Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Mkuu mm sipingi.
Huo umati ulioelezea hapo ni mkubwa mno kiasi kuwa hawa wawili tu ndio uliwaona ww (au umehadithiwa Mkuu?) pia si vibaya ushatusaidia, halafu zaidi heading inasema "wananchi wa Bukoba wataka...." wakati mkutano ni wa CUF waliohudhuruia hapo ni wanachama wa CUF(au niseme ni wa Lwakatare),halafu mkuu unaapa? unasema "...ukweli mtupu..."

*Nani alikwambia kwamba mkutano wa hadhara unahudhuriwa na wananchi wa chama kimoja?. Kwa taarifa yako watu walionipa taarifa ni wanachama wa vyama 3 maarufu nchi hapa ikiwamo sisi M.

*Nimeshakwambia kuwa nimehadithiwa mkuu kama ninavyokuhadithia mimi. Lakini nina source zaidi ya moja.

*Kwa habari ya heading unaweza kuweka unayoona inafaa lakini habaari ndiyo hiyo. Inaumiza lakini sasa ukweli nitaubadili uwe uongo?

*Hapa ndipo vyama vya upinzani mnatuacha hoi. Badala ya kuanza mikakati ya kuwekana sawa na mwenzenu kila kitu mnaona ni uongo.Na hapa ndipo Busanda iliwaponyoka.

*Haya basi subiri matokeo utajua MF alikuwa anasema nini. Au mpaka usome kwenye magazeti?
 
Kwenye umati mkubwa unaweza kuhesabu mikono na kuona miwili tu?

Wanacheza hawa, either kulikuwa na watu wa kuhesabika, au hawakuweza kuthibitisha kwamba ni mikono ya watu wawili tu.

The whole presentation seems like there is a big PR move behind this, wote hawana imani yangu, si CUF wala huyu Lwaka nani sijui, wasanii watupu.

mkuu Bluray

Hili halikushangazi wewe tu, bali hata mimi.
Lakini nakwambia kama unayo source nyingine fanya homework yako badala ya kutaka kubadilisha ukweli kuwa uongo. Nini ambacho hakiwezekani?
Kama huu ni uongo, kaa hivyo hivyo ukifikiri ni PR mwisho wake utauona:(
 
Suala la Lwakatare kupokelewa kwa shangwe, kuhutubia umati na kupewa maelekezo na wananchi akachambua na kufuata siyo habari kabisaaaa. Wao wanasema "Nosindika Atandamile" (Ni sawa na kumsukuma aliyechuchumaa) Siyo kama namkandia Mchukia Fisadi bali nawaweka sawa wasioijua Bukoba na mapenzi ya wanaBK kwa Entare, Lwakeupe, Lwaks, famously known as Lwakatare.

Wakati wengine wanajiua kwa Arsenal kufungwa na manchester, BK alijiua mtu eti kisa Kagasheki katangazwa mshindi. Huyu hata Lwaks mwenyewe hakumjua kwa sura. Visa vya kisiasa vimedudu miaka mitatu sasa utafikiri uchaguzi ni kesho. Harusi na misiba ya watu wa CUF imekuwa kama ni misiba ya kichama. Ujio wa Lwaks Bk siku zote imekuwa kama ujio wa mkombozi.
 
Pundamilia07,
Hapana mkuu mimi siitazami picha hii kama unavyoitazama. Kwanza kumbuka maelezo yote aliyoambiwa Lwakatare ni nje ya kiofisi, hakuna barua wala maelezo yalitolewa na uongozi wa CUF kwa nini jina lake halikuteuliwa kugombea tena kiti hicho, jambo ambalo hata mke wa Kaisali asingeweza kujisafisha maadam talaka imeshatolewa..Unajisafisha ili iwe nini?...utajisafisha wakati tuhuma zinapowekwa mbele yako na hujapoteza ndoa lakini sii baada..Lolote utakalo sema halina turufu kwani mume kisha fikia maamuzi ya kuvunja ndoa hata kama hukufanya baya lolote...kifupi ameshakuchoka!

