Ma sheikh arusha wamtambua meya wa arusha

Bramo

JF-Expert Member
Oct 21, 2009
13,160
10,007
Katika hali inayoonesha kuwa lengo lao ni kuwajibu Maaskofu wa ARUSHA, Viongozi wa dini ya Kiislam wamesema wanamtambua Meya wa ARUSHA na watampa Ushirikiano wote.

Haya sasa Mary Chitanda (Chanzo cha yote), tukusikie ukiwaambia Mashekh nao wavue Kobaz, Misuli, Kanzu, vilemba na Balaghashia (Kama ulivyowaambia Maaskofu wavue Majoho sijui ulikuwa unataka wabaki Uchi) na kuingia ulingo wa SIASA.
Au ulikuwa unamaanisha kuingilia kwao siasa ni kwenda kinyume na matakwa ya CCM
 
Katika hali inayoonesha kuwa lengo lao ni kuwajibu Maaskofu wa ARUSHA, Viongozi wa dini ya Kiislam wamesema wanamtambua Meya wa ARUSHA na watampa Ushirikiano wote.

Haya sasa Mary Chitanda (Chanzo cha yote), tukusikie ukiwaambia Mashekh nao wavue Kobaz, Misuli, Kanzu, vilemba na Balaghashia (Kama ulivyowaambia Maaskofu wavue Majoho sijui ulikuwa unataka wabaki Uchi) na kuingia ulingo wa SIASA.
Au ulikuwa unamaanisha kuingilia kwao siasa ni kwenda kinyume na matakwa ya CCM

Source??
 
Katika hali inayoonesha kuwa lengo lao ni kuwajibu Maaskofu wa ARUSHA, Viongozi wa dini ya Kiislam wamesema wanamtambua Meya wa ARUSHA na watampa Ushirikiano wote.

Haya sasa Mary Chitanda (Chanzo cha yote), tukusikie ukiwaambia Mashekh nao wavue Kobaz, Misuli, Kanzu, vilemba na Balaghashia (Kama ulivyowaambia Maaskofu wavue Majoho sijui ulikuwa unataka wabaki Uchi) na kuingia ulingo wa SIASA.
Au ulikuwa unamaanisha kuingilia kwao siasa ni kwenda kinyume na matakwa ya CCM


Mary Chitanda alikosea lakini na wewe hujatumia busara maana ya maaskofu yalikua ya Mary. lakini wewe kuwatukana masheikh ni ujinga wako unauonyesha na chuki za kidini.
Yawezekana mary aliona kosa na akikiri hata rudia lakini safari hii unamshawishi aendelee kufanya ujinga

Hujatumia busara kusuluhisha tatizo vinginevyo useme hayo ni maneno umeamua kuwatukana masheikh
 
Katika hali inayoonesha kuwa lengo lao ni kuwajibu Maaskofu wa ARUSHA, Viongozi wa dini ya Kiislam wamesema wanamtambua Meya wa ARUSHA na watampa Ushirikiano wote.

Haya sasa Mary Chitanda (Chanzo cha yote), tukusikie ukiwaambia Mashekh nao wavue Kobaz, Misuli, Kanzu, vilemba na Balaghashia (Kama ulivyowaambia Maaskofu wavue Majoho sijui ulikuwa unataka wabaki Uchi) na kuingia ulingo wa SIASA.
Au ulikuwa unamaanisha kuingilia kwao siasa ni kwenda kinyume na matakwa ya CCM

Kama ni kweli viongozi wa kiislam watakuwa hawafanyi vema??? Naona kama wanasababisha tu mambo kuzidi kuwa shaghalabaghala. Wangeanza wao kutoa kauli ya kumtambua huyo meya ningesema labda wana sababu za msingi!!!! Lakini kwa hapa naona wanachemsha tu.... Kwanini wasubiri kilichosemwa na maaskofu ndo waende kinyume nacho.... huu ni udini...Mimi ningeshauri kama wenzao wametoa kauli waangalie ni kwa nini ikiwezekana wajadiliane nao kwanza kupata sababu na malengo kabla hawajaenda against.. otherwise wanyamaze tu itawapa heshima zaidi kuliko hii ya kupinga tu ili mradi na wao wasikike!!!

