MAAJABU: Nyoka afa na mmiliki wake Songea

MAAJABU: Nyoka afa na mmiliki wake Songea

Mkuu, nimeishi huko na ninayokuambia mbona ni kama chai tu kule, yaani si cha hajabu kwa wakazi wa kule. Ukiwa tu pale mjini huwezi kujuwa chochote ila huko vijijini, usisikie. Kuna vituko si kawaida na hicho nilichosema ni cha mtoto. Nimeshaona mtu anaruka na ng'ombe kuja kutua shambani, na hii utabisha? Nakuambia nimeshuhudia.
Ha ha ha sina uhakika
 
Kwa lugha rahisi sana huyu mmiliki wa nyoka ndg Komba (26) mkazi wa Songea alikuwa na MAHABA. Yawezekana alikuwa anamtegemea sana ktk maisha yake.

Hivyo huyu nyoka alikuwa sehemu ya akili na mwili wa ndg Komba.

Hivyo kitaalamu kilicho muua Komba ni tele-empathy (telempathy), kwa kiswahili ni midadi. Midadi huja pale ambapo mtu amebeda hisia kali juu ya kitu/mtu. Komba alikuwa anamhurumia nyoka wake kiasi kwamba alikuwa anayabeba maumivu ya kipigo cha nyoka.

Nyoka wake alipokufa, Komba akawa amepatwa na maumivu ya kihisia kwa kiasi kikubwa na kupelekea kinga yake kushuka mno.

Pia ktk mwili wake palitokea reactions ambazo ni negative kwa afya na uhai wake ndiyo maana akaanza kutokwa mapovu na hatimaye kifo chake. Kuna Uhusiano Mkubwa Sana Kati Ya Hisia Na Uhai.
 
Hapo umezungumzia vitu viwili tofauti!
1: Alikuwa anamtegemea sana! Kivipi? Kama kiungo cha mwili, mlinzi au nguvu za giza; a bread winner?!
2: Tele-empathy! Je hii ni sawa na a deep emotional attachment to the serpent?
Tusaidie kidogo hapo!
 
hivi Sayansi inaamini katika mapenzi na hisia??
au sayansi asilia??
 
Japo Sayansi haiamini Uchawi ila Sayansi yenyewe ni Uchawi wa hali ya juu, sawa na mbweha na mbwamwitu tu.
 
Kama ulifwatilia. Huu mkasa jamaa kazikwa Jana. Kabla ya kuzikwa nduguze walizinguana vilivyo, wakisema azikwi mpaka aletwe nyoka wake azikwe nae ndio usia aliotoa.

Hali ya mzozano iliendela hadi serikali za mitaa wakaonekana na kusuluhisha ikiwemo kuelezwa nyoka yuko chini ya mamlaka ya serikali kwa sasa kumpata ngumu sana.

Ndipo wakakubaliana azikwe bila nyoka wake.
 
Back
Top Bottom