Lusinde: Serikali isifikirie adui ni CHADEMA, ni watendaji!

Lusinde: Serikali isifikirie adui ni CHADEMA, ni watendaji!

agatony8l

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2010
Posts
453
Reaction score
103
Duu kumbe huyu jamaa wakati mwingine aliweka kando itikadi za kisiasa huwa anaongea point.

Kasema - Mawaziri WABUNGE wakitembelea vijiji wapewe maji wanavyokunywa wanakijiji ili wajue shida ya maji vijijini.

Pia kasema CHADEMA sio adui, maadui ni watendaji wa Serikali.

Pia kaponda uchimbaji wa visima kwa gharama kubwa. Kashangaa ilikuwaje Serikali ya Nyerere iliweza kujenga mabwawa na Serikali hii imeshindwa.

Kkamalizia kwa kutounga mkono hoja
 
ameongea akiwa anaota au?????sasa alikua wapi kuyasema hayo siku zote,,au amenong'onezwa kuwa 2015 c mbali
 
Haaminiki huyo muda wowote anaweza kuharibu kauli.!!
 
Wamegundua kuwa anguko lao linakuja kubwa sana, inabidi wabembeleze hruruma ya CDM
 
wagonjwa ndivyo walivyo ngoja kimpande ndo utamjua vizuri!!!!
 
Leo mchana nimebahatika kumsikia Mh, saana Job Lusinde, akichangia hoja Bungeni kuhusu swala la Maji!

Alisema kwamba swala la Maji ni swala nyeti sana na si la Kisiasa kama ambavyo inachukuliwa!
Aliendelea kusema kwamba kama Wabunge wataendelea kumbana sana Profesa na Dokta, [Nadhani alimaanisha Waziri wa Maji na Naibu wake] itakua sio sahihi!

Japo alisema swala la Maji tusifanye Siasa, hapo hapo akajisahau na kuchomekea eti kua kama swala ni Uprofesa na Udokta, mbona tunao Profesa na Dokta waliogombea Urais mara nyingi na wameshindwa!!

Point ya mwisho aliyoiongea alisema kwamba swala la Maji Waziri ahakikishe wanalishugilikia kwa ukamilifu na kwamba Serikali inaweza ikadhani Adui yake ni CHADEMA, kumbe sio ila Adui ni Matatizo yanayowakabili wananchi!
Baada ya kuongea mambo mengi sana alimalizia kwa kusema Haungi Hoja Mkono!

Huyo ndio Lusinde Mbunge Kijana na Msomi kutoka Jimbo la Mtera!!
 
Mheshimiwa.

Salaam.

Umechangia vizuri sana leo. Umeonekana kama mheshimiwa hasa na umependeza sana kuitwa mheshimiwa leo. Siku nyingine unakuwaje?

Umechangia vizuri sana. Kwa maneno mazuri, matamu na yenye ukweli kabisa.

Umesema vizuri kuwa kana maji yakitoka mwakani wenzenu yaani Chadema bila bila shaka watasema ni kwa ajili ya kampeni. Ni kweli. Lakini kwa nini umetumia neno "wenzetu" badala ya maneno yako yale machafu ya zamani? Bila shaka umekuwa mtu mzima sana na uheshimiwa unakustahili.

Mwisho. Hivi ni kwa nini hukuogopa kusema kwa ujasiri kuwa huungi mkono hoja? Ujasiri huu umeutoa wapi? Wewe ambaye mwanzoni ulionekana kama bendera fuata upepo? Bila shaka umetambua ukweli kuwa huwi mpinzani kwa ajili ya kusema ukweli. Utakuwa mkweli hata ukiwa ni muumini wa CCM.

Kwa kweli leo umenifirahisha sana leo na mimi NAKUUNGA MKONO.

Hongera Mheshimiwa wetu. 2015 ni wetu.
 
Duu kumbe huyu jamaa wakati mwingine aliweka kando itikadi za kisiasa huwa anaongea point.

Kasema - Mawaziri WABUNGE wakitembelea vijiji wapewe maji wanavyokunywa wanakijiji ili wajue shida ya maji vijijini.

Pia kasema CHADEMA sio adui, maadui ni watendaji wa Serikali.

Pia kaponda uchimbaji wa visima kwa gharama kubwa. Kashangaa ilikuwaje Serikali ya Nyerere iliweza kujenga mabwawa na Serikali hii imeshindwa.

Kkamalizia kwa kutounga mkono hoja

Atafuta kauli muda si mrefu.
 
kuna badhi yao wana akili, isipokuwa wanakuwa hawajaelemika, viva chadema kwa kazi nzuri, wote waliopotea tutawarudisha kwenye mstari. hiyo pia inatokana na moto uliowashwa na chadema huko mikoani na mwitikio wa wananchi kuwaunga mkono.
 
These guys they have realized that matusi yao yanaijenga Chadema na hasa baada ya matusi ya last week wamejua mwelekeo wa Watanzania si kama walivyo dhani .Sasa wanaanza kurudia akili zao .
 
Au amenukuliwa vibaya? Siamini kama anaweza kuwapa complement chadema.
 
Nadhani ni mwezi mzuri tu, vinginevyo ametishwa jimboni kwake kwamba ukikisema vibaya CHADEMA hatutakuchagua tena.
 
Labda wazee wa Chama Chetu Sikivu wamemuweka chini na kumfunda kwamba lugha chafu zinamuharibia.Ngoja tuone kama mwalimu wake amefanikiwa.
 
Back
Top Bottom