Ni hayo tu.:A S 27::A S 27::A S 27:
 
huyo anayeomba source leo jana alikuwa wapi kusikiliza vyombo vya habari?! Mbona suala lipo uchi! By the way hao masheikh wasituzingue bana walikuwa wapi kumkubali kabla mpaka waone maaskofu wamemkataa nao ndio wanajitia kimbelefront kumkubali kama si unafiki ni nini?
 
Mleta mada ni mchukia uislam habari yake haina source na uislamu umekataa kuuwa/kudhulum nafsi hao mashekh watakaohalalisha mauaji yale ya Arusha watakuwa si mashekh ni mashehena.

{{Wala msiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu amekataza (kuiua) isipokuwa kwa haki (Akahuhumu hakimu kuwa mtu huyo anastahiki kuuawa na akatoa amri ya kuuawa). Na mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi Tumempa nguvu mrithi wake (juu ya muuaji huyo, akitaka ataomba kwa hakimu kuwa amuuwe kama alivyomuuwa mtu wake na akitaka atamsamehe, na akitaka atamtoza kitu). Basi (huyo mrithi asifanye fujo katika kuua kwa ajili ya huyo mtu wake aliyeuliwa). Hakika yeye atasaidiwa (na Sharia maadamu anayo haki).}} [17:33]
Tukiegemea kwenye aya hii, hairuhusiki kwa Uislamu kuua mtu yeyote asiye na kosa kwa baadhi ya makosa ya jinai. Ni vyema tukakumbuka katika nukta hii, tofauti iliyofanywa hapo juu baina ya Qur-aan na Sunnah, na Waislamu; ni Qur-aan na Sunnah pekee ndizo zilizoafikiwa kuwa zinaendana pamoja na matakwa ya Muumba, wakati Waislamu wanaweza sana kutetereka. Hivyo, kama Muislamu yeyote ataua mtu asiye na hatia, Muislamu huyo ametenda dhambi mbaya kabisa, na hakika tendo hilo haliwezi kudaiwa kuwa limefanywa "kwa jina la Uislamu".
 
huyo anayeomba source leo jana alikuwa wapi kusikiliza vyombo vya habari?! Mbona suala lipo uchi! By the way hao masheikh wasituzingue bana walikuwa wapi kumkubali kabla mpaka waone maaskofu wamemkataa nao ndio wanajitia kimbelefront kumkubali kama si unafiki ni nini?

Siwezi kukataa ila ukweli utabaki paleplae hao masheikh ni wale wa jumuia ya Kiislam ya CCM inaitwa BAKWATA. Wao wapo kwa ajili ya maslahi ya chama zaidi.
 
Siwezi kukataa ila ukweli utabaki paleplae hao masheikh ni wale wa jumuia ya Kiislam ya CCM inaitwa BAKWATA. Wao wapo kwa ajili ya maslahi ya chama zaidi.

MUONGO MKUBWA,fanya utafiti acha kueleza uongo mradi utetee hoja yako.Masheikh wa BAKWATA si wote wako CCM na BAKWATA si organization ya kisiasa,kwahiyo tuseme maaskofu wako CHADEMA kwakuwa wali-condemn mauaji ya Arusha,wao walikuwa wanatimiza wajibu wao na BAKWATA imetimiza wajibu wake......Kwakuwa wametofautiana kauli kwenye hili la meya ndo unaanza kuwasema kwa kejeli???Lini na wapi imeandikwa kwamba BAKWATA na MAASKOFU wakubaliane kwenye kauli zao.......i call this cheap arguments,thats demorcracy and there is freedom which allow us to differ in our opinions for God's sake.Eti wako kumaslahi ya chama zaidi?????kama wewe ulivyo kwa maslahi ya chama zaidi na ndo maana unasema uongo kutetea hoja ya chama fulani iliyoungwa mkono na maaskofu.
 
am not sure...but akili yangu inanituma watanzania sasa mbegu ya udini inanza kuchipua kwenye mioyo yetu..the way pipo zinavyochangia mada yenye mwelekeo wa kidini hasa matamko ya viongozi wa kidin....it seems kila mtu anavutia upande wake(dini anayoiamini ) tunaelekea wapi bandugu????????????
 
