Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

CUF inajiita chama mbadala bila kuwa na mbunge sehemu kubwa ya nchi, mpiganaji kama Lwakatare inatakiwa ajiunge na wapiganaji wenzake akina Zito Kabwe, Dk Slaa, Freeman Mbowe, Tundu Lisu nk. Kubaki CUF atakosa hii oportunity, Isitoshe Hesabu yake ni nzuri kwa kuwa ameona akigombea ubunge kupitia CHADEMA uwezekano wa kupata utakuwa mkubwa. Lakini awe makini maana kila mwaka CCM wanakuja na mbinu mpya, Uchaguzi uliopita walinunua shahada za wakazi BK mjini hatujui safari hii watakuja na ipi. Nadhani ameona mbali let him go.
 
Siyo siri CUF wanahitaji mabadiliko makubwa. Nilifurahi sana kusikia Bwana Kuchilingulo & Co. wameondolewa kwani sitasahau waliyoyafanya kwa wagombea wa Ubunge 2000. Manake pesa za wagombea zilipotelea njiani. CUF ilikuwa imetoa kiasi fulani kuyasaidia majimbo yaliyokuwa imara lakini fedha hizo hazikufika. Wagombea walilalamika lakini hakuna kilichotokea. Hii iliwavunja moyo potential candidates wengi sana Tanzania bara.
 
Mugo"The Great";496318 said:
Siyo siri CUF wanahitaji mabadiliko makubwa. Nilifurahi sana kusikia Bwana Kuchilingulo & Co. wameondolewa kwani sitasahau waliyoyafanya kwa wagombea wa Ubunge 2000. Manake pesa za wagombea zilipotelea njiani. CUF ilikuwa imetoa kiasi fulani kuyasaidia majimbo yaliyokuwa imara lakini fedha hizo hazikufika. Wagombea walilalamika lakini hakuna kilichotokea. Hii iliwavunja moyo potential candidates wengi sana Tanzania bara.

Mkuu,
Bwana Kuchilingulo ndiyo nani?
 
Mie nashukuru tu yale mashaka tuliyokuwa nayo wengine dhidi ya chama cha CUF yanadhihirika sasa!
 
kuna mawili, nayo ni kuwa mwansiasa----kama ajira, na kuwa kujiunga na chama, Lwakatare anasema anangoja ushauri wa familia kuhusu yeye kuendelea na siasa au la, akiendelea na siasa, anaweza kujiunga na chama chochote (au kubaki alipo) LAKINI kuna mambo ni lazima ayapiganie kimaslahi kwani hapo siasa ni career lazima upiganie uwe kiongozi--kama una sifa ili upate mshahara na posho kama waajiriwa wengine. kwenye hili, sioni kama atabaki CUF

Akiamua kuwa siasa basi, then anaweza kujiunga na chama chochote na asigombee uongozi wala ubunge, awe kama wengi wetu!
 
Nakubaliana nawe Pundamilia07. kwa nini muingie PM. Tupo wengi tunafaidika na mijadala yenu endeleeni kulumbana -tutaungana nanyi baada kukuchambueni mnayosema.
 
Mkuu,
Bwana Kuchilingulo ndiyo nani?

Sijui nafasi aliyokuwa nayo kabla ya kuondolewa hivi karibuni kwani Niliacha kufuatilia siasa za CUF tangu 2001. Hata hivyo alikuwa anahusaika sana na mambo ya Uchaguzi na alikuwa karibu sana na Mh. Lipumba. Nadhani safari hii baada ya kushindwa Busanda, Mh. Lipumba ameshindwa kumvumilia yeye na team yake.
 
