Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

wameitaja JF au?

Yah, Imetajwa kwenye kikao. Na baadhi ya wajumbe ambao wanaweza kumudu hii njia mpya ya mawasiliano wamepewa jukumu la kujiunga na kujibu mapigo. Kuanzia sasa angalia ID za wachangiaji wa hoja za CUF/Lwakatare nyingi zitakuwa ngeni na mpya.
 
duh! safi sana

ngoja nitafute thread moja ya zamani niliwakandia ile kichizi Maalim sefu nione watakao kuja kuchangia
 
Yah, Imetajwa kwenye kikao. Na baadhi ya wajumbe ambao wanaweza kumudu hii njia mpya ya mawasiliano wamepewa jukumu la kujiunga na kujibu mapigo. Kuanzia sasa angalia ID za wachangiaji wa hoja za CUF/Lwakatare nyingi zitakuwa ngeni na mpya.

Pamoja na maelezo mazuri nadhani wewe huenda ni muhusika mkuu na wa karibu sana katika hili suala la Mh Lwakatare. Na kwa kuwa tayari umeshaonesha kufahamu mengi ya ndani, basi si vibaya ukatuambia ni kwanini Mh Lwakatare hajazungumzia kwa undani au kujisafisha dhidi ya tuhuma za ubadhirifu wa fedha za chama chake?
 
Hili swali uliniuliza kwenye thread ya Kutoka kwa Lwakatare. Ulisema hivi:

Pundamilia07 said:
Je, kwanini Mh Lwakatare hajisafishi katika tuhuma ambazo aliambiwa kuwa alifanya ubadhirifu wa fedha ya chama? Kukaa kimya maana tutaelewa kuwa tuhuma zilikuwa ni za kweli.

Nikajibu hivi:

Omutwale said:
Baada ya kujitambua kuwa nina extreme affection na Lwakatare sikupenda kabisa kuwa mchangiaji katika hii thread. Maana nilijua kwa ukweli kabisa kuwa siwezi kuwa neutral. Sipendi kuwabore kama yule ndg yetu ambaye akipenda mtu hataki asemwe vibaya.

Pia ukapata majibu kwa urefu sana toka kwa Mkandara.

Sasa tena:

Pamoja na maelezo mazuri nadhani wewe huenda ni muhusika mkuu na wa karibu sana katika hili suala la Mh Lwakatare. Na kwa kuwa tayari umeshaonesha kufahamu mengi ya ndani, basi si vibaya ukatuambia ni kwanini Mh Lwakatare hajazungumzia kwa undani au kujisafisha dhidi ya tuhuma za ubadhirifu wa fedha za chama chake?

Labda nirejee maneno ya Prof. Lipumba. Lwakatare HANA TUHUMA YOYOTE NDANI YA CUF. Hiyo unayoikomalia kama tuhuma aliisema mwenyewe Lwakatare mbele ya Balaza akitaka viongozi watamke wazi na bayana kuhusiana na minon'gono ambayo mahasidi wake wamekuwa wakiitoa kama sababu za yeye kutoteuliwa tena. Ni sababu mbili wamekuwa wakitoa:

!. Lwakatare ni mbadhirifu (Japo bila uthibitisho wa viongozi wakuu wala si tuhuma rasmi)

2. Uwezo wa kiutendaji wa Lwakatare umepungua.

Toka hapo juu sifikiri kama inawezekana usikie minon'gono, uje nazo mbele ya Balaza kujishtaki, Balaza na viongozi waseme huna tuhuma yoyote, halafu wewe uanze kujitetea.

Labda ebu niambie Pundamilia07; nguo iliyo safi kabisa iliyonyooshwa tayari kwa kuvaliwa, huwa unairudisha laundry ifuliwe pasipo kuchafuka kwanza?
 
Niliona tu kwamba jamaa alikuwa anaandaa njia ya kuondoka CUF. Viongozi kama hawa ndio wanataka wakabidhiwe nchi?


Lwakatare: CUF imepoteza mwelekeo

*Asema hakuingia kwenye siasa kutafuta umaarufu

Na Theonestina Juma

“HARAKATI za kambi ya upinzani kupata kura za kutosha ili kuwa na idadi kubwa ya uwakilishi Bungeni, sio jambo lahisi bali linahitaji mpango kabambe, tutaendelea kuomba makanisani na misikitini lakini hatuwezi kupata mafanikio”

Kauli hiyo nzito, ilitolewa hivi karibuni na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia Chama Cha Wananchi (CUF), kuanzia mwaka 2000 mpaka 2005, Bw. Wilfred Lwakatare, alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye Uwanja wa Mashujaa, Mjini Bukoba, mkoani Kagera.

Haikuwa rahisi kwa wafuasi wake, kuamini uamuzi aliochukuliwa Bw. Lwakatare ambaye mwaka 2005, alishindwa kutetea kiti hicho kwenye Uchaguzi Mkuu. Mpaka anatangaza kujivua rasmi uanachama wa CUF, Bw. Lwakatare alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho.

Bw. Lwakatare aliwaeleza wananchi hao kuwa, hakuingia kwenye siasa kwa lengo la kutafuta umaarufu kwenye vyama visivyokuwa na mwelekeo wa kuwasaidia wananchi.

“Nilipokuwa Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, nilijaribu kuwa karibu kuwa na watu wa rika zote kwa sababun ya tabia yangu ya kusema ukweli, lakini inapofikia hatua ya kuwepo kwa majungu na fitina ambazo hazijengi, kazi ya ziada inahitajika kuondokana na tatizo hili,” alifafanua Bw. Lwakatare.

Bw. Lwakatare ambaye ametangaza rasmi kuondoka CUF, aliwataka wananchi hao, wasimuhukumu kwa maneno wanayoyasikia pembeni, bali wamuhuku kwa yale atakayosema mwenyewe akisisitiza kuwa, utamaduni alionao ni kuweka mambo mezani ili yajadiliwe na kushindna kwa hoja.

Anasema kwa mujibu wa utaratibu na kanuni za nchi, katika uchaguzi wa mwaka 2010 atagombea Ubunge katika Jimbo la Bukoba Mjini. Alifafanua kuwa, uvumi uliopo kwamba yupo mbioni kuhamia kwenye Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ni hoja iliyopandikiwa na viongozi wa CUF, kwa makusudi.

Anafafanua kuwa, pamoja na vyombo vya habari nchini kumtafa awaeleze sababu za kuchukua uamuzi huo, hakuwa tayari kuwaeleza mabapo kusudio lake ni kutaka kuelezea sababu hiyo kwa wananchi ambao ndio mtaji wake kisiasa na kufanya ajulikane.

Aliongeza kuwa, pamoja na kuondoka CUF, kamwe hawezi kuhamia CCM kama inavyodhaniwa na wananchi wengi. Sera ya CCM, sio kutengeneza maisha bora kwa wananchi bali ni inatengeneza maisha magumu kwa ari, nguvu na kasi mpya, hivyo hana sababu ya kujiunga na chama hicho.

Anasema mfumo wa vyama vingi vya siasa ni msukumo mzuri kimsingi unaofanya kazi ya kuwasaidia Watanzania ili chama kinachopo madaraka kisijisahau kutimiza malengo ya kuwasaidia wananchi.

“Naomba niwaambie ndugu zangu, katika vyama vya siasa wamo baadhi ya viongozi ambao wameanza kuvibadilisha kama vichaka vya kufanyia ubinafsi, ufisadi na kuendeleza mambo mengine yasiofaa.

“Ikifikia hatua ya chama kupata ruzuku, viongozi wengine wanaona wamefika mwisho wa reli Kigoma, bila kujua kwamba bado tunaendelea kutafuta maisha bora, lakini ikishafikia hapo vyama vya siasa vinajisahu kwa hilo,” anasema.