MUONGO MKUBWA,fanya utafiti acha kueleza uongo mradi utetee hoja yako.Masheikh wa BAKWATA si wote wako CCM na BAKWATA si organization ya kisiasa,kwahiyo tuseme maaskofu wako CHADEMA kwakuwa wali-condemn mauaji ya Arusha,wao walikuwa wanatimiza wajibu wao na BAKWATA imetimiza wajibu wake......Kwakuwa wametofautiana kauli kwenye hili la meya ndo unaanza kuwasema kwa kejeli???Lini na wapi imeandikwa kwamba BAKWATA na MAASKOFU wakubaliane kwenye kauli zao.......i call this cheap arguments,thats demorcracy and there is freedom which allow us to differ in our opinions for God's sake.Eti wako kumaslahi ya chama zaidi?????kama wewe ulivyo kwa maslahi ya chama zaidi na ndo maana unasema uongo kutetea hoja ya chama fulani iliyoungwa mkono na maaskofu.

Mama wewe ndio umesema maneno hayo kwenye rangi nyekundu, Uislam unasema tukemee uovu na dhulma ya aina yoyote ile hausemi anaekemea yupo chadema. Toa fikra ya kidini soma vizuri maoni yangu utaelewa naamanisha nini. Na kama huijui bakwata soma historia yake ilivyoanzishwa na nani aliianzisha kwanini na kabla ya hapo kulikuwa na chombo gani cha waislamu na kwanini kilivunjwa!
 
mleta mada ni mchukia uislam habari yake haina source na uislamu umekataa kuuwa/kudhulum nafsi hao mashekh watakaohalalisha mauaji yale ya arusha watakuwa si mashekh ni mashehena.

{{wala msiue nafsi ambayo mwenyezi mungu amekataza (kuiua) isipokuwa kwa haki (akahuhumu hakimu kuwa mtu huyo anastahiki kuuawa na akatoa amri ya kuuawa). Na mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi tumempa nguvu mrithi wake (juu ya muuaji huyo, akitaka ataomba kwa hakimu kuwa amuuwe kama alivyomuuwa mtu wake na akitaka atamsamehe, na akitaka atamtoza kitu). Basi (huyo mrithi asifanye fujo katika kuua kwa ajili ya huyo mtu wake aliyeuliwa). Hakika yeye atasaidiwa (na sharia maadamu anayo haki).}} [17:33]
tukiegemea kwenye aya hii, hairuhusiki kwa uislamu kuua mtu yeyote asiye na kosa kwa baadhi ya makosa ya jinai. Ni vyema tukakumbuka katika nukta hii, tofauti iliyofanywa hapo juu baina ya qur-aan na sunnah, na waislamu; ni qur-aan na sunnah pekee ndizo zilizoafikiwa kuwa zinaendana pamoja na matakwa ya muumba, wakati waislamu wanaweza sana kutetereka. Hivyo, kama muislamu yeyote ataua mtu asiye na hatia, muislamu huyo ametenda dhambi mbaya kabisa, na hakika tendo hilo haliwezi kudaiwa kuwa limefanywa "kwa jina la uislamu".
hapo ndo nakukubali sokomoko ukweli utakuweka huru mkuu. Naunga mkono hoja yako mkuu nimekugongea naliasante.
 
Mama wewe ndio umesema maneno hayo kwenye rangi nyekundu, Uislam unasema tukemee uovu na dhulma ya aina yoyote ile hausemi anaekemea yupo chadema. Toa fikra ya kidini soma vizuri maoni yangu utaelewa naamanisha nini. Na kama huijui bakwata soma historia yake ilivyoanzishwa na nani aliianzisha kwanini na kabla ya hapo kulikuwa na chombo gani cha waislamu na kwanini kilivunjwa!