Uamuzi uliofikiwa ni sawa na ule wa Mzee Malecela alipotaka kugombea Urais, jina lake liliondolewa hata kabla ya wajumbe kupiga kura. Kama kweli Lwakatare angekuwa hivyo wanavyodai basi hapakuwa na haja ya kuondoa jina lake maanake kura asingezipata..sidhani kama wajumbe wangeweza kumchagua mtu wa aina hiyo tena chama chenyewe CUF!..Hivyo binafsi nina imani kabisa kwamba viongozi wa juu wa CUF walikosa imani na mtu huyu yapo maswala mazito zaidi ya madai yaliyotolewa pengine hata hizo tuhuma za kuhamia Chadema ama yawezekama pia msimamo wake kuhusiana na swala la RA linapingana na mtazamo wa viongozi wa CUF kina Lipumba..

Kifupi mkuu wangu CCM wamekwisha ifanya kazi wanayotakiwa kuifanya kabla ya uvhaguzi wa mwaka 2010..Vyama vya Upinzani vimebakia dhaifu kabisa, kujitoa kwa Zitto, Lwakatare na wengine kibao watafuata wakiwa na sababu za msingi kabisa..
Mwisho wa picha nzima mkuu wangu - NJAA mkuu wangu njaa ndiye adui mkubwa wa Umaskini angalia kilio chote cha Lwakatare kimeishia wapi?..kalia na tumbo lake akatiwe japokuwa kidogo maanake haoni mbele (future) nje ya CUF pamoja na majigambo yote yaliyotangulia...

Mkandara,
Umenichekesha sana hapo unaposema njaa ni adui mkubwa wa umasikini. Probably jamaa ilikuwa kweli akiingia ndani ya 18 ya pesa hafanyi makosa lazima apige bao hata kama ni la Maradona?!

Kimsingi pia ninakubaliana na wewe kuwa jamaa huenda alikuwa na matatizo mazito zaidi. Kwa mfano sidhani kama ni sahihi kumwambia mwenyekiti wake kuwa Mimi Lwakatare nilifanya jinsi kadhaa na ndiyo maana leo wewe ni mwenyekiti, inaonesha kuwa jamaa pia amekuwa na dharau au kiburi ambacho kimekuwa ni kikwazo ndani ya chama. isitoshe CUF bara haifanyi vizuri hilo linatosha kabisa kumpa nafasi mtu mwingine aweze kuchukua nafasi yake na kuleya mawazo masokumo mpya. Ninakataa katakata pale anapojisifia kuwa yeye bado ni kiongozi bora bila ya kuwaachia watu wamjaji. Pia nimepata jibu la kwani alioganaizi mapokezi pale Bukoba siku alipokuwa anatoka Dar es Salaam. Inawezekana amedhoofisha chama CUF kwa kujijenga yeye mwenyewe kwa malengo binafsi - kutafuta Ubunge tu.
 
.....Lwakatare aliitisha mkutano huu ili kueleza wanachama wa CUF na wapenzi wake kisiasa nini kimetokea na kumlazimisha ajiuzulu uongozi wote ndani ya CUF....

...... Umati mkubwa sana uliokuwa umehudhuria ni watu wawili tu walionyoosha mkono kwamba aendelee kubakia CUF na wengine wote ......wanataka ahamie Chadema.

Hivi ndo stori uliyopata kwa source wako wa uhakika inavyosema,sasa hawa "wengine wote", wamo pia wa hivyo vyama 3 vikuu, ambao na wao wamenyoosha mikono yao kumtaka ahamie CHADEMA, wanachama wa SISI EMU walikuwapo na wao pia walimtaka ahamie CHADEMA? hii vp Mkuu...
 
Suala la Lwakatare kupokelewa kwa shangwe, kuhutubia umati na kupewa maelekezo na wananchi akachambua na kufuata siyo habari kabisaaaa. Wao wanasema "Nosindika Atandamile" (Ni sawa na kumsukuma aliyechuchumaa) Siyo kama namkandia Mchukia Fisadi bali nawaweka sawa wasioijua Bukoba na mapenzi ya wanaBK kwa Entare, Lwakeupe, Lwaks, famously known as Lwakatare.

Wakati wengine wanajiua kwa Arsenal kufungwa na manchester, BK alijiua mtu eti kisa Kagasheki katangazwa mshindi. Huyu hata Lwaks mwenyewe hakumjua kwa sura. Visa vya kisiasa vimedudu miaka mitatu sasa utafikiri uchaguzi ni kesho. Harusi na misiba ya watu wa CUF imekuwa kama ni misiba ya kichama. Ujio wa Lwaks Bk siku zote imekuwa kama ujio wa mkombozi.

