Kuvilaumu vyama vya siasa ilihali havina vyanzo vya fedha kuleta maendeleo ni kosa kubwa sana.
Na kukilaumu chama tawala ilihali hakina ofisi kwenye serikali kuu nalo ni kosa kubwa sana.
Wa kulaumiwa ni watendaji walioaminiwa na kuteuliwa na jamhuri na wao kwa ridhaa yao uwatunuku ndugu zao,jamaa zao na wazazi wao kwenye nafasi nyeti ilihali hawana sifa na uwezo wowote kiutendaji,ni wababaishaji,wabishi,wenye vibuli na dhalau kwa kuzani kuwa wao ndio serikali.
Watumishi wa namna hii hawafai na ndio hao hao wanaokwamisha mipango mingi ya maendeleo ya ujumla kwa watu.
Ni wajibu wetu kuwabaini na ikiwezekana tuiombe serikali ifanye haraka operation maalum ya kuhakiki watumishi wake
kuanzia taaluma zao,uwezo wao wa kuzalisha/tija na uwajibikaji wao kwa wananchi.
Wengi wa watumishi wa umma wanafurahi sana pindi lawama zao zinapotupwa ndani ya chama tawala na mbaya zaidi ndani ya chama tawala hicho mwenye mamlaka juu yao ni Rais pekee (Mteuzi mkuu wa nafasi nyeti za nchi).
Katika hili ni vema tukabadili fikra juu ya nani alaumiwe kwani si chama kinachopelekewa fedha za maendeleo bali watendaji wa serikali ambao hawatekelezi wajibu wao ipasavyo na muda mwingi wao ni kuwaza kula,kunywa na kuvaa vizuri tu.
Kama mnabisha jaribuni kutembelea walau ofisi za chama tawala za matawi muone walivyo choka na wengi wao maisha yao ni ya kuungaunga na kuombaomba kwenye ofisi za umma/serikali.