Mkuu Mtanzania,
Huyu Lwakatare amechukua njia sahihi kabisa,ukiona unakaa kwenye timu ambayo ina mwelekeo wa kutotoa dalili ya kubeba mataji ni budi kuondoka na kujiunga na timu yenye ari ya ushindi.Mfano mzuri ni "Mashujaa wa kupambana na ufisadi wa CCM" ambao wanajua fika kuwa waliwekewa kwenye account zao mgawo wa fedha za EPA,halafu wanaendelea kupayuka hadharani kuwa wanapiga vita ufisadi ni kioja na unafiki mkubwa.
Mpiganaji Lwakatare ameamua kwendelea kutafuta mataji kwa kuingia kwenye timu iliyojaa modern politicians wenye ari ya kuleta mabadiliko kwenye jamii ya Kitanzania.CCM na vyama vingine vina makada ambao ni Nationalists waliopambana na Wakoloni,hivyo wana hangover ya kuendelea kupambana na ulimwengu uliojaa challenges mpaya ambazo wao hawana mbinu wala utashi wa kushindana.
 
Hayo 'matatizo kibao' ndiyo yaliyomuondoa Lwakatare CUF mara baada ya kutemwa Unaibu Katibu Mkuu. Inaonekana ile hoja ya ubadhirifu ni valid. Inawezekana Mheshimiwa alikuwa anamalizia shida zake kwenye kofia ya Unaibu Katibu Mkuu na mara baada ya kuondolewa sasa inakuwa imeshakuwa taabu, CUF haiwezi kukalika.

Mheshimiwa ameonesha kuwa yeye ni kiongozi mbinafsi wa hali ya juu kabisa hasa pale anapoitaka CUF iweke sera maalum za kuwaenzi 'wastaafu' baada ya yeye kutemwa katika safu ya uongozi wa juu. Ni kwanini hakupigania hili wakati akiwa kiongozi kwa ajili ya wale ambao tayari si viongozi tena? Au aliona kuwa yeye yuko mbali na ukweli siku moja naye hatakuwa kiongozi wa juu?

Pili, inaonekana kuwa Mheshimiwa pamoja na kuwa na juhudi nyingi lakini hakuwa na vision na hili linadhihirika pale baada ya muda mfupi kutolewa katika madaraka ya juu analalamika jinsi ambavyo CUF imekosa mwelekeo katika siasa za bara na hata kudiriki kusema CUF inatia aibu. Hapa Mheshimiwa anasahau kuwa yeye ndiye aliyekuwa namba tatu na pia akiwa na jukumu la pekee la kusimamia shughuli za chama kwa upande wa bara?

Mheshimiwa Lwakatare, nadhani hana jipya zaidi ya kusaka kiti cha Bukoba Mjini. Kwa mtazamo wangu Lwakatare angekuwa radhi kwenda CCM ili mradi tu kama angehakikishiwa kuwa atapendelewa ateuliwe kugombea kiti cha ubunge cha Bukoba Mjini. Lakini kwa utaratibu ambao CCM wameamua kuuchukua si rahisi kwa mtu kama Lwakatare aweze kupenya na kufikia jina lake kuwekwa kama mgombea wa CCM. Safari yake ya kwenda CHADEMA ameiona kuwa inaweza kumnufaisha kwa vile chama hicho kwa sasa kinaangalia sura ya mtu na jinsi anavyoweza kuwapatia ushindi hata kama anamushkeli.

Kwa kweli, pamoja na matatizo yote ya Lwakatare, hayo yanayoitwa matumizi mabaya ya fedha hayapo, maana Lipumba aliulizwa swali na kujibu, "hatumdai wala hatuna kashfa yoyote dhidi yake" na hiyo ni kauli ya uhakika, maana hakukuwa na tuhuma zozote zilizojadiliwa katika vikao vyote kabla na baada ya Lwakatare kuondolewa katika Unaibu Katibu Mkuu.

Lakini, tujue suala moja hapa kwamba, hakuna mtu anayeingia katika siasa kuwa mtumishi tu wa wengine, wote wana matarajio ya kupanda ngazi.