Anasema kwa hali ilivyo sasa ndani ya CUF, hali si shwari baada ya kupoteza mwelekeo na kushika kisiasa na matokeo juu ya hilo, ni kushindwa katika chaguzi ndogo zilizofanyika katika majimbo mbalimbali.

Aliongeza kuwa, alikipenda CUF kwa sababu ya uwazi na ukweli uliokuwepo awali tofauti na sasa ambapo matatizo mengi hayawekwi hadharani na kutafutiwa ufumbuzi wa haraka

Anasema licha ya badhi ya wananchi kumtaka aende CHADEMA, atakaa na familia yake na kujadili suala hilo kwa makini na kutoa jibu badae.

Katika moja ya vitabu alivyotunga Bw. Lwakatare ameelezea jinsi asivyoridhishwa na mafao yake ndani ya CUF, licha ya wajumbe kumwona nadhifu akiendesha VX ambalo anadai kuwa, alilipata kutokana na kura za wana Bukoba mwaka 2000.

Sula lingine aliloandika kwenye kitabu hicho ni jinsi CUF ilivyo na utaratibu mbovu wa kutowatambua waasisi wa chama hicho. Anasema kwa upande wa Tanzania Bara maendeleo ya chama hicho ni hafifu na hayatii matumaini hali inayoonesha dahihiri kuwa, CUF ipo kwa ajili ya kusindikiza vyama vingine kutokana na chama hicho kutokuwa na mwakilishi hata mmoja bungeni kama ilivyo kwa vyama vingine.

Pia kitabu hicho, kinaelezea mpango ulioandaliwa kumuondoa katika nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Taifa, na kuonesha namna ambavyo aliweza kutulizwa na Makamu Mwenyekiti wa CUF Taifa, Bw. Yusuph Machano ya kumtaka asibweteke kutokana na mabadiliko yaliofanywa na chama.

“Ni kweli nilipata mshtuko wa mabadiloiko hayo, baada ya kujitathimini mara mbili zaidi juu ya uwezo wangu kiutendaji kwa kuzingatia kuwa wenzangu kwa upande wa Zanzibar, Bw. Juma Duni Haji, jina lake lilirudi na kufanikiwa kutetea kiti chake na jina langu likaachwa,” anasema.

Bw. Lwakatare ni miongoni mwa waasisi wa CUF, kama kiongozi mwandamizi na mwenye uwezo mkubwa wa kupanga mikakati na mipango mbalimbali ya kukijenga chama pamoja na kuhakikisha kinapata ushindi katika chaguzi zake mbalimbali.
 
Hili swali uliniuliza kwenye thread ya Kutoka kwa Lwakatare. Ulisema hivi:



Nikajibu hivi:



Pia ukapata majibu kwa urefu sana toka kwa Mkandara.

Sasa tena:



Labda nirejee maneno ya Prof. Lipumba. Lwakatare HANA TUHUMA YOYOTE NDANI YA CUF. Hiyo unayoikomalia kama tuhuma aliisema mwenyewe Lwakatare mbele ya Balaza akitaka viongozi watamke wazi na bayana kuhusiana na minon'gono ambayo mahasidi wake wamekuwa wakiitoa kama sababu za yeye kutoteuliwa tena. Ni sababu mbili wamekuwa wakitoa:

!. Lwakatare ni mbadhirifu (Japo bila uthibitisho wa viongozi wakuu wala si tuhuma rasmi)

2. Uwezo wa kiutendaji wa Lwakatare umepungua.

Toka hapo juu sifikiri kama inawezekana usikie minon'gono, uje nazo mbele ya Balaza kujishtaki, Balaza na viongozi waseme huna tuhuma yoyote, halafu wewe uanze kujitetea.

Labda ebu niambie Pundamilia07; nguo iliyo safi kabisa iliyonyooshwa tayari kwa kuvaliwa, huwa unairudisha laundry ifuliwe pasipo kuchafuka kwanza?