Sina fikra za kidini ila wewe unazo kwakusema kwenye post yako BAKWATA wako kwa maslahi ya chama zaidi,naijua historia ya BAKWATA,hatuko kwenye mfumo wa chama kimoja,kuna watu kwenye hiyo jumuiya wako CUF,CHADEMA,APPT nakadhalika nawafahamu,sasa wewe kusema wako kwa maslahi ya chama ndo nikasema ni uongo mweupe, na nikatoa mfano sijasema ndivyo ilivyo naona una badili mwelekeo wa point yangu ya msingi,kwamba je kwakuwa maaskofu walitimiza wajibu wao ambao mi naona wako sahihi kabisa wa kupinga kile kilichofanyika Arusha,je tuseme nao wako CHADEMA na wako kwa maslahi ya chama??? Nilichotaka kusema ni kuwa BAKWATA wamesema wanavyoona wao na wakaamua kumuunga mkono meya ambaye kuchaguliwa kwake kulikuwa na utata,lakini si kwamba wako kwa maslahi ya chama,kwa kuwa wanajumuiya ya BAKWATA si wanachama wa chama kimoja.
 
ni haki yao ya msingi na wanajua wanacho fanya,may be kwao kutumia nguvu ndo msingi wa uongozi so wako huru kutoa maoni
 
sina fikra za kidini ila wewe unazo kwakusema kwenye post yako bakwata wako kwa maslahi ya chama zaidi,naijua historia ya bakwata,hatuko kwenye mfumo wa chama kimoja,kuna watu kwenye hiyo jumuiya wako cuf,chadema,appt nakadhalika nawafahamu,sasa wewe kusema wako kwa maslahi ya chama ndo nikasema ni uongo mweupe, na nikatoa mfano sijasema ndivyo ilivyo naona una badili mwelekeo wa point yangu ya msingi,kwamba je kwakuwa maaskofu walitimiza wajibu wao ambao mi naona wako sahihi kabisa wa kupinga kile kilichofanyika arusha,je tuseme nao wako chadema na wako kwa maslahi ya chama??? Nilichotaka kusema ni kuwa bakwata wamesema wanavyoona wao na wakaamua kumuunga mkono meya ambaye kuchaguliwa kwake kulikuwa na utata,lakini si kwamba wako kwa maslahi ya chama,kwa kuwa wanajumuiya ya bakwata si wanachama wa chama kimoja.
kama hawako kwa manufaa ya chama wako kwa manufaa ya nani kwa kuunga mkono dhuruma mimi naungana na sokomoko!
 
Sina fikra za kidini ila wewe unazo kwakusema kwenye post yako BAKWATA wako kwa maslahi ya chama zaidi,naijua historia ya BAKWATA,hatuko kwenye mfumo wa chama kimoja,kuna watu kwenye hiyo jumuiya wako CUF,CHADEMA,APPT nakadhalika nawafahamu,sasa wewe kusema wako kwa maslahi ya chama ndo nikasema ni uongo mweupe, na nikatoa mfano sijasema ndivyo ilivyo naona una badili mwelekeo wa point yangu ya msingi,kwamba je kwakuwa maaskofu walitimiza wajibu wao ambao mi naona wako sahihi kabisa wa kupinga kile kilichofanyika Arusha,je tuseme nao wako CHADEMA na wako kwa maslahi ya chama??? Nilichotaka kusema ni kuwa BAKWATA wamesema wanavyoona wao na wakaamua kumuunga mkono meya ambaye kuchaguliwa kwake kulikuwa na utata,lakini si kwamba wako kwa maslahi ya chama,kwa kuwa wanajumuiya ya BAKWATA si wanachama wa chama kimoja.

Mimi sio muislam na itapendeza mambo ya waislam tuwaachie wenyewe. Lakini hata tukitumia nguvu, kejeli matusi bado ukweli utabaki kuwa palepale kuwa BAKWATA kwa namna moja ama nyingine ni chombo cha propaganda cha watawala. Na hili litaendelea hata kama TLP itatawala nchi maana tatizo la Bakwata sio taasisi yenyewe bali mfumo wake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom