Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Hayo niliyohighlight kwa wino mwekundu ni ya kweli?
Mbona nyie mliokunywa maji ya kijani mtachomwa moto kwa uongo wenu wa mchana kweupe?
Wooooooooooooote waliokuwa upinzani na wakarudi chi chi mafichadi hamkuwapa kitu?????
Mimi nataka kugombea uenyekiti wa mtaa tu kupitia chama cha upinzani naombwa nipewe tupesa kidogo na kuahidiwa vitu vingi. leo itakuwa ubunge?

Kwa mtazamo wangu Lwakatare angekuwa radhi kwenda CCM ili mradi tu kama angehakikishiwa kuwa atapendelewa ateuliwe kugombea kiti cha ubunge cha Bukoba Mjini. Lakini kwa utaratibu ambao CCM wameamua kuuchukua si rahisi kwa mtu kama Lwakatare aweze kupenya na kufikia jina lake kuwekwa kama mgombea wa CCM.


Mchukia Fisadi,
Wewe unadhani Lwakatare angekwenda CCM angepenya kirahisi katika mchakato wa kura za maoni? Kura za maoni zinapigwa na wanachama wa matawi yote katika jimbo husika, kama kweli angekuwa na ubavu huo angekwenda CCM lakini hili ni gumu, ni sawasawa na kupanda mlima Kilimanjaro na green-vest ya kijani.
 
Tunaitaji viongozi waadilifu na wakweli bila kujali wanatoka chama gani. Viongozi wetu inabidi wawe wakweli tu, hapo tutapiga hatua. Karibia chama chochote kaka.
 
Asante kwa kuniondoa wasiwasi. Nilifiri ni mimi tu ndiye anielewi. Nilitaka kumkatiza Shemu yenu hapa kumpa cha pili ili niandike verse ya kumjibu. Ila sasa ebu nimpe haki yake.

Mkuu,
Hapa jamvini tunashindanisha hoja na pia kila mtu ana haki ya kuwa na mawazo huru kabisa. Kama unapokuwa huna hoja ya msingi ni busara tu ukakaa kimya na haihitaji ushauri wa third party.

Bado ninatoa tahadhari kuwa Lwakatare ajisafishe sasa na asisubiri wakati ambapo hali ni ngumu kwake ambayo ninaona hatari hiyo mbele yake,
 
i support the move for the benefit of himself. Mana mwelekeo wa kafu/CUF siuelewi, hata sasa wananchi tunashindwa kuelewa mwelekeo wao

nadhani CUF haina dira wala mwelekeo.........except for zanzibar...zanzibar...zanzibar....too much. wanahitaji kujihusisha zaidi na mambo yanayogusa watanzania walio wengi ambao si wazanzibari...
 
nadhani CUF haina dira wala mwelekeo.........except for zanzibar...zanzibar...zanzibar....too much. wanahitaji kujihusisha zaidi na mambo yanayogusa watanzania walio wengi ambao si wazanzibari...
Kama wanataka kuonekana kuwa kweli ni chama cha tanzania kwa ajili ya watanzania
 
na Asha Bani

UAMUZI wa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Winfred Lwakatare, kujiuzulu nyadhifa zote na tetesi za kukihama, zimezidi kukichanganya chama hicho.

Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba, amemsihi asikivuruge chama hicho baada ya kuwapo tetesi kuwa kuna baadhi ya viongozi wa CUF wanataka kukihama.

Akifungua kongamano la siku moja la vijana lenye lengo la kushinikiza serikali kuunda tume huru ya uchaguzi na kudai mabadiliko ya Katiba ya Tanzania, lililofanyika katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni, jijini Dar es Salaam, Lipumba alisema wanaheshimu uamuzi wowote akatakaochukua Lwakatare.

Alisema hatashangazwa kama atasikia Lwakatare kaihama CUF kwa kuwa ni kawaida ya viongozi wa Tanzania Bara waliomo ndani ya vyama vya upinzani kuhama chama mara yanapotokea mabadiliko ya uongozi.
Lipumba alisema tabia hiyo ya kuhama inaonekana kuanza kuwa sugu, lakini ni vema wanaohama wakajenga utamaduni wa kutambua na kukubali mabadiliko yanayofanyika ndani ya vyama vyao.

“Lwakatare ana haki na uhuru wa kuhama CUF, lakini asivuruge amani ndani ya chama,” alisema Lipumba.

Lipumba aliwataja baadhi ya viongozi waliokihama chama hicho baada ya kutokea mabadiliko ya uongozi kuwa ni Shaibu Akwilombe, aliyehamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Tambwe Hizza, aliyehamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Alisema si busara kwa viongozi waliopo madarakani kufikiri kuwa watakaa madarakani milele katika CUF, kwa kuwa ni chama cha wananchi, kinachoendeshwa kama taasisi.

Alibainisha kuwa hata yeye muda wake ukiwadia ataondoka ndani ya chama hicho, kwa vile atakuwa anaheshimu uamuzi wa wanachama wake na kukubali matokeo.