Asante mkuu kwa kuwa wazi zaidi.
Wengi hapa hawapajui Bukoba vizuri. Wakati fulani nilikuwa napaita Pemba ya Bara:D
Lakini hapa hakipendwi Chama, anapendwa mtu:cool:
 
Hivi ndo stori uliyopata kwa source wako wa uhakika inavyosema,sasa hawa "wengine wote", wamo pia wa hivyo vyama 3 vikuu, ambao na wao wamenyoosha mikono yao kumtaka ahamie CHADEMA, wanachama wa SISI EMU walikuwapo na wao pia walimtaka ahamie CHADEMA? hii vp Mkuu...
Bila shaka ndivyo ilivyokuwa mkuu junius.
Kwani hujui wanaokuchagua kuwa mwakilishi wao si wote wale wa chama chako? FYI hata wasiojua vyama ni nini pamoja na wengine kutoka katika vyama pinzani na wewe, wanaweza kukupatia kura wewe Kwani hujui hili?
 
Bukoba hakipendwi chama, anapendwa mtu! Lwakatare ni bomu linaloelekezwa kuimaliza CHADEMA. Nikiwa mwanachama wa CHADEMA, nimeshuhudia ujio wa Guninita, Akwilombe, Chacha Wangwe na wengine ambao hatima yao tunaijua. Nimewahi pia kuwepo kwenye mmoja kati ya mikutano ya op. Sangara na kushuhudia wananchi maskini kabisa walivyoitikia wito wa viongozi wa chama kutoa michango ili kufanikisha ziara za operation hiyo. Wametoa michango ya sh 500/=, 1,000/= nk kila mtu kwa uwezo wake, huwezi amini kiasi kilichopatikana. Hawa ndio aina ya wanachama wanaohitajiwa na vyama vyetu hivi.
Huyu Lwakatare miongoni mwa sababu zinazomtoa CUF ni chama kushindwa kumlipa mafao na kushindwa kumlipia gharama za kesi yake. Kama kuna kiongozi wa CHADEMA ambaye yuko radhi kutoa pesa yake mfukoni kum-bail huyu Lwakatare, sina ugomvi. Lakini ikitumika hela ya chama inayotokana na ruzuku na michango ya wanachama maskini hawa wasio hata na uhakika wa mlo wa siku, I'll be the first member to raise hell.
Kuna member hapa JF anayejitambulisha kama Omutwale, ninayo kila sababu ya kuamini kuwa yuko karibu sana na Lwakatare. Kuna post moja kaandika kuwa ameongea na Lwakatare jinsi baadhi ya viongozi walivyojisajili kwa majina yao halisi lakini baadaye wakaishia kwa majina mengine na kumtaja mmoja kama Mr Dowans. Huyu ni kiongozi anayetaka mchango wake CUF utambuliwe kwa kuwa amekuwa huko tangu chama kikiwa CCW lakini anasahau kuwa huyu anayemkebehi kuwa ni Mr Dowans amechangia kwa kiasi kikubwa chama kinachonyemelewa hadi kukifikisha hapa kilipo. Zito amewahi kuandika kuwa kwa Kigoma CHADEMA ni zaidi ya chama. Wameondoka kina Kabourou lakini CHADEMA bado inapeta. Huko Tarime kuna watu walidhani wakimnunua Wangwe na hatimaye kuondoa uhai wake chama kingekufa, lakini chama ndio kwanza kinashamiri.
Nafahamu kuwa viongozi wengi wa CHADEMA ni members hapa. Jengeni chama huko Bukoba kama taasisi na si kutaka kubebwa mgongoni kwa Lwakatare. Mkishindwa kutimiza matakwa yake atawabwaga chini huyu.
 