Aliwahi kusema Dr. Gharib Bilali, kwamba, "mimi ni mwanasiasa, nimeshakuwa Waziri Kiongozi, kwa hiyo lazima niangalie juu zaidi, kuanzia urais wa Zanzibar hata wa Jamhuri ya Muungano". kwa hiyo kama mwanasiasa anaona maslahi yake kisiasa yanahatarishwa katika chama husika, na kwa kuwa ni mwana mageuzi, chaguo la kwanza ni kwenda katika chama ambacho anaona kimeshika chati katika eneo husika, na kwa sasa Chadema ndicho chama cha upinzani chenye nguvu bara. Chaguzi ndogo za hivi karibuni zimedhihirisha.

Lakini jambo lingine lililo wazi ni kuhusu CUF kuanza kupoteza kuungwa mkono kwa wao kuamua kwenda "kivyao vyao" wakati wananchi na wanasiasa wenzao wakiwamo wa CCM wamebadili mbinu na kwenda kwa wananchi na kufuata wananchi wanavyotaka. Kwa sasa hata hao munaowaita mafisadi, wanahutubia na kusema "wanapambana na ufisadi" na hiyo ndiyo turufu ya sasa. Sasa Lwakatare anaangalia alama za nyakati.

Pamoja na kuwa sipendi, si vibaya kwake kwenda hata CCM ikiwa CHADEMA watamkataa (miujiza) kwani siasa ni popote, inategemea na mkakati wa mtu mmoja mmoja. Naamini Lwakatare hayuko sawa na kina Akwilombe na Tambwe Hiza, kwa kuwa amewahi kuwa Mbunge na Kiongozi wa Upinzani. Ana wafuasi na imedhihirishwa na mikutano yake. Mwanasiasa ni watu.

Suala la mwisho, ni kwamba kwa muda mrefu sana Lwakatare amekuwa na msimamo wa kuwa na ushirikiano na vyama, na wenzake walikuwa hawataki mahusiano na CHADEMA na ndio maana amekuwa akituhumiwa kutoa "siri" kwa CHADEMA. Naamini hakukuwa na siri zozote bali ni mambo ya uninafsi tu, ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya fedha na mikataba feki. Kuna mambo mengi ya ovyo ikiwa ni pamoja na aibu ambayo ikipasuka itakiabisha chama cha CUF, ikiwa ni pamoja na kuwapo taarifa za mizigo yake kukamatwa mpakani ikitumika kukwepa kodi na mfanyabiashara ambaye ameingia mikataba ya ovyo na viongozi. Wao wenyewe ndani wanalalamika, lakini Lwakatare aliwatetea na leo hii hata waandishi wakimuuliza anagoma kutoa hiyo siri ikiwa ni pamoja na kukataa kutoa siri ya RA na CUF.

Mwacheni Lwakatare aamue pa kwenda hata ikiwa ni CHADEMA ama CCM
 
Vyama vingi vya Upinzani havipo kama TAASISI, vipo kwa majina na UMAARUFU wa watu flani. Ndio maana watu hao wakihama kwa sababu yoyote ile vyama hivi vinakufa kifo cha kawaida kabisa. Lwakatare analijua hili kwamba jimbo lake(na kabila yake?) ni yeye ndiye CUF na CUF ni yeye. Inampa kiburi ambacho hata huko atakakohamia(isipokuwa CCM ambayo ni Taasisi), haitamsaidia sana. Amuulize Mrema madhara ya staili hii ya kumiliki wafuasi.
 
Pundamilia07 said:
Mheshimiwa Lwakatare, nadhani hana jipya zaidi ya kusaka kiti cha Bukoba Mjini. Kwa mtazamo wangu Lwakatare angekuwa radhi kwenda CCM ili mradi tu kama angehakikishiwa kuwa atapendelewa ateuliwe kugombea kiti cha ubunge cha Bukoba Mjini

Pundamilia07
Rejea post zangu za nyuma. Offer hii itolewe mara ngapi?!
Niliileza bayana jinsi CCM ilivyoomba ahamie kwao. Nilisema CCM walikuwa tayari kumjengea Babu (Kagasheki) mazingira ya ku-step down ili Lwakatare ndiye agombee kupitia CCM. Niliwapasha juu ya Mjumbe wa CUF alitumwa Ibwera, kijijini kwao na Lwakatare ili kumwomba Baba amshauri mwanae asihame. Na mwisho nikatoa angalizo la kutotaka kuhojiwa juu ya mantiki/logic ya CUF kupitia Baba mtu.
 
