Maana ya Ushindi wa CCM Igunga kuelekea Chaguzi nyingine zijazo

Kwa mujibu wa matokeo ya Nape Nnauye CCM imepata kura 26266 na CDM kura 22443, hii ikiwa ni tofauti ya kura 3823. Kwa wachambuzi makini wa siasa(wasio na ushabiki), ushindi huu si dalili njema kwa CCM, kwa sababu zifuatazo:
1. CCM imeporomoka kutoka kura 35674 hadi kura 26266 ikiwa na maana zaidi ya wapiga kura 9408 wameikataa CCM ndani ya miezi 11
(okt 2010-sept 2011)
2.Upinzani umepanda kutoka kura 11321 hadi zaidi ya kura 22443, ikiwa na maana kuwa imani kwa upinzani imeongezeka
3. CCM imeshindwa kuvunja rekodi yake yenyewe, kwa hiyo anayetakiwa kutembea kifua mbele si CCM bali CDM

Nasema hii ni dalili mbaya kwa CCM kwa kuchukulia mfano thabiti wa Uchaguzi mdogo wa jimbo la Biharamulo julai 2009. CCM walishinda kwa kura 17561 dhidi ya upinzani uliopata kura 16898(CDM 16700 na TLP 198), lakini ulipofanyika uchaguzi mkuu 2010, CDM waliibuka kidedea baada ya kulitwaa jimbo hilo.

Kama taarifa ya Nape ni sahihi, CCM wanaweza kufurahia kwa kuwa wameudhibiti ubunge wa Igunga, lakini wasifurahie kuwa wameshinda. Ni ishara nzuri sana kwa CDM na wapenda mageuzi kwa ujumla, hata Nape na makada wengine wa CCM wanajua hili.

CCM, TAA NYEKUNDU IMEWAWAKIA. FURAHINI KWA TAHADHARI
I STAND TO BE CORRECTED
Nape ni msemaji mkuu wa tume ya uchaguzi???mbona mnatuchanganya??matokeo halisi si yanatangazwa na Tume??Nape katoka wapi hadi aisemee tume ya uchaguzi??tutaamini vip hayo matokeo?? Wakati hizo taarifa zinawasilishwa kwa Nape kutoka Tume ya uchaguzi Nape alikuwa mwenyewe wakati anayapokea hayo matokeo??mbona hapa anataka kutujengea hofu juu ya utaratibu mzima wa kutoa matokea???
 
Umeongea vizuri lakini mshindi ni mshindi hata kwa kura moja tu still ameshinda, jaribuni tena baadae. Katika analysis zako ulisahau kuwa magwanda walikuwa hawakuweka mgombea kabla ya miezi 11.

Nnawapa pongezi sana magwanda kwa kujitahidi, na nnawapa pongezi sana CCM kwa ushindi. Wote watazame matokeo na wajifunze kwa hayo matokeo ili chaguzi zingine ziwe na changamoto zaidi.

Naamini kuwa Serikali yoyote hufanya vyema zaidi pale kwenye upinzani mzuri zaidi, kwani wakiteleza tu, upinzani unachukuwa madaraka.

Hongera wana Igunga wote bila kujali itikadi yao kichama. Mbunge aliyechaguliwa aanze kazi ya kuwatumikia wananchi na isiwe kama wabunge wengine ambao hugombea kwa sababu zao binafsi.

What???
Ni wewe FF au kuna mtu kakwiba password yako?

Anyway, tunasubiri matokeo halali ama haramu yatakayotangazwa na magayane ili twende mbagala kuwaona waliokumbwa na maafa ya kuezuliwa nyumba zao.
 
Umeongea vizuri lakini mshindi ni mshindi hata kwa kura moja tu still ameshinda, jaribuni tena baadae. Katika analysis zako ulisahau kuwa magwanda walikuwa hawakuweka mgombea kabla ya miezi 11.

Nnawapa pongezi sana magwanda kwa kujitahidi, na nnawapa pongezi sana CCM kwa ushindi. Wote watazame matokeo na wajifunze kwa hayo matokeo ili chaguzi zingine ziwe na changamoto zaidi.