Bukoba hakipendwi chama, anapendwa mtu! Lwakatare ni bomu linaloelekezwa kuimaliza CHADEMA. Nikiwa mwanachama wa CHADEMA, nimeshuhudia ujio wa Guninita, Akwilombe, Chacha Wangwe na wengine ambao hatima yao tunaijua. Nimewahi pia kuwepo kwenye mmoja kati ya mikutano ya op. Sangara na kushuhudia wananchi maskini kabisa walivyoitikia wito wa viongozi wa chama kutoa michango ili kufanikisha ziara za operation hiyo. Wametoa michango ya sh 500/=, 1,000/= nk kila mtu kwa uwezo wake, huwezi amini kiasi kilichopatikana. Hawa ndio aina ya wanachama wanaohitajiwa na vyama vyetu hivi.
Huyu Lwakatare miongoni mwa sababu zinazomtoa CUF ni chama kushindwa kumlipa mafao na kushindwa kumlipia gharama za kesi yake. Kama kuna kiongozi wa CHADEMA ambaye yuko radhi kutoa pesa yake mfukoni kum-bail huyu Lwakatare, sina ugomvi. Lakini ikitumika hela ya chama inayotokana na ruzuku na michango ya wanachama maskini hawa wasio hata na uhakika wa mlo wa siku, I'll be the first member to raise hell.
Kuna member hapa JF anayejitambulisha kama Omutwale, ninayo kila sababu ya kuamini kuwa yuko karibu sana na Lwakatare. Kuna post moja kaandika kuwa ameongea na Lwakatare jinsi baadhi ya viongozi walivyojisajili kwa majina yao halisi lakini baadaye wakaishia kwa majina mengine na kumtaja mmoja kama Mr Dowans. Huyu ni kiongozi anayetaka mchango wake CUF utambuliwe kwa kuwa amekuwa huko tangu chama kikiwa CCW lakini anasahau kuwa huyu anayemkebehi kuwa ni Mr Dowans amechangia kwa kiasi kikubwa chama kinachonyemelewa hadi kukifikisha hapa kilipo. Zito amewahi kuandika kuwa kwa Kigoma CHADEMA ni zaidi ya chama. Wameondoka kina Kabourou lakini CHADEMA bado inapeta. Huko Tarime kuna watu walidhani wakimnunua Wangwe na hatimaye kuondoa uhai wake chama kingekufa, lakini chama ndio kwanza kinashamiri.
Nafahamu kuwa viongozi wengi wa CHADEMA ni members hapa. Jengeni chama huko Bukoba kama taasisi na si kutaka kubebwa mgongoni kwa Lwakatare. Mkishindwa kutimiza matakwa yake atawabwaga chini huyu.

Gag,

Itabidi wamtumie kama alivyo. Karibu CHADEMA Lwaks. Hope Chadema works a team.
 
duh! hii habari ilivokaa,yaani sijazowea kwenye JF kuona habari imekaa kama hivi.. duh! yaani bora itowe halafu utunge vyengine angalau ikae uzuri..
 
Soma vizuri habari hiyo tena. Ondoa hapa uzushi wa kitu ambacho sikukiandika.

*Hakuna nilikoandika kuwa mkutano ulihudhuriwa na wana kafu peke yao.
*Wala sikusema wale wawili walionyoosha mkono against kafu walikuwa wana kafu.

Kama wewe una data za hakika weka thread yako usilete upotoshaji hapa. Hizi habari nimezipata kutoka kwenye zaidi ya source tatu kule Bukoba.


Mkuu, heshima mbele!!
Habari ya upotoshaji haipo hapa, ninachohoji ni uhalali wa Lwakatare kuitisha mkutano, ni lazima aliitisha kama kiongozi wa CUF, na kwa mantiki hiyo wahudhuriaji wengi wanaweza kuwa ni wanaCUF (siyo lazima imaanishe wote). Huna haja ya kutake personal hii issue, nilikuwa nahoji idadi kuwa ya wanCUF kumwambia ahamie Chadema, labda kama na wao walishahama CUF au wako mbioni kumfuata mtu wao Chadema.
Thread uliyoianzisha ndiyo inafaa kujadiliwa, usikimbilie kuniambia nianzishe thread, ukiwa na lengo la kukwepa maswali. Jifunze uvumilivu wa kukubali kuhojiwa kwa kile ulichosema, si lazima kiwe katika mwono na mtazamo wako.
 
Mimi naijua full story ya lwakatare.Alikuwa mpiga debe wa hali ya juu CUF,mwaka 2000 lipumba akamteua kuwa naibu katibu mkuu bara na baraza kuu la uongozi la chama chake likampitisha,then baada ya uchaguzi wa ndani ya chama wa CUF wa mwaka 2004 Lipumba aliposhinda alimteua kuwa naibu katibu mkuu tena.

Mwaka 2005 nyote mnakumbuka Chama chake kilipigana naye bukoba mjini lakini wakashindwa kwa balozi kagasheki(kagasheki alimshinda lwakatare kwa kura 130 tu)Baada ya kushindwa alifungua kesi ya kupinga matokeo hayo,yeye lwakatare ndiye aliyeongoza chama chake CUF katika chaguzi ndogo kadhaa za tunduru,mbeya vijijini na kwingineko(isipokuwa busanda).