Politics ni kazi kama zilivyo zingine,hivyo unatafuta palipo na maslahi,we kwenye akili yako kweli kuna kiongozi Afirka hii anayetetea maslahi ya wananchi bila yeye kunufaika kwanza? muacheni akajilie huko Chadema.
 
Mkuu Nsaji,

Sina tatizo na Lwakatare kuhamia CHADEMA maana huenda ameona atafanikiwa zaidi akiwa CHADEMA.

Wasiwasi wangu ni hiyo njia aliyotumia wakati wa kujitoa. Hata kwenye ndoa, ukitaka kutoa talaka, hakuna haja ya kuelezea mapungufu ya bwana/mke unless ni muhimu sana.

Mimi huwa nawaogopa sana watu ambao leo anakuita sweetheart lakini mkikosana anaanza kukutukana na kutoa siri za ndani.

Ni mambo kama ya akina Tambwe ambaye alipokuwa Upinzani alikuwa anaongea tofauti na sasa CCM anasema tofauti. Nawashangaa hata CCM wanampa nafasi mtu kama huyo.

Vinginevyo ninamtakia mafanikio mema huko CCM, ila mambo yakigoma sitashangaa nikisikia kaenda CCM.

Mkuu Mtanzania,
Huyu Lwakatare amechukua njia sahihi kabisa,ukiona unakaa kwenye timu ambayo ina mwelekeo wa kutotoa dalili ya kubeba mataji ni budi kuondoka na kujiunga na timu yenye ari ya ushindi.Mfano mzuri ni "Mashujaa wa kupambana na ufisadi wa CCM" ambao wanajua fika kuwa waliwekewa kwenye account zao mgawo wa fedha za EPA,halafu wanaendelea kupayuka hadharani kuwa wanapiga vita ufisadi ni kioja na unafiki mkubwa.
Mpiganaji Lwakatare ameamua kwendelea kutafuta mataji kwa kuingia kwenye timu iliyojaa modern politicians wenye ari ya kuleta mabadiliko kwenye jamii ya Kitanzania.CCM na vyama vingine vina makada ambao ni Nationalists waliopambana na Wakoloni,hivyo wana hangover ya kuendelea kupambana na ulimwengu uliojaa challenges mpaya ambazo wao hawana mbinu wala utashi wa kushindana.
 
Ukisoma vizuri alama za nyakati, CUF imepoteza mvuto wa kitaifa na kimkoa. Mgombea mtarajiwa yeyote mwenye kupiga hesabu vizuri hata kama anao mtaji wa wapiga kura, kugombea kupitia CHADEMA ndiyo turufu yenye uwezekano mkubwa wa kushinda ubunge.
.....adha yoooote hiii..eti anagombania nafasi ya uongozi ili aje atutumikiye sisi wananchi!...subutu!!!!
 
Ukisoma maelezo ya Lwakatare ana shida mbili kwa sasa: Pesa na Cheo. Hayo mengine ya kiuendeshaji si mapya kwake; angeweza kurekebisha au kuondoka siku nyingi.

Anahitaji pesa kwa ajili ya kesi na uendeshaji maisha. Kwa sasa anachoweza kukipata Chadema ni pesa si cheo. Ama ubunge uwezekano mkubwa ni kugawa kura na CCM Kushinda.
 
