Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Ranmarwa,
Mkuu hii inaonekana kama hadithi simulizi zaidi ya Ukweli maanake kila naposoma kuna majungu, visokorokwinyo na kadhalika..
Hawa viongozi wa CUF kama kweli Lwakatare alipewa millioni30/ na akatumia Millioni 5 tu iweje washindwe kumuuliza/kumwajibisha ila wammezee ati wamsubiri ktk uchaguzi!.. hao viongozi wa CUF walitegemea kuwaeleza nini wananchi ikiwa millioni 30 zimetumika vibaya na sii fedha toka mifukoni mwao..hizo millioni 25 pungufu zimehesabika vipi ktk vitabu vya chama ikiwa Lwakatare ataondoka chama kabla ya kutakiwa kujieleza..

Kisha unasema ati Lwakatare aliulizwa sababu ya kupinga jina la Joram akashindwa kujibu.. Mkuu tafadhali, Lwakatare alikuwa naibu Katibu mkuu iweje ashindwe kujibu ikiwa jina lake limeenguliwa wakati viongozi wengine wote majina yao yalirudi! Na wala sioni sababu ya kuulizwa swali hilo ikiwa hao viongozi wa CUF wameliondoa jina la Lwakatare bila kumweleza yeye sababu.. Kwa nini wao watake kujua sababu ya kupinga ikiwa kahupewa sababu ya kutolewa...maamuzi yao hayakuwa na maelezo..

Kifupi ni hivi CUF wamechoka Lwakatare na sababu zipo nje kabisa ya matumizi mabaya ya fedha kwani kama ingekuwa hivyo basi wanachama wa CUF wangeisha pewa hesabu hizo na matumizi hayo mabaya.. Na nakuhakikishia sii Lipumba wala Seif wanaweza ku raise hii issue kwa sababu hawa wote ni Opportunist nina hakika wametumia fedha vibaya kuliko huyo Lwakatare..Opportunist mwninge..
Kifupi wanasiasa wengi Bongo kama sii wote ni Opportunist, hawakuingia siasa bila kutegemea malipo bora na ujanja ujanja laa sivyo wangekuwa wakiachia nafasi hizo baada ya awamu mbili za kushindwa ama kuweka ushindani wa kweli within vyama hivyo.
Mara zote utakuta nafasi ya Mwenyekiti wanagombea Lipumba vs Mkandara asiyejulikana kabisa wala uanachama wake.
Makamu mwenyekiti, Sief against Mkandara!
sijui kiti cha nini Duni against Mkandara..basi ili mradi kurudi kwao madarakani ni LAZIMA..

Mkandara,
Jamaa mwenyewe alishasema hii ni story japo akasema full story lakini inabaki ni story vilevile. Hapo kaongea kikurya angaongea kiswahili angesema "hadithi." Labda tumwulize kama Sara Dumba aalivyokuwa akiwauliza watoto wa kipindi cha mama na mwana RTD enzi zileeeeee. "Hadithi hiyo alikufundisha nani na inamaanisha nini?"
 
Ranmarwa,
Mkuu hii inaonekana kama hadithi simulizi zaidi ya Ukweli maanake kila naposoma kuna majungu, visokorokwinyo na kadhalika..
Hawa viongozi wa CUF kama kweli Lwakatare alipewa millioni30/ na akatumia Millioni 5 tu iweje washindwe kumuuliza/kumwajibisha ila wammezee ati wamsubiri ktk uchaguzi!.. hao viongozi wa CUF walitegemea kuwaeleza nini wananchi ikiwa millioni 30 zimetumika vibaya na sii fedha toka mifukoni mwao..hizo millioni 25 pungufu zimehesabika vipi ktk vitabu vya chama ikiwa Lwakatare ataondoka chama kabla ya kutakiwa kujieleza..

Kisha unasema ati Lwakatare aliulizwa sababu ya kupinga jina la Joram akashindwa kujibu.. Mkuu tafadhali, Lwakatare alikuwa naibu Katibu mkuu iweje ashindwe kujibu ikiwa jina lake limeenguliwa wakati viongozi wengine wote majina yao yalirudi! Na wala sioni sababu ya kuulizwa swali hilo ikiwa hao viongozi wa CUF wameliondoa jina la Lwakatare bila kumweleza yeye sababu.. Kwa nini wao watake kujua sababu ya kupinga ikiwa kahupewa sababu ya kutolewa...maamuzi yao hayakuwa na maelezo..

Kifupi ni hivi CUF wamechoka Lwakatare na sababu zipo nje kabisa ya matumizi mabaya ya fedha kwani kama ingekuwa hivyo basi wanachama wa CUF wangeisha pewa hesabu hizo na matumizi hayo mabaya.. Na nakuhakikishia sii Lipumba wala Seif wanaweza ku raise hii issue kwa sababu hawa wote ni Opportunist nina hakika wametumia fedha vibaya kuliko huyo Lwakatare..Opportunist mwninge..
Kifupi wanasiasa wengi Bongo kama sii wote ni Opportunist, hawakuingia siasa bila kutegemea malipo bora na ujanja ujanja laa sivyo wangekuwa wakiachia nafasi hizo baada ya awamu mbili za kushindwa ama kuweka ushindani wa kweli within vyama hivyo.
Mara zote utakuta nafasi ya Mwenyekiti wanagombea Lipumba vs Mkandara asiyejulikana kabisa wala uanachama wake.
Makamu mwenyekiti, Sief against Mkandara!
sijui kiti cha nini Duni against Mkandara..basi ili mradi kurudi kwao madarakani ni LAZIMA..

Mkuu
Ndiyo maana mimi siamini mabadiliko kuletwa na chama ,Na mimi nionavyo ktk hali halisi iliyopo saizi Tz kubadili chama si majibu sahihi na kukiacha chama madarakani pia si viable soln.Sasa chagua ama kunyowa.
 
Nawashauri wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CUF Wafanye haraka kuifanyia mabadiliko katiba yao ili wakutane tena Mwezi Ujao na wapitishe kwa Umoja kuwa sasa NAFASI YA NAIBU KATIBU MKUU itakuwa ni ya KUDUMU tena ni Kwa Mhe LWAKATARE Hadi mwisho wa Maisha yake hapo ubishi utakuwa umekwisha na MASANGARA atayatapika nakurudi kwa kasi katika nafasi yake na CUF haitakuwa tena na Makosa mbele yake kama ilivyo hivi sasa Kwa Kuchanganyikiwa kwake alivyojichanganya kutoka Kwenye TAASISI na Kukimbilia Kwenye UZAWA na UMAJIBO
 
Siasa ni kama soka ya kulipwa. Ukiona team uliyopo haikupatii kikombe una tafuta usajili sehemu nyingine.
 
Wadau JF.
Nimekuwa nikijiuliza swali hili, siku nyingi baada ya sakataka la Lwakatare kuanza ndani ya CUF.

Nawauliza CHADEMA ambao wakati fulani niliwaona majasiri jinsi walivyosimama kidete kudhibiti hali ya mchafu koge ndani ya chama chao iliyokuwa ikichochewa kwa mbaali na mashushu na mamluki wa CHAMA TAWALA,wakisaidiwa na usalama wa taifa,kwa wao CHADEMA kujua au bila kujua, hapa nazungumzia sakata la Marehemu Chacha Wangwe.
Leo katika mazingira kama hayo CUF wanakumbana na hali hiyo au kama hiyo.

Kiufupi tu, imekuwa ikiripotiwa katika vyombo na mitandao mbalimbali ya habari huko Tanzania kuhusu hatua ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Mh.W.Lwakatare ya kwanza kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi ndani ya chama na pili tetesi zinazodai kuwa yupo mbioni kujiunga na chama chengine cha upinzani, chadema.

Swali langu ndo linakuja hapa kuwa, ukizingatia sababu za Lwakatare kusuguana na viongozi wake mpaka akaamua kuachia ngazi,je huko anakotaka kwenda, wenyeji wake wanakitu gani wamemtayarishia Lwakatare ambacho amekikosa alipokuwa CUF na anamatarajio ya kukipata huko?

Chadema wasisahau kuwa,hakuna asiyejuwa kuwa sababu kubwa ya Lwakatare kununa na kuchukua hatua anayochukua hivi sasa ni "vita ya Madaraka".

Ingawa vyombo vya habari vimenukuu sababu tofauti anazodai Lwakatare kuwa ndizo zimemfanya aamue kuachia ngazi CUF, lakini hakuna hata moja kati ya hizo yenye kuingia akilini, Lwakatare aliwahi kuripotiwa akidai kuwa sababu ya kuachia ngazi ni kitendo cha Mwenyekiti wa CUF, Prof.Lipumba cha kuwatimua akina Kuchilingulo, Mmari na Wandwi kwa madai ya kukihujumu chama katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Busanda.

Wakati huo huo amenukuliwa na vyombo mbalimbli vya habari akidai kuwa sababu kubwa ya kuachia ngazi ndani ya chama na kufikiria asiendelee na chama cha CUF ni kutokana na jina lake kuachwa kwenye uteuzi wa kutetea nafasi yake kwasbabu za kifitna na majungu yaliyojaa ndani ya CUF. Amenukuliwa akiwashutumu Juma Duni na Bi. Ashura Mustafa kuwa ndio wanaompakazia na kueneza fitna hizo.
Chochote na kisemwe na aseme Lwakatare ni uhuru wake, laikini awaambie watu ukweli kuwa kuishi bila ya wadhifa kama aliowahi kuwa nao katika chama cha CUF ni ngumu kwake, vilivyobakia ni visingizio tu.

Katika hali kama hiyo ndo nikapata swali la kujiuliza chadema watampa nini Lwakatare? Nikakumbuka ile kadhia nduchu ya Hiza Tambwe katika staili kama hiyo ya Lwakatare, akahama na kukimbilia CCM ambako alipewa anachokitaka. CHADEMA MTAMPA NINI LWAKATARE?
Tatizo la viongozi hawa wa upinzani ni uchu wa madaraka
 
Ameandaliwa kadi na sera za CHADEMA

Hivyo vyote alikuwa navyo alipokuwa CUF, tena analala navyo kwake.

Alikua navyo vya CUF siyo vya CHADEMA.

ahahahahahahah uuuuuuuuuuwwwwwwwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
Hii imenichekesha sana.
Junius, Lwakatare kakuumizeni sana sio??????
Si mwacheni afuate hayo madaraka Chadema ili mradi kafu hamnayo? Sasa shida iko wapi?
Wala hajasema anafuata madaraka huko chadema. Nyie kafu hii mmeipata wapi?
Si mwacheni afuate hayo madaraka yaliko?
Nina imani yeye bado ni mali ya kafu. Usitie hofu:D
 
Tatizo la viongozi hawa wa upinzani ni uchu wa madaraka

Niambie wa sisi M asiyehitaji madaraka nyie watu!!!!!!!!!!!!!
Mbona walipigana juzi tu tena kwenye baa mpaka JMK aliwashangaa!!!!!!!!!
Ukitaka kuishi bila ya kuwa kiongozi hata nyumbani kwako, ujue umekwisha.
Naturaly mwanadamu kaumbwa kutawala. Asiyetaka kutawala ....................
 
CUF imo ndani ya nyoyo za wananchi,wanachama wengi wa CUF wameamka kimawazo na hawamthamini kiongozi zaidi ya Chama Chao hivyo wananchi wanaimani kuwa viongozi wamewekwa na wao na kiongozi akiondoka huwa hawababaiki nguvu zilizotumika kumfanya huyo alieondoka awe mashuhuri ndio hizo hizo zitakazotumika kumuinua mwengine na huo ndio mtaji wa CUF ,ni rahisi kuubadili moyo wa kiongozi kuliko moyo wa mwanachama wa CUF na hiyo ndio hazina ya CUF.
Bukoba wanachama wa CUF nyoyo zao ziko kwa Cuf au Lwakatare?
 
ahahahahahahah uuuuuuuuuuwwwwwwwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
Hii imenichekesha sana.
Junius, Lwakatare kakuumizeni sana sio??????
Si mwacheni afuate hayo madaraka Chadema ili mradi kafu hamnayo? Sasa shida iko wapi?
Wala hajasema anafuata madaraka huko chadema. Nyie kafu hii mmeipata wapi?
Si mwacheni afuate hayo madaraka yaliko?
Nina imani yeye bado ni mali ya kafu. Usitie hofu:D
MM wala sijaumia sijuwi CUF wenyewe vp?
Ninachoweza kusema kuwa ni Lwakatare mwenyewe amenukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa ameamua kujivua uongozi CUF kuwa amekuwa sidelined katika uongozi.
Na yeye mwenyewe ndiye aliyeitisha mkutano BK kuwauliza watu wake kama aende chadema au abakie CUF, kwa yeye Lwakatare huko anakowaomba wananchi wake wamruhusu aende (chadema) hatokuwa sidelined katika uongozi, ndo ninawauliza chadema vp watampa anachokitaka?
 