Naamini kuwa Serikali yoyote hufanya vyema zaidi pale kwenye upinzani mzuri zaidi, kwani wakiteleza tu, upinzani unachukuwa madaraka.

Hongera wana Igunga wote bila kujali itikadi yao kichama. Mbunge aliyechaguliwa aanze kazi ya kuwatumikia wananchi na isiwe kama wabunge wengine ambao hugombea kwa sababu zao binafsi.
Hapo sasa FaizaFox nakuunga mkono, umeonyesha ukomavu wa kisiasa umeisha tambua kuwa CCM wako kwenye wakati mgumu!!!!!! Kweli bila ubishi CDM noma huko tunako elekea sijui itakuwaje!!!!!!!! Maana watoto wa miaka 15 wote watapiga kura, na hao ukiwaeleza taabu yetu wanakuelewa, CCM imeshinda vijijini watu wangine hata kiswahili hawajui, wangoje secondari za kata watapata majibu yao!!!!!!!!!!Huyo mbunge aliye chaguliwa si ndiye aliyefanya mikataba ya Buzwagi???????? Wana Igunga hiyo migodi yenu ya Sheluhi chunga saana huyu jamaa Kafumu asiiuze akawaacha hoi, ndio zake hizo muulizeni Lembeli mbunge wa Kahama!!!!!!
 
Kwa mujibu wa matokeo ya Nape Nnauye CCM imepata kura 26266 na CDM kura 22443, hii ikiwa ni tofauti ya kura 3823. Kwa wachambuzi makini wa siasa(wasio na ushabiki), ushindi huu si dalili njema kwa CCM, kwa sababu zifuatazo:
1. CCM imeporomoka kutoka kura 35674 hadi kura 26266 ikiwa na maana zaidi ya wapiga kura 9408 wameikataa CCM ndani ya miezi 11
(okt 2010-sept 2011)
2.Upinzani umepanda kutoka kura 11321 hadi zaidi ya kura 22443, ikiwa na maana kuwa imani kwa upinzani imeongezeka
3. CCM imeshindwa kuvunja rekodi yake yenyewe, kwa hiyo anayetakiwa kutembea kifua mbele si CCM bali CDM

Nasema hii ni dalili mbaya kwa CCM kwa kuchukulia mfano thabiti wa Uchaguzi mdogo wa jimbo la Biharamulo julai 2009. CCM walishinda kwa kura 17561 dhidi ya upinzani uliopata kura 16898(CDM 16700 na TLP 198), lakini ulipofanyika uchaguzi mkuu 2010, CDM waliibuka kidedea baada ya kulitwaa jimbo hilo.

Kama taarifa ya Nape ni sahihi, CCM wanaweza kufurahia kwa kuwa wameudhibiti ubunge wa Igunga, lakini wasifurahie kuwa wameshinda. Ni ishara nzuri sana kwa CDM na wapenda mageuzi kwa ujumla, hata Nape na makada wengine wa CCM wanajua hili.

CCM, TAA NYEKUNDU IMEWAWAKIA. FURAHINI KWA TAHADHARI
I STAND TO BE CORRECTED


Umezungumza kama mchambuzi makini wa siasa. kama CDM itashindwa haipaswi kuregret. Hoja ya ko ni dhahiri hata kwa kuangalia matokeo ya uraisi ya NEC, 2010

TABORA
WILAYA YA IGUNGA
IGUNGA
Candidate
Political Party
Number of Votes
Percentage Votes
KIKWETE JAKAYA MRISHO
CCM
34,090 69.39
SLAA WILLIBROD PETER
CHADEMA
8,874 18.06
LIPUMBA IBRAHIM HARUNA
CUF
3,181 6.47
KUGA PETER MZIRAY
APPT - MAENDELEO
818 1.67
RUNGWE HASHIM SPUNDA
NCCR-MAGEUZI
143 0.29
DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA
UPDP
77 0.16
MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT
TLP
57 0.12
SPOILT VOTES 1,888 3.84
TOTALS 49,128 100
 
Faizafoxy,
I can't believe my eyes. Huyu ni wewe kweli au kuna mtu kaiba ID yako? Au ile safari Marekani imekufungua macho?
Ni huyo Faiza amebadilika amesoma alama za nyakati, kwa mtindo nadhani tutaelewana!!!!!!!
 