Pundamilia07
Rejea post zangu za nyuma. Offer hii itolewe mara ngapi?!
Niliileza bayana jinsi CCM ilivyoomba ahamie kwao. Nilisema CCM walikuwa tayari kumjengea Babu (Kagasheki) mazingira ya ku-step down ili Lwakatare ndiye agombee kupitia CCM. Niliwapasha juu ya Mjumbe wa CUF alitumwa Ibwera, kijijini kwao na Lwakatare ili kumwomba Baba amshauri mwanae asihame. Na mwisho nikatoa angalizo la kutotaka kuhojiwa juu ya mantiki/logic ya CUF kupitia Baba mtu.

Omutwale,
Hayo maneno ya hapo juu hayawezi kutamkwa na mtu mwingine yeyote isipokuwa Lwakatare tu. Si maanishi kuwa wewe ni Lwakatare mwenyewe.
Hiyo habari ya kwenda CCM Lwakatare katu asingekubali kwani nia yake ni kiti cha ubunge. Hata kama angekwenda CCM lakini anajua kabisa kwa taratibu mpya za CCM katika uteuzi wa wagombea, nafasi yake ya kupita ni 50-50. Kwa mantiki hiyo, mahali ambapo anaweza kupata upendeleo maalum ni chama kingine chochote isipokuwa CCM.
Kwa hiyo ninaposema kuwa malengo ya Mh Lwakatare ni kiti cha ubunge wa Bukoba Mjini sijakosea hata kidogo. Kama lengo ni kuleta mabadiliko ya kisiasa basi pia angeweza kufanya kazi ya kuimarisha upinzani kwa kuwatengeneza wabunge wengi zaidi kutoka katika kambi ya upinzani (Tukumbuke huyu alikuwa Naibu Katibu Mkuu - Bara).
Kwa mantiki hiyo bado ninaona kuwa Lwakatare hana jipya zaidi ya kutaka kuonekana nadhifu na labda kubadilisha shangingi lingine mwakani.
 
Hayo 'matatizo kibao' ndiyo yaliyomuondoa Lwakatare CUF mara baada ya kutemwa Unaibu Katibu Mkuu. Inaonekana ile hoja ya ubadhirifu ni valid. Inawezekana Mheshimiwa alikuwa anamalizia shida zake kwenye kofia ya Unaibu Katibu Mkuu na mara baada ya kuondolewa sasa inakuwa imeshakuwa taabu, CUF haiwezi kukalika.

Mheshimiwa ameonesha kuwa yeye ni kiongozi mbinafsi wa hali ya juu kabisa hasa pale anapoitaka CUF iweke sera maalum za kuwaenzi 'wastaafu' baada ya yeye kutemwa katika safu ya uongozi wa juu. Ni kwanini hakupigania hili wakati akiwa kiongozi kwa ajili ya wale ambao tayari si viongozi tena? Au aliona kuwa yeye yuko mbali na ukweli siku moja naye hatakuwa kiongozi wa juu?

Pili, inaonekana kuwa Mheshimiwa pamoja na kuwa na juhudi nyingi lakini hakuwa na vision na hili linadhihirika pale baada ya muda mfupi kutolewa katika madaraka ya juu analalamika jinsi ambavyo CUF imekosa mwelekeo katika siasa za bara na hata kudiriki kusema CUF inatia aibu. Hapa Mheshimiwa anasahau kuwa yeye ndiye aliyekuwa namba tatu na pia akiwa na jukumu la pekee la kusimamia shughuli za chama kwa upande wa bara?

Mheshimiwa Lwakatare, nadhani hana jipya zaidi ya kusaka kiti cha Bukoba Mjini. Kwa mtazamo wangu Lwakatare angekuwa radhi kwenda CCM ili mradi tu kama angehakikishiwa kuwa atapendelewa ateuliwe kugombea kiti cha ubunge cha Bukoba Mjini. Lakini kwa utaratibu ambao CCM wameamua kuuchukua si rahisi kwa mtu kama Lwakatare aweze kupenya na kufikia jina lake kuwekwa kama mgombea wa CCM. Safari yake ya kwenda CHADEMA ameiona kuwa inaweza kumnufaisha kwa vile chama hicho kwa sasa kinaangalia sura ya mtu na jinsi anavyoweza kuwapatia ushindi hata kama anamushkeli.