Mwaka jana 2008 alikuwa kwenye mgogoro mkubwa na viongozi wake wa juu baada ya kutumia tshs 30,000,000(milioni thelathini) vibaya (alipewa pesa hizo akasimamie zoezi la daftari la wapiga kura kwa muda wa mwezi mzima) lakini akawashangaza wakubwa pale aliporudi baada ya wiki moja na kudai pesa zote zimekwisha huku ushahidi wa maafisa wa ngazi za chini alioenda nao ukionesha pesa zilizotumika kwa hiyo wiki moja hazizidi hata 5,000,000(milioni tano).Hiyo haikuwa mara ya kwanza,inasemekana huko nyuma alikuwa na rekodi chafu ya matumizi ya pesa ndani ya chama chake.

Inasemekana wakubwa walitaka kumuondoa mara moja lakini wakaona itaharibu sura ya chama chao,wakalimezea suala hilo na kukaa kimya kwani walijua bado miezi sita tu uchaguzi mkuu mwingine wa ndani ya chama ufanyike na walikuwa wakimtegea hapo.Uchaguzi mkuu wa chama cha CUF uliofanyika mwezi march mwaka huu ndio uliwaleta tena madarakani lipumba,machano na seif sharif na ndipo wakamtema lwakatare.

Inasemekana katika mkutano huo mkuu wa chama lwakatare alichaguliwa tena kuwa mjumbe wa baraza kuu la uongozi la taifa la chama hicho na tena alikuwa ana matumaini makubwa kwamba lazima atateuliwa kuwa naibu katibu mkuu kwani inasemekana aliwahi hata kutamka kwamba bila yeye tanzania bara chama hakipo.Siku ya uteuzi wa wakurugenzi na manaibu katibu wakuu wa zanzibar na tanzania bara ilikuwa siku moja baada ya mkutano mkuu wa chama.

Wajumbe wapya wa baraza walikutana ili kupokea uteuzi na kuukataa au kuukubali na mmoja wa wajumbe hawa alikuwa lwakatare huku akiwa anaamini kwa asilimia 100 kwamba lazima atateuliwa kuwa naibu katibu mkuu.Inasemekana alipata mshtuko mkubwa pale ambapo yalitajwa majina mawili kwa upande wa bara huku lake likiwa halimo na ndipo wajumbe wa baraza wote wakampigia kura JORAM BASHANGE.

Kutokana na mshtuko alioupata lwakatare palepale hakuchelewa alisimama na kutamka kikaoni hapo kwamba yeye anapinga uteuzi wa JORAM BASHANGE,alipoulizwa sababu ya kupinga akawa hana,na ndio kutokea hapo ikawa haieleweki;akaanza kuwaponda CUF na LIPUMBA na wengineo kwamba hawafai na wamekipeleka chama hicho kubaya.

Ikumbukwe kwamba lwakatare alikuwa anaongoza mambo yote ya utendaji wa chama na mikakati upande wa bara,na amekuwa katika kuongoza utendaji wa chama chake kwa miaka 10,iweje leo hii asipewe nafasi ya juu ndo anaanza kusema chama kimepoteza mwelekeo?

Nashauri ma-thinker wote walitizame suala hili vizuri bila ushabiki,iweje mtu anyimwe nafasi ya juu ndo anaona chama kibaya na waliomo hawafai?
Hivi tuseme leo hi lwakatare angekuwa ameendelea kuachiwa nafasi ya naibu katibu mkuu angetangaza kukihama chama chake?
Hivi leo hii mtu akinyimwa nafasi mahali ndio anahama? Viongozi wa namna hii sio wazuri hata kidogo.

Mimi nadhani ni yeye ndiye anajimaliza,ninamaanisha lwakatare anajimaliza mwenyewe- sote tunachojua ni kwamba anahitaji kulirudisha jimbo la bukoba vijijini mikononi mwake tena anakiri kwamba jimbo lile ni lake kwani alinyang'anywa na ccm mwaka 2005,if that is the case alihitaji kutulia ndani ya cuf na kuimarisha mtandao wake ili apate madaraka aliyokuwa anayahitaji.

Kwa kuhama kutoka cuf it means anaanza upya na chadema na najua ha taweza kuondoka na hata nusu ya wafuasi wa cuf bukoba mjini na hiyo itam-cost kwenye uchaguzi ujao kwani atamrahisishia kazi kagasheki iwapo cuf watamsimamisha mgombea mwingine anayekubalika.