MATOKEO YA NAPE YATAUMBUA CCM ZAIDI KUHUSU UCHAKACHUAJI WAO WA
KUNUNUA KURA ZA CUF NYUMA YA PAZIA IGUNGA



Hebu fikiria

1. mtokeo ya kata moja iitwayo
MBUTU yametolewa mara mbili kwa takwimu za aina mbili tofauti huku CCM ikipata kura nyingi mno katika mazingira hiyo tata (Matangazo ya Nape).

2. Katika hali isiokawaida,
kura za CUF zimepotelea wapi ghafla wakati ni chama kimojawapo kilichokua nga nguvu sana Igunga???????

3. Kwa nini Nape kama kiongozi mojawapo wa vyama vinavyoshindana katika kinyang'anyiro hicho
aachiwe jukumu la KUTANGAZIA TAIFA matokeo ya uchaguzi???

4. Kwa Mujibu wa 'Matokeo ya Nape', CCM imeshinda kwa kura
26,266 na CHADEMA 22,443 lakini kwa kura zilizotokana na kata 22, je kura za kata zingine 4 ziko wapi na kitu gani kinatuminisha kwamba ushindi unaweza ukapatikana bila kata hizo 4???????????

5.
Kwa nini Tume ya Uchaguzi ishindwe mpaka sasa hivi kujumlisha na kutangaza matokeo ya Igunga mpaka hivi sasa lakini Nape na CCM wao waweze????????????

Bila HAKI uchaguzi Igunga bado haujafanyika kamwe!!!!!!!!!!!!!!! Kweli hizi ni Saisa uchwara mtupu chini ya CCM inayoelekea kufa kabla ya 2015.

Eti kwa sheria za tume ya uchaguzi inaruhusiwa chama kitangaze matokeo kabla ya tume?????? Kuna nini hapo wadau????????
 
Umezungumza kama mchambuzi makini wa siasa. kama CDM itashindwa haipaswi kuregret. Hoja ya ko ni dhahiri hata kwa kuangalia matokeo ya uraisi ya NEC, 2010

TABORA
WILAYA YA IGUNGA
IGUNGA
Candidate
Political Party
Number of Votes
Percentage Votes
KIKWETE JAKAYA MRISHO
CCM
34,090 69.39
SLAA WILLIBROD PETER
CHADEMA
8,874 18.06
LIPUMBA IBRAHIM HARUNA
CUF
3,181 6.47
KUGA PETER MZIRAY
APPT - MAENDELEO
818 1.67
RUNGWE HASHIM SPUNDA
NCCR-MAGEUZI
143 0.29
DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA
UPDP
77 0.16
MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT
TLP
57 0.12
SPOILT VOTES1,888 3.84
TOTALS 49,128 100


Kumbe Slaa alibwagwa vibaya sana kura 26% ya alizopata Kikwete, wako mbali sana kama mbingu na ardhi.
 
nimekaa nikatafakari nikaona kuwa siasa nchi hii ni ugonjwa wa moyo. Hasa unapokutana na ccm. Tatizo la ccm ni kuifanya siasa kuwa chanzo chao kikuu cha maisha-kipato. Yani ni watu ambao bora ukutane na mamba kuliko wana ccm katika mazingira ya uchaguzi. Ccm tumewachoka mtuache jama. Hatuwapendi tena bali mnajipendekeza kwetu. Mnatawala kwa chuki na hila kwa kuwa mnajua hampendwi tena. Mnaogopa kuachia dola kwa kuwa mnajua ni sehemu yenu ya maisha. Pai mnaogopa kwa kuwa mkiachia dola hii nchi itakuwa chungu kwenu. Siku yenu iko
 
Umeongea vizuri lakini mshindi ni mshindi hata kwa kura moja tu still ameshinda, jaribuni tena baadae. Katika analysis zako ulisahau kuwa magwanda walikuwa hawakuweka mgombea kabla ya miezi 11.