MM wala sijaumia sijuwi CUF wenyewe vp?
Ninachoweza kusema kuwa ni Lwakatare mwenyewe amenukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa ameamua kujivua uongozi CUF kuwa amekuwa sidelined katika uongozi.
Na yeye mwenyewe ndiye aliyeitisha mkutano BK kuwauliza watu wake kama aende chadema au abakie CUF, kwa yeye Lwakatare huko anakowaomba wananchi wake wamruhusu aende (chadema) hatokuwa sidelined katika uongozi, ndo ninawauliza chadema vp watampa anachokitaka?
Siwezi wajibia Chadema. Ili mradi viongozi wengi wako hapa wakiona sababu watakujibu kama wanaweza kumpa au hapana.
Hivi ngoja kwanza niulize kwani kafu walimpa nini kiasi kwamba asitoke kafu?
Nyerere alisema chama sio mama yake. Anaweza kuki bull shit
 
MkamaP,
Mkuu nakusikia sana na ndio maana siasa za Bongo nimesema mimi siziwezi hata kidogo. Matatizo ya ndani CCM, CUF Chadema sijui TLP yote hayatokani na maauzi yoyote yanayohusiana na maamuzi kwa ajili ya wananchi..Wote hawa ugonvi wao mkubwa ni viti vya Uongozi..
wapinzani wameshindwa kuungana sio sababu za mrengo, sera wala rangi ya bendera isipokuwa nani atakuwa nani ktk muunganmo huo. Mvutano wa nguvu ya watu hawa ndio imevuruga muungano na haitawezekana hata siku moja..
Unajua kuna rafiki yangu Myahudi, yeye alinambia kitu kizuri sana jinsi alivyowasoma watu weusi na hasa Waafrika.. Tunajali sana Title yaani jina la cheo kuliko kila kitu... Mtu mwenye degree yake akipewamkazi ya kufagia klakini akiitwa MD basi ataikubali hiyo kazi bila hata kuuliza mshahara, wala majukumu ya kazi hiyo maadam apate hilo jina la Managing Director..

Sasa huko ktk vyama utasikia nafasi kama hizi zipo wazi ni lazima watu watatoana roho..TITLE mkuu wangu Wabongo tunapenda sana jina kubwa bila kujali responsibility zake.. Sasa tazama majivuno ya Lwakatare! kila anachojivunia ilikuwa part ya kazi alizobidhiwa alitakiwa/tegemewa kufanya nini chini ya hapo!..
Hivi kweli angekuwa hana madaraka hayo angeyafanya yote yale kwa roho nyeupe?...na hivi kama asingekuwa CUF angeweza kulitengeneza jina lake nje ya Bukoba!.... sidhan, sidhani sidhani.. mafanikio yake yametokana na kuwepo CUF na sii kinyume. CUF haikumtegemea Lwakatare!

Hata hivyo pamoja na yote haya sikuona mahala Lwakatare akizungumzia chama au kuwalumu wana CUF isipokuwa uongozi wa juu wa CUF.. Na mapendekezo yake hata kama akiondoka CUF ni muhimu wayafanyie kazi..Waswahili wanasema - Hata mchawi husema ukweli...
 
Waungwana,

Kama viongozi wa CUF - Mwenyekiti Lipumba na Katibu wake Hamadi wanatuhumiwa kung'ang'ania viti vyao, basi nafikiri na huyu ndugu yetu ni mng'ang'anizi wa cheo chake. Yale yale ya Tambwe Hiza. Viongozi wote wa Tanzania ndivyo walivyo. Pakiwa na mtetereko wowote katika nyadhifa zao basi zinatafutwa sababu za kuhamia kwingine kwa matumaini ya kuendelea kuwa madarakani.

Wangapi tunafiri au kudhani Nyerere angebaki TANU au CCM kama angenyang'anywa uongozi? Nkrumah alilikikimbia chama cha wazee wake akaanzisha cha kwake ili mradi tu awe kiongozi. Na Zuberi Mtemvu hivyo hivyo. Na mimi pia. Cheo kizuri bwana, hata kama ni cheo tu! Tuna kaaazi kweli kweli.
 
Hivi punde CUF-Taifa wamemaliza mkutano wa siri. Mkutano huu ulikuwa na lengo la kujadili jinsi ya kumdhibiti Lwakatare kwa kurejea aliyoyazungumza kwenye mikutano yake (wa ndani na wa hadhara) tarehe 19/06/2009 mjini Bukoba.

JF ndiyo imekuwa chanzo cha Uongozi kujua nini kinaendelea Bukoba na kupata mwanga wa kinachoendelea ndani ya chama.

Paparazzi wetu ambaye ni Shehe aliyeweza kupata nafasi katika altare ndani ya kanisa ambamo ulifanyika mkutano huo anatuandalia taarifa kamili.
 
DVD ya Mkutano wa Lwakatare alioufanya Bukoba tarehe 19/06/2009 inapatikana Sasa.
Kwa wale walioko Dar es Salaam tuwasiliane kupitia 0717041781
 
Back
Top Bottom