Lakini pia napata bad news sasa hivi kwamba imebainika baadhi ya wabunge wetu wa CHADEMA wanachangishana ili kumuongezea nguvu lwakatare huko na tena jana usiku kulikuwa na kikao kati ya madiwani wa CUF walioko bukoba vs Lwakatare na viongozi wa chadema na madiwani wale wameahidiwa kupewa pesa za kampeni za uchaguzi mkuu ujao iwapo watang'oka CUF na kujiunga CHADEMA.

Habari hizi ni za uhakika na hivi ndio vyama vyetu vya upinzani.
 
Wadau JF.
Nimekuwa nikijiuliza swali hili, siku nyingi baada ya sakataka la Lwakatare kuanza ndani ya CUF.

Nawauliza CHADEMA ambao wakati fulani niliwaona majasiri jinsi walivyosimama kidete kudhibiti hali ya mchafu koge ndani ya chama chao iliyokuwa ikichochewa kwa mbaali na mashushu na mamluki wa CHAMA TAWALA,wakisaidiwa na usalama wa taifa,kwa wao CHADEMA kujua au bila kujua, hapa nazungumzia sakata la Marehemu Chacha Wangwe.
Leo katika mazingira kama hayo CUF wanakumbana na hali hiyo au kama hiyo.

Kiufupi tu, imekuwa ikiripotiwa katika vyombo na mitandao mbalimbali ya habari huko Tanzania kuhusu hatua ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Mh.W.Lwakatare ya kwanza kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi ndani ya chama na pili tetesi zinazodai kuwa yupo mbioni kujiunga na chama chengine cha upinzani, chadema.

Swali langu ndo linakuja hapa kuwa, ukizingatia sababu za Lwakatare kusuguana na viongozi wake mpaka akaamua kuachia ngazi,je huko anakotaka kwenda, wenyeji wake wanakitu gani wamemtayarishia Lwakatare ambacho amekikosa alipokuwa CUF na anamatarajio ya kukipata huko?

Chadema wasisahau kuwa,hakuna asiyejuwa kuwa sababu kubwa ya Lwakatare kununa na kuchukua hatua anayochukua hivi sasa ni "vita ya Madaraka".

Ingawa vyombo vya habari vimenukuu sababu tofauti anazodai Lwakatare kuwa ndizo zimemfanya aamue kuachia ngazi CUF, lakini hakuna hata moja kati ya hizo yenye kuingia akilini, Lwakatare aliwahi kuripotiwa akidai kuwa sababu ya kuachia ngazi ni kitendo cha Mwenyekiti wa CUF, Prof.Lipumba cha kuwatimua akina Kuchilingulo, Mmari na Wandwi kwa madai ya kukihujumu chama katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Busanda.

Wakati huo huo amenukuliwa na vyombo mbalimbli vya habari akidai kuwa sababu kubwa ya kuachia ngazi ndani ya chama na kufikiria asiendelee na chama cha CUF ni kutokana na jina lake kuachwa kwenye uteuzi wa kutetea nafasi yake kwasbabu za kifitna na majungu yaliyojaa ndani ya CUF. Amenukuliwa akiwashutumu Juma Duni na Bi. Ashura Mustafa kuwa ndio wanaompakazia na kueneza fitna hizo.
Chochote na kisemwe na aseme Lwakatare ni uhuru wake, laikini awaambie watu ukweli kuwa kuishi bila ya wadhifa kama aliowahi kuwa nao katika chama cha CUF ni ngumu kwake, vilivyobakia ni visingizio tu.

Katika hali kama hiyo ndo nikapata swali la kujiuliza chadema watampa nini Lwakatare? Nikakumbuka ile kadhia nduchu ya Hiza Tambwe katika staili kama hiyo ya Lwakatare, akahama na kukimbilia CCM ambako alipewa anachokitaka. CHADEMA MTAMPA NINI LWAKATARE?
 
Mimi naijua full story ya lwakatare.Alikuwa mpiga debe wa hali ya juu CUF,mwaka 2000 lipumba akamteua kuwa naibu katibu mkuu bara na baraza kuu la uongozi la chama chake likampitisha,then baada ya uchaguzi wa ndani ya chama wa CUF wa mwaka 2004 Lipumba aliposhinda alimteua kuwa naibu katibu mkuu tena.