Ninanukuu maneno ya Mh Lwakatare


"Baada ya kuyapitia alimhoji Mwenyekiti kuwa kwa nini Jina la Wilfred M. Lwakatare halikuwemo na hasa ikizingatiwa kuwa ndiye hadi kipindi hicho alikuwa ni Naibu Katibu Mkuu (Bara) alihoji iweje Juma Duni Haji apewe fursa ya kutetea nafasi yake aliyokuwa nayo lakini Wilfred Lwakatare asipewe nafasi hiyo pia.



5. Mhe. Mwenyekiti na Wah. Wajumbe wa Baraza Makamu Mwenyekiti alijibiwa na nyie wenzake wawili kuwa Lwakatare ana matatizo. Na matizo yake ni kuwa si mwaminifu katika Masuala ya fedha, ni mbadhirifu na mtumia madaraka yake vibaya kwa kulazimisha hati za malipo anazotaka zifanyiwe malipo zilipwe iwe isiwe.

Makamu Mwenyekiti alizidi kuwauliza wenzake iwapo imeshindikana kumuita Lwakatare na kumuonya kuhusu tabia hiyo na akashindwa kujirekebisha kuliko kuacha jina lake kabisa. Anasema akajibiwa kuwa tabia zote Lwakatare
anaweza kuonywa na kujirekebisha lakini kwa masuala ya fedha ni sugu hawezi kusikia cha mtu. Mwishowe uamuzi wa kulitosa jina la Lwakatare ukaridhiwa na wote watatu na huo ndio ulikuwa ukweli wa suala lenyewe.




Alimalizia Mhe. Machano Makamu Mwenyekiti wetu



==============================

Omutwale, hayo maneno ni makubwa na mazito sana, kama Lwakatare atakaa kimya bila ya kujisafisha hapo basi ajue kwamba hatahuko anakokwenda yatakuja kumkuta na vilevile kwa vile hizi tuhuma ni nzito kwa mwanasiasa kama yeye na hataki kuziongelea inawezekana kabisa zina ukweli ndani yake.

Tuhuma hizo unaweza kuzipa jina lolote baya kuanzia majungu, fitna nk ili mradi tu uweze kuziondolea uzito. Mimi bado ninaona kuwa Lwakatare anawajibika katika kutoa maelezo ya kina na hasa ningemuona kuwa ni mtu safi kama angeamua ufanyike uchunguzi dhidi yake. Zaidi tumeona katika maelezo yake akilalamika zaidi kwa kucheleweshewa malipo yake ya 'kustaafu' na kutopewa hadhi 'maalum' ndani ya CUF.
Hukumu ya Lwakatare aidha kwa mema au mabaya aliyoyafanya ndani ya CUF hayawezi kutolewa na CUF bali ni wananchi nikiwemo mimi mmojawapo.

Bado nitahitaji Lwakatare aeleze juu ya jambo hili kwani hatukulisikia kutoka kwa viongozi wa CUF bali yeye mwenyewe ndiye aliyelizungumza tena mchana kweupe hapa ndani ya JF.

 
Last edited:
Soma hapa chini:

Na matizo yake ni kuwa si mwaminifu katika Masuala ya fedha, ni mbadhirifu na mtumia madaraka yake vibaya kwa kulazimisha hati za malipo anazotaka zifanyiwe
malipo zilipwe iwe isiwe.

Hivi haya maneno asingeyasema na kuyaandika Lwakatare wewe na wengine wangeyapata wapi? Unataka hayaseme kwa mtindo upi ili uridhike?! Huwezi kujiweka pingu, ukajipeleka polisi, kisha ukajiongoza kizimbani na kujishtaki ilihali ukiwa unajua unamakosa.
 