Nnawapa pongezi sana magwanda kwa kujitahidi, na nnawapa pongezi sana CCM kwa ushindi. Wote watazame matokeo na wajifunze kwa hayo matokeo ili chaguzi zingine ziwe na changamoto zaidi.

Naamini kuwa Serikali yoyote hufanya vyema zaidi pale kwenye upinzani mzuri zaidi, kwani wakiteleza tu, upinzani unachukuwa madaraka.

Hongera wana Igunga wote bila kujali itikadi yao kichama. Mbunge aliyechaguliwa aanze kazi ya kuwatumikia wananchi na isiwe kama wabunge wengine ambao hugombea kwa sababu zao binafsi.
FF hayo ndio madhara ya kufikiri kwa masaburi!! Au umesafiri upo kwenda kwenye sayari ya mwezi maana Andrology (hormones huwa very imbalanced)? Mwanzisha thread hajakataa hata kidogo kwamba CCM imeshinda (only if Nape yupo sahihi) ila amesema hii si dalili nzuri mbele ya safari. Pia ni jana tu NEC imekataa watu kujitangazia matokeo wenyewe bali wasubiri NEC ndio watangaze na CCM wakafurahia tangazo hilo baada ya kuona ITV na media zingine zinavyotangaza ukweli (anguko la CCM), leo iwaje Nape afanye hivi? Inauma lakini ukweli ni huo!! Hapa hata CDM ikishindwa itakuwa imeshindwa dhidi ya Kombaini ya CCM+Dola(Polisi na TISS)+NEC+Serikali (eg. DC, RC, DED etc)
 
CHADEMA imedhihirisha ukomavu na VIJANA wa IGUNGA wanastahili pongezi kwa kushindana na mazoea ya wazee wao. Kwa upande mwingine, wake za CCM yaani nikimaanisha CUF, kushnei. Na ni vile wamechanga na mume wao vinginevyo Igunga ilikuwa ya CHADEMA.

Aluta Continua....mapambano yanaendelea..
Peopleoooooos'..power!!!!

 
Are these official results? Itakuwa ni vyema kusubiri official results kutoka NEC.
 
Kwa muono kama huo hutachukuwa nchi hata ufanye nini. Punguza jazba, sherehekea ushindi wa CCM kwa kujipanga na kuanza kuyafanyia kazi yaliyokusibu ukashindwa kura. Kuwalaani wana wa Igunga ni kujipa laana wewe mwenyewe. Wengi hawajakuchaguwa kwa sababu, zitafute hizo sababu ujirekebishe.

Wote wa ccm siwapendi! Na hapa watakuwa wameiba kwa kiwango kikubwa sana kwa ninavyoijua ccm, zaidi ya nusu ya kura zao watakuwa wameiba. Mungu yupo huu utawala dhalimu utaondoka tu, hata kwa namna yeyote
 
Pia wale BAKWATA wa Igunga waliohongwa na CCM kuwanyima Waislam wezao kupigia CDM kura wamechangia CDM kushindwa. Ila umaarufu wao umeishia hapo na hawatamwona Wassira, Makufuli wala yeyote aliyewadanganya tena. Hata hivyo Igunga nawapongeza wamefunguka na wameonyesha upinzani mkubwa kwa Magamba na next time jimbo litanyakuliwa tu kwani miaka 4 inatosha kumpima Kafumu na ahadi za madaraja, maji walizosema akina Makufuli na wassira. Ijulikane kwamba 2015 hakuna wa kumbeba mwenzake kwani Makufuli, wassira, na akina Mwigulu watakua wanajitetea ktk majimbo yao na hapo ndipo Kafumu atagundua hasara ya kubebwa.
 
