Maalim Seif Hamad apinga CUF kuungana na CHADEMA

Maalim Seif Hamad apinga CUF kuungana na CHADEMA

Wadau,

Taarifa za kuaminika nilizopata kutoka chanzo cha kuaminika huko Zanzibar zinasema kuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amepinga kitendo cha baadhi ya viongozi wa chama hicho kuingia makubaliano na CHADEMA ili kupinga muswada wa katiba mpya. Maalim Seif amenukuliwa akisema mbele ya baadhi ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwa uamuzi huo si wa kichama bali ni msimamo wa baadhi ya viongozi wa chama hicho ambao wamepewa fedha na CHADEMA ili wawe na msimamo wa aina moja. Maalim Seif anasema kuwa wanaoratibu mpango huo ni Naibu Katibu Mkuu, Julius Mtatiro kwa kushirikiana na baadhi ya wabunge wa chama hicho kutoka Zanzibar. Taarifa zinasema kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Ibrahim Lipumba inaelekea kuwa ameingia kucheza ngoma ambayo haijui na matokeo yake anaonekana kupoteza mwelekeo na kukosa msimamo. Hoja zilizoainishwa na Maalim Seif za kupinga makubaliano hayo ni hizi zifuatazo;

  1. Hakuna kikao chochote cha chombo chochote cha kiutendaji na kimaamuzi cha CUF kilichoketi iwe Zanzibar au Tanzania Bara kujadili jambo hilo na kuweka msimamo wa chama.
  2. Maoni yaliyotolewa na Kambi Rasmi ya Upinzani juu ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba hayakuwa maoni ya vyama vyote vya upinzani bali yalikuwa ni maoni ya CHADEMA pekee waliyoandaa kwa muktadha wa kujipatia umaarufu Zanzibar
  3. CUF ni moja ya vyama vinavyounda serikali ya umoja wa Kitaifa Zanzibar. Kutokana na ukweli kuwa Serikali hiyo imeshirikishwa na yeye (Maalim Seif) ameshiriki katika kuboresha Muswada huo anaamini kuwa chama hicho kupitia Serikali ya Umoja wa kitaifa ambayo imepewa baraka na Wazanzibari wote kimeshiriki kutoa maoni yake. Hivyo madai kuwa Wazanzibari hawajashirikishwa si ya kweli na ni upotoshwaji mkubwa
  4. Misimamo ya viongozi wa CHADEMA dhidi ya Zanzibar mara zote imekuwa hasi na kwa hali hiyo hali iliyojitokeza ya viongozi wa chama hicho kujipendekeza kwa Wazanzibari imetafsiriwa kuwa ni ulaghai wa kisiasa.
  5. Zanzibar ina viongozi ambao ndio waliopewa dhamana ya kuwasemea Wazanzibari na si mtu mwingine ambaye misimamo yake dhidi ya Wazanzibari inajulikana
  6. Kwa muda mrefu, CHADEMA wamekuwa wakitoa kauli za kuudhi dhidi ya CUF na viongozi wake hasa wale wanaotoka Zanzibar kama vile CUF ni CCM B, CUF ni chama cha Kiliberali ambacho kinasupport ndoa ya jinsia moja na CUF imeolewa na CCM. Kwa kauli hizo, hakika muungano unaosema hasa na CHADEMA si wa kweli bali ni wa maslahi ya upande mmoja.
  7. CHADEMA wanataka kuitumia CUF kama daraja ili kujipatia wafuasi Zanzibar. hii ni kutokana na CHADEMA kuendelea kupoteza mvuto visiwani humo hasa kutokana na viongozi wakuu wa chama hicho kuwa na chuki binafsi dhidi ya Zanzibar. Aibu aliyopata Katibu Mkuu wa CHADEMA alipofanya ziara visiwani humo imechochea viongozi wa chama hicho kuona haja ya kuungana na CUF

Kutokana na hali hiyo, Maalim Seif ametoa msimamo ufuatao ambao anategemea kuuwasilisha kwenye vikao halali vya kiutendaji vya CUF na ambao amesema unaungwa mkono na viongozi wengi wa chama hicho;

  1. Yeye kama katibu Mkuu na mtu anayekubalika na kutumainiwa na Wazanzibari wengi hatashiriki kikao chochote na CHADEMA kujadili jinsi ya kukwamisha mchakato wa Katiba
  2. Yeye kama Katibu Mkuu hatashiriki ziara iliyotangazwa na CHADEMA ya kuzunguka nchi nzima kwa kile kinachodaiwa kuishtaki serikali ya ccm kwa wananchi
  3. CHADEMA wameonywa kutojipendekeza kwa CUF na wamekumbushwa msimamo wao kuwa CHADEMA KITASIMAMA KWA MIGUU YAKE YOYOTE NA HAKIHITAJI MSHIRIKA YEYOTE KATIKA JAMBO LOLOTE

Nawasilisha
I See CCM kwa kweli mmezidiwa, ninyi subirini mzigo mzito wa CHADEMA , NCCR& CUF. kwa taarifa yenu tayari makubaliano yameshafikiwa ya CHADEMA kusimamisha mgombea wa Rais na CUF mgombea mwenza na NCCR itatoa Waziri mkuu. Hivi karibuni kazi itaanza ya kutupa nondo za maangamizo yenye vitu vyenye ncha vitakavyowaumiza wana CCM miyooni mwao kila sehemu. Hii itafuatia na kuachiana nafasi za wagombea wa Serikali za mitaa kwenye stronghold ya kila chama na kupiga kampeini za pamoja. Pia makubaliana yanamtaja kama Maalim KUPITISHWA KUWA MGOMBEA ZANZIBAR Kwa tiket ya vyama muungano na hili analijua hivyo hawezi hata kidogo kutoa kauli hizo kwani ameshagundua kuwa SERIKALI YA MSETO ni changa la macho na yeye yuko pale kama picha lakini mwenye madaraka ni makamu wa pili wa Rais. we kaa na umbeya huyo utakuja kukutana na supprise ya kukuua kama siyo kukupa stroke.
 
Ila kiukweli nimependa sana msimamo wa huyu mtu. ningeshangaa kama angekubali kuungana na CHADEMA maana kwa kufanya hivyo kungehatarisha serikali ya umoja wa kitaifa ambayo kwa sasa imekuwa imara sana

Hapo kwenye red, labda husomi au hufuatilii siasa za Zanzibar. Kwa taarifa yako hiyo serikali ya umoja wa Kitaifa kwa sasa ni taabani kuliko wakati mwingine wowote ule. Huyo maalim mwenyewe kila siku anatukanwa na kudharauliwa na wana CCM lakini kang'ang'ania kama nini, nadhani ni kutokana na hulka yake ya kupenda madaraka....
 
Hii story ya kutunga na inafanana na kauli za nape kwa hiyo si ajabu ni kazi ya buku saba za lumumba....angalia hata wachangiaji wanaochangia ushabiki tu hakuna hoja


Sijasikia popote chadema wamesema wataungana na cuf ..... Bali wote kama wapinzani walisusia muswada....kuungana ni issue nyingine sio rahisi rahisi kama watu wanavyoropoka hapa jukwaani


JF sasa hivi imejaa upotoshaji mkubwa
 
Ccm znz wapo kazini sasa naona seif kaamua kwa dhati kuua cuf maksudi ili arudi ccm rasmi kama ni mpinzani wa kweli sioni faida ya maneno Haya kwa chama cha cuf vinginevyo inapigia chapuo ukandamizaji kwenye hoja za msingi kama ushiriki wa pamoja kwenye rasimu ya katiba!!..
 
Sasa ngoma imeingia patamu. Sijui CHADEMA watakuja na lipi la kutueleza

Ndugu yangu pole sana, hebu chekecha akili yako japo kidogo tu. Sisi wenzako tunaojua kuwaza tunaelewa kuwa hii ni habari ya kutengeneza. Na inafahamika wazi kuwa CUF hawashirikiani na CHADEMA kwa masuala ya kichama bali wameamua kushirikia katika suala la katiba kutokana na umuhimu wake kwa watanzania wasasa ukiwemo wewe na wa baadae. Propagandaa hii ina lengo la kudhoofisha vyama vya upinzani katika umoja wao juu ya suala la katiba. CUF na CHADEMA naomba muwe makini na taarifa za namna hii, pia watanzania wote kwa ujumla wetu tupinge muswada uliopitishwa na wabunge wa CCM wa mabadiliko ya sheria ya mabadiliko ya katiba kwani hauna maslahi kwa katiba bora ya watanzania
 
Ccm znz wapo kazini sasa naona seif kaamua kwa dhati kuua cuf maksudi ili arudi ccm rasmi kama ni mpinzani wa kweli sioni faida ya maneno Haya kwa chama cha cuf vinginevyo inapigia chapuo ukandamizaji kwenye hoja za msingi kama ushiriki wa pamoja kwenye rasimu ya katiba!!..

Msihadaike ndugu na habari za kutengeneza zenye lengo la kudhoofisha jitihada za vyama vya upinzani za kupinga muswaada wa mabadiliko ya sheria ya mabadiliko ya katiba uliopitishwa kimizengwe na wabunge wa CCM. Sasa hv viongozi wa CCM wakiwemo mawaziri wanafanya kila jitihada za kutukatisha tamaa ikiwemo taarifa za namna hii ukizingatia kuwa wamebaini kuwa kama katiba mpya itapita katika sura ambayo wanaipinga itakuwa ni mbaya sana kwa maslahi ya matumbo yao. Tuwe makini na kila taarifa za hapa JF.
 
CCM hatuna muda wa marumbano. Waacheni wafu wazikane.

CUF wamezishtukia siasa za kisanii na kilaghai za CHADEMA.

Marriage of convenience. Mmoja hana base bara na mwingine hana base visiwani.

Hivi vyama ni kichekesho.

They'll never step out of their closed door and 2014 is just around the corner.
 
Ccm znz wapo kazini sasa naona seif kaamua kwa dhati kuua cuf maksudi ili arudi ccm rasmi kama ni mpinzani wa kweli sioni faida ya maneno Haya kwa chama cha cuf vinginevyo inapigia chapuo ukandamizaji kwenye hoja za msingi kama ushiriki wa pamoja kwenye rasimu ya katiba!!..

Mkuu lakin umejaribu kuuliza hata source ya habar?
 
Maalim seif amepewa ela na ccm aropoke,kwan ni kweli kuwa tume ya katiba imeenda zanzibar?? Maalm seif amezeeka na anasubir kufa.
Pili,kwan nan kawaambia cuf watoke nje ya bunge siku ile,mbona wao ndo walikuwa wa kwanza kutoka chadema,cuf na nccr wakafata?
Tatu, kwan maalim seif yeye alisubiri nn kutoa tamko mpaka iposikia kuwa cuf,nccr na cdm wanakubaliana kugomea muswada? Mbona walipotoka nje hakupinga?
Nne,inaelekea cuf ni taasis ya kiislam na si chama cha siasa chenye utaaratibu wa kutoa matamko kwa kuwa,mnyekit wake taifa ameunga mkono,katibu wake amepinga,tena anachopinga et ni kuungana,na si kutoka nje ya vikao vya bunge...
Nne,kauli ya kusema kuwa hawataki kuungana na chadema,si sahihi kwa kuwa si chadema tu ndo waliotoka nje,mbona hawaikan nccr mageuz? Na kitendo cha kuwaita vyama vingine vya kikafri maana ake cuf wao ni waislam na wako kwa ajili ya waislam tu wa nchi hii? Ina maana kuwa,chadema wamekosea kuwa ccm na cuf wanawatetea waislam pekee na kuwaacha wakristo na wasio na dini?
Tano,katiba ni ya nan? Ya maalim seif au kikwete,ya cdm au nccr? Kama wanzanzibar wameshirikishwa kweny rasim ya katiba basi cuf wawaunge ccm mkono na si nccr au cdm,na kuwa kama hawajashirikishwa pia wajitoe pia wawaunge mkono ccm kwa kuwa wanaowatetea wazanzibar et ni makafir,ila waislam ccm na cuf wakisema ruksa... Achen ujinga wa udini utawafikisha pabaya sana..
Sita,nawashaur chadema na nccr kuachana na chama kinachowatukana kuwa wao ni makafri,na kuwa wao cdm na nccr wawatetee watanzania..maalim utabaki kuwa wa hovyo mpaka mwisho wako....
Pia kama wbunge wa cuf walipewa ela na cdm,basi pia cuf walipewa ela na ccm kuunda serikali ya umoja wa kitaifa...
Nawaomba cuf mjiondoe kwenye muungano wa cdm na nccr kwan cdm na nccr wataweza kuwatetea watanzania si lazima ninyi muwepo

Baada ya yote hayo unapaswa kufahamu kuwa hii taarifa imetengenezwa yenye lengo la kudhoofisha wapinzani katika kuupinga muswaada walioupitisha wabunge wa CCM kwa mizengwe
 
watanzania wana miliki viwanda vya uongo-jk
 
CCM hatuna muda wa marumbano. Waacheni wafu wazikane.

CUF wamezishtukia siasa za kisanii na kilaghai za CHADEMA.

Marriage of convenience. Mmoja hana base bara na mwingine hana base visiwani.

Hivi vyama ni kichekesho.

They'll never step out of their closed door and 2014 is just around the corner.

Hatudanganyiki na taarifa za kutengeneza ili kutugawa katika hili la katiba. CUF, CHADEMA na NCCR unganisheni nguvu kutetea watanzania
 
CCM hatuna muda wa marumbano. Waacheni wafu wazikane.

CUF wamezishtukia siasa za kisanii na kilaghai za CHADEMA.

Marriage of convenience. Mmoja hana base bara na mwingine hana base visiwani.

Hivi vyama ni kichekesho.

They'll never step out of their closed door and 2014 is just around the corner.

Acha mipasho na taarabu zako hiz, we subiria majibu ya hiz harakati za CDM na CUF ndo mtatafuta pa kutokea.
 
Duhhhh aseeeee chadema bhana wanazuga sana kuhalalisha kulipana posho za kusafuri aminia
 
CHADEMA mnapaswa kutafakari maneno yaliyoandikwa badala ya kukimbilia kusema kuwa maneno ni ya kutengeneza
 
Hiyo ndio ishara tosha kwamba cuf kuna udini inatoka wapi kuwaita CDM makafiri.Kumbe ndio hao wanaua mapadre na kuwamwagia tindikali.Simwoni kafiri zaidi ya wanaofanya ukatiri wanamna hii na kuzuia imani ya watu wengine.
 
Back
Top Bottom