Msingi mkuu wa yote hayo ni kosa la kuchagua mke. Kuna mahali nilisema mke wa ndoa anapaswa kutambua kuwa ndoa sio uwekezaji wa 50/50. Ili ndoa idumu ni LAZIMA kuwe na clear line kati ya mke na mume, kwamba ni nani mwenye ndoa!!
Sasa kwa ndoa za kisasa ambapo mwanamke na mwanamke wana hisa sawa mwenye ndoa, inahitaji mke mwenye busara na malezi bora mno. Wengi wanaingia wakiwa na mtazamo wa kiuanaharakati ndani ya ndoa ndio products za kina Kiria hizo.
Nikisema mume awe mume namaanisha kwamba mke anatakiwa atambue wazi kuwa maisha yake yanategemea ndoa, kwamba bila ndoa basi dunia kwake ni chungu. Kama ukioa mke ambaye ana mtazamo wa kuwa ukiona sifai nirudishe kwetu, basi jua hukupata mke bali mwanamke. Siku hizi kuna ujinga fulani umetamalaki, kwenye send off ni kawaida kusikia wazazi wa mwanamke wakisema binti huyu hajafukuzwa kwao, hivyo ukiona kakushinda mrudishe kwa amani. Ukisikia kauli kama hiyo jua mwwnamke huyo atabaki na connection na watu wa kwao na atakusumbua kweli.
Nikija kwenyebswali lako, mke akuleta hayo wala hakuna haja ya kuita vikao, MWONYE. Wewe ni mume, umetoa mahali kujenga mji wako sio wenu. Akikusikia umepata mke, la hajakusikia basi jua iko sauti anayoisikiliza huko nje, yaweza kuwa kidume au mashoti zake. Hapo sasa kama atakuwa anarudia na kuleta dharau na kiburi KUWA MWANAMUME. Mrudishe kwao akapumzike kwanza, hilo litamshitua mno kama no mke anayestahili ndoa, tena hawezi kucheza na mambo yako ya msingi.
Mwanamke ukimruhusu akudharau basi jiandae kwa maumivu makubwa zaidi. Lazima ajue kuna mahali umechora mstari na kwamba hatothubutu kuuvuka. Akishajua hilo atakyheshimu na ataogopa kukuletea ujinga. Lakini kunbuka wewe pia unapaswa kuwa mume mwenye kujitambua.