Mwaka 2005 nyote mnakumbuka Chama chake kilipigana naye bukoba mjini lakini wakashindwa kwa balozi kagasheki(kagasheki alimshinda lwakatare kwa kura 130 tu)Baada ya kushindwa alifungua kesi ya kupinga matokeo hayo,yeye lwakatare ndiye aliyeongoza chama chake CUF katika chaguzi ndogo kadhaa za tunduru,mbeya vijijini na kwingineko(isipokuwa busanda).

Mwaka jana 2008 alikuwa kwenye mgogoro mkubwa na viongozi wake wa juu baada ya kutumia tshs 30,000,000(milioni thelathini) vibaya (alipewa pesa hizo akasimamie zoezi la daftari la wapiga kura kwa muda wa mwezi mzima) lakini akawashangaza wakubwa pale aliporudi baada ya wiki moja na kudai pesa zote zimekwisha huku ushahidi wa maafisa wa ngazi za chini alioenda nao ukionesha pesa zilizotumika kwa hiyo wiki moja hazizidi hata 5,000,000(milioni tano).Hiyo haikuwa mara ya kwanza,inasemekana huko nyuma alikuwa na rekodi chafu ya matumizi ya pesa ndani ya chama chake.

Inasemekana wakubwa walitaka kumuondoa mara moja lakini wakaona itaharibu sura ya chama chao,wakalimezea suala hilo na kukaa kimya kwani walijua bado miezi sita tu uchaguzi mkuu mwingine wa ndani ya chama ufanyike na walikuwa wakimtegea hapo.Uchaguzi mkuu wa chama cha CUF uliofanyika mwezi march mwaka huu ndio uliwaleta tena madarakani lipumba,machano na seif sharif na ndipo wakamtema lwakatare.

Inasemekana katika mkutano huo mkuu wa chama lwakatare alichaguliwa tena kuwa mjumbe wa baraza kuu la uongozi la taifa la chama hicho na tena alikuwa ana matumaini makubwa kwamba lazima atateuliwa kuwa naibu katibu mkuu kwani inasemekana aliwahi hata kutamka kwamba bila yeye tanzania bara chama hakipo.Siku ya uteuzi wa wakurugenzi na manaibu katibu wakuu wa zanzibar na tanzania bara ilikuwa siku moja baada ya mkutano mkuu wa chama.

Wajumbe wapya wa baraza walikutana ili kupokea uteuzi na kuukataa au kuukubali na mmoja wa wajumbe hawa alikuwa lwakatare huku akiwa anaamini kwa asilimia 100 kwamba lazima atateuliwa kuwa naibu katibu mkuu.Inasemekana alipata mshtuko mkubwa pale ambapo yalitajwa majina mawili kwa upande wa bara huku lake likiwa halimo na ndipo wajumbe wa baraza wote wakampigia kura JORAM BASHANGE.

Kutokana na mshtuko alioupata lwakatare palepale hakuchelewa alisimama na kutamka kikaoni hapo kwamba yeye anapinga uteuzi wa JORAM BASHANGE,alipoulizwa sababu ya kupinga akawa hana,na ndio kutokea hapo ikawa haieleweki;akaanza kuwaponda CUF na LIPUMBA na wengineo kwamba hawafai na wamekipeleka chama hicho kubaya.

Ikumbukwe kwamba lwakatare alikuwa anaongoza mambo yote ya utendaji wa chama na mikakati upande wa bara,na amekuwa katika kuongoza utendaji wa chama chake kwa miaka 10,iweje leo hii asipewe nafasi ya juu ndo anaanza kusema chama kimepoteza mwelekeo?

Nashauri ma-thinker wote walitizame suala hili vizuri bila ushabiki,iweje mtu anyimwe nafasi ya juu ndo anaona chama kibaya na waliomo hawafai?
Hivi tuseme leo hi lwakatare angekuwa ameendelea kuachiwa nafasi ya naibu katibu mkuu angetangaza kukihama chama chake?
Hivi leo hii mtu akinyimwa nafasi mahali ndio anahama? Viongozi wa namna hii sio wazuri hata kidogo.

Mimi nadhani ni yeye ndiye anajimaliza,ninamaanisha lwakatare anajimaliza mwenyewe- sote tunachojua ni kwamba anahitaji kulirudisha jimbo la bukoba vijijini mikononi mwake tena anakiri kwamba jimbo lile ni lake kwani alinyang'anywa na ccm mwaka 2005,if that is the case alihitaji kutulia ndani ya cuf na kuimarisha mtandao wake ili apate madaraka aliyokuwa anayahitaji.

