wanao chora wizi wa pikipiki ni wastage of time na kutafuta scape goats
 
Tuwe wakweli pale inapobidi,polisi sio miungu wa kuota na kuzuia uhalifu ,kazi yao inategemea ushirikiano wa raia,mauaji ya waendesha pikipiki yalikuwa mengi sana kanda ya ziwa miaka btn 2008-2011 na yalimalizwa na waendesha pikipiki wenyewe.Wao ndio wanaokaa mitaani,wanawafahamu vibaka wote na wanawafahamu dealers wa used spare parts za pikipiki etc kitu walichofanya waendesha pikipiki wa kanda ya ziwa ilikuwa ni kuunda umoja wao against wezi wa pikipiki,walikuwa wanapeana taarifa wanapoona sura inayotia mashaka,wanasaidiana kufuatilia nyendo za watu mbalimbali,wanafuatilia pale mwenzao anapokodishwa na mtu asiye eleweka vizuri na pale mwenzao anapochelewa kurudi etc pia wame track na kukamata wezi mbali mbali na kuwakabidhi polisi,sasa kuandamana wakati wao wenyewe hawafanyi ulinzi shirikishi na baadhi yao ndio wanao chora wizi wa pikipiki ni wastage of time na kutafuta scape goats

Kwa hiyo badala ya waandamanaji kusaidiwa mawazo ya namna ya kuwashughulikia wauaji wao wanauawa?
 
Kibaya zaidi rpc ruvuma anasema risasi za moto zinaruhusiwa ndio maana zipo hapa ndipo nuilipogundua kuwa ili uwe rpc sio lazima uwena na uwezo wa kufanya maamuzi ambayo ni rational na logical,bali unaweza kuwa rpc kama tu kuna mtu anakushika mkono,ndio maana anajribu kutoa majibu mepesi kwa maswali magumu,michael kamuhanda anasema maandamano haya yamechochewa na siasa,lakini anasahau kuwa waandamanaji hao walikuwa wanataka polisi wakomeshe mauaji dhidi ya raia,lakini hatimaye wao ndio wanauwawa,hakika jeshi la polisi chinjachinja ni jeshi la watawala sio kulinda tena usalama wa raia na mali zao.
 
Iwe iwavyo, yote haya yana mwisho. Mwisho wake hauko mbali, yawezekana ukawa kabla ya 2015. Uhakika wake ni 2015, tukiwa na katiba mpya. Duniani kote haki ilipatikana kwa gharama kubwa kama hiyo. Haikupatikana kirahisi.
 
Polisi wetu mnashindwa kuona,wenzenu duniani kote wanafanyaje angalieni greese/ugiriki kunamaandamano makubwa dhidi ya serikali lakini huwezi kusikia watu wamekufa kinyama kiasi hiki wanaacha kutumia risasi za mpira wanatumia risasi za moto,rpc ruvuma kama nchi hii kungekuwa na uwajibikaji leo hii hakutakiwa kuwa ofisini asubuhi ya leo.
 
Nilijua lazma watakuja na tamko la cdm ndio wako nyuma ya mgogoro huo!hv vyombo vya dola bwana!nguvu kubwa kwa raia wasiokua na silaha,nawajue haya mambo wanayofanya ndio yanazidi kuchochea petrol kwenye moto unaowaka dhidi ya chuki na chama tawala, ni wazi kua hata wale waliokua hawana chama au wana support chama tawala wataingiwa na hasira na simanzi pia juu ya udhalimu huu na wataona hiki si chama chenye kujali maslahi na uhai wa wananchi wake!

Jeshi la polisi linatakiwa kutafuta njia mbadala ya kudeal na raia wake,nguvu,vitisho na mauji dhidi ya raia matokeo yake raia wameanza kuzoea na kutoheshimu tena jeshi la polisi, na itafika muda tena si mrefu raia wataanza kupambana na polisi bila uoga! Jirekebisheni na msome alama za nyakati
 
Back
Top Bottom