Ingawa bandiko lako umelijaza Kiingereza bila ya sababu za msingi kuna hoja hapa umeianzisha naona na mimi nichangie. Kwenye mfumo wetu wa kufundishia darasani kuna tatizo kidogo. Mwalimu inaaminika anajua kila kitu wakati mwanafunzi anachukuliwa ana ubongo ulio wazi wa kujazwa kila kitu toka kwa mwalimu. Aina hii ya ufundishaji iko mpaka kwenye vyuo vyetu vikuu.
Wanafunzi wengi wanaosoma masomo ya mchepuo wa sanaa wanafeli zaidi kuliko wale wanaosoma masomo ya mchepuo wa sayansi, na sababu yake ni rahisi kueleweka. Masomo ya Mchepuo wa Sanaa ni rahisi lakini mitihani yake ni migumu wakati masomo ya sayansi ni magumu lakini mitihani yake ni rahisi. Na ndiyo maana mara nyingi wanaoshika nafasi kumi za kwanza kitaifa kwa Mitihani ya Kidato cha Nne na cha Sita huwa wanatoka kwenye mchepuo wa Sayansi.
..Miaka niliyosoma mimi "top cream" walikuwa wanakwenda kusoma science.
..hawa walikuwa wanafaulu masomo yote hata ya biashara, lakini kwasababu wanajiweza kimasomo walikuwa wanakwenda mkondo wa science.
..wanafunzi waliokuwa hawajiweza ndiyo walikuwa wanajaza mkondo wa biashara.
..siku zote wanafunzi wa mkondo wa science ndiyo walikuwa wakiongoza ktk matokeo ya kidato cha 4. Na walikuwa wanafanya vizuri hata ktk masomo kama history n geography kuwazidi wenzao wa mkondo wa biashara.
..ila tulipokwenda high school wanafunzi wa biashara na arts walikuwa na matokeo mazuri ya form 6 kulinganisha na wanafunzi wa science.
..miaka yetu mwanafunzi mwenye div
2 ya arts ilikuwa hawezi kujiunga Udsm kwa shahada ya sheria. Lakini div 2 wa science alikuwa anaweza kujiunga na shahada ya uhandisi.