Lowassa, Rostam sasa kuwasha moto

Lowassa, Rostam sasa kuwasha moto

images


wengine hawa hapa

Duh! wako wengi!
 
Kuna kakikundi kanamdanganya Kikwete lakini muamini msiamini salama yake iko mikononi mwa hao mnaowaita mapacha watatu. Kama ni kuzama basi watazama kwa pamoja na mimi namhurumia sana huyo kijana Nape Nnauye ambaye uropokaji wake utadhani kaurithi.

Kikwete, Lowassa na Rostamu ndio hasa ni mapacha watatu huku Chenge akiwa ni ndugu wa karibu kwa uzao kwenye hilo koo ovu la kifisadi. Ili taifa lisalimike na liweze kusonga mbele inabidi kizazi hicho chote kitokomezwe bila ya kubakizwa hata mtoto wa kufikia.

Ukweli lazima usemwe - mapacha watatu ni Kikwete, Lowassa na Rostamu !
 
NgumiJiwe,
Sina hakika kama umefanya utafiti wowote au unaandika kwa hisani kwa sababu unazojua mwenyewe! Jana nimekuwa na mkutano mkubwa sana wa hadhara Igunga. Utadhani wanaigunga wote walikuja,kwa kuzingatia Igunga ni mji mdogo sana. Wana Igunga walikuwa na hamasa ya ajabu.Watanzania wa Igunga wameiva na kuchoka kama walivyo Watanzania wote. Nilipokwenda Monduli wakati wa Kampeni, Lowasa asubuhi yake alikodisha Mabus kuwahamisha wananchi kwa kuwabeba bure, lakini pamoja na jitihada hizo uwanja ulifurika. Ndio maana pia akashinikiza Chuo cha waalimu kufungwa siku chache tu kabla ya uchaguzi.
Hata hivyo, niliwahi kumwuliza Edward Lowasa ni kwanini alijiuzulu, wakati Fisadi nambari mmoja(JK) hajajiuzulu? Richmond haipo na wala isingeliwezekana bila mkono wa JK na ndio maana ya usanii wote unaoendelea. Ni kwa msingi huo nimemtaka Lowasa atoke hadharani, aeleze ukweli wote kuhusu aliyempa siku 90 ili jamii ijue kuwa hakuwa peke yake. Hivyo, kama kuna mwenye ushahidi mwingine tofauti na nilivyoeleza na siyo hisia amwage hapa jamvini.



watavuna wanachama wengi kwani wanakubalika sana miongoni mwa watanzania..vipi umefurahi sasa?ndicho ulichotaka kukisia hiki!
 
Hongera sana Dr Slaa kwa kuwafunua macho Watanzania katika kila kona ya nchi yetu ili wafahamu uovu mkubwa wa chama kilichopo madarakani.
 
Mkuu inamaana mimi sijaelewa au? Hao mabwana watawasha moto au watagawa mapesa? Nielewesheni aisee!

Wao wanasema half of the story about Tanzania's corruption is not told. Wakieleza ya upande wao hata mnaowaona watu safi watachafuka kuliko hata wao. Maana hata wao walikuwa wakitumwa na wao.
 
Hakuna staili wanayowezakuja nayo kwa Watanzania wa hiki kizazi cha digital, mbinu za analog zimepitwa na wakati ndiyo maana wamekuja na kauli mbiu ambayo hata mtoto wa chekechea anajua, ukimuuliza nani huwa anavua gamba, atakuambia ni nyoka... na ukimuuliza akishajivua gamba anabadilika kuwa samaki? atakujibu anakuwa nyoka yule yule ila ataongeza mng'ao na nguvu zaidi. Hii ina maana sasa tunakwenda kwenye mng'ao wa mafisadi wapya ambao jamii haitawashtukia haraka mpaka JK amalizie ungwe yake iliyobakia...
 
Kuna mtu ametunga jina zuri sana la hawa ma celebrity wa UFISADI

RACHEL = (R)ostam, (A)ziz (Ch)enge, (E)dward (L)owassa
 
ili changes zitokee lazima contradictin ziwepo.
hapa sasa tunaelekea kuzuri sana, waache wachokozane na waharibine lakini mwisho wa siku
wataishia kubyatu na hyo CCM yao inakufa kifo kibaya sana.
 
Awazalo mtu ndilo linalomtokea na walipanda mahindi sasa wanataka kuvuna zabibu ama kweli MAGAMBA wamekosa cha kufanya;ccm haifai ila ule wimbo aliotunga Komba bado unavutia'ccm ccm ooh chama cha majambazi ccm namba wani'
 
Jamani tusidanganyike hivi kweli Nape anafanya kazi ya ukuu wa wilaya kiufanisi maana hajaenda ofisini muda mrefu kwanini asifukuzwe kazi au watendaji wapi wa serikali wanaotakiwa kufukuzwa pia hajui anachoongea anao uwezo wa kutekeleza anenayo?
 
Dah,hii thread kumbe tamu nami nimedandia tu kwa mbele ybidi nirudi step one nisome kwa makni.
So the twins had to advertice that.'we will be using kype to relatives'someone is pushing lies here.
 
Mi sidhani kama JK anajua anachokifanya. eye ndo swahiba wao mkuu, amekuwa akiwakumbatika kwenye tuhuma nyeti kama za Richmond, Dowans na nyingine nyingi. Leo atawatosaje? In short JK ndo gamba kuu
 
You must be joking mkuu or you are out of your mind!
Yaani RO wa UWT,CDF wa JWTZ na IGP wa Police wako kwenye payroll ya RA,EL na AC?
That is a serious, irrelevant and unwarranted proposition.
I doubt you know what you are talking about.

Yaani huyo yupo sawa kiakili ile mbaya. Mzee wangu hujaona ya firauni!
 
CCM haiwezi kujivua gamba na kubaki hai kwa sababu ndani ya CCM hakuna aliye safi. Yaani ina maana kwamba Rostam, Lowasa na Chenge peke yao ndio wameifikisha Tanzania hapa ilipo? C'mon let us be serious! CCM iache kuwahadaa watanzania. Tunakumbuka jinsi rushwa ilivyotawala katika ngazi zote za uchaguzi wakati wa primaries mwaka jana. Watu walikuwa wanagomabania kuingia kweye uongozi kwa gharama yoyote.

Tunakumbuka kuchafuana baina ya wana CCM kulivyoshamiri! Tunakumbuka pia jinsi kikwete alivyoingia madarakani kwa njia ya mitandao na kuchafuana bila kusahau matumizi ya kufuru ya pesa, nyingi pia zikitoka kwa rostam aziz. Nakumbuka kingunge mwiru alikuwa anakesha na viongozi wa wanafunzi wa chuo kikuu usiku kucha ili wamuunge mkono kikwete, na hela nyingi zilitumika kuhonga wanafunzi. Wengine tulinunulia hapo magari. Tunakumbuka jinsi salim ahmed salim alivyochafuliwa na kina kikwete na timu yake. Rushwa na hongo have been institutionalized in CCM.

Huwezi kupata nafasi bila rushwa na hongo. Tangu mwenyekiti wa taifa mpaka mwenyekiti wa shina. Sijui ni nani wa kumvua gamba mwenzake! CCM ni chama ambacho kwa ujumla wake kimepoteza maadili. Kubadilika labda itakichukua miaka 50 ijayo.

Uozo umejikita na kuota mizizi ndani ya CCM kwa miaka zaidi ya 30 iliyopita. Kutoa kafara watu wachahce eti chama kinajisafisha ni kiini macho. je baada ya kuwatoa kafara hao mapacha watatu sisi wanacnhi tutafaidikaje?

SIsI tunataka hela zetu zilizoibwa zirudishwe.Si mmekubali kwamba hao ni mafisadi, filisi mali zao! Nyie fukuzaneni au lindaneni, sisi tunataka hela zetu zote zirudi na iundwe independent commision ya kuziratibu hela zinazorudishwa. Watz sasa hivi tuna akili. Tumeamka.









I say thanks for this useful post, sijui prezidaa alikuwa anafikiri nini hapo, hii ni kuwafanya watanzania wajinga wasio na uwezo wa kifikiri, ni bora hata jk angeacha wakajipigia kampeni wenyewe, sidhani kama wangeshindwa bila kikwete, pili kwani jk aliwapigia kampeni wagombea wote wa ccm, sasa kwa nini hawa. This was a big mis-calculation.
 
Back
Top Bottom