Maajabu ya bongo movie..

Maajabu ya bongo movie..

Movie mtu yuko kijijini ana wave na black.. Au dada anaenda kazini kavaa mavazi ya disco mpaka kero. Au mkaka anaenda kazini lakini kavaa nguo za rangi rangi utafikiri mwanamuziki anaenda kufanya show.. Kila mfanyabiashara anaongelea containers bandarini.. Mtu akiigiza fani ya mtu mfano uhasibu au udaktari haombi kupigwa msasa na wenye fani yao.

Nafikiri kwenye quality tunaweza jitetea gharama but basi hata userious kwenye kazi. Hili kwenye bongo movies silioni, naona ulipuaji tu wa kazi. Makosa kibao sio kwenye uigizaji wala kwenye subtitles wala kwenye editing.

Nawashauri bongo movie wawe serious na kazi hata kama quality ya picha sio nzuri sana at least content na flow ya matukio inaweza vutia wazalendo kuangalia.
 
Tatizo wanataka kuigiza maisha ambayo kiuhalisia hata wao hawajayaishi ndiyo maana wanapoteza uhalisia
 
1.Wachawi wanakamatwa na Mgambo
2.Majeruhi na maiti zinabebwa kwa mikono mitupu
3.Jini anavuka barabara anaangalia kulia na kushoto anaangalia usalama kwanza
4.Risasi inachukua Dakika kumfiki mpigwaji
5.Mtu yupo na demu wake supermarket wanachukua nusu saa nzima wakati movie ina saa moja na nusu
6.Mtu akipigwa ngumi anaangalia pakuangukia kwa usalama wake
7.Milio ya Risasi kama unawasha njiti za kiberiti
8.Kahaba lazima avute sigara
9.Jambazi lazima livae koti refu na miwani meusi
10.Mganga wa kienyeji lazima awe porini,mchafu,halafu anaongea kwa ukali!
11.Kwenye subtitle mgeni anaitwa New People
12.Hospitalini wapo wao tu
13.Jambazi anavua viatu akavamia kwenye nyumba
14.Mtanga na Serengo lazima wawe walinzi
15.Jini lazima awe mwanamke
16.JB anavaa shati moja kwenye movie sita
17.Tukio linaonywshwa lilitokea mwaka 1977 halafu ukutani kuna picha ya Rais wa sasa Magu
18.Familia ya kitajiri lazima waongee kizungu Dadii!!..Mamii!!
19.Tajiri lazima amuoe maskini
20.Gereza ni nyumba ya mtu yenye madirisha ya chuma
21.Kila anayetoa habari za maisha yake ya nyuma lazma anyanyue uso juu
22.Mapenzi yanaanza pale mwanamke anapoalibikiwa na gari afu mwanaume anatokea kusaidia
23.Mlinzi wa getini lazima awe hana akili nzuri
24.Kitu pekee kinachoharibika ni Glass tu
25.jambazi laziwa awe na sura mbaya na awe ananuna muda wote
26.Movie inaanza mtoto mweusi kichwani kipilipili cha nguvu, akiwa mkubwa ni mweupe na nyele za kiarabu
Nalog Off bongo movie
Malizia na ww.
We jamaa umenichekesha mpaka basi.!
 
Mkuu asante kwa kuufanya usiku wangu kuwa wenye furaha maana nimecheka almanusura kutapika
 
2abdd5dad61b82c37d41829b0b0e5c30.jpg

Kwa mwendo huu vipi ?
 
Kwani lazima kila mtu aanzishe thread ya aina hii kuhusu Bongo movie? Hiyo text inazunguka kuanzia mitandaoni... haina jipya.
 
Nafikiri wanafikiria vitu vikubwa sana ambavyo vinataka bajeti kubwa sana. Waigize maisha ya kawaida ya watanzania na waafrika kwa ujumla. Mfano kuna filamu ya Neria na Yellow Card zilikuwa zipo simple sana waligiza maisha ya kawaida ya kiafrika ndo maana filamu hizo bado mpaka leo zinaoneka bora. Kitu kingine ni vipaji kwenye uigizaji nafikiri hapo ndo kwenye tatizo kubwa zaidi sio kila mtu anaweza kuigiza
Akili itumike asilimia kubwa bongo movies walipata sifuri darasani
 
bongo movie wapo tayari bajeti ya filamu 1...waigawanye ziwe filamu 10...
wataweza wapi hayo...matokeo yake wanatoa filamu kama magazeti ya kila wiki..!!.. ufanisi utatokea wapi..??..
 
Hawa wa kwetu wanawaza uchaguzi tu na kampen zake waje na misemo mama mkanye mwanao,maskin hawajui kilicho nyuma ya pazia sasa hakuma pa kula wamegeukia maandamano badala ya kufanya kazi,Hapa kazi tuuu
 
jini yupo porini anakwepa miiba.movie ina party 2 ya nusu saa tuu.camera zenyewe za kwenye harusi
 
Back
Top Bottom