Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,952
- 10,037
Hapo ndipo patamu. Hakuna fisadi hapa, hawa ni watakatifu wa Chama. Hivi jamani tuhuma za ufisadi za Chenge zilianza lini? Jamani Chenge si ndiye alikuwa kwenye Kamati ya Maadili ya CCM wakati wa mchakato wa kuingia kwenye Uchaguzi wa 2010? Kamati ya Maadili si ndiyo iliwaengua baadhi ya wanachama wa CCM kwa kukosa maadili? Chenge kama alikuwa fisadi alipata wapi maadili ya kushiriki kuwaengua wanachama wasiokuwa na maadili? Au ndani ya CCM watu wasiokuwa na maadili ndio wanatumika kuwajua wenzi wao wasio kuwa na maadili? Hawa mapacha watatu si Mafisadi, wanaonewa tu