Kwa kuhama kutoka cuf it means anaanza upya na chadema na najua ha taweza kuondoka na hata nusu ya wafuasi wa cuf bukoba mjini na hiyo itam-cost kwenye uchaguzi ujao kwani atamrahisishia kazi kagasheki iwapo cuf watamsimamisha mgombea mwingine anayekubalika.

Lakini pia napata bad news sasa hivi kwamba imebainika baadhi ya wabunge wetu wa CHADEMA wanachangishana ili kumuongezea nguvu lwakatare huko na tena jana usiku kulikuwa na kikao kati ya madiwani wa CUF walioko bukoba vs Lwakatare na viongozi wa chadema na madiwani wale wameahidiwa kupewa pesa za kampeni za uchaguzi mkuu ujao iwapo watang'oka CUF na kujiunga CHADEMA.

Habari hizi ni za uhakika na hivi ndio vyama vyetu vya upinzani.

Lakini hata SLA alitoka ccm baada ya kunyimwa nafasi lakini bado ni mzuri tu.
Lwaka japo alichohoji ni kwanini sababu ya ubadhilifu wa fedha haikuwekwe bayana na kwanini izungumuziwe pembeni?? kwa hihi sababu tu wengi tungeliangalia namna ya kuondoka chamani.
 
Ranmarwa,
Mkuu hii inaonekana kama hadithi simulizi zaidi ya Ukweli maanake kila naposoma kuna majungu, visokorokwinyo na kadhalika..
Hawa viongozi wa CUF kama kweli Lwakatare alipewa millioni30/ na akatumia Millioni 5 tu iweje washindwe kumuuliza/kumwajibisha ila wammezee ati wamsubiri ktk uchaguzi!.. hao viongozi wa CUF walitegemea kuwaeleza nini wananchi ikiwa millioni 30 zimetumika vibaya na sii fedha toka mifukoni mwao..hizo millioni 25 pungufu zimehesabika vipi ktk vitabu vya chama ikiwa Lwakatare ataondoka chama kabla ya kutakiwa kujieleza..

Kisha unasema ati Lwakatare aliulizwa sababu ya kupinga jina la Joram akashindwa kujibu.. Mkuu tafadhali, Lwakatare alikuwa naibu Katibu mkuu iweje ashindwe kujibu ikiwa jina lake limeenguliwa wakati viongozi wengine wote majina yao yalirudi! Na wala sioni sababu ya kuulizwa swali hilo ikiwa hao viongozi wa CUF wameliondoa jina la Lwakatare bila kumweleza yeye sababu.. Kwa nini wao watake kujua sababu ya kupinga ikiwa kahupewa sababu ya kutolewa...maamuzi yao hayakuwa na maelezo..

Kifupi ni hivi CUF wamechoka Lwakatare na sababu zipo nje kabisa ya matumizi mabaya ya fedha kwani kama ingekuwa hivyo basi wanachama wa CUF wangeisha pewa hesabu hizo na matumizi hayo mabaya.. Na nakuhakikishia sii Lipumba wala Seif wanaweza ku raise hii issue kwa sababu hawa wote ni Opportunist nina hakika wametumia fedha vibaya kuliko huyo Lwakatare..Opportunist mwninge..
Kifupi wanasiasa wengi Bongo kama sii wote ni Opportunist, hawakuingia siasa bila kutegemea malipo bora na ujanja ujanja laa sivyo wangekuwa wakiachia nafasi hizo baada ya awamu mbili za kushindwa ama kuweka ushindani wa kweli within vyama hivyo.
Mara zote utakuta nafasi ya Mwenyekiti wanagombea Lipumba vs Mkandara asiyejulikana kabisa wala uanachama wake.
Makamu mwenyekiti, Sief against Mkandara!
sijui kiti cha nini Duni against Mkandara..basi ili mradi kurudi kwao madarakani ni LAZIMA..
 
Kama ripoti ni accurate (sadly I find myself prefacing most of my positions with that phrase, due to the obvious unreliability of our "press") huyu jamaa si kiongozi, ni mzugaji tu.


Safi kabisa...... Huyu jamaa ni mbabaishaji, huwezi uliza watu swali kama hilo kama kweli ni kiongozi thabiti; he is just desperate to be mbunge again... at any cost!!!
 
Back
Top Bottom