“Hakuna mtu ambaye atakaa katika nafasi ya uongozi ndani ya CUF muda wote, ni lazima kuwe na mabadiliko. Mimi (Lipumba), Maalim Seif Shariff Hamad (Katibu Mkuu) na Juma Duni, muda wetu ukifika hatutang’ang’ania madaraka,” alisema Profesa Lipumba.

Aidha, pia Lipumba alibainisha kuwa wakati wote wa uongozi wake Lwakatare, hakuwa na matatizo ya kiutendaji, kwani alishiriki kikamilifu katika masuala ya chama.

Alisema hata mkutano mkuu uliofanyika mapema mwaka huu, alishiriki na kutumia nafasi hiyo kukabidhi barua ya kujiuzulu.

Alisema Lwakatare hakuteuliwa kushika wadhifa wake wa Naibu Katibu Mkuu, si kwa sababu ya ugomvi au lengo la kumuudhi, bali yalikuwa ni mabadiliko ya kawaida.

“Nilimweleza kuwa lengo la CUF hivi sasa ni kujiimarisha, hasa Bukoba Mjini ambako tunakubalika zaidi, nilimsihi tusikivuruge chama,” alisema Profesa Lipumba.

Wakati Lipumba akisema hayo, mwishoni mwa wiki hii, Lwakatare aliiambia Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka Bukoba kuwa hajajivua uanachama wa CUF, bali alichokifanya ni kujivua uongozi.

“Mpaka sasa mimi bado ni mwanachama hai wa CUF, ingawa wapiga kura wangu wameniomba nikihame chama hiki, nimewaambia ombi lao nimelipokea kwa mikono miwili, nimewaomba wanipe muda nikashauriane na familia yangu, na baada ya muda nitatoa uamuzi wangu wa mwisho,” alisema Lwakatare.

Aidha, Lipumba alitumia mkutano huo kuwasihi wanachama wake kutokatishwa tamaa na matokeo ya uchaguzi wa Jimbo la Busanda, ambapo CUF ilifanya vibaya, tofauti na uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Alisema kutokana na chama kufanya vibaya kwenye uchaguzi huo, tayari viongozi kadhaa wamefukuzwa ndani ya chama hicho.

Aliwataka vijana kujipanga kwa uchaguzi wa serikali za mitaa, ambao unatarajiwa kufanyika mwaka huu, kwa kuchagua viongozi bora na kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Naye Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Juma Duni Haji, alisema ili kuwapo uchaguzi huru ni lazima Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iwe huru, ili kuepuka vitendo vya wizi wa kura. Alisema katika chaguzi zote ndogo za Tanzania Bara na Zanzibar kuna ubadhirifu mkubwa wa wizi wa kura unaofanywa na CCM.


Tanzania Daima.
 
Last edited by a moderator:
Big up to Lwakatare kama kweli atakuwa amehamia au ana mipango ya kuhamia CHADEMA.

Ni dhahiri kwamba kwa sasa chama chenye mvuto wa kisiasa ni CHADEMA baada ya CCM(CHAMA CHA MAJAMBAZI). CHADEMA kwa sasa ndiyo tishio kwa CCM katika medani za kisiasa Tanzania.

Mimi nam-support Lwakatare maana atakuwa amefanya uamuzi wa busara. CUF kweli kina nguvu lakini ni upande mmoja tu wa Visiwani. Kwa hiyo CUF ni kama chama cha Wazanzibar na hasa Wapemba peke yake. Kwa hiyo ukipiga darubini yenye kiona mbali kikali utakuta kwamba ndani ya CUF kuna ka-ubaguzi ka-Udini na ka-Ukabila.

Chama chenye mwelekeo kama huo hakifai kwa mazingira ya Tz.

Nawaomba wana-CHADEMA wampokee Lwakatare kwa mikono miwili.

Makoye.
 
Hakuna mtu ambaye atakaa katika nafasi ya uongozi ndani ya CUF muda wote, ni lazima kuwe na mabadiliko. Mimi (Lipumba), Maalim Seif Shariff Hamad (Katibu Mkuu) na Juma Duni, muda wetu ukifika hatutang'ang'ania madaraka," alisema Profesa Lipumba.
Aidha, pia Lipumba alibainisha kuwa wakati wote wa uongozi wake Lwakatare, hakuwa na matatizo ya kiutendaji, kwani alishiriki kikamilifu katika masuala ya chama.
Alisema hata mkutano mkuu uliofanyika mapema mwaka huu, alishiriki na kutumia nafasi hiyo kukabidhi barua ya kujiuzulu.
Alisema Lwakatare hakuteuliwa kushika wadhifa wake wa Naibu Katibu Mkuu, si kwa sababu ya ugomvi au lengo la kumuudhi, bali yalikuwa ni mabadiliko ya kawaida.
"Nilimweleza kuwa lengo la CUF hivi sasa ni kujiimarisha, hasa Bukoba Mjini ambako tunakubalika zaidi, nilimsihi tusikivuruge chama," alisema Profesa Lipumba....
Ama kweli ukiwa mwalimu mchumi ni bora ubakie ktk kazi unayoijua vizuri.. sasa huyu Lipumba anachojaribu kusema ni kipi hapa?..Unataka kuimarisha Chama Bukoba kisha unamwondoa mtu ambaye kafanya kazi yake vizuri kitaifa na huko Bukoba, matokeo yake chama kimemomonyoka huko Bukoba..

