The Magnificent
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 2,694
- 1,250
huu uzi naona unachangiwa na watu wa ajabu ajabu tu,tena wanasapotiana ujinga ujinga,ngoja me nipite zangu.
Mkuu Ben lisemwalo lipo. Kama Katibu Mkuu amesema kuwa CHADEMA wamepewa fedha kuvuruga mchakato wa katiba, watashindwa vipi kuwahonga hao akina mtatiro na baadhi ya wabunge kufanikisha mpango wao?
Ngoma bado mbichi huyo ndiyo maalim nadhani wazanzibar wamemsuta kuungana na makfir chadema ingekuwa ni kuitukana zanzibar.
CCM hatuna muda wa marumbano. Waacheni wafu wazikane.
CUF wamezishtukia siasa za kisanii na kilaghai za CHADEMA.
Marriage of convenience. Mmoja hana base bara na mwingine hana base visiwani.
Hivi vyama ni kichekesho.
They'll never step out of their closed door and 2014 is just around the corner.
Ndoa sasa itakuwa ndoano sikujua kama chadema ndiyo alikuwa mke na cuf ndiyo mume au vinginevyo.
Sioni sababu ya kijana handsome(chadema-utamani mke wa mtu@CUF)Mkuu, sidhani kama kulikuwa na ndoa hapo ila nilichobaini ni kuwa CHADEMA (mwanamke) alikuwa anamtamani CUF (mwanaume) ila alikuwa anashindwa kumtongoza kwa kuogopa kuchomolewa na kuitwa malaya. uvumilivu ulipomshinda mwanamke akajitosa kumtongoza mwanaume na sasa amechomolewa
Kati ya viongozi hatari kabisa wa CUF ni huyu Maalim Seif,tuhuma alizotoa dhidi ya viongozi wenzake ni nzito(wao kuhongwa)kwa nini asingewasiliana nao kabla ya kutoa tuhuma hizi kwenye vyombo vya habari? Haoni kuwa amewadhalilisha..?Kama ni kweli,Anapotuhumu viongozi wenzake kuwa wamehongwa na CHADEMA kwanini isiwe yeye kuwa amehongwa na CCM?
Wadau,
Taarifa za kuaminika nilizopata kutoka chanzo cha kuaminika huko Zanzibar zinasema kuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amepinga kitendo cha baadhi ya viongozi wa chama hicho kuingia makubaliano na CHADEMA ili kupinga muswada wa katiba mpya. Maalim Seif amenukuliwa akisema mbele ya baadhi ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwa uamuzi huo si wa kichama bali ni msimamo wa baadhi ya viongozi wa chama hicho ambao wamepewa fedha na CHADEMA ili wawe na msimamo wa aina moja. Maalim Seif anasema kuwa wanaoratibu mpango huo ni Naibu Katibu Mkuu, Julius Mtatiro kwa kushirikiana na baadhi ya wabunge wa chama hicho kutoka Zanzibar. Taarifa zinasema kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Ibrahim Lipumba inaelekea kuwa ameingia kucheza ngoma ambayo haijui na matokeo yake anaonekana kupoteza mwelekeo na kukosa msimamo. Hoja zilizoainishwa na Maalim Seif za kupinga makubaliano hayo ni hizi zifuatazo;
- Hakuna kikao chochote cha chombo chochote cha kiutendaji na kimaamuzi cha CUF kilichoketi iwe Zanzibar au Tanzania Bara kujadili jambo hilo na kuweka msimamo wa chama.
- Maoni yaliyotolewa na Kambi Rasmi ya Upinzani juu ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba hayakuwa maoni ya vyama vyote vya upinzani bali yalikuwa ni maoni ya CHADEMA pekee waliyoandaa kwa muktadha wa kujipatia umaarufu Zanzibar
- CUF ni moja ya vyama vinavyounda serikali ya umoja wa Kitaifa Zanzibar. Kutokana na ukweli kuwa Serikali hiyo imeshirikishwa na yeye (Maalim Seif) ameshiriki katika kuboresha Muswada huo anaamini kuwa chama hicho kupitia Serikali ya Umoja wa kitaifa ambayo imepewa baraka na Wazanzibari wote kimeshiriki kutoa maoni yake. Hivyo madai kuwa Wazanzibari hawajashirikishwa si ya kweli na ni upotoshwaji mkubwa
- Misimamo ya viongozi wa CHADEMA dhidi ya Zanzibar mara zote imekuwa hasi na kwa hali hiyo hali iliyojitokeza ya viongozi wa chama hicho kujipendekeza kwa Wazanzibari imetafsiriwa kuwa ni ulaghai wa kisiasa.
- Zanzibar ina viongozi ambao ndio waliopewa dhamana ya kuwasemea Wazanzibari na si mtu mwingine ambaye misimamo yake dhidi ya Wazanzibari inajulikana
- Kwa muda mrefu, CHADEMA wamekuwa wakitoa kauli za kuudhi dhidi ya CUF na viongozi wake hasa wale wanaotoka Zanzibar kama vile CUF ni CCM B, CUF ni chama cha Kiliberali ambacho kinasupport ndoa ya jinsia moja na CUF imeolewa na CCM. Kwa kauli hizo, hakika muungano unaosema hasa na CHADEMA si wa kweli bali ni wa maslahi ya upande mmoja.
- CHADEMA wanataka kuitumia CUF kama daraja ili kujipatia wafuasi Zanzibar. hii ni kutokana na CHADEMA kuendelea kupoteza mvuto visiwani humo hasa kutokana na viongozi wakuu wa chama hicho kuwa na chuki binafsi dhidi ya Zanzibar. Aibu aliyopata Katibu Mkuu wa CHADEMA alipofanya ziara visiwani humo imechochea viongozi wa chama hicho kuona haja ya kuungana na CUF
Kutokana na hali hiyo, Maalim Seif ametoa msimamo ufuatao ambao anategemea kuuwasilisha kwenye vikao halali vya kiutendaji vya CUF na ambao amesema unaungwa mkono na viongozi wengi wa chama hicho;
- Yeye kama katibu Mkuu na mtu anayekubalika na kutumainiwa na Wazanzibari wengi hatashiriki kikao chochote na CHADEMA kujadili jinsi ya kukwamisha mchakato wa Katiba
- Yeye kama Katibu Mkuu hatashiriki ziara iliyotangazwa na CHADEMA ya kuzunguka nchi nzima kwa kile kinachodaiwa kuishtaki serikali ya ccm kwa wananchi
- CHADEMA wameonywa kutojipendekeza kwa CUF na wamekumbushwa msimamo wao kuwa CHADEMA KITASIMAMA KWA MIGUU YAKE YOYOTE NA HAKIHITAJI MSHIRIKA YEYOTE KATIKA JAMBO LOLOTE
Nawasilisha
kuna thread imefutwa haraka niliweka challenge ya CUF ktk hili na umuhimu wa CDM kwa CUF...Nilijua maalimu hatakubali, ila desperately bila CDM kusema neno roho ya CUF haitopona.
CUF wanahitaji heshima, na heshima wataipata kwa kuipa nafasi nafsi CDM..ila itakuja with cost..kwa kukubali faida zote CDM watakazozipata....na CUF hawawezi pata vyote..yaani heshima bila CDM, na wakiikosa heshima ni wazi wataingia shimoni na CCM.
CUF wanahitaji kufuata Njia za CDM kwa kuwa karibuna na CDM ili wapate heshima ya kusimamia misingi ya chama,kuanzia mahakamani hadi uraiani.
Maalimu anayyo shida kukubalina na hiyo hali...nilijua atakumbushia udugu na CCM kuliko aone CDM wakipaa...anajua watakapoingia pemba na CDM km rafiki basi muda si mrefu watakuwa wkaigombania no mbili.
Kati ya viongozi hatari kabisa wa CUF ni huyu Maalim Seif,tuhuma alizotoa dhidi ya viongozi wenzake ni nzito(wao kuhongwa)kwa nini asingewasiliana nao kabla ya kutoa tuhuma hizi kwenye vyombo vya habari? Haoni kuwa amewadhalilisha..?
(2) Umoja ni Nguvu siku zote haoni kuwa ni bora akaungana na vyama pinzani kwa ajili ya kuiwajibisha serikali ya CCM hasa kwa yale ambayo ni ya muhimu sana kitaifa kama suala la Katiba Mpya kwa ajili ya maslahi ya wanainchi na nchi yao zaidi na sio chama..?
(3) Yeye kama Katibu Mkuu wa CUF kwa tamko hili hajamtendea haki Mwenyekiti wake wa chama(Prof.Lipumba) hata kama ameona amekosea isingekuwa busara kumtamkia maneno kama hayo hadharani(anacheza ngoma asiyoijua) jambo hilo ni hatari sana kwa Demokrasia ndani ya chama....anajaribu kuhodhi na kuteka nyara fikra za wanachama wenzake bila hata ridhaa yao(nenda kaseme)
(4) Wana CUF kwa maslahi ya Demokrasia ya hapa nchini kwetu Tanzania ambayo bado ni changa sana na ambayo sisi kama wanainchi lengo letu ni KUIKUZA na KUIBORESHA siku hadi siku,tuwe makini sana,na kufuatilia kwa karibu usemi na mienendo ya viongozi kama hawa ili hatima yake sasa na baadae, tuondokane na kujenga Imani kwa viongozi kama hawa na kuondokana na UTUMWA HUU WA DEMOKRASIA CHANGA ndani ya vyama vetu na Taifa kwa ujumla.
Mkuu utakuwa uli post utumbo kama kawaida yako ndio mana mods waka delete mkuu siku hizi umekuwa mzee huna hoja za msingi mkuu punguza viroba vya mchana jua kali
Naona Anatoa Mawazo Yake Kama Yeye Ndo CUF Peke Yake Lipumba Kahongwa Pesa Mtatitro Kahongwa?? Hayupo Tayr Kuzunguka Tz Kuishtaki CCM Tena Kwenye Mchakato Ulio Andaliwa Na Chadema Huyu Mzee Ikulu Imemnogea Anaona Kama Cuf Wanataka Kuhalibu Mambo!! Viva Lipumba Viva Mtatiro Viva Mbowe
Sasa ngoma imeingia patamu. Sijui CHADEMA watakuja na lipi la kutueleza
Wakiwa ndani ya Muungano wanadai Zanzibar lakini nje ya Muungano kutakuwa na Pemba na Unguja - by J-Kambarage Nyerere.