Siasa za Bongo zimekuwa kama watani wa jadi ktk soka.
Nilikuwa namfuatilia Lipumba kwenye news ambapo alitabainisha kwamba mtu asing'ang'anie madaraka ndani ya chama huku akimpiga kjembe lwakatare bila kumtaja kwamba alidhani atatawala milele.
Swali kwa Lipumba na Seif. je wao ndiyo miungu ya CUF??? why cant they step down na kuachia viongozi wapya waje na changamoto mpya??? maana siasa za CUF ni kam mipasho vile na waimbaji n walewale
 
makahaba ya kisiasa!

Mhe. Mwenyekiti, nilielezea kwa kirefu wakati tukijadili agenda ya kupitia muhtasari
na yatokanayo juu ya kutoridhishwa na namna mlivyopokea na kulishughulikia
suala la Mafao yangu na Matatizo yangu. Mhe. Mwenyekiti na wahe. Wajumbe
pamoja na kuonekana nadhifu na kuendesha gari la vx nililopata kutokana na kura za wana Bukoba mwaka 2000 lakini mimi nina matatizo "kibao" kama nilivyowaambia.
Hayo 'matatizo kibao' ndiyo yaliyomuondoa Lwakatare CUF mara baada ya kutemwa Unaibu Katibu Mkuu. Inaonekana ile hoja ya ubadhirifu ni valid. Inawezekana Mheshimiwa alikuwa anamalizia shida zake kwenye kofia ya Unaibu Katibu Mkuu na mara baada ya kuondolewa sasa inakuwa imeshakuwa taabu, CUF haiwezi kukalika.

Mheshimiwa ameonesha kuwa yeye ni kiongozi mbinafsi wa hali ya juu kabisa hasa pale anapoitaka CUF iweke sera maalum za kuwaenzi 'wastaafu' baada ya yeye kutemwa katika safu ya uongozi wa juu. Ni kwanini hakupigania hili wakati akiwa kiongozi kwa ajili ya wale ambao tayari si viongozi tena? Au aliona kuwa yeye yuko mbali na ukweli siku moja naye hatakuwa kiongozi wa juu?

Pili, inaonekana kuwa Mheshimiwa pamoja na kuwa na juhudi nyingi lakini hakuwa na vision na hili linadhihirika pale baada ya muda mfupi kutolewa katika madaraka ya juu analalamika jinsi ambavyo CUF imekosa mwelekeo katika siasa za bara na hata kudiriki kusema CUF inatia aibu. Hapa Mheshimiwa anasahau kuwa yeye ndiye aliyekuwa namba tatu na pia akiwa na jukumu la pekee la kusimamia shughuli za chama kwa upande wa bara?

Mheshimiwa Lwakatare, nadhani hana jipya zaidi ya kusaka kiti cha Bukoba Mjini. Kwa mtazamo wangu Lwakatare angekuwa radhi kwenda CCM ili mradi tu kama angehakikishiwa kuwa atapendelewa ateuliwe kugombea kiti cha ubunge cha Bukoba Mjini. Lakini kwa utaratibu ambao CCM wameamua kuuchukua si rahisi kwa mtu kama Lwakatare aweze kupenya na kufikia jina lake kuwekwa kama mgombea wa CCM. Safari yake ya kwenda CHADEMA ameiona kuwa inaweza kumnufaisha kwa vile chama hicho kwa sasa kinaangalia sura ya mtu na jinsi anavyoweza kuwapatia ushindi hata kama anamushkeli.
 
Soma hapa chini:



Hivi haya maneno asingeyasema na kuyaandika Lwakatare wewe na wengine wangeyapata wapi? Unataka hayaseme kwa mtindo upi ili uridhike?! Huwezi kujiweka pingu, ukajipeleka polisi, kisha ukajiongoza kizimbani na kujishtaki ilihali ukiwa unajua unamakosa.

