Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Yaani ni shida tupu mpaka wanafunzi wanakuwa na msongo wa mawazo na kutofanya vizuri, mara sayansi, mara viwango vya ufaulu, mara wanasitisha ajira yaani nivurugu tu hii nchi, naawanaoathirika zaidi ni watoto wa masikini.


Naongezea: mara uhakiki, rara kuwanyang'anya digrii wale wahitimu hata walio kazini ambao kwa mtazamo wake hawastahili au hawakustahili kuwa kusoma hadi kufikia kiwango cha hizo digirii...
 
Hii akili mbovu kwa hawa watoto ni sisi wenyewe tunawajaza, tunaenda kimazoea kwenye elimu. Tatizo la watoto kutokusoma huanzia chini kabisa kwenye ngazi ya familia, wazazi hawajali, wao wanachojua mtoto kaenda shule basi, mengine yote wanamuachia yeye ku~make decisions, ni vigumu mtoto kujitambua kama hasukumwi, tatizo kubwa pia ni kua wazazi wenyewe wengi hawajasoma hata sekondari hawajafika, wanajiona kama hawana la kuchangia kwa watoto kwa kua watoto wenyewe tayari wanawashinda elimu, hapa sasa ndipo mwalimu anatakiwa aingie kati, afundishe vizuri lakini pia atoe motivation kwa watoto, kama hawaoni value yoyote kwenye elimu na hamna cha kuwasukuma lazima watafeli tu.

Nawakumbuka sana walimu wangu wa Chemistry na Physics Olevel, walikua wanatusukuma kwa nguvu, mwisho wa siku mambo yalivoanza kueleweka wote tulijikuta tunayapenda haya masomo, wengi tulikua tunatoka na A wa mwisho alikua na C, I'm thankful hadi leo hii nimekua mtu wa sayansi moja kwa moja, ningefeli haya masomo nisingekua hapa nilipo. Naamini inawezekana kabisa, ni system iliyopo tu imewaacha wanafunzi na wazazi wajijue kivyao, no direction zaidi ya curriculum tu, hata walimu hawana motisha ya kupiga kazi vizuri, hawaipendi kazi yao, wanaenda darasani ilimradi tu liende.
Nimekuelewa na nakubaliana na wewe.
Ila hili jambo la kuwasukuma wanafunzi, kwa kweli ni ngumu.
Mimi mwenyewe ni mwl. Tena wa chem na Biol...
Tunajitahidi sana hapa shuleni kuwalazimisha wanafunzi kusoma masomo hayo, tena kwa kuwapa umuhimu wa kusoma hayo tangia wanaingia kidato cha kwanza..
Ila in return, mrjrsho unakuwa ni kwa wachache. Wengi washakata tamaa kabisa mkuu.
Mie pia naona nia nzuri aliyonayo Dr. Ndilichako, ila hapa hofu yangu ni utayari wa wanafunzi hawa wa sasa....
Yaani hapa ni kumlazimisha punda kwenda mtoni atafika, ila hilo la kunywa maji, hapo inategemea na utayari wake kunywa au kutokunywa.
Kwa wanafunzi hao wa zamani, au walioko katika shule zile tunazoziita maalumu hilo labda linaweza kuwa na mrejesho chanya, ila kwa hawa wanaoitwa wa shule za St. Kayumba, hakiyamungu.. Hapa shida ipo na hamna cha maana mkuu kitakachopatikana in return....
All in all, unachokisema kinaleta maana na nakubaliana na wewe ila hapa tatzo liko katika hayo ukiyoyasema,
Wazazi hawako responsible,
Waalimu hawana molari ya kufanya majukumu yao,( sasa waalimu wengi wako kwenye ajira kama ajira zingine, motisha haziko.. Watu wana msingo wa mawazo. Wako kwa kuwa wanataka ajira ila utayari wa kutoil kwa ajili ya mtoto, mmmmmmh hilo halipo.)
Na jambo la siasa kwenye elimu nalo ni shida......
 
MAMA NDALICHAKO YUKO SAHIHI 100 %. KWANI TATIZO MNALOLIONA HAPO NI LIPI?

MIMI NIMESOMA MASOMO YOTE TISA(9) O LEVEL, nothing i lost. ADVANCED LEVEL nikasoma mchepuo wa Arts yaani HGE.
namshukuru MUNGU C ya mathematics na Ds za physics, chemistry na biology (biology na chemistry siyo sana) ila applications zake nimezitumia sana mpaka university wakati nasoma bachelor ya ECONOMICS.
Mwenye reason ya kusema tamko hilo ni wrong atueleze.
Wapo walioko vyuoni walikimbilia arts o level leo wanatamani warudi wakasome mathematics na physics tena.
Acheni wasome yote kama mimi atakaye feli masomo ya science kama mimi hata razimishwa kuyasoma advance.
Lakini atakuwa na knowledge kama yangu tofauti na aliyekimbia kabisa kama mnavyowashauri.
Wewe umesoma masomo tisa sawa, lakini kumbuka hawa wanaosoma masomo ya biashara wana commerce % bk ina maana wao watasoma masomo 11 alaf wakati huo huo watakao pewa vipaumbele ni wale watakaoendelea na sayansi hivi hauoni kwamba wanafunzi wa biashara watakavyonyanyasika??

Alaf baadhi ya shule kuna masomo ya ziada kama vile ICS, additional math ,bible,french,food&nutr, na agriculture

Alaf kumbuka baadhi ya shule zina wanafunzi zaidi ya 400 sasa jaribu kufikiria mitihani ya prac itafanyika vp?? Mwisho wa siku ndio tunarudi kulekule mambo ya alternative to prac
 
Wakuu naomba niulize japo ni nje ya mada kidogo. Hivi ndalichako ana mume?? Au ana mtoto yeyote yule anayesoma??
 
Kwa nini ndalichako na wenzio msifuate sheria?
Viboko ni suala la sheria.
Pia michepuo
Kama hamtki badilishen sheria

Michepuo ni nguzo safi kwan inamfanya mwabafunzi kukobsetrate na masomo yake ayapendayo
Nenda German michepuo inaanza after grandschule kulingana na vipawa vyake

Boreshen mazingira ya sayans pia arts mtaona manufaa y a michepuo

Viwanda kweli viwanda viharibu elimu yatu
Bah
 
Kusaka vyeti feki , ameacha kuimarisha elimu ili tupate educated and pure generation, sasa anatumia nguvu kubwa kusaka vyeti feki. Mfumo ulikuwa mbaya huwezi kuadhibu watu coz ya mfumo na watu walitumia orpotunity hiyo. Please tuipende Tanzania na sio kujitafutia umaarufu wa kibinafsi wa kutoa matamko kila kukicha
 
The Boss na katika hii global village tunahitaji watu watakao weza ku communicate effectively kwa Kiingereza tukiwa kama moja ya nchi za jumuiya ya madoa, tunahitaji malawyer wazuri wakuweza kusimimia mikataba ya rasilimali zetu, sasa kama nguvu zote zikitupwa kwenye physics na chemistry huko kwingine tutaendelea kuumizwa.
Hii jumuiya ya 'Madoa' imeanza lini!? Na sisi Watanzania tupo ndani yake toka lini!? Nijibu tafadhali nahitaji kuelimika kuhusu hayo Madoa.
 
Nilishasema toka awali kua huyu mama anakurupuka sana watu wakapinga vikali. Mpaka hapa sijaona mwelekeo wa mafanikio kwa uwepo wa huyu mama Wizara ya Elimu. Wizara ya ELIMU sio NECTA, sio taasisi ndogo! Hii wizara ndio moyo wa nchi.