Ikiwa mnategemea kuchukuwa uongozi kwa mawazo kama hayo, basi ujuwe ni bado sana. Nilidhani mtakuja na jipya la maana kumbe hamna lolote zaidi ya majungu.

Tutachukua tu na huzuii kitu chochote, uwe hai au usiwe hayo yatafanyika mapema sana hata pasipo sanduku la kura ikibidi. Kila utawala dhalimu huwa na mwisho mbaya
 
Tutachukua tu na huzuii kitu chochote, uwe hai au usiwe hayo yatafanyika mapema sana hata pasipo sanduku la kura ikibidi. Kila utawala dhalimu huwa na mwisho mbaya

Utawala dhalim unaujuwa au unausikia tu? ni nini ulichodhulumiwa wewe na utawala uliopo madarakani?
 
kwa mujibu wa matokeo ya nape nnauye ccm imepata kura 26266 na cdm kura 22443, hii ikiwa ni tofauti ya kura 3823. Kwa wachambuzi makini wa siasa(wasio na ushabiki), ushindi huu si dalili njema kwa ccm, kwa sababu zifuatazo:
1. Ccm imeporomoka kutoka kura 35674 hadi kura 26266 ikiwa na maana zaidi ya wapiga kura 9408 wameikataa ccm ndani ya miezi 11
(okt 2010-sept 2011)
2.upinzani umepanda kutoka kura 11321 hadi zaidi ya kura 22443, ikiwa na maana kuwa imani kwa upinzani imeongezeka
3. Ccm imeshindwa kuvunja rekodi yake yenyewe, kwa hiyo anayetakiwa kutembea kifua mbele si ccm bali cdm

nasema hii ni dalili mbaya kwa ccm kwa kuchukulia mfano thabiti wa uchaguzi mdogo wa jimbo la biharamulo julai 2009. Ccm walishinda kwa kura 17561 dhidi ya upinzani uliopata kura 16898(cdm 16700 na tlp 198), lakini ulipofanyika uchaguzi mkuu 2010, cdm waliibuka kidedea baada ya kulitwaa jimbo hilo.

Kama taarifa ya nape ni sahihi, ccm wanaweza kufurahia kwa kuwa wameudhibiti ubunge wa igunga, lakini wasifurahie kuwa wameshinda. Ni ishara nzuri sana kwa cdm na wapenda mageuzi kwa ujumla, hata nape na makada wengine wa ccm wanajua hili.

Ccm, taa nyekundu imewawakia. Furahini kwa tahadhari
i stand to be corrected

Nadhani na voters turnout imekuwa pia katika hiyo miezi 11 hawa walioongezeka possibly walikuwa chadema sympethisers amabao hawakupiga kura ile october vile chadema haikusimamaisha mgombea,..........hata hivyo hali si nzuri kwa ccm
 
Dada FF kuna mtu kakwapua password yako au ni wewe ?.Dada FF najua una akili sana na maarifa makubwa kuliko baadhi ya watu wanavyokufikiria kwa faida ya jamvi natoa ombi maalumu kwako endeleza michango ya aina hii.

Umeongea vizuri lakini mshindi ni mshindi hata kwa kura moja tu still ameshinda, jaribuni tena baadae. Katika analysis zako ulisahau kuwa magwanda walikuwa hawakuweka mgombea kabla ya miezi 11.

Nnawapa pongezi sana magwanda kwa kujitahidi, na nnawapa pongezi sana CCM kwa ushindi. Wote watazame matokeo na wajifunze kwa hayo matokeo ili chaguzi zingine ziwe na changamoto zaidi.

Naamini kuwa Serikali yoyote hufanya vyema zaidi pale kwenye upinzani mzuri zaidi, kwani wakiteleza tu, upinzani unachukuwa madaraka.

Hongera wana Igunga wote bila kujali itikadi yao kichama. Mbunge aliyechaguliwa aanze kazi ya kuwatumikia wananchi na isiwe kama wabunge wengine ambao hugombea kwa sababu zao binafsi.
 
Back
Top Bottom