Ni ishara zipi za wakati wake yeye kung'atuka! Ni kina nani ambao wako responsible na Uteuzi wa nafasi zao (yeye na Maalim) ktk nyadhifa walizoshika maanake anajigonga kichizi..Uteuzi unaoliondoa jina la aliyekuwa naibu katibu hauwezi kuwepo bila sababu za msingi hasa pale anaposisitiza Lwakatare kafanya kazi yake vizuri tu na ati sababu kubwa ni kukiimarisha chama Bukoba..wamekiimarisha vipi chama kama sii kuzua ugonvi na haya yote yasingetokea kama Lwakatare angebakia ktk majina ya uteuzi na akaja shindwa ktk uchaguzi..Wajumbe ndio sikio la chama ikiwa mtu hafai wajumbe hawataweza kumpakura hata kidogo..
 
na Asha Bani



Mimi (Lipumba), Maalim Seif Shariff Hamad (Katibu Mkuu) na Juma Duni, muda wetu ukifika hatutang’ang’ania madaraka,” alisema Profesa Lipumba.
.
Khee. Hivi huo muda wenu lini utafika? Si uliishia pale ulipomalizika uchaguzi wa 2005. Ondokeni Bwana-mnagharibu bahati za CUF
 
CUF wanavuna walichopanda kwa miaka dahari! wenzao wanaimarisha chama wao wanaua chama yawezekana ikawa ni kutokana na dua za wapinzani wao japo dua la kuku halimpati mwewe lakini hapa yawezekana kabisa dua la kuku likampata mwewe, unamnyima nafasi zote Lwakatare za juu ili iweje? mtu ambaye alifanya kazi kubwa kuuaminisha uma wa Tz kuwa CUF si chama cha kidini ndiyo maana yeye Wilfred kupewa u-Naibu katibu mkuu sasa sijui kwa kutoka CUF atabadili yale aliyowahi kutuhubia siku moja katika uwanja wa chipukizi mijini Tabora? any way twa subiri kwa hamu attoka na mpya ipi maana ndo wana siasa wetu hawa
 
"Prof wa Pumba akiwa kazini!"
________________________

Masanilo:
Wee Bwana wee, mbona wanivunja mbavu? Ni kweli kabisa. Profesa ni mfano wa the biggest failure katika historia ya vyama vya upinzani katka nchi hii. Ni zaidi hata disappointment ya Mzee Lyatonga!

Hivi muafaka basi? Mbona hauzungumzii kabisa? Yaani baada ya ile chenga ya CCM "ya kupeleka makubaliano kwa wananchi" ndiyo nyonga imekwisha kazi?
 
personally,i have the feelings that Lwakatare IS MUNIPULATED by ccm!ccm nawajua vizuri sana,wanajua sana kuzitumia opportunities.

The thing is,watu wanatakiwa kujiuliza WHAT IS NOT RIGHT WITH LWAKATARE?making judgement in favour of lwakatare will not help
 
Lipumba na Maalim wamekuwepo kwenye uongozi wa CUF tokea 1994. Wamegombea mwaka 1995, 2000, 2005. Wakubali tu wao ni vign'ang'anizi kama wengine. Wenzetu wengine ukishindwa chaguzi moja tu basi mtu unajiuzulu kwenye uongozi na mtu kupewa ugombea hata mara mbili ni kazi kweli. Sasa watu wapo kwenye madaraka ya chama kwa miaka 15 anasema siyo ving'ang'anizi? Wakubali tu wanataka hayo madaraka.
 
Lwakatare ni loser tu acheni aende kwa wachovu wenzio huko Chadema. CUF walikuwepo akina Mapalala, Nyaruba, Akwilombe, Hiza, Msafiri nk wameondoka na CUF bdo ngangari.

Lwakatare ni opportunist tu na kwa uchovu wa vyama vyetu atatengezewa cheo huko chadema nako atavurunda na his final destination ni CCM

Mark my words...
 
Big up to Lwakatare kama kweli atakuwa amehamia au ana mipango ya kuhamia CHADEMA.


Kwa hiyo CUF ni kama chama cha Wazanzibar na hasa Wapemba peke yake. Chama chenye mwelekeo kama huo hakifai kwa mazingira ya Tz.

Nawaomba wana-CHADEMA wampokee Lwakatare kwa mikono miwili.

Makoye.
Nafikiri Makoye una maoni muwafaka tu. CUF haifai Bwana!!!. Hicho sio Chama !!
 
Lwakatare ni opportunist tu na kwa uchovu wa vyama vyetu atatengezewa cheo huko chadema nako atavurunda na his final destination ni CCM...

the bolded part of th quote is the clear picture of ccm's munipulation of lwakatare
bravo masatu!good work!good job
 
Back
Top Bottom