Omutwale,
Hizi ni siasa, kama aliamua kusema yale maneno kwa faida za kisiasa basi ajue amejiingiza mahali ambapo hawezi kutoka kwa kupiga gia ya rivasi au kama hivyo. Hapa kinachotakiwa ni kwamba kama yale maneno hayakuwa na maana yeyote basi hakuwa pia na sababu ya kuyatamka.
Kwa vile aliyatamka mwenyewe, basi hana budi kuchukua hatua muafaka za kujisafisha dhidi yake. Vinginevyo ukweli utabaki kuwa hivyo na atapata taabu kubwa pale ambapo tuhumu zikirudi kutoka upande mwingine.
Nina wasiwasi mkubwa yale maneno yana ukweli ndani yake japo kuwa wewe unataka yawe diluted.
 
Ukisoma vizuri alama za nyakati, CUF imepoteza mvuto wa kitaifa na kimkoa. Mgombea mtarajiwa yeyote mwenye kupiga hesabu vizuri hata kama anao mtaji wa wapiga kura, kugombea kupitia CHADEMA ndiyo turufu yenye uwezekano mkubwa wa kushinda ubunge.

hiyo ni sawa lkn chaguo sahii kwa uchaguzi wa 2010 ni ccm
 
Omutwale,
Hizi ni siasa, kama aliamua kusema yale maneno kwa faida za kisiasa basi ajue amejiingiza mahali ambapo hawezi kutoka kwa kupiga gia ya rivasi au kama hivyo. Hapa kinachotakiwa ni kwamba kama yale maneno hayakuwa na maana yeyote basi hakuwa pia na sababu ya kuyatamka.
Kwa vile aliyatamka mwenyewe, basi hana budi kuchukua hatua muafaka za kujisafisha dhidi yake. Vinginevyo ukweli utabaki kuwa hivyo na atapata taabu kubwa pale ambapo tuhumu zikirudi kutoka upande mwingine.
Nina wasiwasi mkubwa yale maneno yana ukweli ndani yake japo kuwa wewe unataka yawe diluted.

Ni mimi ndiye napata taabu sana kukuelimisha wewe na si Lwakatare kueleweka kwa wapiga kura. Ningeweza ningeweka Mkanda wa Mkutano wake alioufanya BK trh 19 mwezi huu ili nawe ujionee na kujisikilizia.

Tunafua nguo chafu, tusafisha viatu walau hata kama vina vumbi lakini je, tunaweza kuyaosha maji yaliyo safi?

Pundamilia07, naona tunaanza kuufanya mjadala kuwa wetu. Waonaje tusi-bore na tuingie vyumba vya ndani (PM)?!
 
Ni mimi ndiye napata taabu sana kukuelimisha wewe na si Lwakatare kueleweka kwa wapiga kura. Ningeweza ningeweka Mkanda wa Mkutano wake alioufanya BK trh 19 mwezi huu ili nawe ujionee na kujisikilizia.

Tunafua nguo chafu, tusafisha viatu walau hata kama vina vumbi lakini je, tunaweza kuyaosha maji yaliyo safi?

Pundamilia07, naona tunaanza kuufanya mjadala kuwa wetu. Waonaje tusi-bore na tuingie vyumba vya ndani (PM)?!

Mkuu,
Mimi sina tatizo na kuhamia kwenye PM, lakini labda haitakuwa vibaya kama tutakubaliana at the end of the day kwamba tutarudi hapa kuwaeleza other interested parties kuwa kumekubaliana kukubaliana/kutokukubaliana. Mimi huwa ninaamini si kila mtu amayefuatilia hapa lazima atoe komenti, la wengine husoma tu na kuangalia how the thread is moving.
Hata hivyo mjadala wa wazi unafaida zake ambazo mawazo mbalimbali hujitokeza zaidi na kuboresha jinsi tunavyofikiria.
Bado ninaamini kuwa Mheshimiwa has to do something na yale maneno, kwangu mimi ni lazima kuna ukweli kwa kiasi fulani. Arekebishe sasa na wala asingije kuja kufanya kazi ya ziada huko mbele ya safari.
 
Back
Top Bottom