Maandamano makubwa Songea!

Maandamano makubwa Songea!

nimesikitishwa na kauli kwamba wanasiasa na wanaharakati ni chanzo cha maandamano songea soma zaidi kauli hii songeayetu.blogspot.com
 
Tuwe wakweli pale inapobidi,polisi sio miungu wa kuota na kuzuia uhalifu ,kazi yao inategemea ushirikiano wa raia,mauaji ya waendesha pikipiki yalikuwa mengi sana kanda ya ziwa miaka btn 2008-2011 na yalimalizwa na waendesha pikipiki wenyewe.Wao ndio wanaokaa mitaani,wanawafahamu vibaka wote na wanawafahamu dealers wa used spare parts za pikipiki etc kitu walichofanya waendesha pikipiki wa kanda ya ziwa ilikuwa ni kuunda umoja wao against wezi wa pikipiki,walikuwa wanapeana taarifa wanapoona sura inayotia mashaka,wanasaidiana kufuatilia nyendo za watu mbalimbali,wanafuatilia pale mwenzao anapokodishwa na mtu asiye eleweka vizuri na pale mwenzao anapochelewa kurudi etc pia wame track na kukamata wezi mbali mbali na kuwakabidhi polisi,sasa kuandamana wakati wao wenyewe hawafanyi ulinzi shirikishi na baadhi yao ndio wanao chora wizi wa pikipiki ni wastage of time na kutafuta scape goats

Polisi kutawanya maandamano kwa madai hawakupewa taarifa sawa ni halali, lakini kwanini watumie risasi za moto waandamanaji walikuwa na silaha gani? kwanini RPC akimbilie madai waandamanaji wamepiga mawe ofisi za ccm, inaniudhi kauli hii. kwanini alete siasa? kwanini waue watu, ria wa nchi hiii?
 
Iwe iwavyo, yote haya yana mwisho. Mwisho wake hauko mbali, yawezekana ukawa kabla ya 2015. Uhakika wake ni 2015, tukiwa na katiba mpya. Duniani kote haki ilipatikana kwa gharama kubwa kama hiyo. Haikupatikana kirahisi.

Na sio kufika mwisho tu,na hawa wauaji wote wa raia bila makosa,kuanzia viongozi wao mpaka mfyatua risasi wa mwisho dhidi ya roho za raia wema watakua accountable na watawajibika kwa haya maisha ya watu yanayopotea hovyo!waache walete mzaha tu,wataiona nchi chungu hii
 
Kiukweli binafsi nimesikitishwa na mauji haya,Kwanini polisi watumie risasi za moto ile hali waandamaji hawakuwa na silaha kali kasi hicho?swali je jeshi limeishiwa mbinu?haki ya kuandamana ambayo ni ya kikatiba iko wapi?Rais aliyeapa kuilinda na kuitetea katiba yuko wapi?
 
Polisi kutawanya maandamano kwa madai hawakupewa taarifa sawa ni halali, lakini kwanini watumie risasi za moto waandamanaji walikuwa na silaha gani? kwanini RPC akimbilie madai waandamanaji wamepiga mawe ofisi za ccm, inaniudhi kauli hii. kwanini alete siasa? kwanini waue watu, ria wa nchi hiii?

kujikomba kwa wakuu ili ionekana ni sahihi walichofanya kwa vile walikua wanalinda ofisi za chama zisidhurike!ila angekuwepo Julius K Nyerere ndio kiongozi wa nchi nafikiri sasa hv wahusika wote wangekua wamewajibishwa na wapo lupango!
 
Nilisema jana kuwa tusubirie viongozi wetu majuha waje na kauli za kijinga kuwa maandamano haya yameletwa na wanasiasa na hasa CHADEMA..

Mimi nasema hata kama hao waandamanaji wangekuwa wamepiga mawe ofisi ya CCM ni sahihi kabisa,kwasababu ndio chama kilichopo madarakani,na hao watu wanaoongoza mkoa kuanzia mkuu wa wilaya,mkuu wa mkoa na jeshi la polisi lipo chini ya CCM.

Sasa sitashangaa wananchi kupiga mawe ofisi zao kuonyeshea hisia zao juu ya chama hiki.Wanafanya hivyo kwa nia nzuri kuonyesha kuwa watawala waliowekwa na CCM mkoani hapo hawafanyi kazi vyema.
 
inasikitisha kuingiza siasa katika hili

anataka watu waamini kuwa cdm ndio

chanzo cha vurugu na ccm wampe credit

kuwa anadhibiti upinzani kama ilivyokua

enzi za kina mahita
 
Haya ndiyo maneno ingawa muda si mrefu utaambiwa unaombea vita ije.

Hii hata mie huwa natamani sana kuitaja ila inafutwa fasta nina wasiwasi na njia tutakayotumia kuikomboa nchi hii.Ukito ushauri kuwa jeshi lichukue nchi unaambiwa unachochea uasi. Nchi nyingine za wenzetu wamefanikiwa sababu ya kuwa wazi
 
m naona kwenye vurugu kama hzo wawatumie wanajeshi,kwani wanajeshi hawatumii silaha nyngne zaid ya mikanda..
 
Mabomu ya machozi yameisha?,risasi za mpira nazo zimeisha?Haya ndo maswali hasa RPC anatakiwa atujuze mpaka watumie risasi za moto kwa wananchi wasiokuwa majambazi wanaoandamana kutaka ukweli.Mungu iko siku atatoa majibu ya haya mateso wanaopata wananchi hawa.
 
Tumefika mahali ambapo nchi inahitaji ukombozi wa kweli kutoka mikononi mwa mkoloni mweusi! ambaye sasa anaonekana kuwa ni mbaya zaidi ya mkoloni mzungu!

Haiwezekani polisi waendelee kuuwa watanzania wanyonge wanaondamana kufikisha kilio chao kwa watawala kwa njia ya amani!. Hiki kisingizio cha kisiasa ambacho sikuhizi polisi wanatumia kuhalalisha mauji wanayoyafanya kwa raia hakikubariki hata kidogo.

Polisi wanapashwa kulinda raia na mali zao na kamwe hawapashwi kuwa wauaji!!!
 
Issue ni moja tu!

This has proved that the so called governors of the district and region, representative of the president in that locality are a bunch of mediocre, incompetent gunnery of our time.

kwa nini Watu walivyotaka kuongea na Mkuu wa Mkoa, yeye asingetumia busara kidogo tu, akatoka na kuwatuliza, akayafanya aliyoyafanya baada ya mauaji?
Baada ya mauaji, eti mkuu wa mkoa ndo anaitisha mkutano na viongozi wa mitaa na viongozi wa polisi!!!! My foot.
 
Ndugu zangu, kutokana na jeshi la polisi jana kuua kwa "makusudi" wananchi waliokuwa wanaandamana kupinga mauaji ya wananchi yanayoendelea pasipo jeshi la polisi kuchukua hatua yoyote, huu ndio ukweli na sio maelezo ya RPC-Ruvuma MICHAEL KAMUHANDA alivyodanganya Taifa.

Mosi, RPC anasema kuwa maandamano yale yalichochewa na ushabiki wa kisiasa huku akidai waandamanaji walipiga mawe ofisi ya CCM. Ndugu zangu hapa RPC kadanganya, waandamaji wengi walikuwa madereva wa pikipiki (boda boda) ambao ndio waathirika wakubwa wa mauaji yale na sio CHADEMA, pili, kamanda anadai walifanya maandamano bila kuomba kibali, uzuzu mwingine wa RPC ni huu, hivi polisi ndo wanaolalamikiwa then utoke ukaombe kibali kwao(polisi) ili uende kwa RC kuwalalamikia polisi.

Kituko eee! Halafu RPC asiwe mbumbumbu wa sheria. Polisi hawaombwi kibali cha maandamano bali wanapewa taarifa ya muda, madhumuni na kutakiwa watoe ulinzi kwa waandamanaji. Mwisho RPC anataka ajifiche ili aonekane ameua ili kulinda CCM (watawala) dhidi ya CHADEMA ili asihojiwe na watawala kwa mauaji aliyofanya.

Mbunge wa songea mjini Dr.Emanuel Nchimbi (0754 033388) RPC-Ruvuma (0754 252415) . Said mwema(0754 705557). Je hawa ni watu au miungu wenye haki ya kuua?


[songea]

Jaribu kuuwa mnyama wa hifadhi uone sheria inavyofanya kazi laki POLICE kuuwa binadamu ni sawasawa na mwanadamu kuuwa chawa.
 

Attachments

Polisi kutawanya maandamano kwa madai hawakupewa taarifa sawa ni halali, lakini kwanini watumie risasi za moto waandamanaji walikuwa na silaha gani? kwanini RPC akimbilie madai waandamanaji wamepiga mawe ofisi za ccm, inaniudhi kauli hii. kwanini alete siasa? kwanini waue watu, ria wa nchi hiii?
hata kama walipiga mawe, wanataka waendee kupiga mawe ofic za cdm kwan wao ndo wanawamiliki polisi? kama walipigwa mawe ccm , wanastahili hayo kwa kuwa polisi wao wameshindwa kuzuia mauaji ya raia zaidi wanaongezea mauaji ya raia
 
Sikuamini pale nilipomuona RPC akijibu kwa jeuri sana"Ndio maana polisi wanabeba risasi za moto,wanaruhusiwa kuzitumia kwa mujibu wa sheria.Hauwezi kuona unazidiwa nguvu alafu ukaacha kutumia risasi za moto"!Sasa jiulize kulikuwa na ulazima gani jana kutumia risasi za moto?

Waliopigwa risasi wote wamepigwa wakiwa wanakimbia polisia.Sasa hapa kipi kinampa ulazima askari kutumia risasi ya moto tena kwa lengo la kuua?Utafikiri ilikuwa ni mapigano kati ya majambazi yenye silaha kali na polisi!Au polisi wetu hawajui kutofautisha operation?

Nashangaa mwananchi anauawa na kunyanyaswa na hawa askari polisi na huku kuna watu wanaitwa jeshi la wananchi wa Tanzania wamekaa tu!

Kwanini hawamlindi mwananchi dhidi ya uvamizi huu wa ndani unaofanywa na maharamia waliojivika sare iliyoruhusiwa kuua?Hakuna umuhimu wa kuwa na jeshi la wananchi wakati hao wananchi wenyewe wanauawa kila siku na kikundi haramu cha ndani!
 
Ah! Najuta kupigia kura CCM mwaka 2005. Ewe mwenyezi natubu dhambi zangu leo. Ni heri ya makaburu wa A/kusini enzi zile kuliko utawala wa CCM na serikali yake inayoua wanaowaongoza.
 
Wananchi wanjua kabisa CCM ndo RPC,DC,POLISI,JK,MAHAKAM,BUNGE,kwa sisi viongozi tujuwe kuwa kuna siku tutapigwa mawe tu.Muulize Vua Nohodha---"kama mimi wamenipiga je mtu wa kawida(RPC,DC,Polisi,CCM nk) itakuaje?"mwisho wakunukuu.
 
Kilicho baki sasa nikuwageuzia kibao hawa miungu watu
 
Back
Top Bottom