Lowassa katika kashfa mpya! Ni ya uuzwaji kiholela wa UDA

Naomba kama ni waumini kweli tukumbuke tutahukumiwa kwa kauli zetu na matendo yetu. Tumuogope mungu mambo mengine. Tusijidanganye kwamba tutasamehewa dhambi zetu tukitubu; dhambi ikishaandikwa haifutiki adhabu yake kaburini na kiyama.
 
Hajawahi kukaa kwenye idara yoyote bila kuiba huyu bwana, imani yangu haiwezi potoka kuwa endapo ataruhusiwa kwenda ikulu tutashuhudia wizi mkubwa sana ndani ya serikali.

Huyu ni wa kumkwepa kama UKIMWI
 
Kura yangu kwa lowassa tyuu, dr masaburi ametoa majibu kwa makalio hajatumia ubongo, na hatudanganyiki ng'oo
 
Mmechelewa na kashfa zenu hata kama kafanya kweli hakuna wa kukuelewa tunajua mnamuonea tu
 
Hivi huyu Lowassa ni genius kiasi gani? Hakuna mtu anayeweza kumzuia kufanya lolote nchi hii? Inawezekana kweli? Ni huyu huyu Masaburi wakati wabunge wa Dar wanamshambulia bungeni kuwa kauza UDA alisema wabunge wa Dar wanafikiri kwa kutumia Makalio. Leo hii nae Kaanza kufikiri kwa kutumia makalio?

Kuna mtu mwingine wa hatari anajiita joka la makengeza.
Noma sana.
 
Akizungumza kwenye mdahalo uliondaliwa na kurushwa na AZAM TV jana, Mgombea Ubunge jimbo la Ubungo, , Dr. Didas Masaburi(CCM), alisema anayepaswa kulaumiwa kwa uuzwaji holela wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam(UDA) ni LOWASSA, aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, kwani ndiye aliyekuwa msimamizi wa mchakato huo mwaka 2006 hadi 2008.

"Kwa mujibu wa sheria , Waziri Mkuu ndiye msimamizi wa Serikali za Mitaa", alisema Dr. Didas Masaburi katika mdahalo uliohudhuriwa pia na wgombea wengine, Said Kubenea wa Chadema, Zangina Shangana(ACT-Wazalendo) na Renatus Muhabi(CCK).

Awali ilidhaniwa kuwa hoja ya uuzwaji wa UDA ungempa wakati mgumu Dr. Masaburi, lakini hali haikuwa hivyo kwani alitumia nafasi hiyo kutoa ufafanuzi ulioeleweka na kumtupia lawama Lowassa. Mbali na Richmond, Lowassa pia anatuhumiwa kuwa na hisa katika kampuni ya Integrated Property Limited inayohusishwa na ujenzi ambayo haikuiorodhesha kwenye Tume ya Maadili kwa mujibu wa sheria kama mtumishi wa Umma.

Mimi sijahusika na ufisadi katika uuzwaji wa UDA, nilichokifanya ni kupandisha bei yake kutoka bil.1 hadi sh.bil. 5.7nilipoingia kwenye UMEYA na kukuta shirika hilo limeuzwa isivyo halali.

Meya 2011niligundua mkataba usio sawa wa uuzwaji wa UDA baada ya kuajiri kampuni ya Ukaguzi wa hesabu ya KPMG, Bei yake haikulingana na thamani ya mali za shirika hilo, hivyo niliamuru mnunuzi, Simon group kuongeza fedha.

Soma zaidi RAIA TANZANIA.
View attachment 289852

Au ndio maana jamaa alijiharishia kweupee baada ya kusikia habari hizo. Magufuli go go go go!!!!! Ikulu yako
 
Yapo mengi yanayomuhusu mzee mamvi.
Wakati mnategemea kashifa ya uda itamgusa Masaburi ili Kubenea imbebe kwenye kampeni zaubunge ubungo, ukawa Bila kujielewa mmemkaanga lowasa tena.
No research no right to speak
 
Mweney macho haambiwi tazama,

Walikuwa wapi iku zote hizo? Scandal hizo mbona zilivuma sana hawakusema na nyngine wali husika nazo mbona hawatajwi? Kwa nini wanao tajwa ni walio jitenga na Chama?

Wana mabadiliko kaza kamba, haya yote wna CCM wana yataja kwa sababu tu wameona wananchi wameanza kujitambua, mkirudi nyuma tu mmekwishaaa! Mkikaza kamba zaidi ndiyo pona yenu kwani watafunguka zaidi na mali zenu zitakuwa salama na pengine kurejeshwa! Msidanganyike hadi trh 25 Oct 2015 bado siku chache tu...
 
Huyu mzee sasa anatia uvivu hata wa kudhani kuwa angegombea urais. Watanzania tuamke nchi inaenda kuuzwa hiii. Mtu anakuwa na kashfa lukuki za uuzwaji wa ranchi za ufugaji ng'ombe taifa, richmond na sasa UDA. Tuachaneni na huyu mtu jamani.

Sema niachane na huyu mtu siyo tuachane hujatumwa.
 
ukifuatilia kwa makini mazungumzo yote ya CCM ktk kipindi hiki cha kampeni utagundua kuwa kwa hakika ni wakati madhubuti wa kufanya mabadiliko ya UKWELI
ukimsikiliza MAGUFULI analalamika kwa dhati kuwa khali mbaya ya WATZ imesababishwa na uongozi dhaifu wa CCM
mf akiwa KAGERA analalama kuwa alikerwa na kuumizwa na ubinafsishaji kiholela wa ranchi 52 za Taifa na kuongeza hata rais KIKWETE naye alikerwa pia. JIULIZE ni muda gani umepita mpaka leo wananchi wameumia kiasi gani? rais anahuzunika na waziri wake anahuzunika nani wa kutoa maamuzi,
vinginevyo alipaswa atuambie kuwa wakati akiwa waziri alimshauri rais wawanyan"ganye wale waliobinafsishwa akakataa au akagwaya hivyo apewe rungu sasa ili atekeleze urejeshwaji huo vinginevyo na yeye ni DHAIFU, mdanganyifu muomba kura kwa hila.
akumbuke kuwa kama yeye anakerwa na uuzwaji wa ranchi 52 nasi pia tunakerwa na uuzwaji wa nyumba za serikali na hata rais KIKWETE alisema kuwa si vyema kuuza mali za serikali kiholela wakati alipoulizwa juu ya urejeshaji wa nyumba hizo alikerwa na maamuzi hayo ya uuzwaji lkn alibanwa na mfumo, hivyo mgombea wa CCM hawezi fanya mabadiliko ya kweli ni kiini macho tu. tusisite UKAWA kuna majibu ya mahitaji yetu.

Hata mumsafishe vipi fisadi ni fisadi tu, hatuko tayari kuuzwa tunajiona, lowasa ana mengi yakujibu nawashangaa leo eti amekuwa shujaa kisa kahama ccm, hata kama tunataka mabadiliko si kwa style hiyo, huo ni usanii live
 
CCM mnaangaika sasa si mmeshaambiwa na TWAWEZA mtashinda kwa asilimia 63%sas shida ya nini UKAWA elezeni kura tuache hawa waendelee kulalamika mafisadi wakati walikuwa na uwezo wa kumkamata na kumfungulia mashtaka sasa wanalilia lia nini.Lowasa hata kama utashinda chukua mwa yangu wewe chuma ubabaishi na kitu weka sera mbela
 
Dah ndo nazidi kumkubali kumbe jamaa ni mafia hivi hii nchi akiichukua itafika mbali Sana mana anajua kutafuta pesa za Maendeleo lowassa atosha
 
Back
Top Bottom