Lwaitama: Kwenye maslahi ya nchi, adui yetu ni CCM

Zitto anayapokea maneno haya kwa sikio la kushoto halafu yanatokea sikio la kulia. Huwa haelewi kabisa.
ZITTO ni mnufaika kwa Raslimali za TAIFA ndio maana alitoka kwenye Chama halisi cha UPINZANI na kwenda kwenye Ccm B Chama kilichoanzishwa na Ccm
 
Ukabila na undugunization upo CCM.
Hebu elezea ukabila wa CDM au Mbowe
Leta safu ya ungozi wa chadema ndio utajua ukabila wa huyu mwamba ni wa kiwango cha kutisha,amejaribu saana kumpaisha yule mvuta bangi wa Arusha sio kwamba ana uwezo bali ni kwa kuwa ni binamu yake
 
ZITTO ni mnufaika kwa Raslimali za TAIFA ndio maana alitoka kwenye Chama halisi cha UPINZANI na kwenda kwenye Ccm B Chama kilichoanzishwa na Ccm
Acha kujitoa ufahamu aisee,umesahau kuwa cdm ndio ilibeba mwanchama wa ccm hadi akagombea urais wa nchi hii?
 
Zitto anayapokea maneno haya kwa sikio la kushoto halafu yanatokea sikio la kulia. Huwa haelewi kabisa.

Kwanini tusiwe na mawazo +ve tu kama Prof. Lwaitama? Kulikoni kufikiria -vely tu? Watu huwa hawabadiliki?

Tusiwe na uadui wa kudumu, tuyang'oe ma CCM kwanza. Ndiyo ulio msingi wa hoja kuntu kabisa yake Prof. Lwaitama.
 
Muungano wa vyama hautawezekana hadi pale wananchi watakapshtuka kuwa mdudue cdm si chama cha siasa bali ni kampuni binafsi inayotumia mgongo wa ccm kwa ajili ya faida ya wanahisa ambao ni mzee Mbowe na Baba mkwe wake.

Sentensi ya mwanzo kabisa kwenye mada pale inakuhusu sana ndugu:

"Ukweli mchungu kwa ma CCM na vibaraka wao."
 
Ukweli mchungu kwa ma CCM na vibaraka wao:

View attachment 2926733

ā€œMukitaka kufika mbali lazima muwe na sauti ya pamoja hata kama munatofautiana kwa itikadi ya vyama vyenu lakini linapokuja suala la kutetea maslahi ya nchi lazima mushikamane, hamuwezi kuondoa chama kilicho madarakani kwa kujitenga." Amesema Lwaitama.

Tupambanao dhidi ya CCM, letu ni moja. Tunapaswa kuwa wamoja.

"Zimwi likujualo hali kuli likakwisha."

Prof. Lwaitama, muumini wa mfano wa dhana ya jamili ya kutokuwa na maadui au marafiki wa kudumu katika siasa.
Hahaha... Ila kweli
 
ZITTO ni mnufaika kwa Raslimali za TAIFA ndio maana alitoka kwenye Chama halisi cha UPINZANI na kwenda kwenye Ccm B Chama kilichoanzishwa na Ccm

Prof. Lwaitama kayasema akiwa katupia jezi ya ACT.

Kumtoa CCM yataka kuwiva sana na kuweza kuona mbele zaidi ya mawazo ya kuendekeza uadui.
 
Acha kujitoa ufahamu aisee,umesahau kuwa cdm ndio ilibeba mwanchama wa ccm hadi akagombea urais wa nchi hii?

Tunatambua kuwa umoja wetu ni mwiba mchungu mno kwa CCM na vibaraka wao.

Agenda yetu dhidi ya CCM inapaswa kuwa thabiti yenye kuwahusisha hata walioko CCM ndani huko, sembuse waliowahi kuja?
 
Mbona Zitto amekuwa adui wa misukule yote ya chadema

Hayo ni mawazo yako. Usisahau Prof. Lwaitama ni:

"Mjumbe wa bodi ya wadhamini wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). "
 
Back
Top Bottom