Sijui mwaka huu vyuo vikuu vingapi vitakavyopokea wanafunzi wa fani za Sayansi. Utaratibu wa kizamani sana huu.
Analinda kibarua maana kaishatumbuliwa mara ya kwanza sasa ivi anafanya kazi kumfuraisha mtawala
 
Unavyoongea km una uhakika vile..halaf ni ufaulu sio ufahulu mkuu..ungekua unajua kuiandika ufaulu vizuri mbona tungekoma[emoji23][emoji23]
Asante kwa kunikosoa, lugha mama yangu huwa tunapata tabu ya matumizi ya sauti za h, r na l. Lakini naamini ujumbe umeupata vizuri mkuu.
 
Sure mkuu...dizain kama wanakurupuka flan hivi.....matamko ya rais yanageuka kuwa sheria kwao
 
Basi mkuu physics uliitupa pembeni au hukuielewa vizuri au unachokifanya ni kuoperate vitu ambavyo ni already made na huna passion ya kubuni kitu chako mwenyewe, we unadhani hizo automation ya hizo machines anayefanya ni nani? ambaye hajasoma physics? tukitaka kuwa na viwanda tusitegemee tutanunua kila product nje, vitu vingine ni custom built lazima tuweze kuvitengeneza sisi wenyewe, we unataka hadi machine ya kupima vitu na kukata twende nje tukanunue huku its very basic physics?

Physics ni muhimu sana, mimi niliisoma na hadi leo hii ninaitumia kwenye kazi zangu mara kibao tu, siku nyingine narudi kuchimba vitabu vya university physics kuangalia principles nikiwa nimezisahau. Kama ni kutengeneza viwanda tunahitaji watu waliosoma physics, huwezi tengeneza engine ya gari bila physics, huwezi tengeneza game la computer, hata kiatu bora cha kuvaa unapima strength ya material, heat absorption na dissipation, hadi vitu basic kama rangi nyeupe inafanya reflection na nyeusi inafanya complete absorption ni concepts nyepesi lakini very important ikija kwenye decisions ya rangi ipi itumike sehemu flani. We idea yako ya viwanda kumbe ni kununua kila kitu nje alafu tukaoperate wenyewe? Hehehe, mimi idea yangu ni kununua vichache nje, alafu vingi tukatengeneza sisi wenyewe.
Tatizo wapo waliosoma physics ila hata baiskel kujaza upepo hawezi au kuziba pancha, pia nawajua wanafunzi wengi wana degree ya umeme ila hawezi kutandaza nyaya ye anajua theoretically tu
 
Ni ubunifu mpya only in Tz. Hao walimu wa sayansi watatoka wapi? Nchi ina uhaba wa walimu wa hili somo halafu eti somo la sayansi lazima!
walimu wengi ni wa jiografia na historia sasa hiyo physics atafundisha nani? Tungeanza kwanza kuviambia vyuo vikuu vyetu vidahili walimu wa sayansi zaidi ili uamuzi utakapofanyika pawepo walimu wa kufundisha.
 
Nadhani tunaingiza siasa katika mambo ya msingi,?lengo la waziri ni zuri na baada ya muda mrefu litasaidia sana taifa. Changamoto ni nyingi kwa sasa kwa uamuzi huu ila hii sio sababu ya kuchelewesha uamuzi sahihi. Hii ni basic Science hadi kidato cha nne tu, wanafunzi wanaotaka kwenda michepuo ya Biashara au Sanaa watafanya hivyo kidato cha tano.
 
Nadhani tunaingiza siasa katika mambo ya msingi,?lengo la waziri ni zuri na baada ya muda mrefu litasaidia sana taifa. Changamoto ni nyingi kwa sasa kwa uamuzi huu ila hii sio sababu ya kuchelewesha uamuzi sahihi. Hii ni basic Science hadi kidato cha nne tu, wanafunzi wanaotaka kwenda michepuo ya Biashara au Sanaa watafanya hivyo kidato cha tano.
Itakuwa imesaidia nini kama wataacha baada ya kidato cha NNE????
 
Anadhani kusoma Physics na Chemistry ndo kuweza kuoperate viwanda!
Kwanza machine za siku hizi siyo manual ni automated computerized.

Nimesoma mimi physics na chemistry lakini sijawahi kuiapply popote!, hata huko viwandani hawaangalii physics umefauluje
 
Back
Top Bottom