Hayo niliyohighlight kwa wino mwekundu ni ya kweli?
Mbona nyie mliokunywa maji ya kijani mtachomwa moto kwa uongo wenu wa mchana kweupe?
Wooooooooooooote waliokuwa upinzani na wakarudi chi chi mafichadi hamkuwapa kitu?????
Mimi nataka kugombea uenyekiti wa mtaa tu kupitia chama cha upinzani naombwa nipewe tupesa kidogo na kuahidiwa vitu vingi. leo itakuwa ubunge?
 
Ni mimi ndiye napata taabu sana kukuelimisha wewe na si Lwakatare kueleweka kwa wapiga kura. Ningeweza ningeweka Mkanda wa Mkutano wake alioufanya BK trh 19 mwezi huu ili nawe ujionee na kujisikilizia.

Tunafua nguo chafu, tusafisha viatu walau hata kama vina vumbi lakini je, tunaweza kuyaosha maji yaliyo safi?

Pundamilia07, naona tunaanza kuufanya mjadala kuwa wetu. Waonaje tusi-bore na tuingie vyumba vya ndani (PM)?!

Kwa kumuelewesha PundaM unasumbuka tu. Huyu hajawahi kukubali ukweli unaohusu watu walio kwenye vyama vya upinzani Tanzania.
Alikunywa maji ya kijani. Habadiliki hata katika ukweli. Anang'ang'ania tuuu point ambayo haina hoja ndani yake. Mwache na msimamo wake.
Usim PM. No need.
 
Kwa kumuelewesha PundaM unasumbuka tu. Huyu hajawahi kukubali ukweli unaohusu watu walio kwenye vyama vya upinzani Tanzania.
Alikunywa maji ya kijani. Habadiliki hata katika ukweli. Anang'ang'ania tuuu point ambayo haina hoja ndani yake. Mwache na msimamo wake.
Usim PM. No need.

Asante kwa kuniondoa wasiwasi. Nilifiri ni mimi tu ndiye anielewi. Nilitaka kumkatiza Shemu yenu hapa kumpa cha pili ili niandike verse ya kumjibu. Ila sasa ebu nimpe haki yake.
 
Omutwale,
Hayo maneno ya hapo juu hayawezi kutamkwa na mtu mwingine yeyote isipokuwa Lwakatare tu. Si maanishi kuwa wewe ni Lwakatare mwenyewe.
Hiyo habari ya kwenda CCM Lwakatare katu asingekubali kwani nia yake ni kiti cha ubunge. Hata kama angekwenda CCM lakini anajua kabisa kwa taratibu mpya za CCM katika uteuzi wa wagombea, nafasi yake ya kupita ni 50-50. Kwa mantiki hiyo, mahali ambapo anaweza kupata upendeleo maalum ni chama kingine chochote isipokuwa CCM.
Kwa hiyo ninaposema kuwa malengo ya Mh Lwakatare ni kiti cha ubunge wa Bukoba Mjini sijakosea hata kidogo. Kama lengo ni kuleta mabadiliko ya kisiasa basi pia angeweza kufanya kazi ya kuimarisha upinzani kwa kuwatengeneza wabunge wengi zaidi kutoka katika kambi ya upinzani (Tukumbuke huyu alikuwa Naibu Katibu Mkuu - Bara).
Kwa mantiki hiyo bado ninaona kuwa Lwakatare hana jipya zaidi ya kutaka kuonekana nadhifu na labda kubadilisha shangingi lingine mwakani.

Ndiyo, uko sahihi kabisa hapo juu kulingana na mtazamo na fikra zako.
 
Back
Top Bottom