Maafisa Kikosi cha Zimamoto na Polisi kumlipa Vanessa Bryant fidia ya USD Milioni 28.8 kwa kusambaza picha za Ajali ya Mumewe

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,553
Vanessa Bryant atalipwa na Maafisa wa Polisi na Zimamoto wa Kaunti ya Los Angeles zaidi ya Bilioni 65 za Kitanzania kwa kusambaza Mtandaoni picha za Ajali Mbaya ya Helkopita iliyoua Mumewe na Binti yake Januari 26, 2020

Kwa kuzingatia Ibara ya 16 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayosisitiza Haki ya Faragha, Unazungumziaje hali halisi ya Utunzaji wa Faragha za watu iliyopo kwenye Mazingira yetu?

====

Vanessa Bryant ambaye ni Mke wa Staa wa mpira wa kikapu wa Marekani Marehemu Kobe Bryant, amekubali kulipwa fidia ya dola za kimarekani milioni 28.8 ($28,850,000) kutokana na makosa yaliyofanywa na Nchini Marekani ya kusambaza picha za ajali ya Helikopta iliyomuua Mumewe a Mtoto wao January 26 mwaka 2020.

Kwenye kesi hiyo iliyofunguliwa na Vanessa Bryant a Chris Chester ambaye naye alipoteza Mke a Mtoto kwenye ajali hiyo, waliwashitaki Maafisa hao kwa kitendo cha kuchukua picha za mabaki ya Binadamu waliofariki kwenye eneo la tukio kama "ukumbusho" na kuzisambaza, kitendo ambacho Vanessa alisema kilimfanva apitie changamoto za kihisia na kuweweseka usiku hivvo akaiburuza Taasisi hivo Mahakamani kwa uzembe na uvamizi wa haki za faragha.

Habari kutoka Los Angeles zinasema sasa Vanessa (40) amefikia makubaliano ya mwisho na Kaunti ya Los Angeles na kukubali kulipwa dola za kimarekani milioni 28.85 kutoka kwa Bodi va Wasimamizi wa Kaunti hivo ambapo makubaliano hayo yanajumuisha madai kutoka kwa Vanessa na yanahusu madai yoyote ya baadaye kutoka kwake na Watoto wa Kobe ambao ni Natalia (20), Bianka (6) na Capri (3).


Jimbo la California tangu wakati huo limepitisha sheria ya jimbo inayokataza Maafisa vya Vikosi vya Dharura na Uokoaji kupiga bila ruksa picha za Watu waliofariki katika eneo la ajali au uhalifu.

Chanzo: Millard Ayo
 
Kama ni bongo, ukiweza kutumia sh 100,000 kwa siku × mwezi 1 ambao ni siku 30 × mwaka 1 ambao ni siku 360 × miaka 27 = ndio unamaliza 1 billion.
Hiyo ni sawa na umetumia 1% ya 65 billions alizo lipwa Vanessa Bryant
 
Kama ni bongo, ukiweza kutumia sh 100,000 kwa siku × mwezi 1 ambao ni siku 30 × mwaka 1 ambao ni siku 360 × miaka 27 = ndio unamaliza 1 billion.
Hiyo ni sawa na umetumia 1% ya 65 billions alizo lipwa Vanessa Bryant
Au Kwa sisi wapenda bata,ukitumia laki 5 kila siku,Kwa miaka 27 ndio unakuwa umetumia billion 5,zinabaki billion 60!
 
Kila jamii ina tamaduni zake
Wala hakuna tamaduni. Hiyo ni sheria na katiba. Sheria ya faragha
Hiyo ndiyo USA. Hapa bongo unajiunga bando la saa 24. Mtandao unakata unaandika emergence na unashida kuongea na mtu. Siyo kwasababu ni simu yako mbovu hapana ni wao mtandao unazingua. Mtandao unarudi na kifurushi kimeisha. Hakuna fidia.
 
Subiri kwanza
IMG-20230302-WA0079.jpg
 
Bongo ujuaji mwingi sana. Katiba na sheria imewekwa mfukoni. Mtu unadhulumiwa haki yako ila sasa kudai, huo mlolongo wa kudai haki yako. Utachoka
Haya ni mambo ya kitaaluma mkuu, mbona Plea bargain huku inatumika?
Mbona gazeti likitoa taharifa ya uwongo linakulipa ukidai fidia?
So huku wengi hawajui haki zao ila waki yakanyaga kwa wachache wataisoma.
 
......Kwa kuzingatia Ibara ya 16 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayosisitiza Haki ya Faragha, Unazungumziaje hali halisi ya Utunzaji wa Faragha za watu iliyopo kwenye Mazingira yetu?........
juzi tu hapa tumeshuhudia madudu ya law enforcer wetu huko Zanzibar....


Bongo hakuna faragba
 
Haya ni mambo ya kitaaluma mkuu, mbona Plea bargain huku inatumika?
Mbona gazeti likitoa taharifa ya uwongo linakulipa ukidai fidia?
So huku wengi hawajui haki zao ila waki yakanyaga kwa wachache wataisoma.
Soma habari kisha ilete hapa Tanzania.
Maafisa wa polisi (serikali) wanaweza kukulipa? Kwa watu au mashirika binafsi watakulipa ila unaweza kulipwa au usilipwe. Ila utekelezaji ni 50%.
Hii serikali ya CCM inayohujumu uchaguzi na kuwazuia watu wasifanye siasa wakati katiba na sheria inaruhusu?
Mkuu wa mkoa anaenda kuchapa walimu na hachukuliwi hatua? Tusidanganyane.
 
Back
Top Bottom