MAAJABU: Nyoka afa na mmiliki wake Songea

MAAJABU: Nyoka afa na mmiliki wake Songea

Licha ya kwamba ni mzawa wa huku haimaanishi natetea kuhusu uwepo wa uchawi,ninaamini upo kama ilivyo katika maeneo mengine nchi hii.
Ninachokikataa ni watu kurank sumbawanga km sehemu ambako uchawi ni tishio si kweli,unaweza kunieleza ni mkoa gani Tz ambako hakuna uchawi?


Ukipita mitaa utaona vibao tu vyajieleza:
Mganga kutoka sumbawanga
Mganga kutoka Tanga
Mganga kutoka Kigoma

Ila kuna baadhi ya sehemu huoni waganga kutoka huko...
We huoni yatosha kujieleza kuwa maeneo hayo yana uchawi mwingi?
 
Ukipita mitaa utaona vibao tu vyajieleza:
Mganga kutoka sumbawanga
Mganga kutoka Tanga
Mganga kutoka Kigoma

Ila kuna baadhi ya sehemu huoni waganga kutoka huko...
We huoni yatosha kujieleza kuwa maeneo hayo yana uchawi mwingi?
Mganga kutoka Machame
 
Isije ikawa hao wanaojiita '' wananchi wenye hasira" walimtembezea kichapo na huyo mmiliki wa nyoka halafu watung story baada ya kuona mambo yameharibika. Nawashauri polisi wasisikilize " illusion" wafanye uchunguzi wa kina bila ushabiki wala hisia za kijamii na pathologists wafanye kazi yao kwa umakini ili kujua chanzo cha kifo cha kaka yangu KOMBA
 
Mh...! mambo mengine sijui yanawezaje kufanyiwa utafiti wa kisayansi ili kufahamu uhusiano uliopo kati ya kupigwa kwa nyoka na kuuwawa kwa mmiliki wa nyoka.
kwenye maabara ya asili ya afrika kaka inawezekana.lakini kwenye maabara ya wazungu sijui!
 
Ukipita mitaa utaona vibao tu vyajieleza:
Mganga kutoka sumbawanga
Mganga kutoka Tanga
Mganga kutoka Kigoma

Ila kuna baadhi ya sehemu huoni waganga kutoka huko...
We huoni yatosha kujieleza kuwa maeneo hayo yana uchawi mwingi?
Kama mtu aliyesoma Cambridge na mwingine UDOM
 
[QUOTE="namwakalima, post: 19060625, member: 2653iRebirth katika mwili mwingine au katika nafsi ingine ? Yaani kutoka ng'ombe hadi chui?[/QUOTE]
Sijui kutoka aina moja ya mnyama kwenda mwingine exceptional kwa binadamu kurudi kama binadamu tena au mnyama fulani.
Kuna ukoo fulani naufahamu maeneo ya Mangula huko morogoro wazee wakifariki wanageuka kuwa simba. Nililikataa hili ila nilikuja kushuhudiwa na mtoto mmoja wa huyo mzee aliyegeuka simba. Stori ni ndefu sana
 
mshana jr umeahidi utakuja na ufafanuzi nimesubiri sijakupata naomba utapofafanua unitag nijifunze
 
Bado hatujajua pengine jamaa alikuwa ni msanii...kama wale ambao hucheza na majoka


Jaribu kutumia akili si kila kitu lazima utafute majibu yasiyowezekana. Umeona wapi mfugaji kuku anakufa baada ya kuku wake kuchinjwa na anakataza watu wasichinje kuku wake kwani wakichinja naye atakufa? Nimeishi hii mikoa na miji yake hiyo niliyotaja hapo juu, kule usanii huu ni wa kawaida sana. mshana jr njoo utoe somo kidogo kwa watu wasiopenda ukweli, tafadhali nakuomba ndugu yangu.
 
Muwe mnaandika vitu mkiwa na uhakika,unamewahi kusikia tukio gani la ajabu kuhusu uchawi Sumbawanga? watu wanatia chumvi mno kumbe uhalisia wake hata sio hivyo.


Mkuu, nimeishi huko na ninayokuambia mbona ni kama chai tu kule, yaani si cha hajabu kwa wakazi wa kule. Ukiwa tu pale mjini huwezi kujuwa chochote ila huko vijijini, usisikie. Kuna vituko si kawaida na hicho nilichosema ni cha mtoto. Nimeshaona mtu anaruka na ng'ombe kuja kutua shambani, na hii utabisha? Nakuambia nimeshuhudia.
 
Watanzania tunatumia 1/10 ya uwezo wetu wa akili...kwa utafuti wangu kifo cha jamaa kilisababishwa na kuumwa na nyoka aliyekuwa amemficha kwenye koti na hakuna ushirikina hapo
 
Masihara jamaa anagongwa gongwa kwa nyuma na joka inaonekana Uyo mwenye joka marehemu alikuwa na masihara na maisha ya dereva boda boda acha afee
 
Imeandikwa, 'amelaaniwa amtegemeaye mwanadamu na kumfanya..............' Sasa we unaenda kumkabidhi mganga roho yako, halafu yeye anaikabidhi kwa nyoka, unategemea nini hapo kama c kumjaribu Muumba?
 
Back
Top Bottom