Ma sheikh arusha wamtambua meya wa arusha

Toka lini mashekhe wakaunga mkono maaskofu? mara nyingi hizi huwa ni pande mbili zinazokinzana, sijui ni kwa nini. Lakini mwisho wa wote ukweli utajulikana whether ni hao mashekhe au maaskofu

Kuna wakati nimetokea habari za viongozi hawa wakifanya kazi pamoja km katika kufuatilia athari za mazingira katika migodi, mapambano dhidi ya ukimwi, mauaji ya albino, ukeketaji, kuombea taifa amani, n.k. Hivyo ndugu zangu tujihadhari sana na wanasiasa waliofilisika hasa wa nyakati hizi ambao wakisaidiwa na mafisadi wananunua viongozi wa dini kuimarisha ajenda zao muflisi zinazoelekeza taifa kwenye hatari kubwa.

Hakuna ubishi kwamba hivi sasa kuna kitu kimeharibika sana ndani ya chama tawala kinachopelekea kukumbatiwa na kuenezwa kwa hoja ya udini katika kila suala muhimu kwa maisha ya watanzania. Nasikitika zaidi kwamba inawezekana hata UwT wanatumika kupepea cheche za moto huo ili kutuondoa kwenye mantiki na umakini wa kushughulikia matatizo yetu kistaarabu. Baadhi ya viongozi wa dini (zote) wanatumika kama mamluki. Tuamke kulipinga hili kwa nguvu zote.
 
IGP Mwema na JK ni dini gani na wao walikuwa na mamlaka ya kuzuia yote haya...

Mleta mada ni mchukia uislam habari yake haina source na uislamu umekataa kuuwa/kudhulum nafsi hao mashekh watakaohalalisha mauaji yale ya Arusha watakuwa si mashekh ni mashehena.

{{Wala msiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu amekataza (kuiua) isipokuwa kwa haki (Akahuhumu hakimu kuwa mtu huyo anastahiki kuuawa na akatoa amri ya kuuawa). Na mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi Tumempa nguvu mrithi wake (juu ya muuaji huyo, akitaka ataomba kwa hakimu kuwa amuuwe kama alivyomuuwa mtu wake na akitaka atamsamehe, na akitaka atamtoza kitu). Basi (huyo mrithi asifanye fujo katika kuua kwa ajili ya huyo mtu wake aliyeuliwa). Hakika yeye atasaidiwa (na Sharia maadamu anayo haki).}} [17:33]
Tukiegemea kwenye aya hii, hairuhusiki kwa Uislamu kuua mtu yeyote asiye na kosa kwa baadhi ya makosa ya jinai. Ni vyema tukakumbuka katika nukta hii, tofauti iliyofanywa hapo juu baina ya Qur-aan na Sunnah, na Waislamu; ni Qur-aan na Sunnah pekee ndizo zilizoafikiwa kuwa zinaendana pamoja na matakwa ya Muumba, wakati Waislamu wanaweza sana kutetereka. Hivyo, kama Muislamu yeyote ataua mtu asiye na hatia, Muislamu huyo ametenda dhambi mbaya kabisa, na hakika tendo hilo haliwezi kudaiwa kuwa limefanywa “kwa jina la Uislamu”.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom