Maajabu ya bongo movie..

Maajabu ya bongo movie..

Wazushi tu,picha za kiswahili lakini zina majina ya kiingereza.
Picha inavyoanza tu, tayari mtu unafahamu itaisha vp.
Hazina ubora wa sauti na picha.
Lazima movie iwe na part one and two.
 
Saidia kukuza ubora wa filamu Tanzania
Saidia kukuza ubora wa filamu Tanzania
Ukisikia hii sauti ujue dada wa kazi yupo sebleni na kashika remote
haha haya bana hii ido accurate sana nana hujakosea umelenga mulemule
 
Nafikiri wanafikiria vitu vikubwa sana ambavyo vinataka bajeti kubwa sana. Waigize maisha ya kawaida ya watanzania na waafrika kwa ujumla. Mfano kuna filamu ya Neria na Yellow Card zilikuwa zipo simple sana waligiza maisha ya kawaida ya kiafrika ndo maana filamu hizo bado mpaka leo zinaoneka bora. Kitu kingine ni vipaji kwenye uigizaji nafikiri hapo ndo kwenye tatizo kubwa zaidi sio kila mtu anaweza kuigiza
 
Kwangu hakuna mtu anayeangalia upuuzi wa bongo movies, even hata beki tatu huangalia series za kikorea .
 
Waachane tu na hiyo kazi mana ishawashinda.
Tusubir vizazi vijavyo huenda wakawa wako vzur
 
Kitu nilichoona wameweza ni maandamano,kweli yalikuwa mazuri stealing Bashite alimudu sana nafasi yake.
 
uki
Wazushi tu,picha za kiswahili lakini zina majina ya kiingereza.
Picha inavyoanza tu, tayari mtu unafahamu itaisha vp.
Hazina ubora wa sauti na picha.
Lazima movie iwe na part one and two.
ukiangalia movie lazier ukase na remote pembeni main mara husikii mara makelele base ball tutu
 
Hawa bongo muv ni utumbo tu kwenye filamu ya mchawi wa kijij et mchawi anaua kwa panga na shoka si ungese huu
 
Bongo movie wapuuzi hawajielewi kabisa. Movie zao mbaya,hazina quality nzuri ya Picha wala sauti,maudhui mbaya wanachojua kuvaa vi pants na mapaha yao yenye miinuko na mabonde kama milima ya nyika
 
sawa mimi pia siwapendi maana BONGO MOVIE wanabolonga bolonga. lakini pia mvuto wao unapungua zaidi kwasababu ya wao kukosa Uhuru wa kuutumia uhalisia, nikimaanisha kuwa wapewe haki ya kuigizia na gwanda halisi za jeshi au polisi, kutumia vituo halisi vya polisi, mahospitaki, makambini na hata sehemu nyingine zote zenye kuleta mvuto na uhalisia wenyewe. Pia Basata isimamie Kazi zao kulingana na kile walichokifanya,
Aisee, hii ni kweli kabisa!
 
bongo movie yenyewe majanga, bora hata wajishughulishe na shughuli nyingine za uzalishaji mali..KILA SIKU VITU VILEVILE
 
1.Wachawi wanakamatwa na Mgambo
2.Majeruhi na maiti zinabebwa kwa mikono mitupu
3.Jini anavuka barabara anaangalia kulia na kushoto anaangalia usalama kwanza
4.Risasi inachukua Dakika kumfiki mpigwaji
5.Mtu yupo na demu wake supermarket wanachukua nusu saa nzima wakati movie ina saa moja na nusu
6.Mtu akipigwa ngumi anaangalia pakuangukia kwa usalama wake
7.Milio ya Risasi kama unawasha njiti za kiberiti
8.Kahaba lazima avute sigara
9.Jambazi lazima livae koti refu na miwani meusi
10.Mganga wa kienyeji lazima awe porini,mchafu,halafu anaongea kwa ukali!
11.Kwenye subtitle mgeni anaitwa New People
12.Hospitalini wapo wao tu
13.Jambazi anavua viatu akavamia kwenye nyumba
14.Mtanga na Serengo lazima wawe walinzi
15.Jini lazima awe mwanamke
16.JB anavaa shati moja kwenye movie sita
17.Tukio linaonywshwa lilitokea mwaka 1977 halafu ukutani kuna picha ya Rais wa sasa Magu
18.Familia ya kitajiri lazima waongee kizungu Dadii!!..Mamii!!
19.Tajiri lazima amuoe maskini
20.Gereza ni nyumba ya mtu yenye madirisha ya chuma
21.Kila anayetoa habari za maisha yake ya nyuma lazma anyanyue uso juu
22.Mapenzi yanaanza pale mwanamke anapoalibikiwa na gari afu mwanaume anatokea kusaidia
23.Mlinzi wa getini lazima awe hana akili nzuri
24.Kitu pekee kinachoharibika ni Glass tu
25.jambazi laziwa awe na sura mbaya na awe ananuna muda wote
26.Movie inaanza mtoto mweusi kichwani kipilipili cha nguvu, akiwa mkubwa ni mweupe na nyele za kiarabu
Nalog Off bongo movie
Malizia na ww.
 
Back
Top Bottom